Nani amesema kuwa Freeman Mbowe atagombea tena uenyekiti CHADEMA?

Nani amesema kuwa Freeman Mbowe atagombea tena uenyekiti CHADEMA?

Tangu jana, mara baada ya Wakili Tundu A.M. Lissu kutangaza kugombea uenyekiti wa Taifa wa CHADEMA, kumekuwa na 'kuwapambanisha' Mwenyekiti wa sasa Freeman Mbowe na Lissu kwenye uchaguzi wa CHADEMA utakaofanyika mwakani.

Kuna siku nilimsikia Lissu akisema kuwa mtia-nia yeyote ndani ya CHADEMA huwasilisha nia yake hiyo kwa Katibu Mkuu wa CHADEMA. Hadi hapo, taarifa rasmi za mtu fulani kugombea nafasi fulani ndani ya CHADEMA hutolewa na mgombea mwenyewe au Katibu Mkuu.

Sikuwahi kumsikia Mbowe au Katibu Mkuu Mnyika kutoa taarifa rasmi kuwa Mbowe atagombea tena uenyekiti wa CHADEMA Taifa kwenye uchaguzi ujao. Sasa, nani hasa anatuaminisha kuwa Mbowe na Lissu watapambania uenyekiti wa CHADEMA?

Binafsi, naona kumeshakuwa na maridhiano na makubaliano baina ya Mbowe na Lissu kuachiana nafasi hiyo ya uenyekiti. Kama Mzee Mtei alivyomwachia Hayati Bob Nyange Makani; Makani alivyomwachia Mbowe ndivyo sasa Mbowe anavyomwachia Lissu.

Endapo Mbowe atagombea, mchuano utakuwa mkali na CHADEMA haitabaki salama baada ya uchaguzi huo. Kwa kauli za Lissu juu ya uchaguzi huru na haki na endapo atashindwa, namuona (kama nilivyomuona Mchungaji Msigwa) Lissu akiondoka CHADEMA.
Hicho ndicho cha kushangaza. Lakini nadhani itakuwa busara kwa Mbowe kuweka wazi azma hiyo ya kutogombea ili joto lipoe kidogo. Mimi sidhani kama Mbowe hakujua kuwa hii ilikuwa nia ya Lissu ya muda mrefu kidogo. Matamshi na matendo yake kwa muda sasa yameashiria kuwa haridhiki na hali ilivyo ndani ya chama chake. Hatua ya mwisho ya kupuuza kikao kilichoitwa na kubakia Singida kuhudhuria mazishi ya mgombea wa CDM ilikuwa ishara kubwa.

Sasa hivi anaweza kufanya ya fuatayo:
1. Ajiunge na wakina Msigwa n.k. kwa kusema wazi kuwa anayesababisha matatizo yote ni Mbowe. Itabidi aeleze anayoona kuwa ni mapungufu yake ( k.m. matumizi mabaya ya pesa za chama, utawala wa kiimla, ukabila, kupoozwa na wapinzani wake, kuwatilia fitna wasiokubaliana na hata kuhusika katika shambulio dhidi yake na wengine) kwa uwazi kabisa. Hii itakuwa ni kutangaza vita ya kung'oa wale wote anaoamini kuwa wanakipeleka chama kubaya ili kiweze kuzaliwa upya.
2. Kuweka wazi kuwa hana ugomvi na Mbowe ila anatofautiana nae katika mpango mkakati wa namna ya mwelekeo wa CDM. Kuwa yeye anataka kiwe cha grassroots zaidi kwa kubebwa zaidi na wanachama na wafuasi wake. Badala ya kutegemea zaidi ruzuku na michango ya matajiri, ada na michango midogo midogo kutoka kwa wafuasi ndio zitaendesha chama kwa kiasi kikubwa. Ili kuepuka criticism za unafik itabidi aweke wazi mapato yake na matumizi ya michango ambayo imekuwa inakusanywa kwa niaba yake. Kwa kufanya hivi itakuwa ameonyesha kuwa hizi tofauti ni za kwenye principle na sio personal. Hiyo itaweza kusaidia kuepusha mpasuko ambao hautakisaidia chama na tayari wasiotakia mema chama chake wameanza kutumia.
3. Kutangaza kuwa yuko tayari kushindana na yeyote yule na muhimu zaidi kukubali matokeo ya uchaguzi kama utafanyika kwa uwazi na kufuata taratibu zilizowekwa.
4. Kusema kama ataendelea katika nafasi yake ya sasa hivi au atajitoa ili aweke nguvu zake katika kujiandaa kwa ajili ya uchaguzi ujao.

Ingawa ni haki ya Lissu ya kufanya alivyofanya lakini ni lazima ajue kuwa yeyote atakayekuwa Mwenyekiti baada ya uchaguzi atakuwa na kazi kubwa sana ya kukiunganisha chama chake. Hatari kubwa ni kuwa hata kama atashinda itakuwa ni pyrrhic Victory.

Kuna usemi kuwa unatakiwa kuwa muangalifu unapo muomba kitu Mungu kwa sababu anaweza kukupa.

Amandla...
 
Ni hawa akina mama wa UWT ndiyo wanashadadia mambo ya CHADEMA huku CCM hakujawahi kufanyika uchaguzi wa Mwenyekiti hata siku moja, kuhusu Lissu kuondoka CDM haiwezi kufa aliondoka Zitto, Slaa, Halima na haijafa sembuse Lissu? Lissu siyo tishio kama watu wanavyodhani isipokuwa ni tishio sababu anapata support ya CHADEMA.
Hahaha
 
Maccm yamehamaki sana Lissu kugombea uenyekiti wa Chadema.
Kwa sababu yanajua misumari yake ni ya moto sana. Na akimuongeza Heche, lazima vijana waende barabarani , ya Asadi yatakuja mapema sana hata kabla ya uchaguzi mkuu wa 2025. Hicho tu ndicho ccm wanaogopa.
Mageuzi ya katiba mpya na tume huru hawataki, kutoka au kuachia madaraka kwa hiari kama mzee kifimbo, hawataki, kuanzisha mchakato wa maridhiano pia hawataki. Sasa mimi huwa najiulizaga, hivi hawa ccm wanataka ni haswa? ni kukaa madarakani hadi lyamba Yesu arudi na kusahau kwamba kila generation ina mahitaji yao au ni nini haswa kinacho wakwamisha kutatua matatizo ya nchi yetu haswa hili lka katiba na tume huru. Mbona ni wagumu sana kukubari na wawape watanzania kitu wanachotaka? CCM tafadharini waungwana, leteni mabadirko ya haraka kwa nchi bila ajizi na hiyo ndiyo salama yenu huko mbeleni, si vinginevyo.
 
Ni hawa akina mama wa UWT ndiyo wanashadadia mambo ya CHADEMA huku CCM hakujawahi kufanyika uchaguzi wa Mwenyekiti hata siku moja, kuhusu Lissu kuondoka CDM haiwezi kufa aliondoka Zitto, Slaa, Halima na haijafa sembuse Lissu? Lissu siyo tishio kama watu wanavyodhani isipokuwa ni tishio sababu anapata support ya CHADEMA.
Hivi wale vibaka ya CDM bawacha watakuwa wapo upande gani ?
 
Sipati picha, Lissu Mwenyekiti John Heche Katibu Mkuu, wengine ongezea wewe...........................
 
Ni hawa akina mama wa UWT ndiyo wanashadadia mambo ya CHADEMA huku CCM hakujawahi kufanyika uchaguzi wa Mwenyekiti hata siku moja, kuhusu Lissu kuondoka CDM haiwezi kufa aliondoka Zitto, Slaa, Halima na haijafa sembuse Lissu? Lissu siyo tishio kama watu wanavyodhani isipokuwa ni tishio sababu anapata support ya CHADEMA.
Namuona pia J. Heche akiwa makamu mwenyekiti.
 
Back
Top Bottom