Nani anafahamu jinsi ya kusali Novena ya Mtakatifu Rita wa Kashia anisaidie?

Nani anafahamu jinsi ya kusali Novena ya Mtakatifu Rita wa Kashia anisaidie?

Halafu jamani kwanini kama kitu mtu hukijui au huna jibu usikae tu kimya?matusi, kejeli, dharau kwa imani za watu wengine ni ya nini?Kama imani yako haiko kwenye imani za wengine kwanini uone wanakosea?
Kila mtu ana namna yake ya kumuomba Mungu ili afanikishiwe mambo yake au amshukuru Mungu.
Tusiwe hivi jamani tujitahidi kuwa wavumilivu wa imani za wenzetu na huo ndo ukomavu wa kiroho.
Ukileta imani yako hapa JF lazima ukubaliane na reactions zote.

Vinginevyo kama hutaki ikosolewe, Baki nayo huko mwenyewe.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Haya mambo niliona ni upuuzi nikaacha nakwenda kanisani kabisa, yaani unakaa unategemea binadamu mwenzako akusaidie ufanikishe mambo Yako ilihali yeye mwenyewe ameozea aridhini, Dini hizi zililetwa kutupumbaza akili tu na kutuongezea umasikini, ulaya watu wanachangishana pesa wanajenga shule full equipped, watoto wao wanapata maarifa ya kupambana na maisha, sisi tunachangishana pesa kujenga mikanisa mikubwa tunaenda kuimba litania ya Lita na Maria, na kunywa maji ya upako Ili tupate maisha mazuri
Waafrika wamepumbazwa haswaa

Waka pumbazika.

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Huyo mtakatifu Rita ni mzungu au mwafrika? Yupo hai au alishafariki?? Kama alishafariki maanake unaanudu mzimu wake au??
 
Huyo mtakatifu Rita ni mzungu au mwafrika? Yupo hai au alishafariki?? Kama alishafariki maanake unaanudu mzimu wake au??
Waafrika ni watu wa ajabu sana.

Wana sali na kuomba roho za wafu wa wazungu ziwasaidie halafu roho za mababu zao wana zikemea.

Roho za wafu wa wazungu wana ziita Watakatifu halafu roho za mababu zao wana ziita mizimu.

Waafrika wamelogwa..!!!

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
 
Utumwa mwingine huu hapa Kiranga njoo umeone huyu
Mkuu Africa hakuna therapy watu wanafanya dini kuwa ndiyo psychotherapy yao.

Kwa upande mwingine, nawaachia tu uhuru wao wa kikatiba wa kuamini wanachotaka.

Mtu akiwa anatimiza haki yake ya kuamini tu mimi sina tatizo naye sana, nina tatizo anapoanza kuhubiri na kusema dini yake ndiyo ya kweli.
 

Attachments

  • FB_IMG_1646910666536.jpg
    FB_IMG_1646910666536.jpg
    132.9 KB · Views: 17
Tafuten pesa achaneni na mambo ya kipuuzi hayo yaliyo tutia umasikini miaka na miaka
Mshauri asali kwa jina la Bibi yake Mzaa Baba kupitia mizimu yao badala ya Marehemu wa kizungu wanaoitwa Watakatifu

Ujinga Mtupu
 
Nenda kwenye play store download app ya Mt.Rita wa Kashia kuna sala zote pale.
Kama tayari unayo unataka kusali ya masaa 15 au ya siku 9
[emoji1787][emoji1787][emoji1787] sijui Mtaacha lini huu Utumwa na Ujinga
 
Waafrika ni watu wa ajabu sana.

Wana sali na kuomba roho za wafu wa wazungu ziwasaidie halafu roho za mababu zao wana zikemea.

Roho za wafu wa wazungu wana ziita Watakatifu halafu roho za mababu zao wana ziita mizimu.

Waafrika wamelogwa..!!!

Sent from my Infinix X657B using JamiiForums mobile app
Bado sanamu
230489528.jpg
 
naomba ushuhuda wa jambo moja ulilojibiwa na hiyo sala tafadhali.
Mkuu, unahitaji Ushuhuda wa Majibu ya Novena ya Mt. RITHA WA KASHIA...

Naomba, nishuhudie aliyonitendea mimi binafsi, na ingewezekana pia ungepata shuhudiwa na wale wanaonifahamu.

Kwa Ufupi.
Ipo, hivi nilikuwa na changamoto ya uvimbe ambao ulinisumbua kwa miaka kadhaa, na sio siri wengi wa wanaonizunguka/wanaonifahamu walikuwa wanauona na kwa kipindi chote ilikuwa ni changamoto kuutoa au kufanyiwa upasuaji.

Pindi, niliponuia na kuanza kusali Novena ya Mt. Ritha wa Kashia nilipata msukumo wa ajabu na kurudi Hospitali ambapo huwezi amini kwa taratibu za ile hospitali (ni moja ya Hospitali kubwa hapa nchini) ingeweza chukua zaidi ya miezi na miezi hadi upasuaji ila ndani ya mwezi 01, kwa jinsi operation ilivyokimbizwa hadi kupatiwa booking ya kwenda theater ni muujiza ambao ninaweza kuandikia story yake nyingine.
Ila kwa ufupi nimefanikiwa kufanyiwa upasuaji na sasa ninaendelea kurecover vizuri kabisa, Mimi ni ushuhuda wa majibu chanya ya Novena ya Mt. RITHA WA KASHIA, hapa nimeandika kwa kifupi ila in between huo mwezi mmoja wa Matibabu kuna mengi yalikuwa yanatokea am sure bila ya usimamizi wa huyu Mama yasingeweza kutokea na kufanyika (kuna muda hadi Matabibu walikuwa wanashangaa kwa jinsi mambo yanavyoenda kipindi wakiwa wananihudumia).

Hitimisho.
Najua katika forum hii kuna watu wa imani mbalimbali pamoja na wale wasio na imani hivyo ni vyema kushikiria kill ambacho unakiamini na unatarajia kinakupeleka katika wokovu, kwangu mimi huyu Mama amekuwa msaada kwangu na nitaendelea kumkimbilia kwa mambo yote yalishindikana.

Nb. TUSIBEZE AU KUPUUZA NGUVU YA SALA.
 
Back
Top Bottom