Nani anamdanganya Rais Samia kuwa kati ya Watanzania mil 65, ni milioni 2 tu wanaolipa kodi?

Ndio huwezi hesabika mlipakodi.kwa sababu uko kwenye informa sector ambako hakutabiriki...
Huwezi kutoza direct tax mifugo inayouzwa mnadani bila kujua muuzaji kapata faida kiasi gani. Direct tax inatozwa kwenye faida, sio kwenye mapato au hasara.
 
Bodaboda, mama ntilie, mawinga, fundi gereji, seremala, wakulima, wavuvi na wamachinga waanze kulipa direct tax.

Kwani hata wakilipa hizo, Kwa serikali hii, tofauti ipi itakuwapo?
 
Hiyo indirect tax wanaolipa wengi wanatumia huduma zaidi ya wanavyolipa kodi, so on balance wanakuwa net takers...
Haya madai yangekuwa na mashiko kama watu wa vijijini ambao ndio wengi zaidi wangekuwa wana barabara za lami, maji ya bomba, shule zenye walimu na hospitali zenye madaktari
 
Imetulia swali la maana sana humu wengi ni wasomi uchwara tu kwani wakilipa indirectly hazifiki serikalini

USSR
Kwani hata wakilipa hizo, Kwa serikali hii, tofauti ipi itakuwapo?
 
Watu kibao wako informal sector na Wana TIN

TIN siyo Kwa biashara tu πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚
 
Haya madai yangekuwa na mashiko kama watu wa vijijini ambao ndio wengi zaidi wangekuwa wana barabara za lami, maji ya bomba, shule zenye walimu na hospitali zenye madaktari
Watu wa vijijini hizo huduma walizopelekewa sasa tu hawajaweza kuzi fund vizuri, tumetegemea sana misaada na mikopo.

Sasa unataka wapelekewe huduma zaidi kwa kodi gani wanayolipa?

Mtu mwenye average GDP per capita ya USD 1200 analipa kodi kiasi gani mpaka aweze ku fund huduma za jamii anazopewa?

Watu wamepelekewa umeme wa bei chee na wameshindwa kujiunga kwenye grid.

Na waliojiunga wanalalamika umeme uko bei ya juu, hata baada ya bei ya umeme Tanzania kuwa heavily subsidized na miongoni mwa bei nafuu Africa.

Katika nchi 10 zenye bei ya juu kabisa ya umeme Africa, Tanzania haimo. That is the top 25%.

Lakini watu bado wanalalamika umeme bei ni ghali. Licha ya wafanyabiashara wakubwa wachache kuchukua mzigo mzito kulipia wengi umeme.

Watu wanasema umeme ni ghali, si kwa sababu bei ni kubwa sana kiuhalisia kwa viwango vya kimataifa, hata Africa tu, bali kwa sababu kipato cha watu kiko chini, uchumi mdogo.

Sasa, badala ya ku fix tatizo la msingi la ku fix uchumi uzalishaji uwe effective zaidi, mna focus kwenye kudhibiti matumizi ya viongozi.

Nakubali matumizi ya viongozi ni tatizo. Lakini hilo si tatizo la msingi. Si tatizo la kiini kabisa. Kuna nchi zina viongozi wana natumizi ya kufuru, lqkini wanaweza kuhimiki matumizi hayo, kwa sababu uchumi unazalisha.

Ukidhibiti matumizi ya viongozi bila ya kuwa na mkakati mzuri wa kuongeza uzalishaji, hata hizo fedha itakazookoa kwenye kudhibigi matumizi ya viongozi hutaweza kuzizungusha vizuri upate uchumi mzuri.

Tatizo letu si fedha, tatizo ketu ni ideas na usimamizi wa hizo ideas zipate matunda nazuri.

Hiki ndilo tatizo la msingi, hili hiki tatizo ndilo linalosabqbisha hata matumizi ya viongizi yawe mabaya. Ukiweza kulitatua tatizo hiki, utatatua mambo mawili kwa wakati mmoja.

Utaongwza ufanisi katika uzalishaji na kupunguza matumizi mabaya.

Hela kama haina project ya maana ya uzalishaji itapotwa tu, sasa unataka kudhibiti matumizi mabaya bila mkakati wa matumizi mazuri?

 
Ina maana Watanzania 65m wote ni watu wazima? Mbona Viongozi wanatuchanganya kama vile sisi hatuelewi?
 
Ni lazima wamdanganye ili waibe zaidi na wasishtukiwe na kufukuzwa kazi !

Kodi inawekwa katika kila bidhaa inayotumiwa na wananchi wote millioni 65 !
Hata mtoto akinunua pipi au biskuti ameshachangia kodi !

Huduma zote zinazotolewa you name it ipo kodi inalipwa humo,
Inawezekanaje waseme eti wanaolipa kodi ni watu milioni 2 tu ???!!! πŸ˜±πŸ€¦πŸ½β€β™‚οΈ
 
Kwa kauli hiii niseme huyu mama hatufai sisi watanzania …… hatakama hajasoma maswala ya tax inamana hata uelewa mdogo tu ameshindwa kujua ni watu wangapi wana lipa kodi
 
Kwani hana kichwa mpaka awe anadanganywa killa siku? Hata kwenye kubet kuna kodi inakatwa...
 
Ina maana Watanzania 65m wote ni watu wazima? Mbona Viongozi wanatuchanganya kama vile sisi hatuelewi?
Waongo sana wanamdanganya Rais Samia

USSR
 
..yeye mwenyewe kwa nafasi yake kama Raisi halipi kodi, halafu anatufokea masikini na wanyonge wa nchi hii.
Afu anasema kabisa kuna mamantilie hawataki kulipa kodi.πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ nacheka kama mazuri.
 
Afu anasema kabisa kuna mamantilie hawataki kulipa kodi.πŸ˜‚πŸ˜‚πŸ˜‚ nacheka kama mazuri.

..kuna Mama mmoja kasema Mama Abduli is not intelligent. Kuwa Rais wa nchi kubwa kama Tanzania kunahitaji upeo mkubwa kuliko alionao Mama Abduli.
 
Tatizo ni kwamba she never expected to assume presidency!
Hii position ni nyeti sana, inahitaji anaeweka nia ajue anachokuja ku accomplish kwa kipindi chake!(vipaumbele)
Sasa yy kwa katiba hii mbovu kaokota dodo chini ya mnazi, frankly speaking naamini na anaamini wengi mnaona mambo inavoenda sasa,ni kama kuna watu wana run nchi na yy ana viji portion vyake vya kusimamia, bora liende,TRA wana sema wamevunja record ya collections juzi, leo kwa kujimix anaongea quite the opposite!
Hela hamna mzungukoni, huo uchumi unaokua ni upi unaozungumzwa?
Project ipi kubwa ameanziasha? sababu hata SGR ya kwenda Kgm imesimama!
Tuache unafki,lets call a spade a spade!
 
Anajifaragua kujionesha kwamba ana akili sana wakati siyo kweli!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…