Nani anatoa fedha za miradi, Rais au Serikali kutokana na bajeti yake?

Hizi kauli zilianza kipindi chaa dikteta uchwara jiwe. Na wapenda teuzi kwa kujipendeza waliifanya iwe sheria
 
Watumie neno "Mh.Rais Samia Sululu Hassan ameidhinisha kiasi.....cha TSh...katika bajeti iliyopitishwa na Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania"
Na kama ni dhalura waseme "ni kutokana na Nia njema ya Mh.Rais kuongea fedha hizo kutoka mfuko wa Hazina ili kuondoa mapungufu yaliyojitokeza katika bajeti iliyopitishwa na Bunge"
 
Rais wa kiafrika ana pesa nyingi sana, yeye huwa anatoa tu miradi isogee
 
Hivi ile elimu ya katiba inaanza kutolewa lini na kwa mfumo gani?
Pia hakuna app au tovuti ya katiba ya jamuhuri ya muungano tuweze kujifunza huko?
 
Elimu elimu elimu. Ulichosema kinahitaji mtu mwenye akili timamu kuelewa. Swali ni je Tanganyika wapo wangapi.
Wako wangapi? Wewe siyo mmoja wao. Yaani hujui kuwa Rais ndiye anayeidhisha miamala ya Consolidated Fund? Hivi unajua Consolidated Fund ni mdudu gani? Wee bakia na ujinga wako wenziyo twasubiri Samia 2030 ZFZMWCCM.
 
Wako wangapi? Wewe siyo mmoja wao. Yaani hujui kuwa Rais ndiye anayeidhisha miamala ya Consolidated Fund? Hivi unajua Consolidated Fund ni mdudu gani? Wee bakia na ujinga wako wenziyo twasubiri Samia 2030 ZFZMWCCM.
Mimi ndiye nimemuelewa mleta mada ndo maan nimesema ili aweze kueleweka kunahitaji watu wenye akili, na nikauliza je hao Tanganyika wako wangapi.

Kwa jinsi tu ulivyomalizia kwa matusi direct kwa kuni attact, wewe ndiyo group kubwa la Watanganyika wasio muelewa mleta mada, hivyo basi ....



.
 
Hili jambo linachefua sana.
Hivi Serikali ndio haipo tena au?
Ilianza kwa mpenda sifa wa awamu ya 5 na sasa imekuwa ni lugha pendwa kwa mama!
Hivi mbona ni kama Nchi nzima imekuwa hatuna akili wala weledi!
CCM hii laana mnayoendelea kuibariki na kuitukuza itakuja kuwatafuna sana.
 
Sawa. Kama mumeamua kujikusanya "nyani huku ngedere kule" basi ni hivyo hivyo. Wewe kaa kundi lako la manyani muendelee kumtukana Rais ni hiari yenu. Lakini mshika masarufu wa Consolidated Fund ni Dr S.S. Hassan. Kila ukipata madaftari darasani au chloride maabara jua kuwa ni yeye kakugea. Na ushukuru - kwa vile asiyeshukuru ni kafiri.
 
Kusema Serikali ya Awamu ya Sita(6) inatosha sana...ila naona nae Mh Rais ni kama anapenda vile, maana hakemii?
 
Inasemwa hivyo kwa kuwa Rais ndie mhidhinishaji wa Bajeti. Yeye ndio meenye saini ya mwisho kutoa idhini ya matumizi katika fungu kuu la Serikali
 
Anayelipa ni Pay Master General baada ya Waziri wa fedha na Rais kukubali (assent) alipe. Nadhani hapo utakuwa umeelewa.
Kila kitu serikalini kinafanyika kwa idhini ya Rais kwani ndiye aliyechaguliwa na wananchi wote awawakilishe kuendesha serikali yao.
 
Je,umewahi kusikia kila Rais anavipau mbele vyake? Kwakuwa mahita ji wananchi ni mengi anaweza kuamua kipau mbele kipi kianze kufanyiwa kazi katika hilo hatuna namna kuona Rais anetoa Pesa kwa mradi uliokusudiwa.Ingawa kiukweli Pesa anayoitoa ni YETU/ nchi.
 
Katiba ya Jamhuri ya Muungano ya 1977 inasema:
33(1) Kutakuwa na Rais wa Jamhuri ya Muungano
(2)Rais atakuwa Mkuu wa Nchi,Kiongozi wa Serikali na Amiri Mkuu.
34(2)Mamlaka ya Serikali ya Jamhuri ya Muungano yatahusu utekelezaji na hifadhi ya Katiba hii na pia mambo mengineyo ambayo Bunge lina mamlaka ya kuyatungia sheria.
35(1)Shughuli zote za utendaji za Serikali ya Jamhuri ya Muungano zitatekelezwa na watumishi wa Serikali kwa niaba ya Rais
63(1)Rais kama sehemu moja ya Bunge atatekeleza madaraka yote aliyokabidhibiwa na Katiba hii kwa ajili hiyo.
(2)Sehemu ya pili ya Bunge itakuwa ndicho chombo kikuu cha Jamhuri ya Muungano ambacho kitakuwa na madaraka ,kwa niaba ya wananchi,kuisimamia na kuishauri Serikali ya Jamhuri ya Muungano na vyombo vyake vyote katika utekelezaji wa majukumu yake kwa mujibu wa Katiba hii.
(3)(c)Kwa madhumuni ya utekelezaji wa madaraka yake Bunge laweza kujadili na kuidhinisha mpango wowote wa muda mrefu au wa muda mfupi unaokusudiwa kutekelezwa katika Jamhuri ya Muungano.na kutunga sheria ya kusimamia utekelezaji wa mpango huo.
 
MACHAWA WANAMPAMBA MAMA KWA KUSEMA YEYE NDIO ANATOKA HUKU WAKIJUA FEDHA ZINATOLEWA NA SERIKALI KWA MUJIBU WA BAJETI
UCHAWA HUU UMEANZA AWAMU YA 5

Sent from my SM-A145R using JamiiForums mobile app
 
Kubishana na watu niliosema Tanganyika tupo wachache ni kupoteza muda wangu bure. Baki na uelewa wako usije kufa kwa kihoro.
 
Hatari Sana mkuu. Unajua machawa kwa kawaida sio Watu wenye aibu linapo kuja swala la kutetea vibarua vyao.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…