Nani anayeihujumu TTCL? Kuna tatizo la kuadimika kwa laini, zinauzwa mpaka 7000

Nani anayeihujumu TTCL? Kuna tatizo la kuadimika kwa laini, zinauzwa mpaka 7000

KARLO MWILAPWA

JF-Expert Member
Joined
Apr 10, 2019
Posts
2,789
Reaction score
4,951
Nani anayeihujumu TTCL kwa kiwango hiki?

Kuna mmbo fulani yanaendelea kwenye TTCL kiasi kwamba tunaona kama ni hujuma kwa TTCL:

Kwanza, kipindi kirefu sasa ukitafuta laini za TTCL kwa mawakala wanakuambia hamna. Ni kweli shirika likose laini ambazo kimsingi ndio mteja na ndio zitachochea usambaaji wa huduma kwa watu wengi?

Pili, laini ya TTCL kupatikana kwake ni mpaka uinunue kwa gharama ya shilingi 5000 mpaka 7000 na hii ni gharama ya maeneo mengi ya Dar es Salaam sijajua upatikanaji na gharama zake mikoani na huku laini za mitandao mengine ni bure kabisa na hadi kifurushi Cha kuanzia unawekewa tena bure. Kwa nini zipatikane kwa gharama hivi?

Tunasikia kila siku TTCL kupata hasara lakini kama mambo yenyewe ndio yako hivi basi hasara ni lazima.

Mitandao mingine ikitumia kila mbinu za kibiashara kuhakikisha zinakuwa na wateja wengi kwa kusambaza laini kwa wingi TTCL wako nyuma kwenye ushindani. Kiuhalisia kabisa, watu wengi sio rahisi kununua laini kwa gharama hiyo. Kama ni kuuza, ingeuzwa hata shilingi 1000.

Mhe. Samia na Waziri Nape tazameni hujuma hizi zinzofanywa dhidi ya TTCL na ikiwezekana libinafishwe tu ili liendeshwe kibiashara zaidi.
 
Miaka 3-4 nyuma lain za TTCL zilikuwepo mtaani, nakumbuka ata vocha zake hazikuwa ngumu kupata, vifurushi vyake pia vilikuwa nafuu kuliko mitandao mingine.

Nasikitika kusema kwasasa si Lain ila ata vifurushi vyake viko juu kuliko mitandao yote nchini!
 
Mitandao mingine ikitumia kila mbinu za kibiashara kuhakikisha zinakuwa na wateja wengi kwa kusambaza laini kwa wingi TTCL wako nyuma kwenye ushindani. Kiuhalisia kabisa, watu wengi sio rahisi kununua laini kwa gharama hiyo. Kama ni kuuza, ingeuzwa hata shilingi 1000.
Hata kuunganishwa na internet ni changamoto Mkuu, tumerudi kwenye zama za kupanga foleni kama ilivyokuwa kupiga simu 1990 kurudi nyuma
 
Miaka 3-4 nyuma lain za TTCL zilikuwepo mtaani, nakumbuka ata vocha zake hazikuwa ngumu kupata, vifurushi vyake pia vilikuwa nafuu kuliko mitandao mingine.

Nasikitika kusema kwasasa si Lain ila ata vifurushi vyake viko juu kuliko mitandao yote nchini!
TTCL vocha zilikuwa hazipatikani ila line zilipatikana.

Tulikuwa tunanunua vocha za TTCL kupitia mitandao mingine, TTCL walianza kuzingua walipoanza kupandisha nao bei, watu wakawasepa

Anyway m naona shirika hili serikali iuze majority shares, ibaki na % chini ya 30% kisha 10% zipelekwe DSE (Ambako sijui kama watu watanunua)
 
Nani anayeihujumu TTCL kwa kiwango hiki?

Kuna mmbo fulani yanaendelea kwenye TTCL kiasi kwamba tunaona kama ni hujuma kwa TTCL:
Mashirika kama haya yenye hasara ndo ya kumpa mwarabu awasaidie kuyaendesha. Mnaenda kumpa bandari inayochangia 36% kwenye Pato la taifa
 
We umepigwa unauziwa line...🤣
Mkuu unahakika ulienda kwenye duka la ttcl au kwa vibaka fulani hivi..?
Hao vibaka mbona hawakutaka kunipiga kwenye Halotel, Airtel na voda? Kwa hiyo kibaka anakusajilia laini na kifurushi anakuungia bure kabisa?
 
Kama ukijua kwamba bandari inahujumiwa, ATCL, TRC na reli vinahujumiwa, DART inajuhumiwa, miundombinu inahujumiwa, TANESCO inahujumiwa, NHIF, PSSSF inahujumiwa, mashirika yote ya serikali yanahujumiwa, benki za serikali zinahujumiwa (mtu mmoja anaweza kukopa mabilioni kwenye benki tano tofauti, kisha akapotea na asijulikane ni nani), basi utamfahamu huyo adui.

Anayeihujumu nchi yetu ndiye adui yule ambaye Roma Mkatoliki amemwimba -- ^Mimi ni Nani?^
 
Genge la wafanyabishara walioishika ikulu, wakiongozwa na wakala wao Nape Nauye.
 
Nani anayeihujumu TTCL kwa kiwango hiki?

Kuna mmbo fulani yanaendelea kwenye TTCL kiasi kwamba tunaona kama ni hujuma kwa TTCL:

Kwanza, Kipindi kirefu sasa ukitafuta laini za TTCL kwa mawakala wanakuambia hamna. Ni kweli shirika likose laini ambazo kimsingi ndio mteja na ndio zitachochea usambaaji wa huduma kwa watu wengi?

Pili, laini ya TTCL kupatikana kwake ni mpaka uinunue kwa gharama ya shilingi 5000 mpaka 7000 na hii ni gharama ya maeneo mengi ya Dar es salaam sijajua upatikanaji na gharama zake mikoani na huku laini za mitandao mengine ni bure kabisa na hadi kifurushi Cha kuanzia unawekewa tena bure. Kwa nini zipatikane kwa gharama hivi?

Tunasikia kila siku TTCL kupata hasara lakini kama mambo yenyewe ndio yako hivi basi hasara ni lazima.

Mitandao mingine ikitumia kila mbinu za kibiashara kuhakikisha zinakuwa na wateja wengi kwa kusambaza laini kwa wingi TTCL wako nyuma kwenye ushindani. Kiuhalisia kabisa, watu wengi sio rahisi kununua laini kwa gharama hiyo. Kama ni kuuza, ingeuzwa hata shilingi 1000.

Mhe. Samia na Waziri Nape tazameni hujuma hizi zinzofanywa dhidi ya TTCL na ikiwezekana libinafishwe tu ili liendeshwe kibiashara zaidi.
Si tumekubaliana kila kitu ni secta binafsi jamani
 
Nani anayeihujumu TTCL kwa kiwango hiki?

Kuna mmbo fulani yanaendelea kwenye TTCL kiasi kwamba tunaona kama ni hujuma kwa TTCL:

Kwanza, Kipindi kirefu sasa ukitafuta laini za TTCL kwa mawakala wanakuambia hamna. Ni kweli shirika likose laini ambazo kimsingi ndio mteja na ndio zitachochea usambaaji wa huduma kwa watu wengi?

Pili, laini ya TTCL kupatikana kwake ni mpaka uinunue kwa gharama ya shilingi 5000 mpaka 7000 na hii ni gharama ya maeneo mengi ya Dar es salaam sijajua upatikanaji na gharama zake mikoani na huku laini za mitandao mengine ni bure kabisa na hadi kifurushi Cha kuanzia unawekewa tena bure. Kwa nini zipatikane kwa gharama hivi?

Tunasikia kila siku TTCL kupata hasara lakini kama mambo yenyewe ndio yako hivi basi hasara ni lazima.

Mitandao mingine ikitumia kila mbinu za kibiashara kuhakikisha zinakuwa na wateja wengi kwa kusambaza laini kwa wingi TTCL wako nyuma kwenye ushindani. Kiuhalisia kabisa, watu wengi sio rahisi kununua laini kwa gharama hiyo. Kama ni kuuza, ingeuzwa hata shilingi 1000.

Mhe. Samia na Waziri Nape tazameni hujuma hizi zinzofanywa dhidi ya TTCL na ikiwezekana libinafishwe tu ili liendeshwe kibiashara zaidi.
Waziri wa habari anataka kuuza. Sasa dodoso litawekwaje
 
Raisi si alishasema kuwa wasimame kutoa huduma hiyo wabakie kwenye mkongo wa Taifa?

Ila previous laini zilikuwa zinapatikana kwa gharama nafuu japokuwa upatikanaji wake ulikuwa adimu.

Ni kama Zantel tu nayo laini zake nimezisahau hadi rangi yake
 
Mkuu sijawahi sajili line yoyote Ile bure pasipokulipia we umepigwa tunatozwa hela lkn sio ya kiwango hicho!
Basi usiwe mbishi bila sababu ,kama umesajli miaka mingi iliyopita sawa ila kama ni karibuni sema kweli ulitoa shilingi ngapi kwa TTCL
 
Nani anayeihujumu TTCL kwa kiwango hiki?

Kuna mmbo fulani yanaendelea kwenye TTCL kiasi kwamba tunaona kama ni hujuma kwa TTCL:

Kwanza, Kipindi kirefu sasa ukitafuta laini za TTCL kwa mawakala wanakuambia hamna. Ni kweli shirika likose laini ambazo kimsingi ndio mteja na ndio zitachochea usambaaji wa huduma kwa watu wengi?

Pili, laini ya TTCL kupatikana kwake ni mpaka uinunue kwa gharama ya shilingi 5000 mpaka 7000 na hii ni gharama ya maeneo mengi ya Dar es salaam sijajua upatikanaji na gharama zake mikoani na huku laini za mitandao mengine ni bure kabisa na hadi kifurushi Cha kuanzia unawekewa tena bure. Kwa nini zipatikane kwa gharama hivi?

Tunasikia kila siku TTCL kupata hasara lakini kama mambo yenyewe ndio yako hivi basi hasara ni lazima.

Mitandao mingine ikitumia kila mbinu za kibiashara kuhakikisha zinakuwa na wateja wengi kwa kusambaza laini kwa wingi TTCL wako nyuma kwenye ushindani. Kiuhalisia kabisa, watu wengi sio rahisi kununua laini kwa gharama hiyo. Kama ni kuuza, ingeuzwa hata shilingi 1000.

Mhe. Samia na Waziri Nape tazameni hujuma hizi zinzofanywa dhidi ya TTCL na ikiwezekana libinafishwe tu ili liendeshwe kibiashara zaidi.
Hii TTCL bora wapewe waarabu tu!!
 
Back
Top Bottom