Naogopa kujichana kwa kiwembe mie mwenyewe

Naogopa kujichana kwa kiwembe mie mwenyewe

NAKWEDE

JF-Expert Member
Joined
Aug 1, 2007
Posts
27,970
Reaction score
35,168
Kuna vidude fulani hivi vinaota pembeni kwenye kucha za mkononi ukifua nguo mie kalikuwepo, ila kalitoka kenyewe tatizo nimevimba sana kidole, ni kidole kidogo cha mkono wa kushoto nimenunua kiwembe ili nijichane usaha utoke, uwiiiiii, naogopa hadi moyo unadema dema nitumie dawa gani ya kukausha huo usaha/uvimbe usiku sikulala usingizi mwororo kwa maumivu yalivyokuwa makali.

😕😕😕😕
APU DEITISI

23/10/2018 nimeenda hospitali ya mkoa wa Mwanza Sekoutoure, wamenifanyia upasuaji mdogo. Ila nimepata kichambo cha kuchelewa kwenda hapo hadi kidole kimekuwa cheusi na usaha unatoa harufu mbayaaa.
Ahsanteni wote mlionitakiwa afya njema, na pia ushauri wenu.
 
Kuna vidude fulani hivi vinaota pembeni kwenye kucha za mkononi ukifua nguo.
Mie kalikuwepo, ila kalitoka kenyewe.
Tatizo nimevimba sana kidole, ni kidole kidogo cha mkono wa kushoto.
Nimenunua kiwembe ili nijichane usaha utoke, uwiiiiii, naogopa hadi moyo unadema dema.

Nitumie dawa gani ya kukausha huo usaha/uvimbe. Usiku sikulala usingizi mwororo kwa maumivu yalivyokuwa makali.

😕😕😕😕
Dawa kulitumbua hakuna namna
 
Njoo pm nikufundishe dawa usijichanje na kiwembe.
Ngoja nije mkuu maana maumivu ni makali sana. Hata hapa kwenye bao bonye nataipu kwa shida sana nisijitoneshe
 
Nunua washing machine shost acha ubahili
mmmh! Nasikia eti zinapausha nguo, hata hivyo kusema ukweli wa kutoka kwenye uvungu wangu, sina mpango wa mkakati wa kununua hiyo kitu.
Nisaidie kwenye huu uvimbe ambao una usaha nitumie dawa gani mai rolimodo?
 
Kama kingekuwa hakijafikia hatua ya kutunga usaha ningekushauri utumie Ampicillin(ni kwa kumeza na maji sio kupaka),huwa inakauka na hakiendelei tena,ila kama kimeshaonesha weupe wa usaha kabisa hauna jinsi ni lazima upasue tu..
 
Kama kingekuwa hakijafikia hatua ya kutunga usaha ningekushauri utumie Ampicillin,huwa inakauka na hakiendelei tena,ila kama kimeshaonesha weupe wa usaha kabisa hauna jinsi ni lazima upasue tu..
Kimevimba na usaha unaonekana, unachoma choma, hata nikikiweka kwenye shavu langu (shavu la usoni), kina moto sana
 
Back
Top Bottom