Naogopa kuwa mama

Naogopa kuwa mama

Dah,
Huyo mama ndo mfano wa mke mwema kwa mujibu wa 'Mithali 31', na ni mama bora kwenu.
Ila sasa inafaa apunguze kudekeza mabinti zake ili mpate kujua vizuri kazi za ndani - kupika, kufua, nk
Hatudeki na sio kama hatujui, ni vile hapendi kusaidiwa nawaza ikibidi nifate nyayo zake itakuaje
 
Mimi naona kabisa sitaweza aisee, naogopa😩😩
Mama yenu ni mchapakazi, lakini anakosea sehemu moja, kuwafanyia kazi na nyie. Hawa fundishi kuwajibika. Mtazoea kufanyiwa kazi, mtapata tabu kwenye nyumba zenu. Mama bora ni yule anayewafundisha watoto wake kufwajibika sio kuwafanyia. Mtoto lazima ujue kufua nguo zako, kufanya usafi na kupika
 
Natumai wazima wote,.

Iko hivi, kila siku zinavyoenda ndivyo ambavyo naogopa kuja kuitwa mama hapo baadae (Mungu anisaidie niondokane na hii hofu😓🥹🙏), hiii inatokana na lifestyle ambayo namwona mama yangu anaishi.

Huyu mwanamke sielewi huwa anapumzika mda gani, yeye ndie mtu wa mwisho kulala kila siku. Yaani hawezi kulala kama kuna mtu bado hajaingia nyumbani, na anahakikisha kila mtu amekula amelala anafunga milango ndipo na yeye alale. Na hata akiingia kulala halitapita nusu saa anapita tena vyumba vyote kuhakikisha mmefunga madirisha, mmeshusha neti na mmejifunika vizuri (anaweza akaamka hata mara 4 kwa usiku mmoja).

Haitaishia hapo, bado kuna sisi ambao inabidi asubuhi tuende kazini na wengine shuleni, wanaoamka usiku kusoma na wanaoamka kusali, kila mtu anamtajia mda wake wa kumwamsha hajawahi kukataa wala kupitiliza kutuamsha, always anakua on time.

Sijawahi kushuhudia ni saa ngapi ameamka ila kila tukiamka asubuhi tayari tunamkuta akiwa macho, kashafanya usafi na kashapika chai tunakunywa tunamwacha Nyumbani. Hatujawahi kuona au kushuhudia akilala mchana, Labda itokee anaumwa (napo ni mara chache sana ). Sijui hua anapumzika mda gani

Hajawahi kuishi na msaidizi wa kazi maisha yake yote, lakini hakuna aliyewahi kufua, kudeki, kupika, kuosha vyombo wala kufagia. Sio kwamba hatutaki kumsaidia Hapana, ni kwamba hatujawahi kuona uwanja ukiwa mchafu, vyombo vichafu na mda wowote ukirudi nyumbani unakuta chakula tayari na usafi wote ushafanywa na nguo zote ziko kambani zinakauka.

Licha ya hayo yote vilevile bado hajawahi kuacha kwenda kazini na shughuli zake nyingine zote za ujasiriamali hajawahi kuacha kufanya, hajawahi kuacha kwenda kwenye jumuiya wala kanisani hata jumapili moja, na kwenye dharura zote iwe hospitali au kikao chochote atakachohitajika mzazi awepo basi ni yeye ndio atakuwepo tena kwa wakati. Na sijawahi kumwona akilalamika, akinung’unika wala akimlaumu mtu kwamba hakuna anayemsaidia kazi hata siku moja.

Haya maisha yake yananiogopesha na yananifanya niogope hata kuwaza jinsi nitakavyoishi na watoto wangu huko mbeleni. Sometimes i wish ningekua wakiume labda ningeishi tu kama baba yangu anavyoishi😓😓😓 (Em assume mtu anafanya haya maisha yake yote)
Tupate wapi tena mtu kama huyu, ambaye Mungu anakaa ndani yake ?
 
Natumai wazima wote,.

Iko hivi, kila siku zinavyoenda ndivyo ambavyo naogopa kuja kuitwa mama hapo baadae (Mungu anisaidie niondokane na hii hofu😓🥹🙏), hiii inatokana na lifestyle ambayo namwona mama yangu anaishi.

Huyu mwanamke sielewi huwa anapumzika mda gani, yeye ndie mtu wa mwisho kulala kila siku. Yaani hawezi kulala kama kuna mtu bado hajaingia nyumbani, na anahakikisha kila mtu amekula amelala anafunga milango ndipo na yeye alale. Na hata akiingia kulala halitapita nusu saa anapita tena vyumba vyote kuhakikisha mmefunga madirisha, mmeshusha neti na mmejifunika vizuri (anaweza akaamka hata mara 4 kwa usiku mmoja).

Haitaishia hapo, bado kuna sisi ambao inabidi asubuhi tuende kazini na wengine shuleni, wanaoamka usiku kusoma na wanaoamka kusali, kila mtu anamtajia mda wake wa kumwamsha hajawahi kukataa wala kupitiliza kutuamsha, always anakua on time.

Sijawahi kushuhudia ni saa ngapi ameamka ila kila tukiamka asubuhi tayari tunamkuta akiwa macho, kashafanya usafi na kashapika chai tunakunywa tunamwacha Nyumbani. Hatujawahi kuona au kushuhudia akilala mchana, Labda itokee anaumwa (napo ni mara chache sana ). Sijui hua anapumzika mda gani

Hajawahi kuishi na msaidizi wa kazi maisha yake yote, lakini hakuna aliyewahi kufua, kudeki, kupika, kuosha vyombo wala kufagia. Sio kwamba hatutaki kumsaidia Hapana, ni kwamba hatujawahi kuona uwanja ukiwa mchafu, vyombo vichafu na mda wowote ukirudi nyumbani unakuta chakula tayari na usafi wote ushafanywa na nguo zote ziko kambani zinakauka.

Licha ya hayo yote vilevile bado hajawahi kuacha kwenda kazini na shughuli zake nyingine zote za ujasiriamali hajawahi kuacha kufanya, hajawahi kuacha kwenda kwenye jumuiya wala kanisani hata jumapili moja, na kwenye dharura zote iwe hospitali au kikao chochote atakachohitajika mzazi awepo basi ni yeye ndio atakuwepo tena kwa wakati. Na sijawahi kumwona akilalamika, akinung’unika wala akimlaumu mtu kwamba hakuna anayemsaidia kazi hata siku moja.

Haya maisha yake yananiogopesha na yananifanya niogope hata kuwaza jinsi nitakavyoishi na watoto wangu huko mbeleni. Sometimes i wish ningekua wakiume labda ningeishi tu kama baba yangu anavyoishi😓😓😓 (Em assume mtu anafanya haya maisha yake yote)
Hao anaoamka usiku mara 4 kuwaangalia wana umri gani?
 
Japo dhamira ilikuwa ni kuonyesha uoga wako na pengine kumpa sifa Bi. Mkubwa wako lakini kiuhalisia ulichoambulia hapa ni kuonyesha jinsi gani mama yako ana watoto wa ovyo kabisa ikiwemo wewe mwenyewe.

Usisubiri mpaka akuombeni msaada ndio mumsaidie. Eti mnaamka na kukuta kila kitu kilishafanywa tayari, hapa ni dhahiri mnaamka mida mibovu kwa kujua mama yupo.

Jaribuni kuamka kabla yake na mumsaidie kazi zake halafu muone kama akiamka na yeye atakasirika kusaidiwa.

Vitu vingine mjiongeze na nyie. Ni fedheha kwa mtoto wa kike kufuliwa na mama yake ama na mtu yeyote yule.

Nyie ndio mtakuja kuwapa ma housegal boxer za waume zenu wazifue.
 
Huyo mama yako atachoka sana akifikia uzeeni
Hao ndio wale wamama ambao kamwe hutasikia ana maumivu ya mgongo au miguu sijui inamuuma atazeeka na nguvU zake. Watoto wake watajua umuhimu wake siku wakibaki wenyewe. Na kila mmoja wao atasema hakika YULE ALIKUWA MTU NA NUSU
 
Madhali unauchezea ule ukuni na ukiwa na kizazi utakuwa tu mama.
Ila naamini hautakuwa bora walau nusu ya mama yako.

Umepata mama bora sana, muombee sana, ni moja kati ya wamama ambao mtoto unakuwa proud kote kote, ukiacha ile sifa ya uzazi ni ana sifa kede.
Wakati nakuwa mama yangu akiwa ana nguvu zake alikuwa kama mama yako, huwa nikimtiza na kukumbuka naishia kutabasamu na kumuombea dua.

Wamama bora kwa watoto wao mungu awaingize tu peponi moja kwa moja kwa kweli,


ISHIKE HII,
"UNAWEZA KUWA MAMA ILA NAAMINI HAUTOKUWA BORA KAMA MAMA YAKO"
 
Binadamu ameumbwa kufanya adaptation to current environment.
The day umebeba mwanao kuba hali flani itakuvaa ambayo itakufanya uweze kufanya kila kitu kwa ajili ya mtoto wako hata wawe kumi bila kuchoka.
Subiri nkupe ushuhuda, kipindi tuna date na wife, alikua mtu wa kulala vbaya mno. Yaan kwa mfano akiingia ndani ijumaa anaweza kutoka j3. Muda woote akimaliza tu kazi zake ni kitanda. Wakati mimi ndo kwanza siku inaanza. Tunaeza kula lets say saa moja usiku, yeye akimaliza tu anaenda kuzima. Mimi nasepa zangu narudi hata saa tano huko ndo nalala.
Lakn tulivopata tu mtoto, alibadilika ghafla. Yaani anaweza kuamka hata mara 9 kwa usiku mmoja. Atanyonyesha, mara kubadilisha diaper, mara kucheza na mtoto n.k.
Na asubuhi mapeema yuko live , mara apike chakula, sijui afue manguo, anijali na mimi na mavitu yote. No complains or anythng. Mtofo muda wote msafi, ana afya kubwa, nyumba iko standard n.k, vitu vyangu ameorganize, chakula on time na mashughuli yote.
So, hata kwako itakua hvyo. The joy of life inatokana na kuona uzao wako.
Kamwe usiogope, tena kama unaweza pata watoto mapema ili ufurahie kuona wakiwa wanakua.
Usitamani kua mwanaume, kuna vitu ambavyo tunapitia, ungeambiwa ungekimbia spidi ya fumanizi.
Kila la kheri
Umesema vyema. Hata mimi wakati nakua nyumbani kulikua na wasaidizi wa kazi, kazi zote nafanyiwa mimi ni kuoga na kufua pichu tu. Majirani walikua wanasema nalelewa vibaya sana nitasumbua baadae. Nikaja kupata mtoto wa kwanza nikajikuta shughuli zote nafanya. Mpaka leo sijazoea kukaa na msichana wa kazi kwanza sipendi, kazi zangu nafanya mwenyewe. Kazi za nje tu ndio nina mtu
 
Watoto wa shangazi yangu waliishi maisha kama hayo uliyoelezea hapa. Siku haina jina wala taarifa mama yao (shangazi) aliugua ghafla akakimbizwa hospital kufika madaktari wakasema hamjaleta mgonjwa bali mmeleta mwili wa marehemu.

Hakuna rangi waliacha kuona wale binamu zangu kwa namna marehemu mama yao alivyokuwa kawadekeza aseeeeee, wanaishi maisha magumu mno!! Hao wakike wamezalishwa bila utaratibu, ni wavivu hakuna mtu anawakubali kuishi nao. Mmoja kaolewa ndoa tatu na zote zimemshinda sababu ya uvivu anaishia kuachika.

Maisha ni maamuzi yako ingawa malezi na makuzi ni muhimu sana hasa unapoanza maisha ya kujitegemea.
 
Hongera Kwa mama yako maana Mimi siwezi kuwa kama yeye hata robo,yaani mwanangu mkubwa wa kujitegemea alale aamke nimeshampikia chai,nguo zake nimemfulia,anachelewa kurudi pengine Hana sababu ya msingi Mimi nimsubirie nihakikisha amekula,bado usiku nikachungulie kama kashusha neti!! Yaani anawajibika Kwa mtoto wa 18+kama anahudumia wasiojiweza? Hivi haya ya kweli au unatania?
 
Huwezi kuwa kama mama yako ila anayoyafanya yawe funzo kwako.

Huenda mama yako hataki wasaidizi wa kazi kwa maana ya kutaka kuwafundisha mwenyewe nafasi ya mwanamke kwenye familia kwa vitendo.

Nimependa ulivyosema huwezi kuishi mwenyewe(unaogopa), changa karata zako vizuri hata ikitokea ukapata mwenza basi awe mwenye kuendana na wewe maana inaoekana unadeka sana pia.

Muhimu: Tengeneza mazingira ya kumsaidia majukumu wewe pamoja na hao ndugu zako ili nae apate kupumzika.
 
Hujawahi kufua wala kupika wala kufagia uwanja wala kuosha vyombo wala kudeki.

Mmemgeuza mama yenu punda? Kumsaidia kazi mnasubiri hadi awaambie?

Mitoto ya hovyo na mivivu! 😎

-Kaveli-
 
Back
Top Bottom