Naomba kufahamu faida za kujenga nyumba kando mwa barabara?

Naomba kufahamu faida za kujenga nyumba kando mwa barabara?

Wakati wa upanuzi wa barabara nyumba yako itawekewa alama ya X nyekundu.
 
Kama huna jibu la hayo unayouliza, nakushauri ule ushibe kwanza.

Kama una kompyuta tafuta, zaidi ya hapo hii ni mada hadaa, inanuka uhasama hasi kwa Jamii ya Watanzania.


Aluta Continua.
Bora umemwambia aka "google" kuliko kutuuliza sisi maswali haya ya kipuuzi
 
Ni kero sana kukaa karibu na ingawa Inategemea ni bara bara gani?hapa kuna nyumba nimepanga chumba ipo road yani nikifungua pazia nipo pembeni ya barabara yani kupata usingizi ni kazi sana usumbufu kelele za magari muda wote naskilizia kodi iishe nisepe.
 
Ninadhani ni rahisi kufika nyumbani kwako.Mfano umeshuka kwenye usafiri pikipiki, bajaji au daladala chapu umeshaingia ndani.
 
Faida yake hata ikitokea dharura ni gari linafika kirahisi... Sema isiwe imeingia tu kwenye eneo la barabara
 
Back
Top Bottom