Naomba kujua faida wanayopata NBC

Naomba kujua faida wanayopata NBC

Mimi ni mshabiki wa mpira ila mpka sasa sijui huyu mdhamini mkuu anapataje faida kwa kudhamini ligi kuu.Ukiniambia anajitangaza na anapata wateja sijui kama ni kweli maana mimi tangu aidhamini sijawahi kuvutiwa kwenye kufungua acc kwao.
Kwa Azam najua anapata faida kwa sababu anatangaza vitu ambavyo ni consumable na watu wote.Hata GSM sijui anapataje faida kwa kuwa mdhamini mwenza maana sijui kitu kingne anachouza zaidi ya Magodoro (Sijui nitanunua godoro lini).

Au kuna watu mlikuwa hamna acc NBC na sasa mmefungua baada ya NBC kuidhamini league?Kuna watu mlikuwa mnanunua magorodo kwingne na baada ya udhamini sasa mnanunua ya GSM?

Kwa Mo najua pale anapiga pesa ndefu maana watu kibao ndani ya Nchi hii wanambea,wanaingia ofsini,wanapiga vibarua,wanavuja jasho kuchimba mitaro huku WAMEBEBA SABUNI MGONGONI.

Narudia tena,Sina mpango wa kununua godoro hivi karibuni labda baada ya miaka 5 ijayo na sina mpango wa kuhamisha maburungutu yangu kupelekea NBC kisa mpira.
Faida ya kwanza ni huu uzi wako, sio lazima ufungue account wao kupata faida kukuza tu brand name na muda wote kutajwa tajwa kwenye midomo ya watu kunaongeza nguvu ya brand.

Kesho NBC wakizindua bidhaa mpya kila mtu ataijua sababu ya brand ina nguvu, ila anzisha chako hata kama quality inaweza kuwa kubwa zaidi hakuna atakayejali.
 
NBC ashindwe mwenyewe tu kupiga pesa ndio muda sahihi wa Marketing na Products development team kuleta products mpya sokoni iwe insurance au chochote kile tayari washapata mileage ya kutosha.
 
Mtoa mada umeuliza vizuri kwenye heading yako, lakini umejipa majibu yanayoonesha hujui dhana ya udhamini na umebewa na uswahili. Pole

Kwa ufupi tu, udhamini Jambo la kwanza hulenga kujitangaza.
Pia mdhamini huweka masharti ya wadhaminiwa kutumia bidhaa/huduma yake. Kwa sababu hii basi, NBC anasimama kama [color-blue] FINANCIAL SPONSOR [/color] wa ligi kuu, hivyo kuanzia TFF hadi vilabu vitatakiwa kutumia NBC kwa mambo yake ya kifedha.

Pia kama vilabu au tff watataka mikopo ya aina yoyote kutoka kwa mdhamini, basi watalazimika kutumia bank hiyo, hapo mdhamini atazidi kutunisha mfuko wake

Kumbuka, mdhamini mkuu ndio financial sponsor na ndio mmiliki (si kauli halisi) wa ligi, hivyo wadhamini wenza wote hulazimika kufuata masharti ya mdhamini mkuu. Sasa hapo hatujui ni masharti gani, lakini kibiashara, utakuwa unajua tu ni vipi mdhamini mwenza anakuja kumnufaisha mdhamini mkuu

Kwa ufupi ni hayo, japo sio ya kiuchumi zaidi
 
Mtoa mada umeuliza vizuri kwenye heading yako, lakini umejipa majibu yanayoonesha hujui dhana ya udhamini na umebewa na uswahili. Pole

Kwa ufupi tu, udhamini Jambo la kwanza hulenga kujitangaza.
Pia mdhamini huweka masharti ya wadhaminiwa kutumia bidhaa/huduma yake. Kwa sababu hii basi, NBC anasimama kama [color-blue] FINANCIAL SPONSOR [/color] wa ligi kuu, hivyo kuanzia TFF hadi vilabu vitatakiwa kutumia NBC kwa mambo yake ya kifedha.

Pia kama vilabu au tff watataka mikopo ya aina yoyote kutoka kwa mdhamini, basi watalazimika kutumia bank hiyo, hapo mdhamini atazidi kutunisha mfuko wake

Kumbuka, mdhamini mkuu ndio financial sponsor na ndio mmiliki (si kauli halisi) wa ligi, hivyo wadhamini wenza wote hulazimika kufuata masharti ya mdhamini mkuu. Sasa hapo hatujui ni masharti gani, lakini kibiashara, utakuwa unajua tu ni vipi mdhamini mwenza anakuja kumnufaisha mdhamini mkuu

Kwa ufupi ni hayo, japo sio ya kiuchumi zaidi
Ooh atleast nimekupata
 
Ooh atleast nimekupata
Kwa kuongezea:
Kuna uzi mwembamba sana uliotenganisha Marketing na Siasa.Hivi vitu ukivifuatilia vinaendana 100%.

Kwa huku nje unaweza usione chochote ila kiuhalisia faida wanaipata NBC kwa sasa ni kubwa kuliko ilivyokuwa mwanzo na hii inachagizwa na aina ya biashara yao,biashara ya fedha ambayo kama walivyoeleza wadau kwamba michakato yote ya kifedha inayohusu ligi hiyo fedha lazima ipitie huko.

Faida anayoipata NBC sasahv ni tofauti na faida aliyokuwa anaipata Vodacom kulingana na aina za biashara zao.

Marketing ni Siasa pure na ni michezo miwili inayotumia akili kubwa mnoo....ni kama vile unavyoweza kuskia kwamba Serikali ya Uganda itoa msaada wa ujenzi wa shule Chato...kwa jicho la kawaida wewe unaweza ukashangaa na usielewe hii,ila huyo aliyetoa hiyo hela shule ijengwe anajua nini anafanya na nini anapata kama return...Biashara nayo ni hivyo hivyo,hakuna anaemwaga hela kizembe,yan ukiona mtu/kampuni inamwaga fedha mahali ujue watu washapiga macalculation na hiyo hela haimwagiki bure.
 
Kwa kuongezea:
Kuna uzi mwembamba sana uliotenganisha Marketing na Siasa.Hivi vitu ukivifuatilia vinaendana 100%.

Kwa huku nje unaweza usione chochote ila kiuhalisia faida wanaipata NBC kwa sasa ni kubwa kuliko ilivyokuwa mwanzo na hii inachagizwa na aina ya biashara yao,biashara ya fedha ambayo kama walivyoeleza wadau kwamba michakato yote ya kifedha inayohusu ligi hiyo fedha lazima ipitie huko.

Faida anayoipata NBC sasahv ni tofauti na faida aliyokuwa anaipata Vodacom kulingana na aina za biashara zao.

Marketing ni Siasa pure na ni michezo miwili inayotumia akili kubwa mnoo....ni kama vile unavyoweza kuskia kwamba Serikali ya Uganda itoa msaada wa ujenzi wa shule Chato...kwa jicho la kawaida wewe unaweza ukashangaa na usielewe hii,ila huyo aliyetoa hiyo hela shule ijengwe anajua nini anafanya na nini anapata kama return...Biashara nayo ni hivyo hivyo,hakuna anaemwaga hela kizembe,yan ukiona mtu/kampuni inamwaga fedha mahali ujue watu washapiga macalculation na hiyo hela haimwagiki bure.
Shukran boss
 
Wachezaji wote viongozi wote wa vilabu,viongozi wa tff na wafanyakazi wote na wadau wote na viongozi wa azam na tbc wanatakiwa walalie magodoro chapa GSM
🤣🤣🤣🤣kumbe.Ndo maana upande wa pili wamemaindi
 
Shukran boss
Mkuu umewahi kusikia neno "BIASHARA NI MATANGAZO" ?

Kama umewahi kusikia, basi fahamu kwamba faida kubwa kuliko zote anazopata NBC ni kujitangaza au kutangazwa.

Sasa, hadi hapo nadhani swali lako litakua "kuitangaza biashara kuna faida gani"

Kama huna majibu ya swali hilo, fanya zoezi moja dogo sana. Anzisha biashara yoyote halafu usimwambie mtu yoyote kuhusu hiyo biashara (iwe ni siri yako). Fanya hivyo kwa miaka kama mitatu hivi.

Hapo utajua nguvu ya kujitangaza na maana halisi ya neno "biashara ni matangazo".
 
Haimaanishi kama voda hapati faida basi na nbc hapati, kumbuka voda kampuni ya simu za mikononi inayoongoza tz kwanini huzani ligi ndio imewafanya waongoze? Vilevile nbc tulishawasahau lakini baada ya kudhamini ligi kuu saivi wanatajwa midomoni, binafsi ninampango wa kuwatembelea nijue product zao
umejuaje au umetumia statistics zipi ambazo ni current zinazoonyesha Vodacom Ni mtandao unaoongoza. Na unaongoza katka Nini.
 
Mkuu umewahi kusikia neno "BIASHARA NI MATANGAZO" ?

Kama umewahi kusikia, basi fahamu kwamba faida kubwa kuliko zote anazopata NBC ni kujitangaza au kutangazwa.

Sasa, hadi hapo nadhani swali lako litakua "kuitangaza biashara kuna faida gani"

Kama huna majibu ya swali hilo, fanya zoezi moja dogo sana. Anzisha biashara yoyote halafu usimwambie mtu yoyote kuhusu hiyo biashara (iwe ni siri yako). Fanya hivyo kwa miaka kama mitatu hivi.

Hapo utajua nguvu ya kujitangaza na maana halisi ya neno "biashara ni matangazo".
Sawa boss ila NBC hata wajitangaze vp mi sina mpango nao.Waambie kabsa
 
umejuaje au umetumia statistics zipi ambazo ni current zinazoonyesha Vodacom Ni mtandao unaoongoza. Na unaongoza katka Nini.
Usipoelewa na hapo sio jukumu langu
IMG-20211004-WA0005.jpg
 
Ndiyo mkuu.


Kwa mfano mimi mwaka 2012 nikiwa kwenye basi nilisikia mtu anaongelea habari ya Dkt Slaa ambayo aliisoma JamiiForums.

Kwa wakati huo sikuwa naifahamu JF.

Lakini baada ya kusikia nikaamua kuitafuta.Mpaka leo JF imekuwa chanzo changu kikuu cha habari....

Lakini kama yule asingeitaja ningechelewa mno kuijua JF au nisingekuwa na mzuka nayo kama ilivyo sasa!
Huyo jamaa angekuwa na knowledge kidogo tu ya marketing angeelewa lakini hapo mtakesha
 
Huyo jamaa angekuwa na knowledge kidogo tu ya marketing angeelewa lakini hapo mtakesha
Ukiielewa marketing raha sana aisee,Hakuna marketing yenye akili kubwa iliyowahi kufanyika Tz kama hii iliyofanyika juzi na GSM.
Jamaa walijua kabisa kwamba huu mkataba tunaokwenda kuingia na Tff hautaweza kukubalika kwa wadau,walijua kabisa lazima ilete mgogoro.Walijua kbs kupitia huo mgogoro bland yao ya GSM itaenda kutajwa sana kwenye vinywa vya watanzania....na ni kweli,mission ikatiki,yan hakuna kipindi gsm imetajwa sana kma wiki ile ya ule mgogoro...hii ndiyo marketing.
 
Haimaanishi kama voda hapati faida basi na nbc hapati, kumbuka voda kampuni ya simu za mikononi inayoongoza tz kwanini huzani ligi ndio imewafanya waongoze? Vilevile nbc tulishawasahau lakini baada ya kudhamini ligi kuu saivi wanatajwa midomoni, binafsi ninampango wa kuwatembelea nijue product zao
Kwa fikra zile hata maana ya product sidhani Kama anajua

Sent from my TECNO CA7 using JamiiForums mobile app
 
Back
Top Bottom