Naomba kujua historia ya Urusi

Naomba kujua historia ya Urusi

Siku ambayo huyu rais wa urusi wa sasa Vladimir Vladimorovich Putin akifa wamarekani na washirika wao watafanya sphere he. Ni umiza kichwa kwao sana, namkubali sana huyu jamaa
Hahahahaaa ndo maana umeweka avart yake Mkuu. Jamaa anatumia akili nyingi sana
 
Ndio maana wapinzani wa chama cha vladimiry Putin hawatakaa wapate madaraka kwa kua mmarekani anawaunga mkono lakini asilimia kubwa ya warusi wanamkubali putini
Ndio maana sikushangaa aliacha urais akawa waziri mkuu na baadae akarejea tena kwenye kinyanganyiro cha urais
Hii ilimpa nafasi ya kuona nchi za mangaribi zinaiwazia nini urusi
Ndio maana amerudi na akili nyingi sana mmarekani anajuta tu pamoja na vikwazo vyote naona vimegonga mwamba
Kuna jarida moja lilitoa neno kwamba Putin anaushawishi mkubwa sana duniani katika nyanja ya siasa
 
COLD WAR: PHASE 3- GREAT DEPRESSION AND THE RISE OF FASCISM IN EUROPE

Baada ya vita ya kwanza ya dunia Marekani ilipata faida kubwa sana kiuchumi; kwa bahati mbaya hawakuweza kutawala uchumi wao hivyo kukawa na viwanda vingi na bidhaa zikawa nyingi sana kwenye mzunguko. Kukawa na overproduction kubwa kuliko consumption. Hii ilianza miaka ya 1929 chini ya utawala wa raisi Hebert Hoover. Ilianza na Collapse ya New York Stock exchange.
Hii ilipelekea watu wengi kupoteza pesa nyingi sana hivyo kufunga biashara zao. Mabenki mengi yalifungwa, viwanda vilifungwa na mamilioni ya watu walipoteza ajira. Nchi ya Marekani iliganda kwa miaka hiyo.
Ikumbukwe kutokana na biashara za kimataifa (International Trade) kati ya Marekani na Ulaya uchumi wa Ulaya nao uliathirika vibaya sana kwasababu makampuni ya Marekani makubwa ya marekani yaliyo ulaya yalifungwa. Tena kwa soko la Ulaya Marekani lilianguka kwa kiasi kikubwa.

Ikumbukwe kwamba kipindi hichi mambo yalikaa vibaya sana kwasababu nchi zilizokuwa huru zilikuwa ni chache. Mataifa mengi ya ulaya yalikuwa na makoloni Africa na Asia hivyo dunia nzima ikaumia.
Pia kwa maana nyingine nchi nyingi zingekuwa huru basi atleast kungekuwa na uwezekano wa kupunguza makali ya GREAT ECONOMIC DEPRESSION.

Sasa Ikumbukwe Kwenye Mkutano wa Versailles 1919 Ujerumani ilipewa adhabu kwa kuanzisha vita ya dunia; kitu ambacho ujerumani ilionewa sana.
Vita ya kwanza ya dunia ilitokana na Miscalculation ya mataifa ya Ulaya, Overconfidence due to the rise of new technologies, Europen Prestige and Glory, Nationalism na Zaidi ya hapo sababu kubwa ilikuwa ni Imperialism.

Ujerumani alipewa adhabu zifuatazo.

  1. Jeshi lake lipunguzwe hadi wanajeshi 100000 (Laki moja tu)
  2. Mjerumani hakutakiwa kuwa na ushirika wa kijeshi, kidiplomasia au kiuchumi na nchi yoyote. Ikumbukwe hii ilifanywa ili kuzuia Ujerumani asirudishe mahusiano na Nchi kama AUSTRIA, TURKEY, BULGARIA na HUNGARY ambao walikuwa upande wa Ujerumani wakati wa vita ya kwanza ya dunia.
  3. Ujerumani aliiambiwa alipe gharama zote za vita (indemnity fee). Ambapo Ujerumani alipewa faini hiyo na muingereza kiasi cha 132 Billions Gold marks. Sasa malipo yalifanyika kwa njia ya kulipa mifugo, technolojia, vichwa vya treni, magari na kadhalika.
  4. Ujerumani alinyang'anywa makoloni yake yote. Akapewa Muingereza na Mbelgiji. Mfano mzuri ni Germany East Africa au DEUTSCHE OSTAFRIKA. Ambapo kulikuwa na Tanganyika na Rwanda-Urundi. Haya ni mfano tu.
  5. Ujerumani ilibidi ipunguzwe. Wazungu wanaita Balkanization. Hivyo nchi kama Latvia, Lithuania, Estonia, Serbia na nyingine nyingi zilitokea hapo. Hizi zinaitwa the Slavik states. Mwanzoni zilikuwa ndani ya Ujerumani.
  6. Ujerumani aliambiwa arudishe migodi ya chuma na makaa ya mawe ya ALSACE NA LORRAINE kwa Mfaransa. Migodi hii alinyang'anywa mfaransa mwaka 1871 kwenye vita ya Franco-Prussian War.
  7. Mfalme wa Ujerumani Kaiser Wilhelm alitakiwa afungwe japokuwa alikimbia nchi. Utawala mpya ukaanzishwa unaitwa THE WEIMER REPUBLIC.
  8. Mjerumani aliambiwa arudishe jimbo linaitwa Shleschwhig kwa nchi ya Denmark ambayo alinyang'anya kwenye vita ya miaka ya 1880's.
  9. Ujerumani aliambiwa avunje mkataba wa Brest Litovsk ambao uliiitoa Urusi kwenye vita ya kwanza ya Dunia.
  10. Ujerumani alikataziwa kujiunga na League of Nations japo baadae alikubaliwa.
  11. Nchi nyingi duniani hazikutaka kufanya baishara na Ujerumani.

Hizi adhabu zilipelekea sana kutokea kwa Mtikisiko wa kiuchumi duniani. Kwasabau Ujerumani nalo lilikuwa taifa kubwa sana duniani.
Ujerumani ilifika pabaya kukawa na Ujambazi, Uporaji na wizi kwasababu watu walikuwa wamechoka sana kiuchumi. Haya mambo ndiyo yaliyopelekea watu kama kina Adolf Hitler kutokea.
Mbaya zaidi uhalifu ulikuwa unafanywa na Wanajeshi wastaafu.

Kwa Upande wa Italy; nyakati za mwisho za vita aligeuka na kumsaliti Mjerumani kwasababu Muingereza na Mfaransa walimhaidi makoloni. Ila baada ya hapo Waziri Wao VITARIO ORLANDO alisaini mkataba lakini mkataba haukutimizwa hivyo uchumi wa Italy nao ukawa mbaya sana. Hapa ndipo watu kama kina Benitho Mussolin Wakatokea.

Haya ikumbukwe Wayahudi wengi walikuwa wanakaa Ujerumani. Ndiyo waliokuwa na biashara kubwa, engineers, Wanajeshi, waalimu n.k. Wakati vita inaendelea mwaka 1917 Waziri mkuu wa Uingereza anitwa Mc Arthur Balfour alitoa tamko kwamba kama Wayahudi watawasaidia kwenye vita basi Watawatengenezea nchi yao Huko Mashariki ya kati Palestina ambapo lilikuwa kolonin la Muingereza.

Wayahudi wengi chini kwa chini waliisaliti ujerumani kwenye vita. Wakawa wanatoa taarifa za kiintelijensia za majeshi ya ujerumani kwa mataifa ya Uingereza hivyo kupelekea Ujerumani kushindwa. Ndiyo maana Hitler alishwahi kusema "Germany did not lose the war; Germany was Betrayed". Na hichi ndicho chanzo cha kuwachukia sana Wayahudi.

Ikumbukwe basi Mtikisiko wa kiuchumi wa dunia(GREAT ECONOMIC DEPRESSION) uliziathiri nchi zote duniani kasoro USSR au URUSI. Hii ilitokana na Urusi kujitenga na mtandao wa kiuchumi wa dunia.
Hivyo nchi za Ulaya zilivyokuwa zinahangaika watu wakona Ukomunisti ndiyo suluhisho la matatizo. Hivyo vyama vya kijamaa, kisoshalisti au Kikomunisti viliweza kujipenyeza Ujerumani, Italy, Ufaransa, Uchina, Hispania, Uingereza hadi Marekani.

Hichi ndicho kilichomfanya Hitler kuwachukia warusi hadi akaanzisha kitu kinaitwa Anti-Communism Band Wagon mnamo miaka ya 1930's ambapo hadi Uingereza, Ufaransa, Marekani walimsapoti Mjerumani.
Hii ilifanywa kwa siri kubwa sana chini ya mashirika ya kijasusi ya ujerumani chini ya NAZI.(The Gestapo, The ABHWER and THE S.S), uingereza (MI5 and MI6), U.S.A (O.S.S) na Italy(The Black shirts Gang).
Walianza mkakati wa kuwaua wakomunisti kwa haraka sana. Hii inatokana na msemo the enemy of my enemy is my friend. Hivyo kichinichini Ujerumani akawa pia anataka kulipiza kisasi kwa Matifa ya Magharibi.

End of Episode 3 stay tuned for Episode four.


cc: @born again pagan, @Erijo , @Gide MK , @Amanito , @Tibet , @Necha Lauwo , @pikachu , @semper saratoga , @MALCOM LUMUMBA , @MeinKempf , @mohamed sai , @mtembea kwa miguu , @Nando , @Abu mohamed , @Mchumba , @Globu , @Vlad , @Bayyo , @t blj , @Walas Ba , @majeshi 1981 , @kireri jr , @shaban hassani , @utafiti , @kilamuruzi , @Mohamed Said
@WhySoSerious
Daaaah Mkuu hii season nimeipenda sana hasa kwenye ukweri kwa nin wajeruman waliwaua kwa kuwachoma moto wayahudi. Maauaji ya holikost. Umenena vyema na umenifungua macho, nimpenzi sana wa DW lakin wakifikaga hapa huwa wanamung'unya maneno. Thanks
 
Wadau Naombeni mnijuze mambo yafuatayo kuhusu USSR na Urusi ya sasa

1. Je ni kwanini USSR ilijiingiza katika mgogoro wa Afghanstan (Soviet Involvement in Afghan War 1989-1991)?

2. Je USSR walizidiwa nguvu na mbinu dhidi ya mahasimu wao hususani nchi za magharibi zikiongozwa na U.S.A ndo maana wakashindwa vibaya vita hiyo?

3. Je ni kwa kiasi gani kushindwa katika vita hiyo ilichangia kusambaratika kwa USSR miaka ya 1990s?

4. Je kwanini China ilikuwa inapambana upande wa wapinzani ama ilikuwa inasaidia wapinzani wa ujamaa wa ujamaa, ikiwa ni mshirika mkubwa wa USSR?

5. Je kushindwa kwa USSR ilikuwa ni mchango mkubwa wa Osama Bin Laden aliyekuwa anatumiwa na U.S.A? Ingawa baada ya vita hiyo akawa mpinzani wa U.S.A, Kumbuka U.S.A huwa wanasema hawana rafiki wa kudumu.

6. Je ni kweli kuwa Baada ya kusambaratika kwa USSR, Urusi ndiyo jamhuri pekee iliyoridhi madeni, mali,teknolojia, uanachama wa kudumu wa baraza la ulinzi la umoja wa mataifa na mambo yote ya iliyokuwa USSR?


7. Mwisho, Je Urusi baada ya kusambaratika kwa USSR ilikuwa na hofu dhidi ya U.S.A na NATO yake pamoja na washirika wake.Hivyo kuifanya Urusi kuwa na hofu kujiingiza katika migogoro mikubwa ya kijeshi. Je kuingia kijeshi Syria mnamo septermber 30,2015 kunaashiria kuanza kwa mvutano mkuwa baina yake na U.S.A kama ule uliyokuwepo kipindi cha vita baridi? Je huu upinzani wa Urusi unaweza kuondoa Dollar economy ya Mmarekani? Je inaweza leta vita ya tatu (WW3 or WWIII) ama Nuclear War baina ya hawa wababe?

************** Nawasilisha
Mkuu haya maswali yako yote ni rahisi sana kwa @The Emperor.
We subiri kidogo tu,atakuja
 
Ndio maana wapinzani wa chama cha vladimiry Putin hawatakaa wapate madaraka kwa kua mmarekani anawaunga mkono lakini asilimia kubwa ya warusi wanamkubali putini
Ndio maana sikushangaa aliacha urais akawa waziri mkuu na baadae akarejea tena kwenye kinyanganyiro cha urais
Hii ilimpa nafasi ya kuona nchi za mangaribi zinaiwazia nini urusi
Ndio maana amerudi na akili nyingi sana mmarekani anajuta tu pamoja na vikwazo vyote naona vimegonga mwamba
Kuna jarida moja lilitoa neno kwamba Putin anaushawishi mkubwa sana duniani katika nyanja ya siasa
Pro-Americans wanasema Russia kuna rushwa,hakuna democracy, kuna ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Kwa upande wa kiuchumi Russia imeadhiriwa na vikwazo vya U.S.A na EU hadi imepelekea Inflation kubwa , kushuka dhamani ya sarafu yao (Rubles), kushuka kwa bei ya mafuta (OPEC members & nonmembers kama Russia), Kuzuia mali za vigogo na warusi wenye ushawishi mkubwa na Ufaransa kubatilisha makubaliano ya kuiuzia Russia Meli za kivita.

Hili unalizungumziaje Mkuu, au ni Western propaganda???
 
Pro-Americans wanasema Russia kuna rushwa,hakuna democracy, kuna ukiukwaji mkubwa wa haki za binadamu.

Kwa upande wa kiuchumi Russia imeadhiriwa na vikwazo vya U.S.A na EU hadi imepelekea Inflation kubwa , kushuka dhamani ya sarafu yao (Rubles), kushuka kwa bei ya mafuta (OPEC members), Kuzuia mali za vigogo na warusi wenye ushawishi mkubwa na Ufaransa kubatilisha makubaliano ya kuiuzia Russia Ndege za kivita.

Hili unalizungumziaje Mkuu, au ni Western propaganda???

Mkuu kwanza inabidi uelewe kuwa warusi ni multi-ethnic society lakini jamii(race) ya slavic ndio inayotawala na kushika nafasi muhimu zote katika uongozi wa nchi. Hii inatokana na jiografia ya nchi yenyewe upande moja upo ulaya na mwingine upo asia. Hii ni historia ndefu ambayo ipo hata kabla ya soviet union. Sasa wahasimu wao wakiongozwa na wamerekani walipofanikiwa kuisambaratisha hiyo soviet union, walibariki pia ubadhirifu, unyonyaji, ukiukwaji wa haki za kibinadamu na uporaji wa mali za uma na kikundi cha watu wachache ili kuidhoofisha kabisa nchi ya urusi(ambayo ilibaki baada ya kusambaratika huko) na ndio mwanzo ama era ya oligarchs wakiwemo Roman Abromivich, Mikhail Khordokovsky na wengine ambao waliweza kuyanunua makampuni makubwa ya serikali kwa njia za bei za kutupwa na kujilimbikizia assets ambao kibongo tungeuita unalala maskini unaamka tajiri. Pia hichi kikundi kiliweza kuwa na ushawishi mkubwa sana kwa serikali na viongozi wengine. Kumbuka pia kipindi hiki nchi ilikuwa chini ya raisi Boris Yeltsin, lakini mnamo mwaka 1999 kuingia 2000 alistaafu ghafla kutokana na sababu za kiafya na kuachia ngazi kwa Vladimir Putin ambaye alikuwa waziri mkuu kipindi hicho. SASA NIRUDI KWENYE MASWALI YAKO

Russia ni nchi yenye historia ndefu na interesting na ni watu wazalendo na wanaopenda tamaduni zao. Hawa oligarchs ndio waliweza kuuleta huo mchezo wa rushwa na kutumia kila njia kupata kila wakitakacho. Huo utamaduni ulishika kasi sana kipindi cha raisi Yeltsin hadi alipoingia Putin ndio mambo yakanza kubadilika. Yeye aliweka mkazo kwenye uchumi na maendeleo ya nchi kiujumla na sio maslahi ya kile kikundi cha matajiri. Hapo ndio mchezo ukadilika na Putin kuonekana mbaya kwa hao jamaa na serikali za magharibi. Kumbuka hawa jamaa walimilki vyombo vingi vya habari na pia walikuwa na ushawishi mkubwa hata na viongozi wakubwa duniani so kuwaharibia hao ni kama unawaharibia wakubwa wengine huko duniani mana walikuwa wanakula wote katika hiyo michezo yao. Kinachoendelea mpaka leo sio kwamba rushwa imeisha urusi lakini imepungua kwa asilimia kubwa mno ukilinganisha na hapo awali kabla ya Putin. Kuhusu democracy na ukiukwaji wa haki kila nchi ina haki ya kujitawala vile inavyotaka kutokana na historia na jamii yake. Hakuna nchi ambayo inalea wahaini au wakwepa kodi au wahujumu uchumi au wapinzani wasiofuata taratibu zilipozo za nchi husika. Na hapa ndio Putin anapowaweza nchi za magharibi mana wanatamani sana atolewe madarakani hata kinguvu lakini mara zote hajawafikiwa.

Kuhusu vikwazo vya kiuchumi ni ukweli usiopingika kama kweli viathiri maendeleo ya nchi husika. Labda tuanzie sababu za wao kuwekewa hivyo vikwazo, ambayo ni mgogoro wa ukraine. Huu mgogoro ni mada nyingine kabisa lakini kiufupi ilichochewa na nchi za magharibi kumshinikiza raisi wa kipindi hicho Viktor Yanukovich kukubali msaada wa kiuchumi ambao iluratibiwa na EU. Bwana Yanukovich pia mezani alikuwa na package nyingine kutoka urusi ambao ilikuwa na masharti nafuu zaidi . Sasa hawa viongozi wa magharibi kutumia wapinzani wa kiongozi huyu na taasisi(NGOs) zake nchi humo waliweza kumuondoa raisi huyo madarakani kwa maandamano makubwa mno(maiden protests) ambayo yalipekea machafuko nchi humo. hayo machafuko ndio sababu kubwa ya urusi kubeba hizo lawama na kuwekewa hivyo vikwazo.

Sasa hivyo vikwazo vimemfanya urusi kuufikiria upya uchumi wake na kujipanga upya. Kumbuka kipato kikubwa alikitegema kutokana na. Mauzo ya oil na gas ambayo bei yake imeshuka kwenye soko la dunia, na wateja wake wakubwa ilikuwa ni EU. Amefanikiwa kupata soko Asia kama nchi ya china na india. Pia imemfanya kukuza uchumi wa ndani zaidi na kuacha kutegemea vitu kutoka nje ambayo pia itawaadhiri sana EU hata kama hivyo vikwazo watavitoa mana itakuwa ngumu kurudi kwenye masoko hayo nchi humo. Pia sio nchi zote EU zinasupport hivyo vikwazo ikiwemo Italy na hasa duniani kwingine kwa sababu kisheria ni lazima viidhinishwe na UN na sio kila nchi zinapokosana basi ruksa kuwekeana hivyo vikwazo. Na pia waatharika wakubwa ni wananchi wa kawaida ambao wanaona wanachofanyiwa n hizo nchi za magharibi na kuongeza chuki kwa hizo nchi na serikali zao.

Kuhusu mgogoro wa meli za kivita ilikuwa ni mkataba ambao waliingia kabla ya huo mzozo wa ukraine. Sasa mfaransa baada ya kukaliwa kooni na mmarekani amekubali kuvunja mkataba huo ambao mrusi alikuwa tayari ameugharamia kwa kiasi kikubwa na hivyo kudai fidia. Swali ni je mfaransa anajenga taswira gani kama business partner kwa mataifa mengine?

Lakini hayo yote ukumbuke tu urusi ni nchi kubwa mno yenye rasilimali nyingi mno na inasemekana ndio nchi pekee duniani inayoweza kujitegemea katika kila kitu. Pia kijeshi binafsi naamini iko juu vizuri hasa upande wa defensive hata zaidi ya marekani na ndio mana hawajawahi kuwaletea chokochoko zaidi ya propaganda.
 
Swali

Mnadhani umoja wa nchi za kisoshalisti unaweza kupanuka tena?

China kwa nini haina uchumi wa kisoshalisti kama urusi japo ni nchi ya kisosholiati?
 
Niliwahi kusoma historia ya Urusi kwa sehemu.
Leo nimejifunza kitu kipya hapa.

I believe kama Tanzania tuna sehemu ya kuiga hapo

Kweli kabisa kuna mambo mengi sana ya kujifunza kama:-
1. kuwa na uzalendo kwa nchi yetu.
2.Kuwekeza kwenye elimu na sayansi.
3. Tujenge uchumi wetu bila kuwa wategemezi wa kila kitu kutoka mataifa makubwa. Hii inasaidia kukwepa makali ya vikwazo vya kiuchumi.
4. Kuwa na morale na spirit ya kufanya kazi kujenga taifa letu.
 
Back
Top Bottom