Naomba kujua walipo waimbaji wa kwaya ya Ulyankulu Bara barabara ya 13

Naomba kujua walipo waimbaji wa kwaya ya Ulyankulu Bara barabara ya 13

Kwangu mpambano uwe

Mapigano ulyankulu barabara ya 22

Vs

kwaya ya Unlyahulu barabara ya 13

Ingawa kwangu wote wakati mnoooo



Kuna kitu umenifumbua macho Leo kwa zaidi ya miaka 30 sikujua kwamba album ya Kwa viumbe vyote imeimbwa na kwaya tofauti na iliyoimba Aliyesamehewa. Zote najua ni Ulyankulu moja kumbe kuna tofauti ya barabara? Asante JF.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
wimbo wao wa mwisho una maneno vumilieni watumishi wote vumilieni huo wimbo ni wimbo wa karne! usikilize na uhusianishe na haya yanayo endelea sasa corona n.k
 
Hii kwaya Ilivumaga sana miaka ya 90 huko, Nyimbo zao maarufu ni pamoja na
Samson na Delilah, Katika viumbe vyote Ayoub.

Hii kwaya ilijipatiaga umaarufu sana enzi hizo, naomba kujua kama hawa waimbaji bado wote wapo hai? Na wengine wapo wap leo hii?

Asante
Hawa jamaa wapo ingiwa baadhi walienda Burundi lakini asilimia kubwa wapo na kwaya yao ipo.
Ulyankulu au Makazi barabara 13.
Na kuna kabisa lao linaitwa kwaviumbe vyote lipo Ulyankulu barabara ya 13C, ukiwa Centre Ulyankulu unaelekea kasikzini uzuri kanisa lao huonekana hata ukiwa Centre maana limejengwa juu ya mlima.
Siyo wakimbizi wote walienda Burundi bado wapo tena wengi kinyama.
Utasikiatu NAMAHOLO {HABARI YAKO}.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Kwaya ya mapigano ulyankulu.

Nakukumbuka kulikuwa na Kanda nyumbani, mzee akinunua betri Basi Hawa walikuwa hawakosekani kabisa.

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Duh ningependa kujua pia!
Hii kwaya ilikuwa moto wa kuotea mbali, Mara ya mwisho niliwaona 1997 Tazengwa - Nzega kulikuwa na kongamano la kwaya
Walikuwa na hit song flan inaitwa
Kisha wana wa manabii
Yaani mpangilio wa sauti humo ni noma

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Hamna mwenye picha yao jamani tuwaone hivi sasa.
 
Umenikumbusha mbali nyimbo hizo alizipenda sana bibi yangu. Rest in peace Bibi kitangiri15
 
Dah! Kitambo sana..
Nimekua nikizisikiliza home na hadi sasa naendelea kuzisikiliza.

"Goliath alijidai kwa nguvu za kibinadamu
Kupigana na majeshi ya Mungu aliye hai
Lakini kijana Daud aliyemtumaini Mungu
Aliweza kumpiga Goliath na kumuua"
 
Back
Top Bottom