Naomba kujuzwa zaidi kuhusu Toyota Passo

Naomba kujuzwa zaidi kuhusu Toyota Passo

Passo ya cc 1290 ina piston nne. Ni nzuri haina shida. Itunze nawe itakutunza. Muda wa kuifanyia huduma ukifika basi usipitishe muda. Usipende kuibebesha mizigo kama hilux. Hiyo gari hata kama mshahara laki sita unaweza kuimudu. Ukibahatika ukaweka full tank yaani kituo cha mafuta unaenda kuomba chenji tu au kununua mafuta ya taa.
 
Passo ya cc 1290 ina piston nne. Ni nzuri haina shida. Itunze nawe itakutunza. Muda wa kuifanyia huduma ukifika basi usipitishe muda. Usipende kuibebesha mizigo kama hilux. Hiyo gari hata kama mshahara laki sita unaweza kuimudu. Ukibahatika ukaweka full tank yaani kituo cha mafuta unaenda kuomba chenji tu au kununua mafuta ya taa.
Nashukulu mkuu, hiv izi za 1290 cc bei zake zipoje nawezapata kwa 4M kwa mtu?
 
Gari ni matumizi na matunzo yako mwenyewe. Hakuna gari mbaya ama rahisi kuharibika.

Ila kibongo bongo utaambiwa ni gari mbovu, haina nguvu, inasumbua, inagonga chini, ac yake haidumu. Hayo yote ni matokeo ya matunzo duni.

Utakuta mtu ana ki Passo na anakaa madongo kuinama kwenye mabonde na makorongo halafu anatarajia gari isigonge chini.

Mara ya kwanza kumiliki Passo ya cc990 piston 3 ilikuwa ni mwaka 2013. Niliinunua used ya Japan kupitia Durban, South Africa.

Niliiendesha kutoka Durban mpaka Dar bila tatizo lolote.

Niliileta maalum kwa ajili ya safari za mjini tu zaidi lami kwa lami.

Nilimuuzia rafiki yangu mwaka 2019 ikiwa full ac, haichemshi, haigongi wala kusumbua chochote.

Jamaa anaishi kimara Bonyokwa, baada ya miezi minne ile gari ilikuwa hata flyover ya Mfugale haina nguvu ya kupanda, yote sababu ya rough usage.

Narudia tena, gari ni matunzo.
Mkuu mbna kama unanishawishi ninunue kapasso na mimi [emoji2][emoji2][emoji2]
 
Ndugu zangu nina Kavitz Kangu huku Tanga Mjini ..kanasaidia kwa mizunguko Ya hapa barabara za namba ,,sasa nimevuta nguvu kidogo nilitaka nipate tena gari nyengine ndogo ya kunisaidia hata nikitaka kutoka nje ya Tanga iwe Rahisi ..nimewaza nikafikiri lakin bado nipo njia panda kwenye pendekezo la gari ipi niwe nayo ..Bajeti Yangu ni hizi hizi gari zetu za mkononi Bei(5M mpaka 8M) naomba nipewe mapendekezo wana JF ..
 
Ndugu zangu nina Kavitz Kangu huku Tanga Mjini ..kanasaidia kwa mizunguko Ya hapa barabara za namba ,,sasa nimevuta nguvu kidogo nilitaka nipate tena gari nyengine ndogo ya kunisaidia hata nikitaka kutoka nje ya Tanga iwe Rahisi ..nimewaza nikafikiri lakin bado nipo njia panda kwenye pendekezo la gari ipi niwe nayo ..Bajeti Yangu ni hizi hizi gari zetu za mkononi Bei(5M mpaka 8M) naomba nipewe mapendekezo wana JF ..
Ukipata
Runx au Alex usijiulize chukua haraka,ist iko poa ila zimezidi mjin
 
Gari dogo nje ndani pana. Kale ka cc990 mafuta kidogo na ac juu unapiga misele ya kutosha ika hakana nguvu na ukiwasha ac unasikia kabisa nguvu yapungua.

Kana tatizo la kugonga miguu so kama waishi mabondeni utakuwa unakatesa.

Kana baadhi ya vipuri bei kuliko hata alteza ila si vingi.

Kama mpenda misele hujali kusimangwa na unaishi town ni kagari kazuri kama kipato chako ni kidogo ili mradi usi kaover use.

Niliwahi kamiliki kwa miaka miwili nilikanunua kwa mhindi fulani nikaakaa nako miaka miwili zaidi ya services za kumwaga oil na kubadilisha brake pads sikuwahi pata changamoto labda ya kubadilisha engine mount.

Nami nikaja nikamuuzia mtu kwa pungufu ya milion 1.3 ya bei nliyokanunua.
Kweli kabisa, mimi ninako ka piston 4, mwaka wa nne sijawahi kufungua injini, ni oil tu na break pad,
Nimeshawahi kwenda Moshi na kurudi kwa siku moja.

Nilitoka Dar alfajiri saa11 nimefika Moshi saa5 asubuhi, saa 7 mchana nikaanza safari ya kurudi, nikafika Dar home Kitunda saa 2 usiku.

Kanafunguka mpaka 140km/h bila stress
 
Back
Top Bottom