Naomba mnisaidie kupendekeza jina zuri na 'unique' la mtoto wa kiume wa Kiislam

Naomba mnisaidie kupendekeza jina zuri na 'unique' la mtoto wa kiume wa Kiislam

Malik ni sifa ya Mungu binadam ataitwa AbdulMaliQ
Hata kumuita Malik pia yafaa sababu Malik maana yake ni "Mfalme" na wafalme wanaadamu wapo. Kisichofaa ni kujiita au kumuita mwengine "Mfalme wa Wafalme". Sababu Mfalme wa Wafalme ni Allah tu.
 
Wanabodi salaam! Nimefanikiwa kupata mtoto wa kiume, sasa kwa jinsi nilivyokuwa na furaha na ujio wake natamani nimpe jina zuri na la kipekee. Najua humu ndan kuna wajuvi wengi so karibuni sana
Sikusudii kukuudhi wala kudharau ila...

Muite MUHAMMAD
Narudia tena muite mwanao (mpe jina la) MUHAMMAD

Kama upo serious lakini

Nitarudi!
 
Hata kumuita Malik pia yafaa sababu Malik maana yake ni "Mfalme" na wafalme wanaadamu wapo. Kisichofaa ni kujiita au kumuita mwengine "Mfalme wa Wafalme". Sababu Mfalme wa Wafalme ni Allah tu.

Soma zaidi maelezo yafuatayo nimeyatoa Alhidaaya.com;

Ama Kuhusu swali lako ni kwamba mzazi au mlezi anafaa kujiepusha kumpatia mtoto wake jina ambalo ni maalum kwa Allaah. Haifai kumuita mtoto kwa jina kama la Al-Ahad (Mmoja pekee), Asw-Swamad (Mwenye kukusudiwa kwa haja zote), Al-Khaaliq (Muumbaji), Ar-Razzaaq (Mwenye kuruzuku) na kadhalika.





Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimbadilisha mtu aliyesilimu aliyekuwa akiitwa Abul-Hakam (baba wa Hukumu) akimwambia kuwa Allaah Pekee Ndiye Mwenye sifa hiyo ya Al-Hakam, na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamuuliza kama ana watoto na majina yao, yule mtu akataja wanawe watatu, Shurayh, Muslim na 'Abdullaah. Basi Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) akamwambia: “Kuanzia leo wewe ni Abuu Shurayh.” [Abu Daawuwd].



Kadhalika Abuu Hurayrah alikuwa akiitwa 'Abdush-Shams (Mja wa jua) lakini alipoingia Uislamu Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam) alimbadilisha jina lakena kumuita 'Abdur-Rahmaan.



Hata hivyo, yapo majina mengine ambayo ni sifa ya Allaah ('Azza wa Jalla) na pia ya wana Aadam kama vile Maalik (mfalme). Kwa hiyo, kumuita mtoto jina hilo hakuna tatizo. Mbali na hayo ni vyema kuwaita watoto majina ya Allaah kwa kufuatanisha na 'Abd (mja). Kwa mfano majina hayo yatakuwa kama 'Abdu-Allaah, 'Abdur-Rahmaan, 'Abdul-Fattaah, 'Abdur-Razzaaq, 'Abdus-Salaam na kadhalika.





Kuhusu swali la pili, ni kwamba haifai kabisa mtu kuitwa 'Abdur-Rasuwl (Mja wa Rasuli), au 'Abdun-Nabbiy (Mja wa Nabbiy, au 'Abdul-Husayn (Mja wa Husayn). Majina haya utayakuta sana kwa Mashia na watu kutoka Asia.



Hakika majina kama hayo hayafai na ni makosa makubwa, kwani uja na utumwa ni wa Allaah Pekee na si wa kiumbe yeyote.



Hao wote kama Rasuli au Al-Hussayn ni waja wa Allaah na watumwa wake na ni wana Aadam na hawawezi katu kuwa waumba au waabudiwa. Hata ikiwa mtu hajakusudia kuwafanya ni waabudiwa au waumba, vilevile ni makosa na haifai.





Majina yapo mengi mazuri na yenye maana nzuri nzuri. Allaah Ana majina mengi ambayo mtu anaweza kuyatumia kwa uja wake na hakuna haja ya kuwatuza viumbe hadi kujipa uja kwao.





Hayo ni matatizo pia yanayosababishwa na ghuluww za watu wanaotukuza maimamu wao hadi kuwapeleka katika daraja ya uungu. Ni hatari kubwa sana kwa mja kuingia katika balaa hilo la kumpeleke katika ushirikina kwa kujua au kutokujua.





Na ikiwa mtu alipewa jina katika majina hayo yasiyofaa na wazazi wake, basi anapaswa kwenda kubadilisha jina hilo hata kama ameshafikia umri mkubwa ili ajiepushe na shirki.



Uislamu unamruhusu mtu kubadili jina lolote baya hata ikiwa kapewa na wazazi wake. Tuchukue mfano wa matukio tuliyotaja juu ya Maswahaba kubadilishwa majina yao na Nabiy (Swalla Allaahu 'alayhi wa aalihi wa sallam).





Na Allaah Anajua zaidi
Asante sana kwa somo zuri shekh wangu
 
Mtume amesisitiza sana katika wanao hakikisha miongoni mwa wa kiume watatu basi hakikisha mmoja anaitwa MUHAMMAD. Hakuishia hapo bali akatoa ruksa hata mtu kuitwa jina la baba yake au ndugu yake wa kuzaliwa (mfano baba MUHAMMAD na mtoto MUHAMMAD au baba na watoto wake zaidi ya mmoja wote kuitwa jina moja))

Watu (waislam) wengi utasikia. Wanakimbilia majina ya waarabu tena bora hata wapate basi muongozo kwa wenye kujua juu ya majina hayo lakini utakuta mtu anajiokotea tu huko ilimradi lijina anampachika mtoto. Nimeshuhudia mtoto anaitwa Rajim sasa kweli unamuita mwanao hivyo!? Mwingine nae ni wa kiume lakini eti nikakuta anaitwa Faraja (yaani ni sawa na Salimu umuite Salama)

Halafu hii mambo ya kusema jina unique sijui ni nani alianzisha hata maana kila mtu utasikia nitafutieni jina ambalo ni la kipekee kabisa kwa mwanangu. Hivi huo upekee unatoka wapi? Labda uunde lugha yako mpya ili kupata jina la kipekee sasa
 
Mtume amesisitiza sana katika wanao hakikisha miongoni mwa wa kiume watatu basi hakikisha mmoja anaitwa MUHAMMAD. Hakuishia hapo bali akatoa ruksa hata mtu kuitwa jina la baba yake au ndugu yake wa kuzaliwa (mfano baba MUHAMMAD na mtoto MUHAMMAD au baba na watoto wake zaidi ya mmoja wote kuitwa jina moja))

Watu (waislam) wengi utasikia. Wanakimbilia majina ya waarabu tena bora hata wapate basi muongozo kwa wenye kujua juu ya majina hayo lakini utakuta mtu anajiokotea tu huko ilimradi lijina anampachika mtoto. Nimeshuhudia mtoto anaitwa Rajim sasa kweli unamuita mwanao hivyo!? Mwingine nae ni wa kiume lakini eti nikakuta anaitwa Faraja (yaani ni sawa na Salimu umuite Salama)

Halafu hii mambo ya kusema jina unique sijui ni nani alianzisha hata maana kila mtu utasikia nitafutieni jina ambalo ni la kipekee kabisa kwa mwanangu. Hivi huo upekee unatoka wapi? Labda uunde lugha yako mpya ili kupata jina la kipekee sasa
Tatizo lako hauna vibe, [emoji3]
Huwezi kutuelewa wazazi wa dar
 
Imamu malicky?

Sent from my SM-G955F using JamiiForums mobile app
Imam Malik jina lake kamili anaitwa Abdullah-Malik ibn Anas kumuita malik ni mazoea ila ni makosa Malik ni miongoni mwa majina ya mwenyezi Mungu maana yake ni (mmiliki) kwakua yeye ndo mmiliki wa kila kitu ila kwa binadam ni lazima iongezewe Abdul maana ya Abdul ni (mja/kiumbe) kwahiyo AbdulMaliQ maana yake (mja wa mmiliki)
 
Tuendelee

Junaid - maana yake shupavu/soldier

Tareef - maana yake kitu ambacho ni adimu na kizuri)

Sawad - maana yake mwenye utajiri wa afya,huruma,upendo (na hata mali inshaAllah)

Au geukia ya asili
Mpili, Akilimali, mbwiga wa mbwiguke, Nishai mtombangile kitwango , au palamagamba.
 
Majina nje ya kiswahili na kilugha ni utumwa wa kifikra
 
Ukimuita Abubakary tu basi ujue kashakuwa gaidi coz magaidi wengi majina yao yanakuwaga aboubakary.

Ukimuita Naseeb Hawa wanakuwaga na bahati saana maishani.
 
Back
Top Bottom