Naomba Nijuzwe kama ni kweli kuna Wamarekani weusi wanahamia TZ kwa wingi

Naomba Nijuzwe kama ni kweli kuna Wamarekani weusi wanahamia TZ kwa wingi

Ni kweli wengi sana wamehamia bongo au wapo kwa muda. Ukiingia youtube utawaona kibao, nilichogundua lakini wengi wao hawajajipanga na hawana jambo la maana wengi wanaishia kuwa youtuber tu kuonyesha hali ya maisha ya africa vs US ni kama trend fulani huko kwao wanajisifia sana kuja africa (wenyewe wanaita motherland).

Wengi wao ukifuatilia wanasema wamekimbia ukandamizwaji wa watu weusi huko kwa Biden (police brutality) na ubaguzi. Lakini kipindi hiki cha c19 wengi wamekimbilia sababu ndio nchi pekee ambayo haina lockdown au masharti ya kukaa ndani.

Kwa ujumla kuna wimbi la wamarekani weusi kuja afrika.

Youtube wamejaa, cheki huyu mmoja.


Baada ya kuona post yako Duksi , imebidi niangalie baadhi ya video mbalimbali youtube kuhusiana na mada tajwa hapo. Nami nikaamua kusumaraizi na kuongezea kidogo.
Hao wamarekani weusi wamejaa wengi sana tena wengine wamepanga mpaka uswahilini. Nimeangalia na nimefanikiwa kujua sababu kadha wa kadha zinazowafanya wamiminike bongo ikiwemo;
i). Ubaguzi ama police brutality huko Marekani kama ulivyosema.
Hapa kuna mzee anasimulia jinsi yeye na mtoto wake (kijana). Alikuwa anahadithia jinsi walivyokamatwa na polisi wa usalama barabarani na kuamriwa kwenda kituoni maana kuna msala walifanya kuwaudhi askari wetu wa usalama (hakutaja ni nini). Walichoshangaa ni pale waliporuhusiwa kuendesha gari wenyewe mpaka kituoni wakati huko kwao wangeoneshewa bastola na pingu juu huku ukiwa na hofu ya kuawa.

ii) Uponyaji wa kiimani (spiritual healing). hapa wengi ni wale wanaopenda mazingira ama nature.
iii) Bongo hamna mambo ya lock down
iv) Urahisi wa maisha. Mtu anapanga mansion kwa dola mpaka 800 wanaona ajabu sana wakati kwao kwa dola 2000 kupata tu nyumba ya kawaida ngumu sana labda upate kachumba tu wenyewe wanaita studio yaani ka ghetto ka kizushi.
v) Bongo kuna beach nzuri sana clear water haswa Zanzibar
vi) Kuna machaguo mengi ya sehemu za kukaa kwa kuzingatia hali ya hewa unayopenda mfano; wanaopenda baridi wanakaa Arusha na wanaopenda mjini wanakaa Dar kwa sababu ya malls ni nyingi na urahisi wa kupata kila unachohitaji
vii) Hii nchi ina amani sana na imetulia
viii) Vivutio vya kitalii ni vingi sana kuanzia Serengeti, mlima Kilimanjaro n.k

Licha ya kufurahi maisha yao hapa bongo na kusema sisi bongo ni wakarimu sana kwa kila mtu, baadhi wamekutana na tamaduni ambazo hawajazoea (culture shock) kwa mfano;
i) Suala la mavazi, waliozoea kuvaa vimini wanapata tabu sana
ii) Too much stare. Hahahaha... imenibidi nicheke kidogo. wabongo tunakodolea sana macho watu, ukipita mtu anakushangaa kama kaona sanamu, wanaona sio kawaida shangaa yetu ya kiajabu.
iii) Bongo ni ngumu sana kupata rafiki wa uhakika sababu wengi wanakuwa rafiki kwa sababu wanaona kama sehemu ya kitonga kupiga pesa za hapa na pale.
iv) wabongo tuko slow sana kwenye suala customer care, kila kitu ni pole pole tu

Pia matamanio yao makubwa kwa bongo ni wao kuweza kupata ardhi na kumiliki kama mzawa bila kupitia TIC (shirika la uwekezaji TZ). wao wanaamini wamerudi motherland sasa kitu kama hiki wanahisi hakijakaa sawa kinawabagua kimtindo. Wengine mpaka wameamua kuolewa na wabongo na sasa wameamua na kujenga nyumba za ndoto zao.
Hawa wamarekani weusi wanazidi kujaa si tu bongo bali Afrika haswa nchi ya Ghana, Gambia, Tanzania, Rwanda n.k na nchi ambayo ina mazingira mazuri sana kwao ni Ghana kwa sababu kule ilianzishwa kampeni mwaka 2019 inaitwa "A year of return" ilikuwa kwamba raisi Akufo Ado(serikali) inawapatia pasipoti ya Ghana, ardhi yako binafsi kwa ajili ya kujenga makazi yako n.k cha kushangaza bongo sio rahisi kama huko Ghana lakini wanajaa na wanaitana wengi sana.
Binafsi ningependa wajichanganye zaidi na wazawa na wawekeze katika maeneo mbalimbali kwani naamini kuishi kwao dunia ya kwanza watakuwa na exposure na ujuzi wa hali ya juu katika kuongezea uthamani kwa kuboresha uwekezaji wa kisasa nchini wasiishie kuwa youtubers tu, labda serikali ikiona mchango chanya toka kwao itaweza kuwapa kastatus fulani.
 
Baada ya kuona post yako Duksi , imebidi niangalie baadhi ya video mbalimbali youtube kuhusiana na mada tajwa hapo. Nami nikaamua kusumaraizi na kuongezea kidogo.
Hao wamarekani weusi wamejaa wengi sana tena wengine wamepanga mpaka uswahilini. Nimeangalia na nimefanikiwa kujua sababu kadha wa kadha zinazowafanya wamiminike bongo ikiwemo;
i). Ubaguzi ama police brutality huko Marekani kama ulivyosema.
Hapa kuna mzee anasimulia jinsi yeye na mtoto wake (kijana). Alikuwa anahadithia jinsi walivyokamatwa na polisi wa usalama barabarani na kuamriwa kwenda kituoni maana kuna msala walifanya kuwaudhi askari wetu wa usalama (hakutaja ni nini). Walichoshangaa ni pale waliporuhusiwa kuendesha gari wenyewe mpaka kituoni wakati huko kwao wangeoneshewa bastola na pingu juu huku ukiwa na hofu ya kuawa.

ii) Uponyaji wa kiimani (spiritual healing). hapa wengi ni wale wanaopenda mazingira ama nature.
iii) Bongo hamna mambo ya lock down
iv) Urahisi wa maisha. Mtu anapanga mansion kwa dola mpaka 800 wanaona ajabu sana wakati kwao kwa dola 2000 kupata tu nyumba ya kawaida ngumu sana labda upate kachumba tu wenyewe wanaita studio yaani ka ghetto ka kizushi.
v) Bongo kuna beach nzuri sana clear water haswa Zanzibar
vi) Kuna machaguo mengi ya sehemu za kukaa kwa kuzingatia hali ya hewa unayopenda mfano; wanaopenda baridi wanakaa Arusha na wanaopenda mjini wanakaa Dar kwa sababu ya malls ni nyingi na urahisi wa kupata kila unachohitaji
vii) Hii nchi ina amani sana na imetulia
viii) Vivutio vya kitalii ni vingi sana kuanzia Serengeti, mlima Kilimanjaro n.k

Licha ya kufurahi maisha yao hapa bongo na kusema sisi bongo ni wakarimu sana kwa kila mtu, baadhi wamekutana na tamaduni ambazo hawajazoea (culture shock) kwa mfano;
i) Suala la mavazi, waliozoea kuvaa vimini wanapata tabu sana
ii) Too much stare. Hahahaha... imenibidi nicheke kidogo. wabongo tunakodolea sana macho watu, ukipita mtu anakushangaa kama kaona sanamu, wanaona sio kawaida shangaa yetu ya kiajabu.
iii) Bongo ni ngumu sana kupata rafiki wa uhakika sababu wengi wanakuwa rafiki kwa sababu wanaona kama sehemu ya kitonga kupiga pesa za hapa na pale.
iv) wabongo tuko slow sana kwenye suala customer care, kila kitu ni pole pole tu

Pia matamanio yao makubwa kwa bongo ni wao kuweza kupata ardhi na kumiliki kama mzawa bila kupitia TIC (shirika la uwekezaji TZ). wao wanaamini wamerudi motherland sasa kitu kama hiki wanahisi hakijakaa sawa kinawabagua kimtindo. Wengine mpaka wameamua kuolewa na wabongo na sasa wameamua na kujenga nyumba za ndoto zao.
Hawa wamarekani weusi wanazidi kujaa si tu bongo bali Afrika haswa nchi ya Ghana, Gambia, Tanzania, Rwanda n.k na nchi ambayo ina mazingira mazuri sana kwao ni Ghana kwa sababu kule ilianzishwa kampeni mwaka 2019 inaitwa "A year of return" ilikuwa kwamba raisi Akufo Ado(serikali) inawapatia pasipoti ya Ghana, ardhi yako binafsi kwa ajili ya kujenga makazi yako n.k cha kushangaza bongo sio rahisi kama huko Ghana lakini wanajaa na wanaitana wengi sana.
Binafsi ningependa wajichanganye zaidi na wazawa na wawekeze katika maeneo mbalimbali kwani naamini kuishi kwao dunia ya kwanza watakuwa na exposure na ujuzi wa hali ya juu katika kuongezea uthamani kwa kuboresha uwekezaji wa kisasa nchini wasiishie kuwa youtubers tu, labda serikali ikiona mchango chanya toka kwao itaweza kuwapa kastatus fulani.
Umeelezea vizuri sana.
Japo pia walalamishi sana, nadhani wanataka kila kitu perfect.

Pengine serikali ifikirie kuwatengea eneo au wanaloweza kununua bila masharti ya kupitia TIC au kuwalegezea masharti, watasaidia kuleta mitaji ya fedha za kigeni wanapata changamoto ya kuishi nchini kwa muda mrefu wanapaswa kurenew visa kila baada ya miezi mi3 kwa kutoka nje ya nchi.
 
Nimesikia kuna Wamarekani weusi wanahamia TZ kwa wingi kwa sababu wanakimbia kuchanjwa kinga ya corona.

Pia sababu nyingine ni kuipenda TZ kwa sababu ya JPM walivyokuwa wanamhusudu.

Ni kweli wengi lakini sio kwa hizo sababu ulizotaja, sababu zipo nyingi ila chache ni kama maisha huku rahisi ukilinganisha na kwao pia pesa yetu haina thamani ukilinganisha na yao, huku mgeni anathaminiwa sana tofauti na kwao mgeni hunathamani tena ukiwa mweusi kifupi hawatupendi wanatudharau, sio salama US mauaji ya bunduki mengi sana.
 
Hakuna watu wapumbav Kama black Americans .. naoongea with experience na Kama unabisha tafuta tour guides au wale vijana wa Zanzibar watakupa stories zao.


Bora ufanye kazi na Mzungu kuliko black Americans

Yes I agree with you, nigga msikie tu , hutaweza kumwelewa mpaka uishi nae sio watu hao
 
Sio black americans tu hadi wazungu....wamekuja wengi mno tunakaa nao streets kwenye vibaa vya kawaida....wazungu wenye hela zao wamejichimbia zanzibar pako full mbaya... Japo pia namfaham black american mmoja ambae yupo hapa bongo na kuna siku alisema kuna team ya wenzake kama 70 anakuja nao next time nikajua ni utalii tu ila naona hii mada inaniunganishia dots...BTW hata huyo black american ninaemzungumzia ni muumini mkubwa mno wa jpm na alikua haishi kumuongelea. So wale mnaobeza mada msizozijua muwe mnatulia kusikia kwa wanaofaham chochote
 
Nimesikia kuna Wamarekani weusi wanahamia TZ kwa wingi kwa sababu wanakimbia kuchanjwa kinga ya corona.

Pia sababu nyingine ni kuipenda TZ kwa sababu ya JPM walivyokuwa wanamhusudu.
Ndio! Wamarekani wengi sana wanahamia Tanzania hasa Wamarekani weusi na hii inatokana na sababu za kidiplomasia na kiintelijensia.
 
Ghana na Tanzania ndio machaka yao sana...

Kwa Tanzania wanajichimbia Chuga na Dar
 
Yes I agree with you, nigga msikie tu , hutaweza kumwelewa mpaka uishi nae sio watu hao
Hao jamaa nimeishi nao Sana ni wajinga sana.

Humu watu wanaongea kwasababu wanawaona kwenye movie na Basketball hawawajui vizuri Black Americans.

Mijamaa ina inferiority complex ya hatari. Wanatuchukia Hadi Watu weusi kutoka Africa ...
 
Siku hizi jitahidi sana usiwaangilie Youtubers/social media influencer kama source yako ya habari/information..

Hao asilimia kubwa wanafanya kwa ajili ya channel zao na manufaa yao binafsi, au kutengeneza video kutokana na jambo linalo trend kwa muda huo, wamekwa wajanjawajanja na waongo waongo sana, wanachojali ni kumonetize chaneli zao.

Sidhani kama ni jambo jepesi mmarekani kuhama nchi yake nakuja kuishi Tz , labda waje vacation tu kutalii au kukaa kwa muda maalumu..

Sheria za kupata/kuwa urai?
Watapata ajira gani ya kuwalipa vizuri huku?
Biashara/uwekezaji??
Huduma bima ya afya hapa Tz kulinganisha na kwao?
 
Ghana na Tanzania ndio machaka yao sana...

Kwa Tanzania wanajichimbia Chuga na Dar
Ni kweli mkuu mfano pale chuga home sweetie home hasa maeneo ya njiro na sakina Kyle wapo wa kutosha ..mfano nilipataga kademu kwao wako tisa no familia na wote wameishi na kuzaliwa marekani, Kale ka manzi kalielewaga tu swaga na min jinsi nnavyovaa Michigan ..kanaitwa 'Kelcy' ..nikirudi bongo (Ila sijui lini) ntakatafuna Tena [emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]
 
Aisee hii kitu ni kweli kuna mwanangu mmoja, amempangisha mmarekani mweusi kule chini Kawe beach jamaa amehamia bongo na familia yake nzima mke na watoto. Anampiga parefu balaa $1700 kwa mwezi. Huyu mwamba ni boss huko kwenye ampuni zao ila anadai kazi anazifanya online.
 
Back
Top Bottom