- Thread starter
- #41
Inabidi kwanza useme ni fundi wa nini!bas kuanzia leo nami niitwe fundi von bishoo ila nitamkwe kijeruman ntatamkwaje...?😂
Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Inabidi kwanza useme ni fundi wa nini!bas kuanzia leo nami niitwe fundi von bishoo ila nitamkwe kijeruman ntatamkwaje...?😂
Hapa naona nikujisumbua tu, hao wazungu wenyewe hawana muda wa kupoteza kujifunza kutamka majina yetu.Naona hili ni tatizo kubwa sana kwa watangazaji wetu wa vituo vyote vya redio kuanzia redio ya taifa mpaka vituo vidogo vya redio linapokuja jina lenye asili ya kijerumani matamshi yanakuwa ndivyo sivyo kabisa. Ni kama wewe umsikie mtu akitamka jina Juma kama Jima au Joma. Au jina Ali kama Hali, James kama Jemesi, Mwajuma kama Mijuma n.k. Hii inaleta ukakasi masikioni. Nitaanza na majina machache na kama yeyote anahitaji usaidizi wa matamshi ya majina mengine au hata maneno ya kijerumani dondosha kwenye uzi huu kwa msaada.
1. Naanza na hili liwasaidie hata walimu na wanafunzi wa fizikia ( physics).
Albert Einstein : Nguli wa fizikia na hisabati - Tamka ALBART AINSHTAIN. Katika sarufi ya kijerumani herufi e na i zikifuatana (ei) hutamkwa kama "ai" na s na t zikifuatana (st) hutamkwa kama "sht"
2. Frank-Walter Steinmeir: Rais wa Ujerumani - Tamka FRANK VALTA SHTAINMAIA. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi W hutamkwa kama tunavyotamka herufi V. herufi "r" ikikaa mwisho wa neno itamke kama "a".
3. Annalena Baebock: Waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani - Tamka ANALENA BEEBOK. Kwenye sarufi ya kijerumani herufi a na e zikifuatana (ae) hutamkwa sawa na ule mlio wa mbuzi (meeee!). Mara nyingi badala ya herufi mbili ae huandikwa tu ä.
4. Jens Stoltenberg: Katibu mkuu wa NATO - Tamka YEENS SHTOLTENBERG. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi J hutamkwa kama tunavyotamka herufi Y.
5. Ursula von der Leyen: Raisi wa Kamisheni ya Ulaya ( EU Commission). Huyu sijui kama kuna siku inapita bila kutajwa. Ni watangazaji wa DW tu nimewasikia wakilitamka jina lake kwa usahihi. Tamka URSULA FON DEA LEYEN. Kwenye sarufi ya Kijerumani herufi V hutamkwa kama herufi yetu F.
6. Olaf Scholz: Raisi wa Ujerumani- Tamka OLAF SHOLZ. Kwenye sarufi ya kijerumani "sch" hutamkwa kama "sh" . Mfano: Kijerumani- Schule, Kiswahili- Shule
Natumaini uzi huu uwasaidie hasa watangazaji wetu maana matangazo yanaenda nje ya mipaka ya nchi pia. Kwa msaada zaidi dondosha swali lako hapa.
YYURGEN KLOPJürgen Klopp...
ü ina sauti kama ya "yi". Inatamkwa like u with round lips. Unaweza kuangalia videos youtube andika German umlauts pronounciation. Zipo video nyingi utaona namna ya kukunja mdomo wako ili kutamka ä,ö na ü.YYURGEN KLOP
Mwanangu nakubali hii lugha unaijua. Me nimeisoma kidogo, kwahiyo nadokoa kimtindoü ina sauti kama ya "yi". Inatamkwa like u with round lips. Unaweza kuangalia videos youtube andika German umlauts pronounciation. Zipo video nyingi utaona namna ya kukunja mdomo wako ili kutamka ä,ö na ü.
Tuko pamoja mkuu. Ukikwama popote niulize. Ila Youtube kuna videos nzuri za kujifunzia. Pitia pia website ya Deutsche Welle wana masomo. Google " Deutsch, warum nicht".Mwanangu nakubali hii lugha unaijua. Me nimeisoma kidogo, kwahiyo nadokoa kimtindo
Eg:-
Ich bin Number ni 26
Ich komme aus Tansania
Mein hobby ist lesen
Mein beruf ist.....
Ich bin.... Jahre alt
Mengine yatakuja tutakapokuwa tunaongea. Hapa nipo napiga hesabu zangu tu nidumbukie huko kwa wa "DEUTSCH" wenzangu [emoji1787][emoji3]
Pamoja mkuuTuko pamoja mkuu. Ukikwama popote niulize. Ila Youtube kuna videos nzuri za kujifunzia. Pitia pia website ya Deutsche Welle wana masomo. Google " Deutsch, warum nicht".
😂😂ujenzi ila saidia fundiInabidi kwanza useme ni fundi wa nini!
[emoji23][emoji23][emoji23]CCM inatamkwa schicem
KINANA inatamkwa chinerner
Chongolo inatamkwa tshonglo.
Jifunzeni kiswahili nyie nzi wa kijani msiwe kama wenzenu nyumbu kila kitu ni kupinga tuu....bahati mbaya wa mizambarauni hata hawajui zzk wao anataka Nini.
Baumeister. Japo hicho ni cheo cha fundi aliyekubuhu!😂😂ujenzi ila saidia fundi