Naomba ufafanuzi kuhusu gari aina ya Land Rover Discovery TD5

Naomba ufafanuzi kuhusu gari aina ya Land Rover Discovery TD5

Hiyo chukua mkuu, kama ni jamaa yako muulize kama amewahi gusa injini au kuichezea fuel injector pump.

Hiyo ni gari ya uhakika kwa safari yoyote na unavuta tela vizuri.
Nimemuuliza mkuu akasema hapana,ni gari ambalo lilikua linatumiwa kwa shughuli za town kwa sana,mikiki mikiki halijapigishwa kiviile.
 
Kwa matumizi na porini Discovery 2 ni nzuri zaidi kuliko Discovery 3 &4 hasa ukiipata ya Diesel..ulaji wa mafuta ni mdogo..Ingine ina nguvu..speed 220km
Iko juu kiasi kwamba kwa porini si rahisi ku buruza chini ..Ni Gari imekaa kikazi na ya kiume. Hutajutia uamuzi wako..kuhusu spares..mara nyingi si magari ya kuharibikaharibika ovyo ila kama zilivyo landrover zingine spares zake ni kwa dealers au maduka maalumu na ni original spares zitakazokupa life span ya landrover yako

Sent using Jamii Forums mobile app
Best comment

Sent using Jamii Forums mobile app
 
mng'ato,
BOss Ahsante sana kwa ushauri wako. Hii gari inaonekana ni very delicate. Sio gari ya kazi kama nilivyokua nafikiria.

Nilikua naweka Class moja na Land Cruiser ama Nissan Patrol Y60 lakini inaonekana ni kimeo hasa kwa sisi tunaopenda gari ngumu zinazoweza kuhimili mikiki ya safari ndefu bila kupita garage mara kwa mara.

Ngoja nijipange tu kwa ajili ya LC 80 Series Au hata nikipata LC 60 series ambayo ipo kwenye good condition nabeba
 
Ndugu yangu nakushahuri usiingie chaka ukanunua gari yeyote ya mataifa mengine tofauti na Japani utajuta tena landrover ndo sio gari kabisa ni matatizo utaumwa mimi nishaendesha zote kuanzia 109, 110, range mpaka ya 2016 ingawa sio zangu ila japani kwa uimara wa gari ni kiboko, tena hzo discover ndio matatizo matupu kaka nunua hata landcruser yenye kilometa lakitatu kuliko discover ya kilometa zero,utanishukuru baadae. Mzee Kigogo,

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Ndugu yangu nakushahuri usiingie chaka ukanunua gari yeyote ya mataifa mengine tofauti na Japani utajuta tena landrover ndo sio gari kabisa ni matatizo utaumwa mimi nishaendesha zote kuanzia 109, 110, range mpaka ya 2016 ingawa sio zangu ila japani kwa uimara wa gari ni kiboko, tena hzo discover ndio matatizo matupu kaka nunua hata landcruser yenye kilometa lakitatu kuliko discover ya kilometa zero,utanishukuru baadae.

Sent using Jamii Forums mobile app
Ungeelezea kwa undani sababu ya kusema hayo, ungemsaidia mleta mada na wengine pia.
 
kzba,
Thanks kaka! Magari ya Kijapan yanajulikana kwa uimara wake hasa brand kama Toyota Land Cruiser.

Ndio maana bei ya Land Cruiser 80 ya mwaka let’s say 1993 huwezi kulinganisha na Range Rover ama Discovery.
 
Discvery simshauri mtu kuinunua, hii ni gari ya matajiri, uinunue na uitunze kama yai au uitupe mapema
Kupata landcruiser sio mchezo hasa kwa bei hiyo. Ila hiyo Discovery sio mbaya lakini inataka matunzo na service nzuri (kwa hiyo engine TD5). Za petrol ni nzuri zaidi ila zinakula mafuta sana. Kama unatafuta gari ya porini unaweza kuifikiria hiyo ika wenye uzoefu nazo watasema zaidi


Sent using Jamii Forums mobile app

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Back
Top Bottom