Naomba uniulize chochote kuhusu kufanikiwa katika Biashara na Ujasiriamali

Naomba uniulize chochote kuhusu kufanikiwa katika Biashara na Ujasiriamali

Sitoi kiki boss. Bundle ni langu kwanini unipangie cha kupost?!

Kwani certified mdokozi ni jina lililopo kwenye passport yako, au unaleta tu unafiki.
passport naitoa wapi ? Ungenipuuza kaka wajasiliamali si wakujibishana na watu kama mm just keep on telling the story
 
Boss kuhusu dawa hua tuna assume mahindi yakivuka magoti basi mashambulizi dhidi ya wadudu ni madogo sana, so hkn dawa tunatumia. Kwa uelewa wangu.

Pia mbolea inategemeana na ardhi boss, so nahisi hapo mpk uwe na vipimo vya maji na udogo. kitu ninachotumia Ruvu kinaweza kuwa tofauti na huko ulipo, mfn mahindi hapa Miono nimetumia urea tu.
Asante, nashukuru sana kaka
 
Boss! Kua connected kwenye biashara ndio kila kitu, naeza sema hii ndio prime factor. Wenzetu wazungu wanapenda kusema "Your network is your net worth."

Na sisi ambao hatukubahatika kuwa na surnames za kiheshimiwa kutengeneza network ni ngumu sana. Yani leo hii wewe na riz1 wote mkipewa mil 10 mfanye biashara, ndani ya mwaka m1 jamaa keshakuacha mbali sana. Maana hata akisema anasupply pipi za ivory kwenye taasis za serikali anaeza hata kuuza pakti elf 20, wewe huku kitaa pakti unauza ef 3.

Ukianza biashara hautaelewa kila kitu in an eye blink. Ni pole pole, kadri unavyozidi kua kwenye game ndio unavyoelewa how it's done na ndivyo unavyozidi kukutana na watu wengi, hawa watu ndio connections zenyewe. Niseme kwa ufupi, kukutana na watu sahihi ndio njia rahisi zaidi ya kutengeneza network yako.

Hata kwenye masoko pia ni hivyo hivyo.
Dah yaani unaposema kukutana na watu sahihi umenikumbusha wakati nilipoanza biashara ya viazi vya chips, jamaa alinifanyia uhuni akanipatia mbegu za viazi badala ya viazi vyenyewe, nikapata hasara ya 7M
 
Mkuu uko vizuri sana kuna maswali nilikuwa najiuliza hasa baada ya mada yako ile kuwa huyu kijana mtaji wa kuanzia hiyo biashara anayoisema aliutoa wapi ila sasa mada hii imenifungua macho zaidi na nimekuelewa vyema..........hiyo project ya kufuga kuku niko naipigia garamba nadhani by nezt year itakuwa hewani Mungu ajaalie
Lakini naomba msaada wako ili niweze kupata mashine za kupanda mpunga na kuvuna mpunga kwa kukodi ni kazi ambayo naiwazia sana kilichonikwamisha ni namna ya kuzinunua ila nishaona urahisi nimeona labda nikikodi naweza fanikiwa,naomba unijuze hapo
 
Kiongozi nafuatilia sana haya mambo ya forex trading lakin bado sijaielewa namna inavofanya kazi je ni website ipi nzuri kwa beginners... Ntashukuru
 
We jamaa sio mchoyo ndio maana unafanikiwa,kupata mtu mwenye biashara na kushare mafanikio yake ni ngumu sana kwa dunia yetu,..kuna jamaa zangu wao hata kwenye kubet tu anakunyima mkeka wa sure,anataka kula yeye tu,ndio maana hawatajiriki wakati wana umri sawa na kampuni za kubeti!...so big up bro,keep up the good spirit of sharing.
 
Mkuu [HASHTAG]#ONTARIO[/HASHTAG] umesema hapo juu kuwa inawezekana, nisaidie jinsi gani ninaweza wekeza laki 3 kwenye forex trading nikapata faida ya milioni moja kwa mwezi?
 
Baada ya kusoma maelezo ya mwanzo na replies zako kwa maswali na comments za wakuu mbalimbali katika uzi huu, na kama nimeelewa vizuri kuhusu umri wako, kuna sehemu umesema unataka uwe na kampuni 5 kabla ya kufika miaka 25, ikiwa na maana hujafikisha miaka 25. Hii inanipa shida kuamini kwamba uko below 25, au labda sijaelewa vizuri kuhusu hilo la kabla ya 25 years. Mkuu kama hutojali, ufafanuzi pls.
Kwani haiwezekani?
 
Kwani haiwezekani?
Inawezekana mkuu. Hapo nilitaka ufafanuzi wa umri wake maana alivyofikia hatua hizo kibongobongo ni ngumu, lakini ukipata maelezo kutoka kwa mhusika inakua nzuri zaidi na pia swali hilo linaamsha mhusika atiririke zaidi. Hata hivyo yeye alinielewa na jibu alilotoa nilimuelewa.
 
Hongera mkuu, ipo siku tutakutana huko majuu acha na sisi tukaze buti
 
Kaka nashukuru kwa fursa hii, nataka kuanzisha biashara ya DAYCARE tafadhali nishauri kama unafaham chochote kuhusiana na biashara hii.
 
Daaah kwenye biashara naona nicheza makidamakida nilijaribu kufuga kuku wa nyama niliishia kuwauza kwa mkopo hadi leo sijajua nilipokosea sasa nilipoona picha za kuku nimekumbuka mbali natamani kurudia biashara hiyo lakini soko imekuwa kikwazo sana kwa mkoa nilipo.........unakuta wapo walioshika soko kwa muda sasa wewe inakutia kwenye mahangaiko sana
Hapana hao walio shika masoko kuna watu au aina fulani ya watu ambao inawalenga, wewe unaweza fanya biashara hiyo hiyo lakini market yako ni watu wa aina fulani tu, focus na watu hao, eels vionjo vinavyo wavutia komaa na subiri na soon utaona mabadiliko.
 
Hapana hao walio shika masoko kuna watu au aina fulani ya watu ambao inawalenga, wewe unaweza fanya biashara hiyo hiyo lakini market yako ni watu wa aina fulani tu, focus na watu hao, eels vionjo vinavyo wavutia komaa na subiri na soon utaona mabadiliko.
Asante sana mkuu unanipa moyo wa kuweza kurudi tena kwenye biashara hiyo
 
Back
Top Bottom