Naomba ushauri kutokana na changamoto ninazopitia ofisini ninapofanyia kazi

Naomba ushauri kutokana na changamoto ninazopitia ofisini ninapofanyia kazi

Unakuta umemaliza kazi zako huna kitu cha kufanya umetulia boss akikuta umetulia huna cha kufanya anaanza kukufokea kwanini umekaa idle

Ukimwambia umemaliza majukumu yako ukoo free anakutafutia kazi yeyote ya kufanya hata kama ikoo njee ya majukumu yako

Shida ni kukosa akili tu ya kujiongeza, kweli unakosa kabisa kazi ya kufanya unakaa tu kama furniture na umeajiriwa?
Hayo ni mambo ya serikalini kama private tafuta tu namna uwe busy hata for nothing siku ziende upate ya kununulia mkate wa kila siku.
 
Kaza mtoto wa kiume, majungu kazini kawaida tu...fanya yanayokuhusu mengine waachie wao punguza kiherehere na ujuaji
 
Unakuta umemaliza kazi zako huna kitu cha kufanya umetulia boss akikuta umetulia huna cha kufanya anaanza kukufokea kwanini umekaa idle

Ukimwambia umemaliza majukumu yako ukoo free anakutafutia kazi yeyote ya kufanya hata kama ikoo njee ya majukumu yako
hakikisha ukimaliza majukumu yako unaenda kumuomba kazi nyingine ili usikae idle. Then jitahidi sana kutabasamu na kuomba samahani, pia dhibiti mdomo wako . Zaidi muombe Mungu sana.
 
Nina kama week mbili tangu nianze kazi ila kuna changamoto ninapitia hapa

1. Changamoto ya kwanza kuna supervisor full time kunifanyia visa mara kila saa natishiwa kufukuzwa kazi

2. Work mate niliokutana nao ofisini hawanipi ushirikiano vitu vingi vya msingi hawanielekezi

3. Upande wa boss wangu ambae alikuwa anakubali utendaji wangu wa kazi sasa hivi kanibadilikia full kunifokea full kupewa maonyo kuhusu kufukuzwa

4. Ofisini nipo kama mwana mkiwa naona kama niko motoni lawama na vitisho vimekuwa vingi

Hapa nilipo sijui hatma yangu katika hii ofisi.
ww ni Imani Gani,,kama ni mkristo jitaid uwe na Roho mtakatifu then umwombe kibali nakuhakikishia hyo ofisi watakua wanakusikiliza ww tu kiufupi ww ndio utakuwa Kila kitu..

Kama ww ni muislam nenda Kwa shehe akutafutie jini likupe nyota ...note njia hii Ina madhara..

Mwisho kataaa kubal vita vyote wenzako tunashindia ktk ulimwengu WA Roho ..then uku mwilin mamb yanafata tuu njia...
 
Kwenye CV unaandika ujuzi wa kutumia Microsoft excel kwa ufasaha,haya tucholee pie chart ya takwimu hizi.
Wanakimbiaga ofisi kijanja hawa , kila siku dharura mara oooh kiukweli mimi najihisi sijawa na mood kufanya kazi ofisi hii .

Hawataki kusema walidanganya ujuzi na mambo yashakuwa mbombo ngafu
 
Itakuwa umeleta umachinoo kazini,wiki 2 uchukiwe na Kila mtu,haiwezekani,Wala usidhani umelogwa,punguza ujuaji hakuna mtu anayependa mtu dizaini hiyo.
 
Kama ww ni muislam nenda Kwa shehe akutafutie jini likupe nyota ...note njia hii Ina madhara..
kuna wakati katika maisha ni busara kukaa kimya na kuacha dhana ya kuwa labda umpumbavu kuliko kuongea na kuondoa shaka yeyote juu ya upumbavu wako.
 
Timiza majukumu ya msingi kwenye kazi yako kulingana na job description yako,andika taarifa ziweke kwa file,wakitaka kukufukuza kazi unawajibu kwa evidence,piga kazi mzee hayo mambo yapo sana makazini,kidole risasi mno
 
Mwaka flan nilienda kampun flan kufanya kaz..namna nilivyopata kaz walitangaza nafasi nikaomba nikaitwa kwenye usaili..wakat usaili ukiendelea nikiwa nimeshatumia kama dk 45 hiv mkurugenzi mkuu (mzungu) akanikubali na na nikaajiliwa..kumbe ile nafasi kuna mbongo mkuu wa idara alitaka ndugu yake ndo achukue ile nafasi..
Nilipoanza kaz nikaona sipat ushirikiano na watu wa idara yangu..chini chini kulawa na maneno "msimpe ushirikiano ili afail..".dogo mmoja wa IT tukiqa tunakunywa chai ndo akanimegea mkanda mzima...kwa kuwa na mimi nilikiwa mkuu wa idaranikatumia nafasi yangu kutaka taarifa mbali mbali...
Baadae nikabaini mambo meengi ya upigaji..nikamuita jamaa kistaarabu nikaamuliza akafoka na kugoma..halafu usiku kama saa saba akaingia whatsup kwenye grp la staff wote..akaoandika vitu vingi kama kunikosoa utendaji wangu..alivyopost nikasoma weee...kisha nikaingia kwenye email yangu nikavuta file lake la upigaji na hasara yoote aliyosababisha...nikapost pale...
Md na staff wengine wakalisoma..uchunguz ukaanza akasimamishwa kaz na kufunguliwa mashtaka na hatimae akafungwa..mwakana anamaliza kifungo...
duuh akitoka si kitaumanaa boss polee snaaa maisha hayaaa
 
Mkuu wewe wapuuze ufanye majukumu yako lakini ukiona mpaka boss anazingua muulize kwa upolee tatizo nini mbona unaona hupewi ushirikiano??? akizingua vumilia timiza wajibu wako ila nae akiwa mkudaaa JIKATAEEEE katika maisha yetu tunatumia masaa mengi kazini kuliko nyumbani kwetu so kazini inabdi iwe sehemu ambayo ukiwepo una amaniii sio ufalaa wa kunyanyaswaaa..
 
Nina kama week mbili tangu nianze kazi ila kuna changamoto ninapitia hapa

1. Changamoto ya kwanza kuna supervisor full time kunifanyia visa mara kila saa natishiwa kufukuzwa kazi

2. Work mate niliokutana nao ofisini hawanipi ushirikiano vitu vingi vya msingi hawanielekezi

3. Upande wa boss wangu ambae alikuwa anakubali utendaji wangu wa kazi sasa hivi kanibadilikia full kunifokea full kupewa maonyo kuhusu kufukuzwa

4. Ofisini nipo kama mwana mkiwa naona kama niko motoni lawama na vitisho vimekuwa vingi

Hapa nilipo sijui hatma yangu katika hii ofisi.
Pole sana huyo ni shetani yupo kazini omba sana
 
Nina kama week mbili tangu nianze kazi ila kuna changamoto ninapitia hapa

1. Changamoto ya kwanza kuna supervisor full time kunifanyia visa mara kila saa natishiwa kufukuzwa kazi

2. Work mate niliokutana nao ofisini hawanipi ushirikiano vitu vingi vya msingi hawanielekezi

3. Upande wa boss wangu ambae alikuwa anakubali utendaji wangu wa kazi sasa hivi kanibadilikia full kunifokea full kupewa maonyo kuhusu kufukuzwa

4. Ofisini nipo kama mwana mkiwa naona kama niko motoni lawama na vitisho vimekuwa vingi

Hapa nilipo sijui hatma yangu katika hii ofisi.
Kwa uzoefu wangu kitu ninachokiona watu wanakutafutia sababu uondoke hapo ulipo

Ushauli wangu jiandae kisaikolojia lakini pia kuanzia sasa anza kutafuta kazi sehemu nyingine taratibu

Pia kipindi hiki kitumie vizuli hapo kazini kutengeneza cv yako mpya kuelekea kazi mpyaa

Sent from my SM-A037F using JamiiForums mobile app
 
Wakuu huko kwenu interns na madogo wa field washaanza kuripoti?
 
kuna wakati katika maisha ni busara kukaa kimya na kuacha dhana ya kuwa labda umpumbavu kuliko kuongea na kuondoa shaka yeyote juu ya upumbavu wako.
Habar ndio hyo..huo upumbavu upo kichwani mwako ndio maana huelewi mambo yanavyokwenda.
 
Wanakufokea tu bila sababu??? Wewe ndio unaleta sababu za kufokewa so jitahidi ufanye kazi inavyotakiwa kuepuka makosa mara kwa mara ili wakose nafasi ya kukufokea na visa.

Ukiwa ofisi mpya sharti uwe mchangamfu ili wakuchangamkie ukijitenga hakuna wakukusogelea watakuacha hapo uhangaike mwenyewe
Changamka!
Jichanganye!
Jifanye mjinga
Jipendekeze
Mkuu, ajipendekeze tena!

Mwalimu Nyerere (Hayati) aliwahi kusema, nanukuu, "utii ukizidi sana unageuka kuwa uoga, uoga ukizidi unageuka kuwa unafiki, unafiki ukizidi unazaa kujipendekeza, kujipendekeza kukizidi kunazaa mauti".

Sasa unamshaurije mkuu ajipendekeze? Hii ni hatua ya juu sana ya utii, itaishia kumgharimu tu.
 
Nina kama week mbili tangu nianze kazi ila kuna changamoto ninapitia hapa

1. Changamoto ya kwanza kuna supervisor full time kunifanyia visa mara kila saa natishiwa kufukuzwa kazi

2. Work mate niliokutana nao ofisini hawanipi ushirikiano vitu vingi vya msingi hawanielekezi

3. Upande wa boss wangu ambae alikuwa anakubali utendaji wangu wa kazi sasa hivi kanibadilikia full kunifokea full kupewa maonyo kuhusu kufukuzwa

4. Ofisini nipo kama mwana mkiwa naona kama niko motoni lawama na vitisho vimekuwa vingi

Hapa nilipo sijui hatma yangu katika hii ofisi.
Mkuu

Wewe ni wa kiroho sana au ni wale kawaida tu so wa church sana wala wa msikitini sana!!?

Kama ni wa kawaida tafuta mtaalamu konki nenda kamweleze tatizo lako atakupa dawa utaoga na kuondoa hiyo kitu,yaani kuna kitu umefanyiwa ndio maana unahangaika!!!

Tafuta HATA shehe wa kisomo uweke mambo sawa!!!!

Najua hutonielewa coz ya usomi na ujuaji lakini hiyo ndio tiba !

Kama wewe ni wa Church sana nenda na SADAKA kwa mtumishi muombaji sana akakate maneno mabayoa na jicho la husda linalokuandama!!

Kinachokusumbua wewe ni tatizo la kiroho lililoanza baada ya Mungu kukupa kazi,SASA kuna watu wanajihisi inferior kwako wanakushughulikia kimya kimya!!
 
Tatizo husemi wewe unazingua nini hapo kazini,alafu watu wa aina yako wanakuwaga walalamishi na kuona wanaonewa kila kitu.
Hapo ni suala la muda tu,hiyo kazi ishakushinda jiongeze na mambo mengine!
 
Back
Top Bottom