Naomba ushauri kutokana na changamoto ninazopitia ofisini ninapofanyia kazi


Shida yenu ni kujifanya wajuaji kila kitu 😅😅
Sasa mtu hufahamu vitu unahitaji kufundishwa unashindwa kujipendekeza kwa wenye ufahamu ili ufundishwe kisa mwalimu nyerere alisema.......
Kila kitu huweza kuwa sawa kulingana na mazingira na uhitaji wa wakati husika.
 
Samahani kama nimekukosea mkuu.

Ila kumbuka umeandika comment yako hapa ili upate maoni mbalimbali, hasi na chanya.

Sasa unataka tukusapoti tu bila kutoa maoni yetu bunafsi ambayo pengine yanaweza kuwa kinyume na wewe?

Sidhani kama hayo ndio madhumuni ya hii forum.
 
Acha kazi!! Rudi ulikokua mbona rahisi tu.
 

Nani alikwambia comments hapa ni kwaajili yakupata maoni? 😅

Maoni mpe aliyeleta uzi sio wachangiaji
 
Nani alikwambia comments hapa ni kwaajili yakupata maoni? [emoji28]

Maoni mpe aliyeleta uzi sio wachangiaji
Mkuu, hata mchangiaji ukipotosha lazima tukurekebishe. Haifai tukuache na ujinga wako upotoshe na wengine [emoji28]
 
Mkuu, hata mchangiaji ukipotosha lazima tukurekebishe. Haifai tukuache na ujinga wako upotoshe na wengine [emoji28]

KIlichopotoshwa hapo nini?
Au mawazo ya wengine kwako sio sahihi, sahihi ni yako?
Kama ndivvyo basi comment wazo lako muhusika ataliona atalichukua
 
KIlichopotoshwa hapo nini?
Au mawazo ya wengine kwako sio sahihi, sahihi ni yako?
Kama ndivvyo basi coment wazo lako muhusika ataliona atalichukua
Mkuu, kuna mawazo mbadala na mawazo ya kijinga.

Mawazo mbadala ndiyo yanapokelewa, ya kijinga yanakanushwa na kupuuzwa.
 
Mi visa ka hivyo nshakutana navyo ila sikuwahi shobobekea boss au kumuabudu,nafanya kaz naendelea na mambo yng,nilikua nahakikisha nna internet bundle muda wote ,so siwi mpweke,na kaz nikiona inanishinda nilikua natafta mtu wa nje anifanyie namlipa imeisha hiyo(sasa unakuta kuna mtu anajua kaz fulan siimudu ntamfata lakin hanioni nikimfata ,alikua anaumia sana,coz zaman nlikua najipendekeza kwake anisaidie nikaona ameanza majungu na dharau ,hakuamin macho yake nilivyombadilikia no shobo ,na sikuwah kumfata tena mpaka naondoka kwny ile office,mpaka wenyewe kwny vikao wanaanza ooh fulan huwa hasalimi,yuko busy na mambo yake had boss mwnyw,so nlikua nasema mtu km unataka kunifukuza nifukuze sio kunitisha ,na kaz nafanya kwa bidii ,hivyo yaan no kuabudu mtu or kujipendekeza just work hard,na fata sheria na taratibu za hapo,wakikufukuza sio mwisho wa maisha alaaa,

Sent from my FRD-L19 using JamiiForums mobile app
 
SAsa hiyo ndiyo maana halisi ya ofisi . Jipongeze kuwa sasa una uhakika kwamba umeanza kazi.
 
Tongoza demu mbovu kuliko wote hapo ,huyo ndo atakupa kampani mpaka uzoee magumashi ya ofisi za kiafrika
 
A very bad beginning
 
Umechafuliwa nyota mkuu
Nicheki nikupe namba ya mtaalamu akusafishe nyota Kila mtu atakupenda wewe.
Sio Kila mtu anafurahia uwepo wako hapo kazini ila ndio maaana unaona mambo magumu

Changamka ndugu Yangu maisha sio lelemama
 
Una wiki mbili kazini, ni kwamba bado upo katika kipindi fulani cha kuoneshwa mazingira na jinsi ya kufanya kazi, au sivyo?
 
Hapo ndo tatizo linapoanzia siku zote boss huwa anataka kuona wafanyakaz wake wako busy muda wote,jitahid kufanya time management na usipende sana kufanya kazi harakaharaka hata Kama ni rahisi ilimradi usitengeneze mazingira ya kuwa idle,fanya kazi zako kwa ufanisi jiamini automatically tu boss ataanza kukuamini,maana nyie watoto wa sikuiz hamchelewi kucheza Hadi rede mkiwa kazini ilimradi tu unajiona umemaliza kazi icho ndo kitu maboss hatupendi!
 
VITA BAADA YA KUPATA
Shida inaweza isiwe wafanyakazi wenzio, shida ni wewe na mizimu/ Wachawi ...

Kuna mipaka ya mafanikio kwenye familia yenu, sasa ndio maana ukipata tu vita inaanza ....

Pia una Roho ya kukataliwa...

Cha kufanya hapa...

Omba Toba na rehema ya kwako na familia yako
1.Kutoa sadaka ya shukurani ya kupata kazi kanisani ili kuweka ulinzi ktk kazi yako...

2. Omba Kibali

3.Toa Kila fungu la kumi la mshahara kanisani...
 
Mkuu hiyo Hali Kwa Nchi za ulimwengu wa tatu hasa Tanzania ni kawaida.

Maofisini Kuna chuki mno, usitarajie upendwe mahala pa kazi. Mimi nilipitia hiyo Hali, Ila niliweza kupita salama.

Cha muhimu Hapo ni ww kufanya kazi katika ubora wa Hali ya juu. Yaani ufanye kazi Kwa 200% . Jiamini, usiongee Sana Wala usipende kutafuta huruma Kwa watu.

Fanya kazi zako Kwa umakini na ubora, Acha juhudi zako ziongee.

Mimi nilifanikiwa kupitia kujituma Sana. Hatimaye nikapandishwa cheo na kuhamishwa Mkoa mwingine.

Komaa Mkuu.
 
Mkuu, hata mchangiaji ukipotosha lazima tukurekebishe. Haifai tukuache na ujinga wako upotoshe na wengine [emoji28]
Hizi mkuu mkuu unazoandika kwa mtu anaekutemea shiti ni uoga na kujipendekeza vile vile.

We piga bati uendelee na comment nyingine. Kuna mademu wana stress za VICOBA humu, wanaweza kukushambulia kwa kuwasilimia tu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…