Kama shida ni nyumba nenda mahakamani mkuuHatujawasiliana toka aondoke kesho anafunga mwezi,
Namshukuru Mungu sasa hivi wala roho yangu haiumii tena, nimeshamwona taka taka, na kusema kweli na mchukia vibaya sana, usiku na mchana naomba asirudi maana sijui ninaweza kumfanya kitu gani
Ameshanitamkia kuwa yupo hapa kwa ajili ya nyumba tu sisi mimi,
Ameshanitamkia mpaka tugawane vyumba,
Hivi huyu shetani tumemkosea nini sie wanadamu?! Huyu bwana bifu lake si na Mungu?! Sasa kisa cha kutuandama wanadamu ni nini wakati yeye bifu lake ni na Mungu Baba?! Hebu angalieni. Kutokana na stori kuwa lirefu sana ikafika wakati nikaamua nisome kwa haraka haraka (kuperuzi) na kwahiyo baadhi ya mistari nikawa nairuka. Sasa shetani alivyo mwanaharamu, nilipofika kwenye quote hiyo hapo, paragraph ya kwanza sikuiona na badala yake macho yakaenda kutua palipoandikwa " Wakati watu wengine wamelala, mimi nikapata viwili." Eti shetani akaniaminisha "ukapata bao mbili za chapchap huku raia wakiwa wamepiga mbonji! NIkajua ni bao zetu zile kupitia ulaji tunda kimasihara! Swali lililopita kichwani fasta fasta ulikula tunda kimasihara na kupata 2 chap chap kwa mazingira gani! Ehee! Naanza kusoma tena kumbe ulipata viwanja viwili!!Sasa ndio kawa Mke , na watoto ndio hao, haraka haraka nikaanza kutafuta kiwanja, Bahati nzuri ni msomaji mzuri wa magazeti nikaoona viwanja vya serikali vinauzwa huko,
Wakati watu wengine wamelala, mimi nikapata viwili. Ikabaki kufuatilia hati, na kwa sababu ulikuwa ni mradi wa kimkakati, hati zilitoka mapema tu, lakini kwa jina langu mimi.
Jamaa eti anafosi mchepuko tuuite mke[emoji38]SIO MKE WAKO MKUU
NA NI KWELI KWA HAYA MATUKIO SIJUI HATA NGUVU YA KUMUITA MKE UNAIPATA WAPI!!!??
KUZAA HATA PANYA WANAZAA (MNISAMEHE WANAWAKE WENZANGU)
[emoji2307][emoji2307][emoji2307]Sasa baada ya kupokea lile fungu la kwanza
30m, mimi haraka sana nikaenda kupunguza madeni yangu, hata hivyo Hays kwisha,
Na yeye nikamwita kwamba tukae chini ili ile 15m yake tuipangie matumizi ya kwanza kabisa,
Ushauri wangu ilikuwa tununue kiwanja kwanza,
Sehemu ambayo sio ghari sana, Hapo sasa ndio kimbembe kilipoanza,
Ila kufupisha story nilimwambia basi wewe unataka tuanze na nini? Akanijibu hiyo pesa anataka afanyie biashara wakati ujenzi unaendelea, nikamwambia biashara mbona tumefanya na tunasnguka, hata hivvyo sio mbaya wewe kutaka kufanya biashara lakini ni bora tuwe na kiwanja kwanza.
Kusema kweli zogo lilikuwa kubwa ananipayukia na mimi natumia ubaba wangu sasa kulazimisha, ndio alipoamka kwenye kiti(tulikuwa tumekaa nje na watoto wanacheza hapo nje).
Alichoniambiakwa sauti kuu na kali ni kwamba
TOKA HAPA NA VISENTI VYAKO UNAVYONIPAGA,
Du ! Leo naambiwa visenti, yaani huyu mwanamke nimekopa pesa, nimempeleka ufundi cherehani, nimemfungulia saloon , grocer, mghahawa, dala dala, mtaji wa kuku wa kisasa.
Anaanguka namyanyua, anakopa vicoba anashindwa kumaliza nammalzia,
Nalipa watoto karo kwa mwaka jaribia Mil 6 na bado watoto ndio kwanza wanasafari, kwa nini ananivunjia heshima namna hii?
Kusema kweli sikujua kama niliokota jiwe au mti au ufagio, nimpige nao akawahi kukimbia, na mimi nikaanza kumfukuza, kama sijamrushia kila kitu ambacho mpaka leo sikijui, nikaanguka chini, yeye akaendelea sijui wapi , kusema kweli sikumwona,
Kuangalia nyuma naona watoto, kumbe na wenyewe wakawa wameshika mawe wanataka kunipigia nayo, nikaamka ili niwafukuze nikaenda chini tena , sasa hapo ndio nikaanza kusikia maumivu, na watoto wale kule wamesimama, sasa na wenyewe wanapaza sauti,
KWA NINI UNAMPIGA MAMA YETU SI UENDE KWENU!!!!!
Nitaendelea
26, sep mwishoni,
Mahafari ya mtoto Dar ,
A
Nasikia kaja lakini kaenda moja kwa moja kwa rafiki,asubuki saa nne nipo, mala nawaona wanakuja, nilienda na rafiki yangu mmoja wa kazini,
Wanafika wote wananipita bila kunisalimia,
Mimi nawasalimu kimya,wamekuja na vyakula vya mtoto na keki,
Hahahhaha[emoji16][emoji16][emoji16]namba yako ninayo utani hadithia whatsaap [emoji16][emoji16]
Kwa nini asimwachie tu hiyo nyumba, bimdo mbona kashatapanya zaidi ya hapo nyumba ni nini?Kama shida ni nyumba nenda mahakamani mkuu
Fanya urudi kwa bi mkubwa
Acha ujinga wewe, kama hii story ni ya kweli, mwachie nyumba na uhame jumla afterall hata mabinti wamekususa.Kusema kweli kama sio kukomaa mpaka sasa hivi ningekuwa nmeshamwachianyumba kwa vituko alivyonifanyia,
Kinachonitia wasiwasi huyo bwana ambaye wanae, kwanza alimwoaga binamu wa mke wangu, wakaachana baada ya bwana kumfumania mke wake na bwana mwingine,
Jamaa alipiga mwanamke karibu aue, haikutoshaakamfuata mwanaume na kumchima visu na kukimbia kijiji, amerudi juzi tu, huko
Kwa hiyo jamaa ni mshari wasiwasi wasije kuunda njama wanipotezee uhai,
Ila Mungu ameendelea kuwa na mimi,
Nimeshaenda kutoa taarifa polisi,
Hivi mzee wangu unachofosi kwa huyo bi mdogo ni nini? Kwani si una mke wako mzuri tuu nyumbani? Si muachane kwa amani tuu kila mtu ajue hamsini zake?Hivi ninavyoandika hapa, tuligombana sana mpaka kumtupia nguo zake na vitu nje, hiyo ilikuwa tar 4 mwezi huu,
Kisa nilishachoka kuondoka bila kuaga, sasa anasema amekodi mashamva huko moro, aliniaga anaenda nikamkatalia, akaenda kwa nguvu, alivyorudi nikamfukuza, na ugonvi mwingi mpaka watoto wakachangia kunitamkia maneno machafu,
Majirani wakaja wakawaombea, nikawaruhusu waingie ndani, tar 9 Jan yaani siku 4 tu toka nimkataze kwenda moro, kaenda tena bila ruhusa yangu,
Hajarudi mpaka leo,
Ila juzi nilipata taarifa ameonekana anatelemshwa Na gari ya jamaa ambaye nilishamtuhumu kuwa ana mahusiano naye kimapenzi, na hata mwezi wa 11 mwaka jana nilifuma message yake akimwalifu tayari yupo Dar
Nikaamua kumpigia simu huyo bwana nakamkoromea kuwa anaharibu famlia yangu akakataa
Baadaye ni kamuuliza bi mdogo huyo bwana anafanya shughuli gani akasema hafahamu,
Baada ya kuulizia nikasikia baba yake kastaafu kazi ya ualimu kamfungulia duka la nguo,
Hapo nyuma huo mwezi wa kumi na moja mke wangu alinionesha vi tisheti vitatu vipya na kitenge kuwa kanunua kumbe jamaa alipokuja Dar alimhonga
Mwachie nyumba, si ana watoto?Huyu mwanamke simtaki tena, lakini naona kama anawapambe,
Nipeni ushauri wapendwa,
Maana ninachokiona siku moja huyu mwanamke anaweza rudimentary hapa kwa gia ya watoto
Haufi bwana ila utavumilia tuNaam kwa mfano nikiwa na manzi ananisumbua nafungua Uzi Kama huu nasoma comments za wachangiaji najua lazima nitapata majibu ya Nini Cha kufanya halafu nachukua huo ushauri nakwenda kuufanyia kazi katika matatizo yangu ..lakini sio eti Mimi nije nifungue Uzi humu [emoji16][emoji16][emoji16] watu humu mnavyo chamba sisi wengine tuna mioyo midogo nitakufa kwa pressure [emoji16][emoji16][emoji119]
Mzee akifanya hivo ataonekana mwanaume suruali ila kwa vile nyumba ina majina yake mbona anaweza ipambaniaKwa nini asimwachie tu hiyo nyumba, bimdo mbona kashatapanya zaidi ya hapo nyumba ni nini?
Huyu mzee sioni kama anahitaji ushauri, picha liko wazi kabisa kwamba mchepuko hamtaki tena ila yeye ndio anafosi kingi tuu.Naomba uniambie kaka unahitaji tukushauri kitu gani?
Kuhusu mimi nimeshaamua huyu mwanamke simtaki lakini wasiwasi wangu ni hii nyumba?Bado hujasema kaka unahitaji ushauri gani kuhusu wewe au shemej
Nyumba ni ya watoto mkuu hakuna Cha kuifanya au haina jina lako?OMBI WAKUU NA USHAURI
hii nyumba niifanye nini, ni nyumba kubwa,
Ipo kwenye kiwanja cha eka moja,
Eneo ni ni zuri sana, sasa hivi nyumba ni nyingi, lakini ya kwangu kila mtu anaitamani,
Ila bado haijaisha,
Madilirisha nilishaweka ya aluminium bado matatu tu ya dining room