Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

kuna wapumbavu wachache wamebahatika kusoma na kupata kazi bila kukaa mtaani

mahusiano ndo wameanza basi wanahisi wamemaliza kila kitu

mtu hata kulogwa hajawahi unategemea atashauri nn
 

With all due respect; hata tuipambaje hakuna siku mke akawa na thamani sawa na mchepuko. Tena kumuita mchepuko ni tunapunguza tu ukali wa maneno/kiubinadamu, ila Kibiblia anaitwa "KAHABA/MALAYA" Huku mke anaitwa "KITU CHEMA", na mke mwema anatoka kwa BWANA.

Mithali 18:22
"Apataye mke apata kitu chema; naye apata kibali kwa BWANA".

Mithali 23:27
"Kwa maana kahaba ni shimo refu.....

Mithali 6:26
"Maana kwa malaya mtu hutiwa katika hali ya kuhitaji kipande cha mkate; Na kahaba humwinda mtu anase nafsi yake iliyo ya thamani".

Na mbele za Mungu kuna agano la ndoa tu; hakuna agano la wazazi wenza. Hata uzae na mtu watoto 100 na huku mkeo hujazaa naye hata mtoto mmoja; bado mkeo atabaki tu kuwa mke. Ndiyo maana hata Hajir pamoja na kuzaa mtoto na Ibrahim ilihali mkewe Sarah hajamzalia, bado thamani/heshima ya Hajir haikupanda akaitwa mke; aliendelea kuwa kijakazi tu. Tena afadhali hata ya mtu ambaye mlizaaga huko ila hamkufanikiwa kuzaa; huyo tutamwita mzazi mwenzako. Lakini ya kwenda kuzaa na mume wa mtu utaitwa kahaba tu period. So haiwezekani, in this life and the next, mke na mchepuko wakawa sawa.

Malaki 2:14
Lakini ninyi mwasema, Ni kwa sababu gani? Ni kwa sababu BWANA amekuwa shahidi kati ya wewe na mke wa ujana wako, uliyemtenda mambo ya hiana, angawa yeye ni mwenzako, na mke wa agano lako"

Sasa mtende mke wa ujana wako; useme kisa unafanya kwa "heshima" humuonyeshei basi ni sawa tu. Lakini sio sawa at all, na utalipia gharama yake

Ndoa na iheshimiwe na watu wote; vivyo hivyo na Mke

N:B Sijacomment ili kumtia unyonge baba wa watu na mkewe mdogo; nilikuwa nasahihisha tu ulichokiandika. Mke sio sawa na mchepuko. Ukiona huwezi kumfanya binti wa watu mke; muache akae asubiri mumewe.
 
Hahah nimejifunza mengi, na kuelewa, ila na nyie fanyeni kazi acheni kutega madanga.
Mimi sitegi madanga kwa kweli nasema mnyooshwe kabisa Hadi muwe vichaa wanawake huwa mnatuchukulia poa eeeh shauri yenu, kuweni makini jamani sasa huyu mzee pressure inaweza muua ikasingiziwa corona inaumiza Sana kutendwa utu uzimani oooh, dah Mungu waepushia kaka zangu na huu ujinga wallah
 
Dah.. hata kukulaumu siwezi... maskini. Huyu dada nimeamini ni shetani
 
Kweli kaka usemacho.Humu sometimes wengine watatumia hyo km fimbo kukuchapa ktk baadhi ya maeneo yaani badala ya msaada au wengine wajifunze wanaishia kukunanga mpk baasi
Humu kuna majitu yanajiona malaika mnooo na wao ndo wamekamilika.
Mimi bado namuonea huruma huyu baba mnooo!sijui kwa nini!

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Mkuu nimefuatilia tangu mwanzo kimya kimya na ninaweza kusema machache kama ifuatavyo;
1. Katika mtiririko wa story yako ulisema uanonyesha una maisha ya huzuni sababu ya purukushani za mke mdogo, lakini bado unatuaminisha mke mkubwa hajui kitu. Hii inatafsiri moja kuwa inawezekana hata kwa mke mkubwa pia mambo sio mazuri ndio maana hakuzingatii kuijua saikolojia yako. Kumbuka awali ulisema mlikuwa na mizozo kabla mama mzazi hajakupa ushauri kiaina utafute mchepuko mbali na pale.
2. Mwishoni unakiri kuwa hii nyumba inayokunyima amani ina thamani karibu 300M endapo utaamua kuiuza,hata kama ukiamua kugawana na mke mdogo utapata karibu 150M na ukaanza maisha yako mazuri bila karaha za bi mdashi. Maisha yangu yote nimekuwa nikiamini amani ndio kitu namba moja kwenye maisha ya mwanadamu.
3. Niwakati muhimu kuwaunganisha wanao wajuana na automatically mzozo unaweza kuisha maana watakusaidia mawazo kuliko hapa JF kuliko na wajuaji wengi wapotoshaji.
Asante sana
 
Well said bro

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Usikariri pia kwa kua mitala haina Amani basi ndo kote ,wapo wenye mitala na wako poa kama hao wenye single wife wanavoishi kwa amani pia.Sio kila mitala ina shida ndani yake

Sent using Jamii Forums mobile app
KWA hizi ndoa za kina darleen na mzee Yusufu kwa kweli hzo ndoa tuwaachie waswahili ndoa miezi talaka na ugomvi juu daily kwa kweli hongera zao
 
Amen

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Nimependa hapo mwishoni, mara moja moja basi uwe unakuwa mpole.
 
Baasi watoto wakubwa na mke wanajua kama una mke mwingine ndugu [emoji3][emoji16][emoji16][emoji16]ila mama mkwe jamani ,hawa wamama zetu unalala kwa bimdogo ambae hajulikani.Ndugu wa mume shikamoooni aseehh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Woow[emoji7]

So many congrats brother. Much respect to u. Hongera sana sana sana. Umeepuka shari kubwa. Hakujawahi kuwa na usawa asilani katika ndoa ya zaidi ya mke mmoja. Na shetani akupitie mbali.

That was so deep.
 
Yaani wananichekeshaga, kwa kujifanyaga victims sasa utafikiri huwa wanashikiwa bunduki.

Mabalaa wanayafukunyua wenyewe, yakiwafika kooni lawama zooote kwa wanawake. Sasa Mungu sijui aliwapa akili za kuvukia barabara[emoji2297][emoji2297]
Wanajikutaga wao malaika. Hawakosei ndo maana makosa yote wanatupia kwetu
 
Tena shikamoo yao kubwa; wanasubiri siku za misiba (God forbid), ndiyo watoa taarifa wakuu. Sio kwa surprise hizi kwenye misiba ya siku hizi
Baasi watoto wakubwa na mke wanajua kama una mke mwingine ndugu [emoji3][emoji16][emoji16][emoji16]ila mama mkwe jamani ,hawa wamama zetu unalala kwa bimdogo ambae hajulikani.Ndugu wa mume shikamoooni aseehh

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Bado unampenda mmnooo tena sana si rahisi km unavyodhani kumtema.Unamchukia kwa kua unampenda

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…