Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Itakuwa hv:

Bi mdogo baada ya kuona nyumba imeuzwa na status yake mtaani kwa washirika kuonekana km imeshuka hv, basi atataka kumharibia Mzee Kwa bi mkubwa.

Pia, watoto wake aliozaa nao watatumika vilivyo na bi mdogo.

Mzee Baba kiuchumi utakuwa umeyumba mno mno na bi mdogo hatakuwa na uvumilivu wowote kwako

Suala likifika kwa bi mkubwa litakuwa suala la Moto sana infact bi mkubwa atakuwa disappointed SANA.

Familia ya bi mkubwa hasa watoto na Jamii nyingine iliyopo kwenye circle yako itakuwa disappointed mno.

Washkaji, ndugu na jamaa wengine watakuelewa tofauti at the end life goes on

Warren Buffet aliwahi kusema "....it takes 20 years to build reputation but it takes one minute to ruin it...."

Kwa minajili ya kujifunza kwa vijana wachanga kimaisha, Je nini kilipaswa kufanyika kabla kisa hakijafika hapa? Tusubiri mwishowe wa kisa, tuone


Ushauri wetu kwako ni upi? Ni hekima na busara kusubiri mwisho wa kisa kizima, lkn haya matatu hayana conditions:

One,
fight for bi mkubwa regardless

Two,
fight for your kids (wote wa bi mdogo na bi mkubwa)

Three,
Achana na bi mdogo akatafute maisha yake mengine, tena asitake mazoea na wewe

Tunaendelea kufuatilia kisa!
Ahaaaa nacheka kama mazuri ila najiuliza wanawake wengine hii bahati wanayochezea hivi wanaitoaga wapi?.huyu dada kinachofata ni majuto. Ulosema yote yatatokea soon
 
NAENDELEA,

Kumbuka hapo tayari tumeshaamia kwenye nyumba yetu (YETU) na baada kama ya miezi sita niliingiza umeme ambao ulinigharimu kama 400000 wakati huo ( nguzo 2)

Mkuu naona kama ni rahisi kutabiri mwisho wake, all in all andika kila kitu ili moyo wako ushushe huo Mzigo ulioishi nao kwa muda mrefu hakika utapata ushauri, ila narudia tena wanaume ehhhh njia kuu ni suluhu ya magonjwa ya moyo, hivii vimchepuko vina tuendesha sana, nilishakataa kuyajenga na mchepuko, mchepuko ni wa kuwaona kama sumu maana ni parasite hawana chochote kwako
 
Yaani wanaume tumeumbwa mateso kuhangaika, kwanza hapo huenda hata hao watoto wa bi mdogo siyo wake, [emoji23] [emoji23] [emoji23] [emoji848] namuwazia tu mwanaume mwenzangu
Unataka kumuongezea presha
 
Watoto wake sasa ndio wamemaliza la saba, nikawatafutia shule nzuri huko kanda, nauli kwenda tu ukihumuisha vikorokoro vyote tokea hapa mpaka afike shule kwa mmoja sio chini ya 200000, bado ada ambayo kwa mmoja kila baada ya miezi 3 ni sh500000 na mwingine kila baada ya miezi 3 ni 450000, na wakirudi unatuma pesa kama 100000, kwa mmoja...
Pole sana baba. Kwa ufupi wewe na mke mdogo soon mtaachana. Ila kachezea bahati sana atajuta atalia kwa uchungu.
 
Kipindi nipo nipo kikazi nje nilikuwa nikimtumia pesa ya matumizi kupitia rafiki yangu wa kazini, ambapo kila baada ya muda alikuwa akienda kuchukua pesa ya matumizi...
Unawezaje kufanya mambo makubwa hivyo mke wako mkubwa hajui, ila mkuu ulitolewa ufahamu kabisa
 
Kipindi nipo nipo kikazi nje nilikuwa nikimtumia pesa ya matumizi kupitia rafiki yangu wa kazini, ambapo kila baada ya muda alikuwa akienda kuchukua pesa ya matumizi...
Unawezaje kufanya mambo makubwa hivyo mke wako mkubwa hajui, ila mkuu ulitolewa ufahamu kabisa
 
Babamdogo pole na stress za dunia
Acha kijana wako nikushauri ..

- Kama bi mdogo ushamuona Ni waruwaru tafadhali hyo pesa ya nyumba asihusike nayo hata kidogo Kama ni kumumegea mpe kidogo ambayo inamfaa kulingana na akili yake uinovyo.

- Tambua Sasa huu ndo wakati wa bi mkubwa atajua ukweli wote kuhusu bi mdogo hapo patachimbika Kuanzia kwa bi mkubwa Hadi watoto wako wa bi mkubwa ..! Je Ni kwa nn nakwambia hyo hela uliyouza nyumba bi mdogo asihusike nayo?? Kumbuka apa umetangaza Vita na nyumba ya bi mkubwa Ni Bora uingie vitani ukiwa na hela kuliko kuingia vitan hela Ni kumlika kwa tochi..aisee utaona kila rangi ya dunia na kumbuka kwa Sasa kimbilio lako Ni kwa bi mkubwa huna namna Kama nyumba ushaipa mkono ..

- Tengeneza zengwe kwa bi mdogo punde installment ya mwisho ikiingia ili uachane nae kabisa

- Nikufungue macho hayo majarbu ya kipesa nk. unayopitia Ni kwa sababu ya huyo bi mdogo anakushusha chin badala akupandishe ..miradi mingapi umemfungulia na yote inabuma hujiulizi kitu apo?

- Mwisho Kama we ni wale wanaume mnadata na wivuu wa kiwango Cha SGR hamtaki kukubali Mambo basi Ushauri wetu Ni bure tunachangamsha genge

Sent using Jamii Forums mobile app
 
Baada ya ujenzi kusimama na matumizi kuwa makubwa, nikamgusia bi mdogo kuhusu kupiga bei kila kiwanja cha pili, kusema kweli kile cha pili kilikuwa kinafahamika kwa bi mkubwa, kiujumla kilikuwa cha kwake, lakini kwa sababu naye ujenzi wa nyumba yake ulikuwa umesisimama nilimshawishi mpaka akakubali tukiuze, nikimwambia mikopo kazini imebizidi kimo, kwa hiyo nusu, nimpigie plasta na mambo mengine kama umeme na maji, akakubali
Aisee
 
Mkuu story bado inaendelea !?
Hata robo bado ndugu yangu wewe una
Una lako jambo! Huchomoki! Umenasa!

Bi mdogo anasubiria mgao wa kikokotoo.

R.I.P Mengi R.I.P Dr P Ng'wandu.
Hakuna jipya chini ya jua!
Jasiri haachi asili, huna cha kufanya!
Utafanya vile atakavyo bimdogo, COZ unataka kuonyesha uwezo wako kummudu na kummiliki!

Everyday is Saturday............................... 😎
wewe mawazo yako mtu akiitwa Bi mdogo basi lazima muwe mmepishana 30 au arobaini,

Hivi nimesema niko 50s na ndio kwanza imeingia na yeye yupo 42, hiyo tofauti ya miaka inaweza lingana na Mar Mengi au Ngwandu, mbona tena mimi naona nakuwa kijana sana zaidi,

Wakati nampata yeye yupo 20s , na ni 20 kweli, mimi nipo 28s na mke wangu wakati huo alikuwa 25,
Wakati mwengine am
Anza juu kwenye story ndio uchangie,

Halafu ni true storynimeomba msaada watu wanisaidie nilipo kengeuka maana mimi ni binadamu, makosa yapo, lakini a kujifunza kupo.
 
Mkuu pole sana,ushauri wangu mke mdogo mtoe katika mahesabu kabisa ila watoto wawe kipaumbele usiwaache kwani kulea mabinti siyo kazi rahisi. Baada ya hapo usiku na mchana sali Mungu akupe uwezo wa kuunganisha hao watoto wawili wa nje na familia yako kubwa. Narudia tena mke mdogo achana nae,ningekuwa wewe hata kulala nae ningeacha atakupa maradhi mzee wangu.
 
Watoto wake sasa ndio wamemaliza la saba, nikawatafutia shule nzuri huko kanda...........nauli kwenda tu ukihumuisha vikorokoro vyote tokea hapa mpaka afike shule kwa mmoja sio chini ya 200000, bado ada ambayo kwa mmoja kila baada ya miezi 3 ni sh500000 na mwingine kila baada ya miezi 3 ni 450000, na wakirudi unatuma pesa kama 100000, kwa mmoja

Sio kwamba nina pesa nyingi kiasi hicho lakini waswahili wanasema maji ukishayavulia nguo huna budi kuyaoga,

Sasa umeshawaingiza huko inabidi tu waendelee na mimi meenyewe umri ndio nnasogemea, na kustaafu Ndio huko kunapiga hodi,

Vijana huko makazini ndio kila siku wanakuuliza ‘utastaafu lini ‘ wakikuona unakopa hata sh 100000 wanakushangaa kweli, maana wanajua una mabillion bank,
Hata ukiwaambia jamani nasomesha, wanakuuliza mpaka sasa hivi una somesha tu? Ee ulichelewa kuzaa, na anayekuuliza hivyo ana miaka 30 hata mke hana, sasa anafikiri mpaka apate mtoto wa 3 tu atakuwa na umri gani?
Mpaka mtoto wa mwisho amalize chuo,

Mimi sasa mwaka kesho mtoto wa tatu anamaliza chuo, na nitakuwa na 51 Mungu akijalia huyu wa form 4 naye amalize chuo nitakuwa na 55, sio mbaya sana

Ok
Sasa pesa ndio hiyo imepotea kwenye kuku,

Wazo lililoniijia haraka baada ya kutafakari sana ni KUPIGA BEI ILE NYUMBA,

Sasa nitamshawishi vipi mwenzangu? Ikawa sasa ni ishu.
Ukitilia maana pale ameshakaa zaidi ya miaka kumi, na ameshajenga mtandao wa kutosha na akina mama wenzake wenye nyumba na kulinga juu,

Ila sasa kabla ya yote hayo kuna mambo yalikuwa yananiudhi mimi binafsi mpaka nikawa naona wazo la kijana linapata nguvu, alikuwa anapenda sana kusifisifia nyumba za watu, kuanzia nyumba imeisha vizuri, ina garden, mala gari nzuri, ingawa hata mimi nilikuwa na gari ya kutembelea baadaye nikaipiga bei,

Mala watu wanamsema kwa kuwa yeye ni binti mdogo kwa nini anakubali kuwa nyumba ndogo, na hivyo vyote ananieleza,
Mimi nikawa namjibu wewe angalia familia yako, kama ni watoto unao, kama shule nzuri hata watoto wako wanasoma shule nzuri, wakati meingine hata kuwazidi wakwao, una as vizuri, mimi nakupenda, unakula vizuri, na hili la kula kuna hata ndugu waliolewa kabisa makanisani , wakija kumtembelea pale Ndio huwa kipindi cha kubadili mboga,

Sasa nikiona amezidi namuuliza niambie hapa wanaokusema wewe, alivyonitajia mpaka nikashangaa, mmoja mme kwa mwaka anakaa hapo nyumbani kwa wiki mbili tu, mwingine mmewe alishafariki muda mwingi yupo baa, mwingine na mume wake wapo wanauza genge la nyanya pamoja,
Watoto hata nguo za kushindia shida,
Mwingine kila siku na mumewe ugonvi, sasa namuuliza wanakuzidi nini hao mpaka uumie na maneno yao,

Nikamwambia PENDA MME NA WATOTO WAKO, hayo mengine ni mwembwe tu za hapa duniani, maisha ni wewe mwenyewe unayachukuliaje, ukiwa wanazidi waambie mimi nampenda huyu huyu.

Lakini nikaona tena yanazidi, mala mume wa mama fulani anasema wewe mbaya sana mbona umekutana naye bars Arabia hukumsalimia, nikamuuliza mbona yeye hakunisalimu, hata hivyo kama ni yule mimi nimemzidi umri yeye ndio alitakiwa anisalimie, lakini hili sio tatizo, kumbe huyo bwana kaniona njiani narudi nyumbani usiku wa 3 mimi akili yangu yote ipo nyumbani,

Nikamwambia ukionesha dalili ya kunidharau hata hao watu watatudharau,

Ila kwa ufupi, yule aliyekuwa na nyumba nzuri na garden sasa hivi yupo gerezani, yule mama mmewe wanaonana kwa mwaka wk mmewe kafariki, yule chapombe naye hatunaye, wale genge ni choka mbaya majuzi nilipita huko,

Hizo taarifa kila alipokuwa akinipa nikawa na Namuuliza umejifunza nini hapo kuhusu maisha,
Lakini haelewi kitu,

Maamuzi niliyochukuani kuuza nyumba na kama nilivyowaeleza hapo mwanzo kile kiwanja kilikuwa eneo linalolipa, kwa hiyo sikupata shida kuuza, na kwa kilikuwa kimeendelezwa sana, kuanzia nyumba kubwa iliyoishia lenta, ile nyumba ya nyumba vitatu tuliyokuwa tukiishi, pamoja na Banda kubwa la kuku, na eneo kubwa tu Kinabalu kwa ajili ya garden na parking hata ya gari ndogo 6

Baada ya yeye kukubali lakini kwa mabishanomakali ,

Tulimpata mteja wa 80M lakini kwa malipo ya 40M kila baada ya miezi 2

Hiyo ilikuwa 2016 November, na ilitakiwa baada ya miezi miwili baada ya kukamilisha malipo tuondoke, ambayo ingekuwa ni April 2017

Kwa ufupi mteja alikuwa muungwana sana,
By December malipo ya kwanza yalikamilika (40,000,000) CASH

nini kilitokea, kumbuka nilikuwa na madeni yanayokaribia mil 15M,
Hapo nyumba imeshauzwa na bado installment 1 ambayo by February lazima ilipwe na sisi tuwaachie wenye nyumba yao, maana sisi hatuna chetu tena, nikama tunarudi kwenye kile chumba kimoja,

JE WEWE KAMA BABA UTAANZA KUFANYA NINI?
Kumbuka kuna katabia fulani nilianza kukaona kwa mke wangu, hasa hasa ka kunidharau na kuwa karibu na vijamaa jamaa.

Na hata wakati mwingine kama simpigii simu anaweza kukaa hata siku nne bila kunitafuta

NGOJA NIONDOE MACHUNGU
ENDELEENI KUNIOMBEA
Pole sana mkuu
 
Back
Top Bottom