Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Naomba ushauri: Miaka 18 iliyopita niliingia kwenye uhusiano na ‘Bi Mdogo’ na kuzaa naye watoto 2

Sasa kabla ya hapo, mwezi huo huo wa December 2016,
Nikaanza kupata taarifa ambazo sio nzuri,
Na aliyenipa hizo taarifa ni mtu wao wakaribu kwenye familia yake,

Siku niliona simu inaingia kwangu, yule bwana nikaona ananisalimia lakini kama kuna kitu anataka kunieleza lakini anasita, baada ya kusalimiana akakata simu, dk 5 tena akapiga, nikaona tena anasita, nikamuuliza vipi ndugu yangu una tatizo, au umekwanma sema tu sisi ni wanaume matatizo tumeumbwa nao,

Huyu bwana tumuite baba M,

Baada ya kusita kidogo, akaniambia, bwana mbona naona kama mkeo ananunua vitu mjini na kuhifadhikwa mdogo wake,?

Nikamuuliza vitu gani hivyo, na kwa nini ahifadhi huko wakati nyumbani kwetu na kwa huyo mdogo wake hakuna umbilical wowote, hata nauli ya Bajaj kwenda hapo nakuja kwetu ni sawa tu
 
Unajua hapo penye chuki ulikuwa hujamuelewa mleta mada, alikuwa akimaanisha kumwelezea bi mdogo kuwa tamaa alizokuwa akiona kutoka kwa wenzie na maisha mazuri ndo yaliyochangia kumfikisha hapo alipo.

Nadhani hapo ilikuwa ni tafsiri tu ya paragraph.

Ok, tuyaache basi hayo yote, tuendelee na mada.
Asipende kujumuisha Mambo aisee. Loooh
 
Wewe Cariha kweli una shida sehemu flani. Mbona jamaa yupo general sana kwenye hii comment yake. Hii comment yake haijakulenga wewe, alikuwa anaongelea in general attitude ya wanawake.
Wewe ndio una shida alivomaanisha na Mimi nimemjibu in general kwanini mje kunishambulia acheni unafiki aisee, hafu sio kila mtu ana mawivu na kutamani Jambo flani sio dhambi mbona hata yeye alichepuka na mchepuko unamsumbua tu.
 
Akanijibu hata wenyewe wanashangaa ila walidhani mimi nafahamu Na namna vinavyohihifadhiwa hivyo vitu ni kama kwa kificho,

Baadaye ndio akatoa ukweli wake,
Kwamba ameona magodoro Mawili ya 7/7
Na mashuka yake kila shuka sijui 200000 ,

Na vitanda viwili na mablanketi ya bei mbaya vilevile mawili,

Na makorokocho mengine,
 
He seems to be a good person despite his past mistakes, sijui kwa nini watu wanaojali na wazuri huishia kukutana na mambo mabaya, maybe ni balance ya nature, Mungu amvushe katika mtihani wake huu.

Huyu bwana ni muungwana sana, nina uhakika hata mkewe mkubwa akimsimulia hii atashtuka mwanzoni ila akifikiria sana atamsamehe tu. Ni makosa ya kibinadamu na kuwa mtu mwema ndio yamemfikisha hapo, muhuni angesha mtosa huyo bi mdogo long time, bila hata kujali watoto wala nini.
 
Wewe ndio una shida alivomaanisha na Mimi nimemjibu in general kwanini mje kunishambulia acheni unafiki aisee, hafu sio kila mtu ana mawivu na kutamani Jambo flani sio dhambi mbona hata yeye alichepuka na mchepuko unamsumbua tu.
Please basi, funga hiyo kitu.
 
Mimi bwana hata sitaki kukuelewa baba yangu. Nisamehe bure. Sijaitambua imani yako mpaka sasa inayoruhusu wewe kuhalalisha MCHEPUKO kuitwa mke. Kwangu atabaki kuitwa MCHEPUKO tu. Mke gani anafichwa kama gunia la bangi.

Halafu mzee wangu katika calculations zako naona kbs umeshapiga hesabu jinsi mambo yakishabumburuka utakavyoanza tengwa maana unatolea mifano hai ya wanafamilia jinsi wamtelekezwa na familia zao wamebaki mama na watoto zao. Binafsi siwezi kukutenga kabisa hata ungekua umetutengaje.

Nikusifie kabisa katika wababa na wewe ni baba. You seem to be a very nice man, friend and father. Nachosikitika akiguswa MCHEPUKO unafura tu.
Nionacho.. MCHEPUKO WAKO NI FUNGU LA KUKOSA. Na mambo yake anajilinganisha na mke halali. Hakuna mke mdogo hapo. Labda tupunguze makali kwa kusema mzazi mwenzako.

Sijui ndo tuseme uchawi, sijui mahaba ama nini sijui. Sijui ni akili zako timamu uliamua iwe hivi sielewi. Ila ulikosea toka mwanzo. Na angeenda kusema kwa mke mkubwa ndo ingekua ahueni kwako. Ilivyo siri hivi ndo inazidi kuharibu. Ndo unazidi mpa nafasi huyu MCHEPUKO azidi kupata nguvu.

Kwa upeo wangu, huyu mchepuko amekua na wewe since day one kwa tamaa. Ulienda na gari ukiwa na nduguye. Akajuona na akajua una uwezo kumzidi nduguye sijui shemeji. Akaja kwako akajolengesha. Alishapiga mahesabu hapa ndo pa kuponea. Wewe unaamini anakupenda[emoji23][emoji23] this is so FUNNY... nakuhakikishia mnaishi kimazoea tu. Fulia mkose hela ya kula ndo utaelewa. Yaan mchepuko una nguvu hivi?

Halaf unakua mkali ukiulizwa juu ya mke mkubwa unampa muda saa ngapi kwanini. Hapa unaulizwa ili watu wabalance story wajue namna ya kukusaidia. Haijawahi kuwepo balance kwenye mapenz asilani. Hapa usituongopee. Kulipa ada na matumizi si kila kitu. Hapo uko hai. Ukadondoka kama leo watoto ndo wanapeleka vurugu na mchepuko kwa mke juu ya mali. Nasema tutauaanaaa...

Kabla hujamalizaaa... chukua mke.. nenda nae vaccation mwambie una mambo wataka mweleza. Mwambie A to Z. Sisi wanawake tukipenda huwa tunakua waelewa sana tukiambia ukweli. Mweleze kila kitu ili uwe huru. Najisikia huruma sana juu yako hakika maana kuhandle mambo makubwa hivi hapana.

Nilichogundua pia mke wako ana mkono wa baraka sana ndo maana Mungu anamjalia anapata sana. Zaidi nasikitika watoto qa mchepuko kukwambia eti si uende kwako. Kwahiyo wanaelewa kila kitu. Kama wangekua wanakuheshim wasingekua na la kusema asilani juu yako. Mama yao pia anawajaza ujinga.

Naomba ukamweleze MKEO kabla hayajamfikia kupitia watu baki usije jutia.
Nakuombea Amani ya moyo sana mzee wangu. Pole sana. Kuna mambo hukutokea na usijue yametokea aje. Kama ametumia nguvu za giza na alijua una ndoa Mungu adeal naye sawasawa na mapenz yake kwa kuvuruga mji wa mwenzake.

ACHANA NA MCHEPUKO. GHARAMA INAZIDI KUPANDA.
Ushauri mzuri sana. Kwenye neno mchepuko umetumia herufi kubwa kuonesha msisitizo eh? 😂
 
Yes naishi na mwanamke sijamuoa. Nayeishi naye sitaki kumuoa namtaka yule mwingine.
Wote wana watoto wawili
Jumla 4 kids
Pair ya kwanza wamepishana miezi 8 wapo vidudu huko.

Pair ya pili wamepishana mwaka mmoja anasimama dede mwingine ndio kwanzaaaa.....

HAKI UCHAWI UPO DUNIANI[emoji3][emoji3][emoji3]

Nakushauri fanya maamuzi haraka, unakoelekea siko. Amua ni yupi unaoa uanze masiha rasmi, usiongeze watoto.
 
Wewe ndio una shida alivomaanisha na Mimi nimemjibu in general kwanini mje kunishambulia acheni unafiki aisee, hafu sio kila mtu ana mawivu na kutamani Jambo flani sio dhambi mbona hata yeye alichepuka na mchepuko unamsumbua tu.
Wewe umemshambulia specifically na wala hukuongea in general kama unavyotaka kubadili gia angani. Acha kutufanya wote wajinga hapa.
 
Samahani km ntakwaza watu lakini mi naupenda uislamu wangu uliohalalisha wake wanne. Kwa kweli toka dunia ianze wanaume hawajawahi kutosha huyo Dada Leo miaka 20 na zaidi anaishia kuitwa mchepuko wakati angekua muislam angemuoa.

Kingine mbona wakurya wana mitala nnao huku kanda maalum yaani mitala kama zote .

Huyo demu nae kimeo 20yrs unakubali kufichwa km Arv vile...!!! Au ndo tamaa ya pesa mweee!pole yake aseh

Sent using Jamii Forums mobile app
Na hiyo ndiyo Raha ya uislamu..

Viongozi wa kikristo wakosee siku Mona waseme mwanaume wa kikristo aoe mke zaidi ya mmoja utaona vurugu lake 😂😂
 
hii story imefanana na baba mmoja namfahamu tofauti tu yeye aliishia kwenye viwanja

hajafanikiwa kujenga na wanawake wore walimove on wana maisha yao Ila yeye kabakia anarandaranda duniani
Duuuh poleeeh yake sana huyo m baba.
 
Back
Top Bottom