konda msafi
JF-Expert Member
- Sep 5, 2018
- 1,696
- 8,763
Hufai kuwa mke wewe,unamaamuzi ya papara ,nadhani Mungu kamuepusha jamaa na majanga makubwa dhidi yako,unakataa kuolewa na mtu mwenye mke huku ukiwa huna ushahidi kuwa ana mke au laah,huku wewe ushahidi upo wazi kuwa una mtoto.Send off ilikuwa tarehe 10 taarifa zinatoka tarehe 8 wakati wameanza safari tarehe 7 Kutoka mbeya, nilimtext mvulana kuwa wasitishe wakati huo wameshafika Kahama,
Suala ambalo mama na mimi tulitofautiana ni baada ya kumweleza mchumba wangu kwamba nina mtoto akasema mi ndo naoa kwakuwa nimekukubali ukiwa na mtoto hakuna shida ila akaomba mtoto atamlea na kumsomesha na ameshamlipia ada ya primary one ya mwaka mzima niwe mkweli, ila akanisihi nisiwajulishe kwao kama mi nina mtoto, hapo ndio mama akakazania kwamba lazima wajue, nikamsihi mama kwamba anayenioa kashamkubali mtoto na anamhudumia ila kwao wataleta mapingamizi nikiwaambia muda huu, hivyo kasema tutawaambia mbeleni, mziki ukaanzia hapo mama akajitoa
Kwanini mlivyopata habari jamaa kaoa hamkuwaambia wahusika ili wasitishe safari? Wewe na ukoo wako mnatabia mbaya
ashafeli kuwa mke bila kuingia kwenye ndoa sikulaumu ila umewapa watu kuyapokea yao hvi unafikri kijan watu alipitia wakat gani embu jiulize.......Ulivyopata habari tu kama kaoa ama la ungemface kumuuliza, upumbavu ni wako...
Angewaambia tatizo kuliko kuwaacha kwenye mataaWaelezee ukweli wakwe zako kwanini ulikimbia, sababu za wewe kukimbia zinaeleweka, kuoa au kuolewa siku hiz ni bahati, kajaribu bahati yako ndoa ni kujipanga coz waliopo kwenye ndoa wanatamani kutoka
Sijui wanawake wamekaririshwa na nani hii aina ya wivu. Wewe una mtoto ambaye hukuzaa na huyo mume mtarajiwa. Kwa upendo wake akaamua kukupokea wewe na mwanao na alijua kabisa hapa sio hadhi yake. Wewe kusikia tu ana mke tena bila uthibitisho unamblock na hasara ya maandalizi kwa upande wa mume mtarajiwa. Wamechangishana weee ila ukaona ni jambo dogo tu usimtafute na kujidhihirishia. Wallah ningekuwa mimi huyo mwanaume eti unakuja kuniomba msamaha ungeangukia kwa watuhumiwa wa uhujumu uchumi. Kuna watu wana maudhi hata unajiuliza walizaliwa kwa ajili gani. By the way baba wa mtoto ulimpa taarifa kuwa unaolewa?Hufai kuwa mke wewe,unamaamuzi ya papara ,nadhani Mungu kamuepusha jamaa na majanga makubwa dhidi yako,unakataa kuolewa na mtu mwenye mke huku ukiwa huna ushahidi kuwa ana mke au laah,huku wewe ushahidi upo wazi kuwa una mtoto.
Tena kwa ubaya zaidi hutaki wakwe zako wajue kuwa ushawahi zaa,hujui kuwa hili litaleta baraa katika familia ya Mme pindi wakijua kuwa ulishawahi zalishwa.
Mwisho nakushauri uachane na kijana Wa watu,tafuta mtu Wa saizi yako,tambua pia ukweni hawana imani na wewe tena vyovyote iwavyo kamwe hawawezi kukuamini na kukuona wewe mtu Wa thamani kwa haya uliyofanya.
Changamoto ilijitokeza gafla na ubaya zaid ikawa sina uungwaji mkono na familia yanguIssue ilikuwa ndogo sana. Baada ya kujua hilo swala mliwasiliana na upande wa pili kuwaambia changamoto mliyoiona.....?!
Sent using Jamii Forums mobile app
Mpaka hapo wewe jiandae kuwa single mother tu, sahau habari za ndoa,maana kwa ulichowafanyia ndugu zangu has ka nakwambia maumivu yao utayabeba mpaka unazeeka!Jamani mambo zenu, Niko katika wakati mgumu
Mimi ni binti wa miaka 29 kwa sasa, nimempata mwanaume ambaye tulipanga mengi sana hadi kupanga jinsi ya kufunga ndoa,
Mwaka fulani niliingia kwenye mahusiano na kijana mmoja toka Mbeya, ila kwa sasa anaishi Afrika ya Kusini kwa shughuli zake ,
Tulikubaliana kuanza kutambulishana kwao, na kwetu
Nakumbuka alinilipia nauli ya ndege nikaenda kwao kutambulishwa nikamshukuru Mungu kwamba nimepata mme sasa,
Tumeendelea na utaratibu na mshenga akatumwa kwetu kusema, baada ya kuondoka nikamweleza mama kuwa kijana sawa ananipenda ila hapendi jambo fulan ambalo kwa ukweli sitalisema hapa, mama akasema kama ndo hivo sitak habari zako za kuolewa,
Ikabidi mchakato uendelee kawaida, wakaleta kishika uchumba mama akawa hataki kushiriki hata kidogo, anasusa, sasa shangazi yangu akaniambia kwamba kwakuwa huna baba naomba ili suala tuwashirikishe baba wadogo na wajomba tuendelee na nchakato,
Baada ya muda tukapanga wataletaje mahari na siku ya send off tukaipanga,
Sasa kabla ya send off siku moja kabla tukapata habari kupitia kwa mjomba kwamba Mwanaume anayeenda kunioa kumbe ana mke mi naenda kuwa mke wa pili, taarifa hii ikawachanganya wote hata wajomba wakasema ngoja wajiweke pembeni, maandalizi ya send off yakavurugika wakati huo wakwe wakiwa njiani kuhudhuria sherehe hiyo , walikodi Costa na magari kadhaa kutoka mbeya hadi Ngara,
Wakanikimbia ndugu zangu wote nami nikachanganyikiwa kwa hasira sikutokea kwenye send off na maandalizi ikawa hasara, wakapiga simu nikazima nilikuwa na hasira sana,
Baadaye nikawasha simu nikakuta mama mkwe mtarajiwa amenitumia meseji kwamba "Sikutegemea kama ungetufanyia haya, sisi tunajiandaa kesho tunarudi lakini baki na amani"
Niliumia sana Akaendelea kunitumia meseji za machungu nikijua naye anajua kuwa Mwanae ana mke na mama huyu tumeongea kila siku niliumia,
Sasa yule mchumba wangu akawa ananitafta sipokei nikamwambia sina Muda mchafu wa kuolewa na wewe, hapo sikumwambia kwanini nimebadili mawazo,
Sasa nakumbuka siku kadhaa baadae naitwa nyumbani kwamba kuna kikao,
Kumbe kuna taarifa kwamba yule kijana hakuwa ameoa ila alichumbia sehemu akalipa mahari ila kumbe hakuoa,
Habari zilisononesha sana
Nikaenda kwa askofu mmoja akanishauri
1.Ama tuombe radhi kwao kuendelea na mchakato
2.Ama tuwape kishika uchumba chao maana mahari alikuwa bado angetoa siku ya send off asubuhi yake,
Naomba ushauri wenu plz
Nimeikosea Sana familia ile, pia hasira baada ya kupungua natamani niolewe naye japo nashindwa naanzaje
Mwanaume alikupenda wewe au aliipenda familia yako?Changamoto ilijitokeza gafla na ubaya zaid ikawa sina uungwaji mkono na familia yangu
Msamehe bure mkuu. Kwao wanatumia simu moja tu na ndio iilikuwa na nmba za mchumba na wazazi wake. Na mmiliki ni yule mjomba aliyeleta habari, hivyo aliizima baada tu ya kufikisha ujumbe.Mwanaume alikupenda wewe au aliipenda familia yako?
Mama yako anaona mbali Kuna kitu kikubwa Sana hapo umeepushiwa bila kujua just move on haikua riziki yako!!Send off ilikuwa tarehe 10 taarifa zinatoka tarehe 8 wakati wameanza safari tarehe 7 Kutoka mbeya, nilimtext mvulana kuwa wasitishe wakati huo wameshafika Kahama,
Suala ambalo mama na mimi tulitofautiana ni baada ya kumweleza mchumba wangu kwamba nina mtoto akasema mi ndo naoa kwakuwa nimekukubali ukiwa na mtoto hakuna shida ila akaomba mtoto atamlea na kumsomesha na ameshamlipia ada ya primary one ya mwaka mzima niwe mkweli, ila akanisihi nisiwajulishe kwao kama mi nina mtoto, hapo ndio mama akakazania kwamba lazima wajue, nikamsihi mama kwamba anayenioa kashamkubali mtoto na anamhudumia ila kwao wataleta mapingamizi nikiwaambia muda huu, hivyo kasema tutawaambia mbeleni, mziki ukaanzia hapo mama akajitoa