Naomba ushauri nimewakosea sana wanaoenda kuwa wakwe zangu kutokana na mkanganyiko wa familia yangu/Sikutokea siku ya Send off

Wanawake mna viherehere kuamini tu jambo usilokuwa na uhakika nalo kabla haujajiridhisha.Inaonekana una kiburi pia maana badala ungemtafuta uzungumze naye kuujua ukweli bado ukaamua kukaa kimya.Kiukweli umemuudhi sana mwenza wako kwanza kwa kutomuamini.Msamaha wako labda Mungu tu asaidie
 
Mbaya zaidi tayari amesharuka ruka sana ujanani mpaka na mtoto juu amepata (single mother)
 
Duuuh kwahiyo ulichukua maamuzi ya kishenzi bila hata ya kumuuliza muhusika Kama ni kwel au uongo ?
Pole aisee ,ukisikia jambo jifunze tabia ya kutafuta ukwel kabla ya kuchukua hatua,
Hapo chamsingi endelea kupiga round kitaa unaweza bahatika kupata mwingine , Ila huyo Wa sasa jaribu tu kumsahau ,maana sijui ni Mani atakuja kuwaweka sawa hao wakwe zako
 
Ukimuomba msamaha akakusamehe...chunga sana! Huyo jamaa atakuja kukulipizia tukio zito zaidi ya hili la kusumbua wazazi wake na kumtia aibu bila sababu.

Mambo ya kiswahili hayo...kama umesikia issue kwanini usimuulize na umshirikishe maamuzi yako ili ajue la kufanya.

Hili umelikoroga, linywe tu
 
Anajifikiria mwenyewe huyu dada alisahau jamaa kakubali kuwa mume wa pili.
Nyongeza kidogo tu kuwasaidia single mazaz


1. Tambua mtoto/watoto ni kielelezo cha maisha yako ya ufuska kabla ya ndoa. Ni alama ya wazi kwamba umechakachuliwa peku na ukaridhika na kutoa yai, ukashika mimba na kuzaa.

2. Jambo hilo ni habari mbaya kwa mwanaume anayekuoa. Asingependa uwe hivyo. Linamsikitisha na itafaa ufanye kila juhudi asahau.

3. Namna nzuri ya kumsahaulisha ni kutomuweka karibu mtoto wako na mume huyo maana kila amuonapo mtoto mumeo atakumbuka habari mbaya kwamba ulishachojolewa mavazi yote na mwanaume mwengine aliyemuwahi, yeye anakula makombo. Mtoto ni kikwazo, akae mbali na mume wako. Mpeleke kwa bibi yake.

4. Usilazimishe mumeo aone suala la wewe kuwa na mtoto sio issue, NI ISSUE tena nzito.
 
Eti jamaa alishaanza hadi kumsomeshea mtoto, sijui naye ni bwege nazi gani tu... bora amedhalilishiwa ndugu zake huenda akazinduka!
Wahuni wamepiga mie nije kusomesha mtoto si uzuzu huu!!?? Bora nitafte dem Love Connect kuliko kuoa hawa "single problem"
 
Wewe ulienda kuchepuka siku ya send off na lijamaa likakushushia dozi hadi ukapitiwa ukalala, kuja kushtuka send off imevurugika. Hapa umeleta drama.
Ushauri:- achana na mambo ya ndoa , tuwekee namba yako hapa na sisi tuonje ulichonacho.
 
Omba msamaha na rudisha kishika uchumba, hamtakuwa na amani kamwe kama mtaendeleza mahusiano.
Mawasiliano ni muhimu sana katika mahusiano, wewe unahasira, unazira, wakati mwenzako hata hajui sababu, na wewe unaona ni sawa?
 
Mwabamke mjinga huvunja nyumba kwa mikono yake mwenyewe,,
Shukuru hata umepanda ndege ,endelea kuwasimulia nduguzo ujinga mlioudanya bila tafakuri ya yoyote
 
Kuna watu huwa wanasema kuwa Single Mothers mna matatizo sana.

1. Umepata taarifa kuwa jamaa ana mke, kwa nini usitafute ushahidi kwa Kumuuliza mhusika?

2. Ndoa haikufai maana kama unaamua kwa kusikia utaenda kuleta matatizo zaidi kwenye ndoa.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
Kwa namna ya maelezo yako ni wazi kuwa
1. Familia yako ina matatizo ya kufikiri na kuamua mambo
2. Wewe mwenyewe una matatizo ya kufikiri na kuamua mambo.

Kwa sasa utulie ili kulea mtoto, hilo lishapita maana ndugu wa Dismas wameshajua kuwa una mtoto.

Pole sana.

Sent from my Infinix X650 using JamiiForums mobile app
 
The worst thing ever katika maisha ni kupewa taarifa na kurukia kwenye conclusion.

Unamuhukumu mtu bila hata kumuuliza yeye mwenyewe? Surely?

Me sijui hata nikushauri nini.
 
Kwanini mlivyopata habari jamaa kaoa hamkuwaambia wahusika ili wasitishe safari? Wewe na ukoo wako mnatabia mbaya
Tena siyo kidogo. Yaani tabia mbaya mno. Unapata taarifa za mtu unakimbilia kufanya maamuzi?

Bila hata kuwashirikisha wahusika?
 
Mbeya mpaka Ngara.. mnaroho mbaya sana ninyi.. haswa wewe no utu.. eti ukaolewe huko tena.. subiri mume mwingine.. ukienda kujisukuma huko usirudi kutusumulia humu majanga yake.. kumbuka Mjomba alikusaidia wewe na Mama yako mfikie lengo la kutotaka kuolewa naye.. utafikiri hakuwa mume mtarajiwa.. hukuongea nae kujua ukweli.. humupendi huyo mwanamume.. usimusingizie Mjomba wako na wengine.. tatizo ni wewe
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…