Naomba ushauri nimewakosea sana wanaoenda kuwa wakwe zangu kutokana na mkanganyiko wa familia yangu/Sikutokea siku ya Send off

Naomba ushauri nimewakosea sana wanaoenda kuwa wakwe zangu kutokana na mkanganyiko wa familia yangu/Sikutokea siku ya Send off

Kama nilivyoeleza awali kupitia Uzi ambao niliuweka week hii

Jamani mambo zenu, Niko katika wakati mgumu

Mimi ni binti wa miaka 29 kwa sasa, nimempata mwanaume ambaye tulipanga mengi sana hadi kupanga jinsi ya kufunga ndoa,
Mwaka fulani niliingia kwenye mahusiano na kijana mmoja toka Mbeya, ila kwa sasa anaishi Afrika ya Kusini kwa shughuli zake ,

Tulikubaliana kuanza kutambulishana kwao, na kwetu
Nakumbuka alinilipia nauli ya ndege nikaenda kwao kutambulishwa nikamshukuru Mungu kwamba nimepata mme sasa,
Tumeendelea na utaratibu na mshenga akatumwa kwetu kusema, baada ya kuondoka nikamweleza mama kuwa kijana sawa ananipenda ila hapendi jambo fulan ambalo kwa ukweli sitalisema hapa, mama akasema kama ndo hivo sitak habari zako za kuolewa,

Ikabidi mchakato uendelee kawaida, wakaleta kishika uchumba mama akawa hataki kushiriki hata kidogo, anasusa, sasa shangazi yangu akaniambia kwamba kwakuwa huna baba naomba ili suala tuwashirikishe baba wadogo na wajomba tuendelee na nchakato,

Baada ya muda tukapanga wataletaje mahari na siku ya send off tukaipanga,
Sasa kabla ya send off siku moja kabla tukapata habari kupitia kwa mjomba kwamba Mwanaume anayeenda kunioa kumbe ana mke mi naenda kuwa mke wa pili, taarifa hii ikawachanganya wote hata wajomba wakasema ngoja wajiweke pembeni, maandalizi ya send off yakavurugika wakati huo wakwe wakiwa njiani kuhudhuria sherehe hiyo , walikodi Costa na magari kadhaa kutoka mbeya hadi Ngara,
Wakanikimbia ndugu zangu wote nami nikachanganyikiwa kwa hasira sikutokea kwenye send off na maandalizi ikawa hasara, wakapiga simu nikazima nilikuwa na hasira sana,
Baadaye nikawasha simu nikakuta mama mkwe mtarajiwa amenitumia meseji kwamba "Sikutegemea kama ungetufanyia haya, sisi tunajiandaa kesho tunarudi lakini baki na amani"

Niliumia sana Akaendelea kunitumia meseji za machungu nikijua naye anajua kuwa Mwanae ana mke na mama huyu tumeongea kila siku niliumia,
Sasa yule mchumba wangu akawa ananitafta sipokei nikamwambia sina Muda mchafu wa kuolewa na wewe, hapo sikumwambia kwanini nimebadili mawazo,
Sasa nakumbuka siku kadhaa baadae naitwa nyumbani kwamba kuna kikao,
Kumbe kuna taarifa kwamba yule kijana hakuwa ameoa ila alichumbia sehemu akalipa mahari ila kumbe hakuoa,
Habari zilisononesha sana
Nikaenda kwa askofu mmoja akanishauri

1.Ama tuombe radhi kwao kuendelea na mchakato
2.Ama tuwape kishika uchumba chao maana mahari alikuwa bado angetoa siku ya send off asubuhi yake,

Naomba ushauri wenu plz

Nimeikosea Sana familia ile, pia hasira baada ya kupungua natamani niolewe naye japo nashindwa naanzaje

Nimeamua kuwaambia ukoo wangu, Kuanzia Mama sina Baba R.I.P
Mashangazi, Baba Mdogo na wajomba nia yangu ya dhati kuiomba msamaha familia ya ambaye alikuwa mchumba wangu,

Naenda kuomba msamaha nikitegemea maswali magumu,

Naenda Kuomba msamaha nikijua maumivu na uchungu hata hasara waliyopata kutoka Mbeya hadi Ngara,

Hatua ya Kwanza
Nimeamua niangalie upepo ndani ya familia yangu, idadi ya wanaonisapot,

Niangalie mtazamo wao juu ya kwanini nasukumwa kuomba msamaha,

Tatu naangalia dhamira yangu na msukumo wa moyo wa dhati,

Nne Nimeamua kuwashirikisha ndugu na kuwaambia sitaenda moja kwa moja kwa wakwe ila ntaenda kwa mshenga

Tutaenda timu ya watu 7 watu wazima sita na mimi nikiwa wa saba, katika timu hiyo mama aneendelea kugoma kutoshiriki, Nimepata shangazi mama mdogo na baba mkubwa,na wengine

Tutaelekea kwa mshenga kuomba radhi, na kueleza sababu za kutokuwapo kwenye send off alafu tumuombe atuombee msamaha,

Baada ya wao kujua tunaomba msamaha kup kwa mshenga

Nimeandaa kishika uchumba walicholipa na nimeandaa wazee 5 na wanisindikize Mbeya kutoka Ngara kwenda kuomba msamaha na pia kabla ya kufika kwenye familia ya wakwe, tutapitia kwenye parokia iliyokaribu kumuona kiongozi wa dini atupe mwongozo na kumuomba atupe ushirikiano kufika kule, pia tutaomba aambatane na wazee wa heshima wa Kanisa, hii nitaifanya tu hata wasipotoa jibu pitia kwa Mshenga

Nikifika nitakuwa na maombi mawili

1.Kuomba kusamehewa na kurudisha kishika uchumba chao

Ama

2.Kuomba kusamehewa na kuendelea na mchakato wa harusi kama watakua bado hawajapata mtu.

Naombenii mawazo yenu mengine pia

asante
 
Jambo zuri sanaa....

Uzuri umetambua kosa lako lakini usisahau sababu iliyokupelekea kufanya kosa.....

Naamini watakusamehe Ila hawatokusahau,na itapendeza kama utawaweka wazi kwamba una katoto Ili uko mbeleni usijeleta balaa jengine.
 
Ni Uamuzi wa Busara kuomba msamaha ila zingatia maswali yafuatayo
1.Kwanini hukutoa nafasi ya Kuwasikiliza juu ya majungu uliyoambiwa na ukatimka?

2.Je Dhamira yako ni kuomba msamaha kweli au ni kwakuwa unataka kuolewa hapo

3.Vipi wakipokea kishika uchumba wakasema tutakujibu, alafu ukasikia kaoa mwingine?

Naona kwanza ungeanza kujua Mwanaume wako Ana mtazamo gani na je anakubali haya?

Britannica
 
Pole kwa yote, kila lakheri uendelee kuleta mrejesho hapa ili uzidi kupata ushauri.
 
Ni Uamuzi wa Busara kuomba msamaha ila zingatia maswali yafuatayo
1.Kwanini hukutoa nafasi ya Kuwasikiliza juu ya majungu uliyoambiwa na ukatimka?

2.Je Dhamira yako ni kuomba msamaha kweli au ni kwakuwa unataka kuolewa hapo

3.Vipi wakipokea kishika uchumba wakasema tutakujibu, alafu ukasikia kaoa mwingine?

Naona kwanza ungeanza kujua Mwanaume wako Ana mtazamo gani na je anakubali haya?

Britannica
Kama atakuwa hanitaki Tena sina Budi kukubaliana na yanayoendelea
 
Dada yangu nakushauri rudisha kishika uchumba cha watu na vitu unavyokumbuka kwa ni moto na vinafunga milango ya baraka hata kama we ni mzuri kiasi gani
Ndio maana kanisa limekushauri hivyo
Vya kuolewa huko hapana kwa furaha ya baadaye
 
Kwan wee ni MUHAYA ???.

Sijaona mantiki yako ya kwenda ukweni kuomba msamaha ukiwa na machaguzi mawili

Et naomba nisameheni , kama mtapenda kunisamehe ili tuendelee na ndoa, au mnisamehe ila niwarudishie kishika uchumba chenu...

Hii inaonyesha ,Bado huna Dhati thabiti ya kuomba msamaha na kile kikichofanya usitokee ndicho kinaendelea kukuweka njia panda kama katoto (kitindamimba ) ka shetani .


Ushauri wangu...


Nenda kwa kusudio la kumuomba msamaha mchumba wako ,asamehe yalotokea muendelee na mchakato.

Ili yeye na wakwao ndio wabaki wenye kuamua !!!!.




Nmefarijika tu kujua wee ni binti wa miaka 29 . .... Umebakiza miaka 2-3 , nawee uaanze kujiita Feminist!!!.
 
Back
Top Bottom