Naomba ushauri nimewakosea sana wanaoenda kuwa wakwe zangu kutokana na mkanganyiko wa familia yangu/Sikutokea siku ya Send off

Naomba ushauri nimewakosea sana wanaoenda kuwa wakwe zangu kutokana na mkanganyiko wa familia yangu/Sikutokea siku ya Send off

We meanamke ni mjinga kiasi cha kutosheleza yani una mtoto alafu uanataka kijana wa watu ye akuoe asiwe hata alikua na mtu wake ulizani angekua anakusubiri weee tu,umesikia maneno tu umeharibu kila kitu hufai kuwa mke hata kidogo una hasira za ajabu ,huna busara,hata elimu yako nahisi hujaelimika ,

Kijana wawatu kajitoa kweli kweli nanukienda ukawasimulia uo ujinga wako eti umeskia kaoa sijui nini na nini sahau ndoa apo,yeameridhia we unaleta ushubwada ,utamtesa kaka wa watu bure
 
Maelezo yooote sioni kama wewe na huyo mwanaume kama mtajenga ndoa nzuri na ya maelewano.

Kwa umri wangu wa kuishi, kila ndoa niloona ni mfano bora kwangu inamawasiliano mazuri ya wanandoa, nnachoona kwenu wote mnacheza na jukwaa.
 
Ni Jambo zuri kuomba msamaha. Ila msamaha utoke ndani ya moyo wako. Usirudishe kishika uchumba.
Kawaambie pia kuwa una mtoto. Nakutakia safari njema
 
Nenda kaombe msamaha, ikiwezekana wape kishika uchumba chao yaishe.

Utapata msamaha wao utaishi kwa Amani na nakusubiria mume mwingine akija itakua sawa kuliko huyo.

Mpaka sasa ndugu wa mumeo kwa uliyoyatenda hawatakua na Amani na ww ata wakisamehe wapo watakao Kia nakinyongo bado na itapelekea mara zote kukitokea jambo watasimama upande wa kijana wao na ww utaona wanakuonea ila ni sababu ulishawawekea mindset ya kutokukuamini tayari

Jitahidi kumuomba Mungu akupe uamuzi sahihi zaidi
 
Ndo maana una miaka 29 na hujaolewa sababu hufai kuwa mke

Wewe na familia yako wote ni wazinguaji
 
Singo maza huo ujasiri uliutoa wapi!? Mtu keshamlipia mwanao na kakubali kumhudumia kama wake, possibly na kwenu alikuwa anawahudumia, huo ujasiri wa kuchagua ulichokichagua kwa hatua za mwisho uliutolea wapi hata kama nduguzo walijiweka kando nawe!? Mazafaka
 
mi sikuurumii maana kwa maamuzi yako ya kukurupuka hufai kuwa mke, plain truth

somo. Usihukumu kwa hatari ya Upande mmoja.
Ila kishingo Upande Polee sana, neema ya Mungu ikufunika
 
Jamani mambo zenu, Niko katika wakati mgumu
Mimi ni binti wa miaka 29 kwa sasa, nimempata mwanaume ambaye tulipanga mengi sana hadi kupanga jinsi ya kufunga ndoa,

Mwaka fulani niliingia kwenye mahusiano na kijana mmoja toka Mbeya, ila kwa sasa anaishi Afrika ya Kusini kwa shughuli zake ,
Tulikubaliana kuanza kutambulishana kwao, na kwetu

Nakumbuka alinilipia nauli ya ndege nikaenda kwao kutambulishwa nikamshukuru Mungu kwamba nimepata mme sasa,

Tumeendelea na utaratibu na mshenga akatumwa kwetu kusema, baada ya kuondoka nikamweleza mama kuwa kijana sawa ananipenda ila hapendi jambo fulan ambalo kwa ukweli sitalisema hapa, mama akasema kama ndo hivo sitak habari zako za kuolewa,

Ikabidi mchakato uendelee kawaida, wakaleta kishika uchumba mama akawa hataki kushiriki hata kidogo, anasusa, sasa shangazi yangu akaniambia kwamba kwakuwa huna baba naomba ili suala tuwashirikishe baba wadogo na wajomba tuendelee na nchakato,

Baada ya muda tukapanga wataletaje mahari na siku ya send off tukaipanga,

Sasa kabla ya send off siku moja kabla tukapata habari kupitia kwa mjomba kwamba Mwanaume anayeenda kunioa kumbe ana mke mi naenda kuwa mke wa pili, taarifa hii ikawachanganya wote hata wajomba wakasema ngoja wajiweke pembeni, maandalizi ya send off yakavurugika wakati huo wakwe wakiwa njiani kuhudhuria sherehe hiyo , walikodi Costa na magari kadhaa kutoka mbeya hadi Ngara,

Wakanikimbia ndugu zangu wote nami nikachanganyikiwa kwa hasira sikutokea kwenye send off na maandalizi ikawa hasara, wakapiga simu nikazima nilikuwa na hasira sana,

Baadaye nikawasha simu nikakuta mama mkwe mtarajiwa amenitumia meseji kwamba "Sikutegemea kama ungetufanyia haya, sisi tunajiandaa kesho tunarudi lakini baki na amani"

Niliumia sana Akaendelea kunitumia meseji za machungu nikijua naye anajua kuwa Mwanae ana mke na mama huyu tumeongea kila siku niliumia,

Sasa yule mchumba wangu akawa ananitafta sipokei nikamwambia sina Muda mchafu wa kuolewa na wewe, hapo sikumwambia kwanini nimebadili mawazo,

Sasa nakumbuka siku kadhaa baadae naitwa nyumbani kwamba kuna kikao,

Kumbe kuna taarifa kwamba yule kijana hakuwa ameoa ila alichumbia sehemu akalipa mahari ila kumbe hakuoa,

Habari zilisononesha sana

Nikaenda kwa askofu mmoja akanishauri

1.Ama tuombe radhi kwao kuendelea na mchakato

2.Ama tuwape kishika uchumba chao maana mahari alikuwa bado angetoa siku ya send off asubuhi yake,

Naomba ushauri wenu plz

Nimeikosea Sana familia ile, pia hasira baada ya kupungua natamani niolewe naye japo nashindwa naanzaje

-----------------------------------

Nimeamua kuwaambia ukoo wangu, Kuanzia Mama sina Baba R.I.P
Mashangazi, Baba Mdogo na wajomba nia yangu ya dhati kuiomba msamaha familia ya ambaye alikuwa mchumba wangu,

Naenda kuomba msamaha nikitegemea maswali magumu,

Naenda Kuomba msamaha nikijua maumivu na uchungu hata hasara waliyopata kutoka Mbeya hadi Ngara,

Hatua ya Kwanza
Nimeamua niangalie upepo ndani ya familia yangu, idadi ya wanaonisapot,

Niangalie mtazamo wao juu ya kwanini nasukumwa kuomba msamaha,

Tatu naangalia dhamira yangu na msukumo wa moyo wa dhati,

Nne Nimeamua kuwashirikisha ndugu na kuwaambia sitaenda moja kwa moja kwa wakwe ila ntaenda kwa mshenga

Tutaenda timu ya watu 7 watu wazima sita na mimi nikiwa wa saba, katika timu hiyo mama aneendelea kugoma kutoshiriki, Nimepata shangazi mama mdogo na baba mkubwa,na wengine

Tutaelekea kwa mshenga kuomba radhi, na kueleza sababu za kutokuwapo kwenye send off alafu tumuombe atuombee msamaha,

Baada ya wao kujua tunaomba msamaha kup kwa mshenga

Nimeandaa kishika uchumba walicholipa na nimeandaa wazee 5 na wanisindikize Mbeya kutoka Ngara kwenda kuomba msamaha na pia kabla ya kufika kwenye familia ya wakwe, tutapitia kwenye parokia iliyokaribu kumuona kiongozi wa dini atupe mwongozo na kumuomba atupe ushirikiano kufika kule, pia tutaomba aambatane na wazee wa heshima wa Kanisa, hii nitaifanya tu hata wasipotoa jibu pitia kwa Mshenga

Nikifika nitakuwa na maombi mawili

1.Kuomba kusamehewa na kurudisha kishika uchumba chao

Ama

2.Kuomba kusamehewa na kuendelea na mchakato wa harusi kama watakua bado hawajapata mtu.

Naombenii mawazo yenu mengine pia

asante
Miaka 29 ulinayo unafanya mambo bila kuangalia side effects sasa ukimkosa huyo mwanaume basi tena. Utajiingiza kuwa single mother mtarajiwa Kwa Hali inavyoonekana utakuepo single mother mtarajiwa
 
Jamani mambo zenu, Niko katika wakati mgumu
Mimi ni binti wa miaka 29 kwa sasa, nimempata mwanaume ambaye tulipanga mengi sana hadi kupanga jinsi ya kufunga ndoa,

Mwaka fulani niliingia kwenye mahusiano na kijana mmoja toka Mbeya, ila kwa sasa anaishi Afrika ya Kusini kwa shughuli zake ,
Tulikubaliana kuanza kutambulishana kwao, na kwetu

Nakumbuka alinilipia nauli ya ndege nikaenda kwao kutambulishwa nikamshukuru Mungu kwamba nimepata mme sasa,

Tumeendelea na utaratibu na mshenga akatumwa kwetu kusema, baada ya kuondoka nikamweleza mama kuwa kijana sawa ananipenda ila hapendi jambo fulan ambalo kwa ukweli sitalisema hapa, mama akasema kama ndo hivo sitak habari zako za kuolewa,

Ikabidi mchakato uendelee kawaida, wakaleta kishika uchumba mama akawa hataki kushiriki hata kidogo, anasusa, sasa shangazi yangu akaniambia kwamba kwakuwa huna baba naomba ili suala tuwashirikishe baba wadogo na wajomba tuendelee na nchakato,

Baada ya muda tukapanga wataletaje mahari na siku ya send off tukaipanga,

Sasa kabla ya send off siku moja kabla tukapata habari kupitia kwa mjomba kwamba Mwanaume anayeenda kunioa kumbe ana mke mi naenda kuwa mke wa pili, taarifa hii ikawachanganya wote hata wajomba wakasema ngoja wajiweke pembeni, maandalizi ya send off yakavurugika wakati huo wakwe wakiwa njiani kuhudhuria sherehe hiyo , walikodi Costa na magari kadhaa kutoka mbeya hadi Ngara,

Wakanikimbia ndugu zangu wote nami nikachanganyikiwa kwa hasira sikutokea kwenye send off na maandalizi ikawa hasara, wakapiga simu nikazima nilikuwa na hasira sana,

Baadaye nikawasha simu nikakuta mama mkwe mtarajiwa amenitumia meseji kwamba "Sikutegemea kama ungetufanyia haya, sisi tunajiandaa kesho tunarudi lakini baki na amani"

Niliumia sana Akaendelea kunitumia meseji za machungu nikijua naye anajua kuwa Mwanae ana mke na mama huyu tumeongea kila siku niliumia,

Sasa yule mchumba wangu akawa ananitafta sipokei nikamwambia sina Muda mchafu wa kuolewa na wewe, hapo sikumwambia kwanini nimebadili mawazo,

Sasa nakumbuka siku kadhaa baadae naitwa nyumbani kwamba kuna kikao,

Kumbe kuna taarifa kwamba yule kijana hakuwa ameoa ila alichumbia sehemu akalipa mahari ila kumbe hakuoa,

Habari zilisononesha sana

Nikaenda kwa askofu mmoja akanishauri

1.Ama tuombe radhi kwao kuendelea na mchakato

2.Ama tuwape kishika uchumba chao maana mahari alikuwa bado angetoa siku ya send off asubuhi yake,

Naomba ushauri wenu plz

Nimeikosea Sana familia ile, pia hasira baada ya kupungua natamani niolewe naye japo nashindwa naanzaje

-----------------------------------

Nimeamua kuwaambia ukoo wangu, Kuanzia Mama sina Baba R.I.P
Mashangazi, Baba Mdogo na wajomba nia yangu ya dhati kuiomba msamaha familia ya ambaye alikuwa mchumba wangu,

Naenda kuomba msamaha nikitegemea maswali magumu,

Naenda Kuomba msamaha nikijua maumivu na uchungu hata hasara waliyopata kutoka Mbeya hadi Ngara,

Hatua ya Kwanza
Nimeamua niangalie upepo ndani ya familia yangu, idadi ya wanaonisapot,

Niangalie mtazamo wao juu ya kwanini nasukumwa kuomba msamaha,

Tatu naangalia dhamira yangu na msukumo wa moyo wa dhati,

Nne Nimeamua kuwashirikisha ndugu na kuwaambia sitaenda moja kwa moja kwa wakwe ila ntaenda kwa mshenga

Tutaenda timu ya watu 7 watu wazima sita na mimi nikiwa wa saba, katika timu hiyo mama aneendelea kugoma kutoshiriki, Nimepata shangazi mama mdogo na baba mkubwa,na wengine

Tutaelekea kwa mshenga kuomba radhi, na kueleza sababu za kutokuwapo kwenye send off alafu tumuombe atuombee msamaha,

Baada ya wao kujua tunaomba msamaha kup kwa mshenga

Nimeandaa kishika uchumba walicholipa na nimeandaa wazee 5 na wanisindikize Mbeya kutoka Ngara kwenda kuomba msamaha na pia kabla ya kufika kwenye familia ya wakwe, tutapitia kwenye parokia iliyokaribu kumuona kiongozi wa dini atupe mwongozo na kumuomba atupe ushirikiano kufika kule, pia tutaomba aambatane na wazee wa heshima wa Kanisa, hii nitaifanya tu hata wasipotoa jibu pitia kwa Mshenga

Nikifika nitakuwa na maombi mawili

1.Kuomba kusamehewa na kurudisha kishika uchumba chao

Ama

2.Kuomba kusamehewa na kuendelea na mchakato wa harusi kama watakua bado hawajapata mtu.

Naombenii mawazo yenu mengine pia

asante
We mkorofi sana hufai hata kidogo.Kwani kuwa mke wa sita nini yani unasumbua wazee wa watu toka uyole hadi ngara halafu unawasusia kwani wao ndo walikuwa wanakuoa?Anyway em niambie ulifanikiwa kwenda,ulisamehewa?Umeolewa?Pole sana ila maisha yana mitihani sana.Usikurupukie kuolewa for the sake of.tafuta akupendaye umpende
 
Kijana yule namjua kiundani ni mpole mno ana Busara sana, najua ataweza kunisamehe ila sijajua namuanzaje na naianzaje familia yake
Usijidanganye kabisa.

SIKUSAMEHI HATA KIDOGO.
Nikikusamehe utanisumbua sana mbele ya safari.

We endelea na mambo yako tu.
 
Send off ilikuwa tarehe 10 taarifa zinatoka tarehe 8 wakati wameanza safari tarehe 7 Kutoka mbeya, nilimtext mvulana kuwa wasitishe wakati huo wameshafika Kahama,

Suala ambalo mama na mimi tulitofautiana ni baada ya kumweleza mchumba wangu kwamba nina mtoto akasema mi ndo naoa kwakuwa nimekukubali ukiwa na mtoto hakuna shida ila akaomba mtoto atamlea na kumsomesha na ameshamlipia ada ya primary one ya mwaka mzima niwe mkweli, ila akanisihi nisiwajulishe kwao kama mi nina mtoto, hapo ndio mama akakazania kwamba lazima wajue, nikamsihi mama kwamba anayenioa kashamkubali mtoto na anamhudumia ila kwao wataleta mapingamizi nikiwaambia muda huu, hivyo kasema tutawaambia mbeleni, mziki ukaanzia hapo mama akajitoa
Achana na hiyo ndoa, huko mbele mtavurugana sana, mama yako yupo sahihi, hata kama ukiomba msamaha mkaoana hamtakuwa na amani kwenye ndoa yenu.
Usilazimishe mambo
 
Yaani nisamehe bure nimejikuta nimekuchukia ghafla kwa upumbavu ulioufanya, ulikua huna sababu ya kuzimia wakwe zako sim kwa vitu vya kuambiwa. Ungemweleza mama mkwe wako ukwel hata kama alikua kashafika huko kwenu, umekasirika kwa ujinga af kumbe habar sio za kwel. Muangalie vizur mama ako sijui kama ana mapenzi ya kwel na wewe. Yote kwa yote pole sana mweleze mwenzio huenda akakuelewa, mama mkwe wako muombe samahan hata kwa text hata kama haitatokea ukaolewa na huyo jamaa. Pole sana
Inaonekana mama yake yupo sahihi anamjua mwanaye vema ndiyo maana katia ngumu, jua mama anapoint kwanini wafiche mtoto wa huyu binti kwa wazazi wa mwanaume hapo mama kaona mbali.
 
Kyusa haturembi,hatua hiyo iliyofikiwa ushukuru sana, ukaleta nyodo
Watu wanaendelea mbele tu,bahati yako umetoka Ngara huko ungekua jirani kishika uchumba tungekifata na mngetupa live.
Nenda huko ukaone namaanisha nini.
Otherwise nakushauri rudisha kwa tigopesa hela ya watu kama kuyajenga na kikolo anza upya ila hatakuamini tena.
Usiende
Alamsiki.
 
Send off ilikuwa tarehe 10 taarifa zinatoka tarehe 8 wakati wameanza safari tarehe 7 Kutoka mbeya, nilimtext mvulana kuwa wasitishe wakati huo wameshafika Kahama,

Suala ambalo mama na mimi tulitofautiana ni baada ya kumweleza mchumba wangu kwamba nina mtoto akasema mi ndo naoa kwakuwa nimekukubali ukiwa na mtoto hakuna shida ila akaomba mtoto atamlea na kumsomesha na ameshamlipia ada ya primary one ya mwaka mzima niwe mkweli, ila akanisihi nisiwajulishe kwao kama mi nina mtoto, hapo ndio mama akakazania kwamba lazima wajue, nikamsihi mama kwamba anayenioa kashamkubali mtoto na anamhudumia ila kwao wataleta mapingamizi nikiwaambia muda huu, hivyo kasema tutawaambia mbeleni, mziki ukaanzia hapo mama akajitoa
Unamwita mchumba wako mvulana. Yani unconsciously humchukulii kama mwanaume bali mvulana. Inakuwaje hajang'amua hili? Ana mushkeli.

Ndoa ni muunganiko wa familia, sio ninyi wawili tu. Hamuishi kwenye kisiwa. Ukweni wanatakiwa wajue kama una mtoto hata kama hawatakubaliana nalo. Halitawazuia kufunga ndoa. Mvulana wako anaonekana hana msimamo ni mtu wa kupelekeshwa ndio sababu hata anawaogopa ndugu zake.

Ulipanic kusikia kuwa ana mke na hukujua, mpaka kwa hasira ukasusa kwenda kwenye sendoff yako. Imagine panic ya wakwe kujua kwamba una mtoto na umewaficha.
 
Back
Top Bottom