Naomba ushauri tafadhali

Naomba ushauri tafadhali

Chendembe

JF-Expert Member
Joined
Oct 20, 2019
Posts
444
Reaction score
488
Salaaam.
Nimekuwa na changamoto katika maisha yangu na familia yangu.
1. Nilikuwa nimeowa mke wa kwanza 1996 na kubahati kuishi kwa miaka 9 ivi na kupata watoto 3. Lakini, ikaja changamoto mke akawa ananishutumu kuwa nawatuma watu wamzalilishe, akawa anakosa amani aliamini kuwa nawatuma watu wamchungulie Hadi chooni/bafuni na hata tunapolala. Nikamuacha kwa kuamini alikuwa analengo lake. Lakini baada ya kuachiwa Hali yake ikawa mbaya zaidi na kuwa mtu aliechanganyikiwa.

2. Nikaowa Tena 2003, lakini baada ya miaka Kama Saba Hali ya yule mke wa kwanza ikajitokeza kwa huyu na kupelekea kukosa Furaha ya ndoa. Amekuwa anasikia na kusema Mambo ambayo wengine tunashangaa tu na ngumu kuamini. Anaweza kuwa ndani lakini akakuambia watu wanamzomea au wanamtuka nje bila wengine kusikia
Mbaya zaidi kunasiku akaamka na kuniambia kuwa ameota kuwa na jitu kubwa na lilimwambia yeye ni mkubwa na aniambie nimwaache. Baada ya mwezi, anadai kuachwa. Naogopa kumwacha kwakuhofia lile la mke wa awali.
3. Wakati napambana na Hilo, mwaka juzi mtotowangu alitoka nyumbani nilikozaliwa na kuanguka na pikipiki na lakini hakuumia sehemu yoyote ile lakini alisema alishangaaa tu ameanguka na hakuwa anajielewa na kujikuta tu anaburuza pikipiki kwa mda mrefu na baada ya kupata fahamu akawasha na kurudi nyumbani anakoishi. Toka siku hiyo akawa anaongea Mambo ambayo ni ngumu kuelewa, atoki ndani mchana na kuchukia kuwa karibu na watu.
Naomba Allah akuongoze kunishauri Hilo maana linanikosesha amani. Naomba saana kwa Allah Ila nakosa maarifa ya kutafakari ndoto zangu.
 
Hapa ndipo Kuna umuhimu wa kuijua Quran na Sunnah... zingatia kisomo sahihi piga Surat Ahad, Falaq na Nnas malizia na Ayatul qursiyu ×3 Nyakati za kulala utakuja kunishukuru...

Au mtafute mbobezi wa Ruqya..
Achana na mambo ya ndumba hayo bwashee
 
Hapa ndipo Kuna umuhimu wa kuijua Quran na Sunnah... zingatia kisomo sahihi piga Surat Ahad,Falaq na Nnas malizia na Ayatul qursiyu ×3 Nyakati za kulala utakuja kunishukuru...

Au mtafute mbobezi wa Ruqya..
Achana na mambo ya ndumba hayo bwashee
Nashukuru, shida sijapita madrasa
 
Hapa ndipo Kuna umuhimu wa kuijua Quran na Sunnah... zingatia kisomo sahihi piga Surat Ahad,Falaq na Nnas malizia na Ayatul qursiyu ×3 Nyakati za kulala utakuja kunishukuru...

Au mtafute mbobezi wa Ruqya..
Achana na mambo ya ndumba hayo bwashee
Shekh, nimeangaika mnoo kwa maustadha bado shida inaendelea.
Nasikiza saaana Quran na kuswali pia.
Nimeenda miskiti kuomba dua, kilichotokea, narudi tu nalopokewa na mke kwamba namswalia kabla hajafa misikitini
 
Nimefika kwa Mchungaji mmoja pia aliniambia ilo, tuliomba likapunguwa kidogo na kurudi kwa kasi. Hali hiyo inajirudia rudia hata pale ninapokwenda kwa waumini wenzangu.
Hiyo ni laana inayoiandama familia yako.
- Umerogwa au ulijifunga katika maagano ulipokwenda kwa mganga au mzazi wako alikupekeka kwa sangoma utotoni.
Sasa unalipia.
 
Naona km una wasiwasi na masuala ya kiswahili elekeza nguvu kwenye kutatua hizo changamoto ktk kila njia kwa wataalam wa saikolojia
 
Pole sana kwa changamoto,
Kua karibu na Mola wako kuliko ulivyowahi kua hapo mwanzo. Amini kabisa hakuna mtu au kitu chchote kinachoweza kukusaidia isipokuwa Allah

Jitahidi kukaa na udhu, dhikri zifanye nyakati zote ( subhanAllah, Allahu Akbar, la ilaha illa llah, la hawla wala quwata ila billah, nk, ayaat kursiyu baqara 255, suraht falaq, nas na ikhlas) ziwe zinapita moyoni mwako) swali rakaa mbili kisha mwombe Allah akuondolee hii mitihani, lia nae sema kama unamuona hakika atakusikia. Jifunze majina ya mwenyezi Mungu na maana yake yeye anajibu , anasikia , na anafanya jambo kua jepesi akitaka.

Ila hakikisha mfumo wako wa maisha unabadilika kbisa. Fanya aliyoamrisha mola wako na acha aliyokataza.
Pia usianze kuruka ruka mara kwa shekh mara kwa mganga mara kwa wachungaji, simama wewe pekee Allah atasikia
Ukisoma pia al fatha imaanishe utapata wepesi

(Mfno pale unaposema iyyak naabudu wa iyyaka nastaghiin hakikisha kwel ni yeye unamuuabudu pekee na kumtaka msaad yeye tu na si mwingin)
Kisha naapa kwa Allah kua kila kitu kitakaa sawa.
Ukiweza pia simama visimamo vya usiku
 
1996+9=?
2003 mwingine

Probably unatuzingua ulikuwa na mchepuko kwa miaka 2 kabla ya kuachana na wakwanza
 
1996+9=?
2003 mwingine




PROBABLY UNATUZINGUA ULIKUWA NA MCHEPUKO KWA MIAKA 2 KABLA YA KUACHANA NA WAKWANZA
Daaa, usipopatwa uwezi juwa maumivu ya dunia,
Ahsante Mungu Amekusoma
 
Pole sana kwa changamoto,
Kua karibu na Mola wako kuliko ulivyowahi kua hapo mwanzo. Amini kabisa hakuna mtu au kitu chchote kinachoweza kukusaidia isipoku Allah
Jitahidi kukaa na udhu, dhikri zifanye nyakati zote ( subhanAllah, Allahu Akbar, la ilaha illa llah, la hawla wala quwata ila billah, nk, ayaat kursiyu baqara 255, suraht falaq, nas na ikhlas) ziwe zinapita moyoni mwako) swali rakaa mbili kisha mwombe Allah akuondolee hii mitihani, lia nae sema kama unamuona hakika atakusikia. Jifunze majina ya mwenyezi Mungu na maana yake yeye anajibu , anasikia , na anafanya jambo kua jepesi akitaka.
Ila hakikisha mfumo wako wa maisha unabadilika kbisa. Fanya aliyoamrisha mola wako na acha aliyokataza.
Pia usianze kuruka ruka mara kwa shekh mara kwa mganga mara kwa wachungaji, simama wewe pekee Allah atasikia
Ukisoma pia al fatha imaanishe utapata wepesi
(Mfno pale unaposema iyyak naabudu wa iyyaka nastaghiin hakikisha kwel ni yeye unamuuabudu pekee na kumtaka msaad yeye tu na si mwingin)
Kisha naapa kwa Allah kua kila kitu kitakaa sawa.
Ukiweza pia simama visimamo vya usiku
Allah akubariki shekh, nashukuru kwa nasaha
 
Back
Top Bottom