Naomba ushauri wa biashara ya malori

Naomba ushauri wa biashara ya malori

Wakuu nawasalimu kwa Jina la JMT.

Kama kichwa cha Habari kinavyojieleza. Nimekuja humu ndani kupata ushauri wa Biashara ya Malori haya ya kubeba mizigo iwe ya Local ama Transit.

Kutokana na Connection nilizonazo nadhani suala zima la kupata Mizigo ya Kusafirisha halitokuwa la kuumiza kichwa.
Changamoto inayonikabili ni funding pamoja na aina ya truck ambayo inapaswa ni nunue.

Kabla ya kuja humu ndani nilishaomba ushauri kwa watu kadhaa ambao wapo kwenye hii industry na wamenijuza truck nzuri ya kununua ni Mtumba SCANIA 124 420 iliyotumika Europe. Hawakunishauri kabisa kununua Truck Mpya ama Refurbished za Mchina, DAF na Volvo wakaniambia zitanitesa maana ndio kwanza naingia kwenye game. Hata nilipouliza SCANIA zilizotumika south Africa wakaniambia ni bora nichukue za europe zinakuwa bado zipo Bora na hazijatembea sana kwenye rough road kwa hizo za SOUTH japo hizo za south walikiri kwa gharama ya manunuzi zipo chini kiasi.

FUNDING
Kama nilivyoeleza awali mimi ni new comer kwenye hii industry hivyo nategemea kujichanga kama 50-60Mil then the rest nichukue mkopo maana nakopesheka vizuri sana. Baada ya kufanya window shopping nimegundua horse scania mtumba inaweza kunicost kati ya 75Mil - 85Mil hapa nitapata gari nzuri tu, Trailer nimeshauri kununua ya Mkononi ambayo imetumika hapa nchini ambapo zina range 25Mil - 30Mil kutokana na hali yake. Nimejaribu kuulizia. Mpya lakini naona bei imechangamka sana USD 28,500.00 flatbed Double tire

TECHNICAL
Nimeshauriwa hapo kwenye trailer kununua super single kwa maana inabeba Mzigo Mkubwa kulinganisha na trailer yenye double tire.
Kwenye Horse kama nilivyoeleza awali nimeshauriwa SCANIA 6x2 124L 420 Mtumba kutoka EUROPE

BUDGET
Ukiangalia makisio ya gharama zote Horse na Trailer budget yake inacheka kati ya 100Mil - 115Mil. 60% Nategemea kuitoa Mfukoni na 40% nichukue Mkopo. Nategemea kulipa Mkopo kwa kutumia Mshahara wangu pamoja na Mapato yatakayokuwa yanapatikana baada ya Truck kuanza kuoperate. Nimekuja kuomba ushauri kwa yeyote mwenye kuielewa biashara hii kwa undani, nimeweka mchanganuo wote hapa ili niweze kupata ushauri mzuri kulingana na information nilizopokea pamoja na uwezo wangu wa kifedha. Nategemea kuna wajuzi wengi humu na nitambulia ushauri mzuri katika kukamilisha hili. Ahsanteni na niwakaribishe kwa Ushauri. Kejeli na dharau hapa si mahala pake.
Kwema mkuu,hongera kwa jitihada,,kwa kua tayar una ka mtaji kadogo,jaribu kuagiza horse ya mtumba thn tafuta taratibu za kukod trailer,ukishafanikiwa kuusoma mchezo utaona mwenyewe kwamba nikikopa ela ya trailer ntaweza kurejesha?

Trailer ya double inapenda kwa sabab kwenye mizani haizidi mzigo,zile single zinasumbua sana kwenye mizani achana na story za vijiweni

Angalia hata mabus mengi wanayafunga terias nyuma siyo fashen n sabab ya mizan mkuu

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
 
Hata mimi naunga mkono chukua scania used europe 124 na trela ya kukodi kwanza usome game maana una uhakika wa mizigo.
Ila inata mda wa kifuatilia Sana Ili wengine wasitajirike badala yako.
Kata bima kubwa,
Biashara zote ni changamoto mafanikio ni kutokata tamaa
Umemshauri vyema lakin kwenye trailer ya kukodi hapana, faida ya gari ikienda na kurudi mara nyingi inakuwa $300 mpaka $500 , sasa Kama umekodi trailer maana yake faida inakuwa inaenda kwa trailer , kibaya zaidi contract ikiisha urudishe trailer Kama ukivyoichukua wakati kuchakaa kwake ndo kufanya kazi kwake:

Ni kama mwenye nyumba akwambie ukitaka kuhama paka rangi nyumba yangu ( haiwezekani)

Kama hauna trailer ya kwako mwenyewe, usinunue horse, kuwa na uhakika wa trailer kwanza ndo ununue horse: vinginevyo utakikuta unahudumia trailer harafu horse yako inakosa msaada
 
Kuna tajiri mmoja aliadithia kipande Cha maisha yake.

Alikuwa anasafiri sana Kuna siku alipanda Basi akaona Basi linajaa mpaka kutapika na huko njian abiria n wengi alivyorud tuu Ile safari akaenda kununua Basi 2 mpya akaziweka barabarani kilichofuata hapo anasema hatokuja kukisahau.

Anasema kwanza aligombana na matajiri wenzake bila sababu za msingi, aligombana na madereva na makondakta mwisho alkua anaishi na stress kila wakati ikabid auze zile basi ili awe na Amani.

Hii inamaana kuwa Biashara ya Gari unahitaji usimamizi mkubwa sana napia maneno ni mengi pia uhasama n mkubwa hvyo unahitajika 100% kwenye usimamizi tofauti na hapo uliowaajiri watajenga na kununua fuso huku wewe nje kukiwa na screpa za giabox, engine mpaka chassis na matairi vipara ukiwa umeyapanga nje kwako ukiamini utayauza.
 
Nipo kwenye mchakato wa kuomba mkopo wa Bajaj, Ila IPO siku ntaomba ushauri Kama huu!!!

Mkuu nakuunga mkono!! Mungu akutangulie
Ushauri wangu!!
Jitahidi Sana kuweka bima ya jadi kwenye gari yako!
75% ya ajali za barabarani zinasababishwa na masuala ya ushirikina...
Ni Hilo tu
 
Ukisha nunua naomba kazi ya uajent kwa mpaka wa kasumulu mkuu.
 
Wakuu nawasalimu kwa Jina la JMT.

Kama kichwa cha Habari kinavyojieleza. Nimekuja humu ndani kupata ushauri wa Biashara ya Malori haya ya kubeba mizigo iwe ya Local ama Transit.

Kutokana na Connection nilizonazo nadhani suala zima la kupata Mizigo ya Kusafirisha halitokuwa la kuumiza kichwa.
Changamoto inayonikabili ni funding pamoja na aina ya truck ambayo inapaswa ni nunue.

Kabla ya kuja humu ndani nilishaomba ushauri kwa watu kadhaa ambao wapo kwenye hii industry na wamenijuza truck nzuri ya kununua ni Mtumba SCANIA 124 420 iliyotumika Europe. Hawakunishauri kabisa kununua Truck Mpya ama Refurbished za Mchina, DAF na Volvo wakaniambia zitanitesa maana ndio kwanza naingia kwenye game. Hata nilipouliza SCANIA zilizotumika south Africa wakaniambia ni bora nichukue za europe zinakuwa bado zipo Bora na hazijatembea sana kwenye rough road kwa hizo za SOUTH japo hizo za south walikiri kwa gharama ya manunuzi zipo chini kiasi.

FUNDING
Kama nilivyoeleza awali mimi ni new comer kwenye hii industry hivyo nategemea kujichanga kama 50-60Mil then the rest nichukue mkopo maana nakopesheka vizuri sana. Baada ya kufanya window shopping nimegundua horse scania mtumba inaweza kunicost kati ya 75Mil - 85Mil hapa nitapata gari nzuri tu, Trailer nimeshauri kununua ya Mkononi ambayo imetumika hapa nchini ambapo zina range 25Mil - 30Mil kutokana na hali yake. Nimejaribu kuulizia. Mpya lakini naona bei imechangamka sana USD 28,500.00 flatbed Double tire

TECHNICAL
Nimeshauriwa hapo kwenye trailer kununua super single kwa maana inabeba Mzigo Mkubwa kulinganisha na trailer yenye double tire.
Kwenye Horse kama nilivyoeleza awali nimeshauriwa SCANIA 6x2 124L 420 Mtumba kutoka EUROPE

BUDGET
Ukiangalia makisio ya gharama zote Horse na Trailer budget yake inacheka kati ya 100Mil - 115Mil. 60% Nategemea kuitoa Mfukoni na 40% nichukue Mkopo. Nategemea kulipa Mkopo kwa kutumia Mshahara wangu pamoja na Mapato yatakayokuwa yanapatikana baada ya Truck kuanza kuoperate. Nimekuja kuomba ushauri kwa yeyote mwenye kuielewa biashara hii kwa undani, nimeweka mchanganuo wote hapa ili niweze kupata ushauri mzuri kulingana na information nilizopokea pamoja na uwezo wangu wa kifedha. Nategemea kuna wajuzi wengi humu na nitambulia ushauri mzuri katika kukamilisha hili. Ahsanteni na niwakaribishe kwa Ushauri. Kejeli na dharau hapa si mahala pake.
Anzia EFTA unalipa 30% ya gharama ya chombo alafu mnakubaliana kila mwezi utapeleka ngap ukimaliza wanakupa kadi yako kumbuka unatakiwa pia ulipe insurance kubwa kwa manufaa yenu wote hasa EFTA
 
Anzia EFTA unalipa 30% ya gharama ya chombo alafu mnakubaliana kila mwezi utapeleka ngap ukimaliza wanakupa kadi yako kumbuka unatakiwa pia ulipe insurance kubwa kwa manufaa yenu wote hasa EFTA
Efta ndo nn mkuu nifahamishe
 
Efta ndo nn mkuu nifahamishe
16463163759644832361637005022684.jpg
16463164319064584316567279159620.jpg
 
Ndugu kila mtu duniani Mungu amempa aina ya riziki yake katika utafutaji. Wewe Mungu amekupa riziki kwenye kilimo na sio Malori.

Aliyepewa Riziki katika malori kila siku anaongeza malori mapya, kuna watu wanafanya biashara ya malori zaidi ya miaka 50 mpaka yameandikwa babu mpaka mjukuu.

Kwahiyo huyu jamaa kinachomsukuma kwenda kwenye malori ni Riziki yake inamwita huko, cha muhimu apewe ushauri mzuri.
Nimetoa ushauri tu! Na ww nakushauri umtie moyo kwa hilo fundisho ulilo niandikia mimi!
 
Nilikuwa mbishi kwenye biashara hiyo hadi niliitwa betri na vijana!
Kilichotokea magari yalipo haribika walaji woote wakasepa na kuniacha na magari yangu mabovu kunguru wanayanyea[emoji24]
[emoji24][emoji24]
Yaliharibika nini kisichotengenezeka?

Inawezekanaje magari yote yaharibike kwa pamoja kiasi cha kushindwa kutatulika?

Inawezekana wewe ni wale wanaolimbikiza magonjwa mpaka gari igome kwenda ndiyo muanze kuunga unga..
 
Nipo kwenye mchakato wa kuomba mkopo wa Bajaj, Ila IPO siku ntaomba ushauri Kama huu!!!

Mkuu nakuunga mkono!! Mungu akutangulie
Ushauri wangu!!
Jitahidi Sana kuweka bima ya jadi kwenye gari yako!
75% ya ajali za barabarani zinasababishwa na masuala ya ushirikina...
Ni Hilo tu
Daah[emoji2][emoji2]
 
Yaliharibika nini kisichotengenezeka?

Inawezekanaje magari yote yaharibike kwa pamoja kiasi cha kushindwa kutatulika?

Inawezekana wewe ni wale wanaolimbikiza magonjwa mpaka gari igome kwenda ndiyo muanze kuunga unga..
Ndio imesha wezekana!
Beyond economic repair...
 
Hahaha umenikumbusha miaka ya nyuma nilikuwa nakodi fuso za jamaa flani kubebea mizigo yangu.

Aisee tajiri wa hizo gari anafuatilia na ni mkali mpaka madereva wanaomba Mungu gari isiharibike.
Tanzania kuna utamaduni kuwa tajiri hapaswi kutembea na gari lake muda wote! Tajiri yoyote anayeonekana kutembea na gari lake eg basi la abiria anachukiwa na kutukanwa sana. Kwa nini?
 
Kwema mkuu,hongera kwa jitihada,,kwa kua tayar una ka mtaji kadogo,jaribu kuagiza horse ya mtumba thn tafuta taratibu za kukod trailer,ukishafanikiwa kuusoma mchezo utaona mwenyewe kwamba nikikopa ela ya trailer ntaweza kurejesha?

Trailer ya double inapenda kwa sabab kwenye mizani haizidi mzigo,zile single zinasumbua sana kwenye mizani achana na story za vijiweni

Angalia hata mabus mengi wanayafunga terias nyuma siyo fashen n sabab ya mizan mkuu

Sent from my SM-A207F using JamiiForums mobile app
Nimeamua kwenye trailer hapo nianze na ya kukodi nione kwanza pesa inavyoingia. Ahsante Mkuu
 
Back
Top Bottom