Naomba ushauri wako juu ya kipi nifanye kwa hiki kilichotukumba kwenye ndoa

Naomba ushauri wako juu ya kipi nifanye kwa hiki kilichotukumba kwenye ndoa

Haya mambo haya mimi kalenda ilinisaliti mpaka mr akaanza kusema au umenibambikizia,kwanza mtoto alikuwa bado mdogo sana jamaa alipanic akasema tuitoe,mi nikamwambia sina mpango huo hata sir God hawezi kunielewa,badae akarudi kwenye mstari mambo yakawa sawa tu.
Yaan mkuu hii ishu yako ni kama yetu, hata mimi nilivurugwa kiasi cha kumuuliza hivyo wife like "au kuna mistake umefanya huko ndio maana unalia" hapa sasa nikachochea moto
 
Nakazia hapa.

Nyie hamkupanga lakini Mungu alipanga kua huyo mtoto lazima azaliwe wakati huo.

Nakumbuka mimi na wife tulipitia stress kidogo baada ya mimba ya mtoto wa pili kuingia wakati wa kwanza bado hajakua vizuri.

Tuliamua kutomwaga damu, isitoshe watoto ni zawadi, tukakubaliana nalo, na Mungu mwema safari ya miezi tisa tumeimaliza.

Hakikisha unakua karibu na mke wako, muonyeshe upendo mkubwa sana.
Sawa sawa chief..kumbe hii ni experience ya watu wengi kidogo kwenye ndoa!!.. napata mwangaza sasa, na ninashukuru wadau kuniweka wazi maana inanitia moyo
 
Yaan mkuu hii ishu yako ni kama yetu, hata mimi nilivurugwa kiasi cha kumuuliza hivyo wife like "au kuna mistake umefanya huko ndio maana unalia" hapa sasa nikachochea moto
Inabidi muwe strong nyie bora mkubwa,mimi ndo kwanza alikuwa na miezi sita,nilipambana mtoto nikamnyonyesha huku na mimba yangu karibia najifungua ndo namuachisha baada ya kujifungua unasahau.
 
Inabidi muwe strong nyie bora mkubwa,mimi ndo kwanza alikuwa na miezi sita,nilipambana mtoto nikamnyonyesha huku na mimba yangu karibia najifungua ndo namuachisha baada ya kujifungua unasahau.
Dada angu kweli wewe ulipambana, mtoto wa miezi 6 naamin kabisa haikua rahisi.
Hapo huwa tunaumizwa na mitazamobya watu, kwamba watatuonaje hawa? Kwamba tunapemda sanaaa mpaka hatuzingatii masuala ya msingi?
 
Ushauri.
Mmoja au wote mfunge kizazi, au wife atumie zile njia za kuzuia uzazi.
Mungu alikupa mwanaume uwezo wa kumjaza mimba mwanamke hata ukiwa na miaka 90, lakini mwanamke 40 tu kupata mimba ni mbinde.

Halafu anakuja mtu anakushauri mwanaume eti kufunga kizazi. Never
 
Wakuu heshima kwenu.

Polen na hongereni kwa majukumu yenu ya kila siku.

Niko kwenye hali fulani ya mkanganyiko kidogo. Nasema kidogo kwasababu ni kama niko njia panda japo kuna njia ambayo kwa mujibu wa misingi ya imani na utamaduni na maadili yangu najua nitaiendea njia hiyo japo naona ni ngumu sana ndio lengo la kusogea kwenu nipate mawili matatu.

Mimi ni mwanaume. Umri wangu ni 35 years. Nina mke yeye ni 36 years na Mungu katubariki kuwa na watoto wa 4 mpaka sasa hivi katika kipindi chote cha miaka 14 toka tujuane na mpaka kufunga ndoa. Tuna miaka 10 toka siku tufunge ndoa rasmi.

Mwanangu wa kwanza ana 13years yuko form 1, wapil yuko class 3, wa 3 yuko class 1 na wa 4 ana mwaka mmoja na miez kama 9 sasa. Katika hawa woote watoto wanne, ni mmoja tu wa kiume wa tatu kuzaliwa alieko clasa 1.

Sasa hapa juz kati tumekuja kufaham kuwa wife kanasa mimba tena. Ni baada mwezi kupita bila kuona kawaida ya kike ya kila mwezi na tukaamua kufanya vipimo tukagundua imoo.

Shida sio mtoto, shida ni mipango. Sikua na mpango wa kuzaa baada ya kufunga miaka 35 ya umri.
Hii imenifanya kuwa na reaction tofaut katika mapokeo ya taarifa ya ugen huu.

Na suala hil hata kwa wife pia lilimtoa machozi. Kiukwel hii taarifa ilitupa shock na imezua mgogoro mkubwa na wife, amenishushia lawama sana hasa kwakua nilipopata majibu haya sikuchukua hatua ya kum comfort. Nafikir ni kwakua hata mimi ilinichanganya. Amekua akinishutumu sana japo najua hii yote yaweza kuwa ni shock ya tukio ambalo hakuna aliyetegemea.

Kwa imani yangu, nimekua nikimuomba Mungu anipe amani na uamuzi sahihi na pia utayari wa kupokea suala hilibkwa mikono miwili. Anisaidie kusiwe na athari yoyote kiroho kwa mtoto kwa jiona kama hatuko tayari kumpokea. Namuomba sana Mungu anisaidie na aingilie kati, pia amsaidie wife aweze kukubaliana na hili, naelewa sana jinsi ambavyo inam frustrate pengine kila anapofikiri kuanza safar ndefu ya miezi 9 yenye kila aina ya vikwazo kiafya na kihisia.

Naelewa ni namna gani huwa inatu consume kusubiri mtoto kuzaliwa na majibu ya maombi yetu kuwa mtoto azaliwe salama mwenye afya njema bila kasoro. Haya yote tunayajua kwa watoto hawa wa 4 tuliojaaliwa.

Sasa sisi tukawa tunahesabu mambo haya tumekwisha yamaliza na hatuta rudi tena huko zaid ya kukaa na kulea watoto na kuwaandalia future yao.

Wakuu nachanganyikiwa japo nimeanza kukubaliana na hili.
Naomba ushauri wenu na kutiwa moyo.

Nafikiri baada ya hili kupita kama Mungu akitujaalia kumaliza mwendo salama, mmoja wetu atapaswa kufunga uzazi, hakuna namna.

Ahsanten na karibun kwa ushauri.

Siku njema
Hebu naomba uni PM
 
Dada angu kweli wewe ulipambana, mtoto wa miezi 6 naamin kabisa haikua rahisi.
Hapo huwa tunaumizwa na mitazamobya watu, kwamba watatuonaje hawa? Kwamba tunapemda sanaaa mpaka hatuzingatii masuala ya msingi?
Ni kweli kila mtu anaongea lake ila unapotezea,alafu nyie umri wenu bado mdogo mi mtoto wa kwanza nilipata nikiwa na miaka 31
 
Kilichokukuta wewe ni kama ambacho kilinikuta mimi miaka 4 iliyopita. Mimi na mke wangu tumejaaliwa watoto 4 kwa sasa.

Plan ya kwanza ilikuwa tuwe na watoto wawili tu. Ila kwa bahati wote wawili walikuja wa kiume. Tukakubaliana tujaribu mara moja ya mwisho napo pia akapatikana wa kiume.

Tuliamua rasmi kuwa kuzaa basi tena. Mke wangu aliweka kitanzi lakini kikawa na madhara makubwa kwake kiafya, akaweka kijiti halkadhalika ikawa na matatizo, akaishia kwenye vidonge vya majira.

Kuna kipindi alipata blood infection kupelekea kutumia antibiotics ambazo kitaalam inasadikika huudhofisha nguvu ya vidonge vya majira. Baada ya muda ikawa hajielewi ikabidi kupima ujauzito na kukuta imo.
Hicho kipindi kilikuwa ni kigumu mno maana iilikuwa kipindi cha Covid, kipato kilitetereka na bado ujauzito umekuja.

Mungu anisamehe, nilimwambia mke wangu atoe ujauzito na mpaka kumfanyia booking ya abortion. Mwanzo alikubali lakini dakika ya mwisho kabisa akabadili mawazo yake na kukataa kabisa kutoa ile mimba. Hii ilileta mtafaruku mkubwa mno baina yetu katika ndoa. Kipindi chote cha mwanzo cha ujauzito hatukuwa sawa mpaka nililipoamua kukubaliana tu na hali halisi.

Baada ya miezi tisa mke wangu alijifungua mtoto wa kike. Mtoto ambae nilikuwa nikitamani kumpata kwa miaka.
mingi. Nafsi ilinisuta na wakati mwingine inanisuta mpaka leo.

Binadamu ni wazuri katika kupanga ya kwetu huku tukisahau kuna mamlaka yenye nguvu zaidi yetu na kila kitu hutokea kwa matakwa yake.
Binti yangu alizaliwa July, 2020, January 2021 mke wangu alipata message instagram toka kwa ad agency kupitia kwenye account ambayo alimfungulia mtoto kama wafanyavyo ma mama wengi. Walitaka kutumia picha za mwanangu kwenye matangazo ya vitu vya watoto.

Mwanzo nilidhani utani lakini baada ya kuangalia account ya huyo mtu ya instagram nikagundua ni ya kweli kutoka Kenya. Process iliyofuatwa ilikuwa ni mkataba wa miaka miwili ambao uliisha January 2023. Malipo hayakuwa makubwa sana ila kwa kipindi hicho ilitusaidia mno kusogeza maisha mbele.

Inawezekana mwanao asije kupata mikataba ya kazi akizaliwa tu kama wangu lakini kila jambo hutokea kwa sababu zake. Mpe moyo mke wako na chukulia kuwa huo ujauzito ni kama baraka kwenu. Mipango ya Mungu daima huwa haina dosari japo kama wanadamu huwa hatuoni mpaka jambo jema litokee mbeleni.

Kila heri mkuu.
 
Ni kweli kila mtu anaongea lake ila unapotezea,alafu nyie umri wenu bado mdogo mi mtoto wa kwanza nilipata nikiwa na miaka 31
HApo nimekuelewa vyema mkuu. Ahsante sana.
Mimi bwana ujana mwingi, mtot wa kwanza nimepata chuo niko na kama 21 yrs hiv 😂😂.
 
Kilichokukuta wewe ni kama ambacho kilinikuta mimi miaka 4 iliyopita. Mimi na mke wangu tumejaaliwa watoto 4 kwa sasa.

Plan ya kwanza ilikuwa tuwe na watoto wawili tu. Ila kwa bahati wote wawili walikuja wa kiume. Tukakubaliana tujaribu mara moja ya mwisho napo pia akapatikana wa kiume.

Tuliamua rasmi kuwa kuzaa basi tena. Mke wangu aliweka kitanzi lakini kikawa na madhara makubwa kwake kiafya, akaweka kijiti halkadhalika ikawa na matatizo, akaishia kwenye vidonge vya majira.

Kuna kipindi alipata blood infection kupelekea kutumia antibiotics ambazo kitaalam inasadikika huudhofisha nguvu ya vidonge vya majira. Baada ya muda ikawa hajielewi ikabidi kupima ujauzito na kukuta imo.
Hicho kipindi kilikuwa ni kigumu mno maana iilikuwa kipindi cha Covid, kipato kilitetereka na bado ujauzito umekuja.

Mungu anisamehe, nilimwambia mke wangu atoe ujauzito na mpaka kumfanyia booking ya abortion. Mwanzo alikubali lakini dakika ya mwisho kabisa akabadili mawazo yake na kukataa kabisa kutoa ile mimba. Hii ilileta mtafaruku mkubwa mno baina yetu katika ndoa. Kipindi chote cha mwanzo cha ujauzito hatukuwa sawa mpaka nililipoamua kukubaliana tu na hali halisi.

Baada ya miezi tisa mke wangu alijifungua mtoto wa kike. Mtoto ambae nilikuwa nikitamani kumpata kwa miaka.
mingi. Nafsi ilinisuta na wakati mwingine inanisuta mpaka leo.

Binadamu ni wazuri katika kupanga ya kwetu huku tukisahau kuna mamlaka yenye nguvu zaidi yetu na kila kitu hutokea kwa matakwa yake.
Binti yangu alizaliwa July, 2020, January 2021 mke wangu alipata message instagram toka kwa ad agency kupitia kwenye account ambayo alimfungulia mtoto kama wafanyavyo ma mama wengi. Walitaka kutumia picha za mwanangu kwenye matangazo ya vitu vya watoto.

Mwanzo nilidhani utani lakini baada ya kuangalia account ya huyo mtu ya instagram nikagundua ni ya kweli kutoka Kenya. Process iliyofuatwa ilikuwa ni mkataba wa miaka miwili ambao uliisha January 2023. Malipo hayakuwa makubwa sana ila kwa kipindi hicho ilitusaidia mno kusogeza maisha mbele.

Inawezekana mwanao asije kupata mikataba ya kazi akizaliwa tu kama wangu lakini kila jambo hutokea kwa sababu zake. Mpe moyo mke wako na chukulia kuwa huo ujauzito ni kama baraka kwenu. Mipango ya Mungu daima huwa haina dosari japo kama wanadamu huwa hatuoni mpaka jambo jema litokee mbeleni.

Kila heri mkuu.
Mkuu i really appreciate your sharing. Thanks alot
 
Kuna pahala umekosea.

Sisi tulikuwa tunafanya kazi ya kulipwa kwa performance, malipo ya ile kazi ilikuwa watu wakiwa wengi malipo kiduchu ila wakiwa wachache malipo makubwa, Guess What...Tulikuwa tunapiga vita mfanyazi kuongezeka ila endapo Bosa alimleta tu anakuwa mwenzetu hatumkatai tena maana ni mwenzetu maana ukimkataa tena hukatai kuongezwa mfanyakazi mpya bali unamkataa mtu SPECIFIC ambae ni JUMA, HAMIS au EMMA sawa na kutaka afukuzwe kazi...CONCEPT NINI ??

Kukataa mtoto kabla ajawa mimba ni sahihi maana huyo mtoto anakuwa bado hana IDENTITY maan hio ina belong kwa watoto wote ambao wajazaliwa bado Duniani ila kumlataa mtoto au kumsema baada ya kuwa mimba tiali hapo sasa unamsema mtoto SPECIFIC ambae yupo has na ni wako.

Namaanisha huyo mwanao ambae ni mimba tiali anauhai na ni wako, kuandika uzi kama huu tu na ulichoeleza maanake ujawa radii na huyo mtoto kifupi ushamkataa ila huna namna hii kama liana kwake.

Ulikuwa na haki kusema kwasasa sihitaji mtoyo mwengine ila una haki tena once mimba ishatungwa hapo STATEMENT IMEBADILIKA hukatai kuwa na mtoto mwengine tena bali unakataa mwanao.
 
Back
Top Bottom