Naomba ushauri wako juu ya kipi nifanye kwa hiki kilichotukumba kwenye ndoa

Naomba ushauri wako juu ya kipi nifanye kwa hiki kilichotukumba kwenye ndoa

Mkuu wewe unaonekana ni mtu unayejali sana familia yako, ni jambo jema na hongera kwa hilo. Mtoto ni baraka kutoka kwa Mungu as long Mungu ameruhusu hiyo mimba jua mlango wa Mafanikio na Baraka zitandamana naye so usiruhusu hofu, mtie moyo wife na play your role as a husband & father.
 
Siogopi kulea kaka. Ni vile tu labda mtazamo, tayar mtoto wa kwanza yuko sekondari halaf tunakua bado tunaonekana tunaendela kuzaa na huku hawa wenfine tayar wana akil zao naona kama kidogo hii inaleta picha flan sio..

Ila tutalea tu na wala hatuta fanya abortion. Ni kinyume na iman yangu
Mkuu haya maisha ni yako, hata siku mmoja usiwaze kuhusu watu wengine watawaonaje, by the way hamna anayejali kuhusu wewe na familia yako. Ni hisia tu ambazo unatakiwa kuzitawala.
 
Yaani umri huo Kaka mkubwa mnadinyana alafu mnaogopa kupata mtoto wa tano ,hapa naona unatamani tukushauri muitoe hiyo mimba Ila Mimi nakushauri msitoe mimba ,lea huyo kiumbe akikuwa fungeni uzazi hiyo ni mistake mshaifanya kubalini uhalisia tu .
Kwa huo umri bado wadogo sana, hata wa sita anawezekana.
 
Watembelee wasio na watoto utaona faida za watoto

Watembelee wenye matatizo mazito kwenye ndoa zao utaona wepesi wa tatizo lako

Usi sahau Kila mtoto huja na sahani yake

Kuna wakati unacho kipata wengine wanakikosa sio kwasababu wewe una bahati Ila nikwasababu ya watoto

Kwa hiyo kumchukia mkeo kwa kuku zalia nikusahau kilicho kufanya umuowe badilika mkuu
Ujumbe murua mkuu
 
Wakuu heshima kwenu.

Polen na hongereni kwa majukumu yenu ya kila siku.

Niko kwenye hali fulani ya mkanganyiko kidogo. Nasema kidogo kwasababu ni kama niko njia panda japo kuna njia ambayo kwa mujibu wa misingi ya imani na utamaduni na maadili yangu najua nitaiendea njia hiyo japo naona ni ngumu sana ndio lengo la kusogea kwenu nipate mawili matatu.

Mimi ni mwanaume. Umri wangu ni 35 years. Nina mke yeye ni 36 years na Mungu katubariki kuwa na watoto wa 4 mpaka sasa hivi katika kipindi chote cha miaka 14 toka tujuane na mpaka kufunga ndoa. Tuna miaka 10 toka siku tufunge ndoa rasmi.

Mwanangu wa kwanza ana 13years yuko form 1, wapil yuko class 3, wa 3 yuko class 1 na wa 4 ana mwaka mmoja na miez kama 9 sasa. Katika hawa woote watoto wanne, ni mmoja tu wa kiume wa tatu kuzaliwa alieko clasa 1.

Sasa hapa juz kati tumekuja kufaham kuwa wife kanasa mimba tena. Ni baada mwezi kupita bila kuona kawaida ya kike ya kila mwezi na tukaamua kufanya vipimo tukagundua imoo.

Shida sio mtoto, shida ni mipango. Sikua na mpango wa kuzaa baada ya kufunga miaka 35 ya umri.
Hii imenifanya kuwa na reaction tofaut katika mapokeo ya taarifa ya ugen huu.

Na suala hil hata kwa wife pia lilimtoa machozi. Kiukwel hii taarifa ilitupa shock na imezua mgogoro mkubwa na wife, amenishushia lawama sana hasa kwakua nilipopata majibu haya sikuchukua hatua ya kum comfort. Nafikir ni kwakua hata mimi ilinichanganya. Amekua akinishutumu sana japo najua hii yote yaweza kuwa ni shock ya tukio ambalo hakuna aliyetegemea.

Kwa imani yangu, nimekua nikimuomba Mungu anipe amani na uamuzi sahihi na pia utayari wa kupokea suala hilibkwa mikono miwili. Anisaidie kusiwe na athari yoyote kiroho kwa mtoto kwa jiona kama hatuko tayari kumpokea. Namuomba sana Mungu anisaidie na aingilie kati, pia amsaidie wife aweze kukubaliana na hili, naelewa sana jinsi ambavyo inam frustrate pengine kila anapofikiri kuanza safar ndefu ya miezi 9 yenye kila aina ya vikwazo kiafya na kihisia.

Naelewa ni namna gani huwa inatu consume kusubiri mtoto kuzaliwa na majibu ya maombi yetu kuwa mtoto azaliwe salama mwenye afya njema bila kasoro. Haya yote tunayajua kwa watoto hawa wa 4 tuliojaaliwa.

Sasa sisi tukawa tunahesabu mambo haya tumekwisha yamaliza na hatuta rudi tena huko zaid ya kukaa na kulea watoto na kuwaandalia future yao.

Wakuu nachanganyikiwa japo nimeanza kukubaliana na hili.
Naomba ushauri wenu na kutiwa moyo.

Nafikiri baada ya hili kupita kama Mungu akitujaalia kumaliza mwendo salama, mmoja wetu atapaswa kufunga uzazi, hakuna namna.

Ahsanten na karibun kwa ushauri.

Siku njema
Ushauri maana yake unapata mawazo yatakayokusaidia (enlighten you) kufanya uamuzi sahihi na siyo mawazo utakayotumia kwenye uamuzi wako. Kwa upande, wangu badala ya ushauri nashangaa kwamba "hukuwa tayari kumpokea mtoto ambaye mmejaliwa kumpata". Ujue hata kama utamficha atakuja tu kujua reaction yako na itamuumiza sana. Unaweza kuwa na reaction kama hiyo kama unajua kama mtoto si wako, lakini kama ni wako, nasikitika sana na najiuliza kwa nini ulikuwa na hiyo reaction. Kuna familia moja walizaliwa watoto 17, kwa sasa wameshabaki 3 tu. Kama wazazi au mzazi mmojawapo angekuwa na mawazo kama yako, angefurahi au angehuzunika? Nakuachia hilo swali.
 
Mimba Ina muda gani?

Kama mko tayari, leeni mimba, mtoto azaliwe.

Kama hamko tayari na kamimba ndo kako mwezi wa kwanza, bado sana hiyo, ni vinyamanyama tu. Katoeni muendelee na maisha.

Wengi tu humu wametoa mimba/wamelazimisha wenza wao kutoa mimba ila hapa watajifanya hawaijui hiyo option.
 
We chizi nini, sasa una ushauri gani unataka, ulipiga pipe, basi pokea hiyo mimba kwa mikono miwili, mengine pambana kiume, iwe ni bajeti ama gharama za maisha pambana kiume.. Ya mungu mengi ya kuku mayai we unajiwekea hao wa4 unahakika ndio hao hao watakuwa moaka uzeeni mwako kama utafanikiwa kuwa na umri mrwfu, usishangae keshokutwa wa4 wako wanapata ajali wanakufa(siombei likukute, mungu akuepushie mbali) unabaki kuiombea dua mimba usiyoita

Mimba ishakuja we lea akizaliwa mtoti hewala, mimba ikiharibika yenyewe hewala lakini usiwe kwenye majuto kw avitu vya baraka kama hivyo.
 
We chizi nini, sasa una ushauri gani unataka, ulipiga pipe, basi pokea hiyo mimba kwa mikono miwili, mengine pambana kiume, iwe ni bajeti ama gharama za maisha pambana kiume.. Ya mungu mengi ya kuku mayai we unajiwekea hao wa4 unahakika ndio hao hao watakuwa moaka uzeeni mwako kama utafanikiwa kuwa na umri mrwfu, usishangae keshokutwa wa4 wako wanapata ajali wanakufa(siombei likukute, mungu akuepushie mbali) unabaki kuiombea dua mimba usiyoita

Mimba ishakuja we lea akizaliwa mtoti hewala, mimba ikiharibika yenyewe hewala lakini usiwe kwenye majuto kw avitu vya baraka kama hivyo.
Nimekuelewa mzee japo umenifokea sana na vitisho juu, ila nimekupata 😅
 
Mkuu haya maisha ni yako, hata siku mmoja usiwaze kuhusu watu wengine watawaonaje, by the way hamna anayejali kuhusu wewe na familia yako. Ni hisia tu ambazo unatakiwa kuzitawala.
Sawa mkuu. Hil nalo ni la kwel, inawezekana najishtukia tu bila sababu za msingi
 
Mkuu wewe unaonekana ni mtu unayejali sana familia yako, ni jambo jema na hongera kwa hilo. Mtoto ni baraka kutoka kwa Mungu as long Mungu ameruhusu hiyo mimba jua mlango wa Mafanikio na Baraka zitandamana naye so usiruhusu hofu, mtie moyo wife na play your role as a husband & father.
Ahsante sana mkuu. Nashukuru
 
Usiwe na bias na children gender mtoto ni mtoto
Ni sahihi kaka. Kwa hili sina shida nalo. Maana kwa dunia ya sasa malezi ya watoto changamoto yake haibaguibwa kike wala wa kiume. Tofaut na zamani. Hili sina tatizo nalo
 
Back
Top Bottom