Naomba ushauri wako nasaha juu ya kufikia malengo ya kuku elfu 5 ndani ya mwaka mmoja na miezi sita

Naomba ushauri wako nasaha juu ya kufikia malengo ya kuku elfu 5 ndani ya mwaka mmoja na miezi sita

Asantee mkuu.
natamani kukufundisha mengi juu ya huo ufugaji lakini ni mambo mengi na nikianza hapa kumaliza ni ngumu kupitia reply moja kikubwa ukitaka kufuga kwanza ni vyema kujua namna ya kuwakinga mifugo yako na magonjwa,wadudu udumavu na ubora wa kile unacho kifuga
kuna vitu huwezi vipata kupitia vitabu bali ni kupitia pale unapofanya
nakushauri anza kumsoma kuku kwanza,hakika hutoyumbishwa nakwambia hivyo kwani na utalamu juu ya hayo mambo kwa zaidi ya miaka 25 nimemsoma kuku kunzia niko kidato cha kwanza, adv katika somo la AGRI sahivi nafikiri limefutwa pale galanos

piga hesabu za ulishaji jua njia za kukata gharama bila kuharibu production, soko lipo endapo kuku wako mtu akiwaona wanavutia.na kwa hiyo idadi kubwa unayotaka kuwa nayo hakikisha unapesa ya kuwalisha hao kuku kwa miezi mitatu mbele hii itakusaidia kutoyumbishwa sokoni
 
Mimi hata sikuagwa nikiambiwa baada ya siku tatu kuku wamefungiwa Banda.

Ikabidi nimtume mtu akawahamushie Kwa Kwa jamaa yangu; niliemtuma nae akanipiga na kitu kizito; huko nako nilikopelekwa ikawa shida.

Nilianzw na kuku wa kienyeji 20 mpaka kijana anaondika walikuwa 170+ niliokuja kuambulia ni 15 tu
Dah..unaweza pata ugonjwa wa moyo..pole sana
 
Sawa mkuu wangu naheshimu Sana maandiko yako,lakini naahidi kuleta progress juu ya hii project na picha kadri mradi utakavyokua unaendelea. Nilichojifunza na ambacho kimenisaidia nikuwa watu wengi wenye elimu hufikiri zaidi kabla ya kutenda na hatimae kutotenda kabisa.
EEeeenHeeeee!
Huo mstari wako wa mwisho umenifanya nicheke kabisa.

Hapana, hao wenye elimu ya namna hiyo wapo Tanzania pekee.

Nikutahadharishe tena; kama utatekeleza (kwanza siamini) ulivyoyaweka hapo kwenye mada yako mwanzoni, jihesabu kuwa hasara sehemu ya juhudi zako.
Kama wewe hujali hasara na kupoteza muda, basi endelea kama ulivyopanga mwenyewe.

Ningekuelewa kama ungekuja hapa katika mada hii na kusahihisha makosa yaliyo wazi katika mpango wako huo, hapo ningekuelewa kidogo na mada yako ingeleta maana.

Lakini kung'ang'ania hapa mpango usioweza kuleta ufanisi, ni kama huu wako na kujidai kuutekeleza, inaondoa kabisa maana ya wewe kuleta mada yako hapa.

Ni kama hakuna lolote unalojifunza, na huku wewe mwenyewe umeanza kwa kuomba ushauri.

Vuta pumzi, angalia upya uliyopanga, na sahihisha yaliyo wazi kusahihishwa katika mpango wako wa mwanzo; kama kweli wewe unayo nia ya kufuga kama unavyodai.
 
Ndio maana Mimi najaribu Kwa mara nyingine ila Kwa makubaliano ya kungawia 40% ya faida
LOOooh!

Jameni, ufugaji huu unawezekana kweli?

Unao kuku wangapi mkuu 'Fursakibao'?

Hata kama kuku hao wangetaga kimiujiza, sasa utapewa taarifa kwamba kuku wamepunguza kutaga; kumbe nusu ya mayai yanayotagwa yanawekwa pembeni.
Sasa hiyo faida sijui itatoka wapi?

Ndiyo maana nasema, kwenye hizi mada hapa JF ni za kujifurahisha tu!

Kwenye mada hii hii kwa mfano, sijasoma mchango wowote ambao ninaweza kusema umekaribiana na hali halisi ya ufugaji unaoweza kuingiza faida katika kazi hiyo.

Nitaonekana kama ninakatisha watu tamaa wasitekeleze ndoto zao hata kama ndoto hizo ni za kusadikika tu, kama ilivyo letwa mada hii tunayoijadili sasa.
 
Ndio maana Mimi najaribu Kwa mara nyingine ila Kwa makubaliano ya kungawia 40% ya faida
Kwa mtindo huo utafanikiwa, sikuhizi biashara ya kumsindikiza mtu kwenye utajiri hakuna 😀!

Ni ama twende wote au niende mimi we ubakie nyuma. Ila sio mie nikupeleke wewe halafu nibakie pale pale. Kila mtu anataka maisha mazuri.

Kuna shemeji yangu ana mradi mkubwa sana wa almost kuku 20,000 kwa sasa sema yeye ni wa nyama wale. Ameajiri manager anamlipa 4M kila mwezi. Yeye ana tender interchick kuwazalishia kuku na wanapiga hela haswaa maana Meneja anafanya kazi kweli kweli.

Hivyo ndio jinsi ambavyo biashara inatakiwa kufanyika sio mambo ya wewe kukutengenezea million 30 kila mwezi halafu mie unipe laki na nusu. Hatuendi hivyo ila kwa percentage utafanikiwa.
 
Sawa mkuu wangu naheshimu Sana maandiko yako,lakini naahidi kuleta progress juu ya hii project na picha kadri mradi utakavyokua unaendelea. Nilichojifunza na ambacho kimenisaidia nikuwa watu wengi wenye elimu hufikiri zaidi kabla ya kutenda na hatimae kutotenda kabisa.
Ukiwaza sana utakata tamaa kabisa.
 
Heshima yenu wakuu
Umri wangu ni miaka 28/32, Sina mtoto wala mke na biashara kadhaa kama 3 tofauti na pia najilipa mshahara wa Mil 1.8 per month kama Gross huu nikwaajili ya matumizi yangu binafsi nakufanya saving Kwa ajili ya kuanzishia biashara mpya Sasa nimeamua niingie katika ufugaji wa kuku.

Mimi binafsi nahitaji nianze ufugaji wa kuku chotara, ambao wanataga na kuatamia, pamoja na kuku wakienyeji. Ingawa Kuna Comment ya mkuu Kalamu niliwahi isoma hapa jukwaani akiisema kuku wakienyeji hawalipi na wafugaji wengi wanafuga ufugaji wa bila faida hasa wa mazoea.

Sasa siku za hivi karibuni naona wafugaji wengine wanafakiwa kuuza kuku mmoja bei ya elfu 30 Jogoo, na jike wanauza elfu 25. Baada yakufanya utafiti kidogo nimeamua ni fanye ufugaji na target yangu ni kuku 5000, kufikia December 2025. Mpaka Sasa nakuku wanane tu, wawili wa kienyeji, sasso 5 na kroila 1. Nimeanza kuku wachache Hawa nikiwa nikiwa naandaa mabanda yakamilike ndio niongenze kuku wengine.

Je Kwa maono yenu wazoefu wa ufugaji kuku, kufuga kuku mchanganyiko wa kienyeji pure, sasso, kuchi, kroila pamoja na Mbegu nyinginezo inaleta tija?.

Je ushauri wenu ni nini juu ya Mimi kufikia target ya kuku elfu 5 ndani ya mwaka 1 na miez 6?.

Sina uzoefu wowote katika ufugaji, lakini nategemea kuwaweka vijana wakike wawili ambao wao niwazoefu katika uangalizi wakuku na ntakua nawalipa kiasi Cha pesa kulingana na makubaliano yangu na wao.

Mabanda yapo mawili Kila Moja nalijenga sehemu tofautina yako mwishoni ili niweze kujua yupi anafanya kazi nzuri ili niongenze nguvu Kwa muangalizi mzuri zaidi.

Budget yangu ni 462,000/= Tzsh. Kwa Kila mwezi ndani ya miezi sita yakwanza, hii nipamoja nakunnua chakula pamoja na kuku wakubwa, vifaranga na chakula bila kusahu dawa na chanjo zake.

Hii 462,000 Tzsh, ninje na makubaliano ya mishahara yao.

Mpango wangu nikuku watakatakapofika 1500/2000 nisinunue kuku yeyote bali wazaliane wao Kwa wao tu.

Nimepanga kuwalipa Kila muangalizi shilling elfu 70 Kila baada ya week 2, nikiwa namaana tare 16 ntawalipa elfu 70 Kila mmoja na tare 2 ntawalipa elfu 70 Kila mmoja, hii iweze kuwasaidia wao katika suala la matumizi binafsi madogo madogo. Pia Kila mtu atakua anakaa mahala hapo kwenye Banda husika, ingawa Mimi Niko mbali kidogo na Banda husika lakini nikihitaji kufika naweza kufika ndani muda mchache usiozidi nusu saa.

Nilikua naomba ushauri wenu juu ya mradi wangu huu, kuhusu masoko ya kuwauza nimepanga hapo baadae kufungua butcha za kuuza nyama za kuku , hizi butcha nimepanga kuzifungulia Dar es Salaam Kwa hapo baadae hasa 2026 kwahio ntaweza kuuza jumla na reja reja, pia ntahitaji kununua kuku wengine kutoka Kwa wafugaji wenzangu kadri soko la wanunuzi wa jumla wakuku litakavyoongezeka.

Mradi wangu naufanyia Tanga mjini wa ufugaji, maana ndipo nimeona aridhi inanunulika Kwa bei rahisi kidogo kulinganisha na Dar es Salaam.

Nimeambatanisha Banda langu mojawapo nalolimalizia pamoja na picha kuku za kuku wangu 3.

Naamini haitokua rahisi kufikia kuku elfu 5, lakini naamini pia haishindikani kufikia malengo.

Asante wakuuu wangu na karibu niweze pata mchango na mawazo yenu kama hamtojali.
Ni dm aisee, maana kwenye miradi ya kuku kuna mengi sana na lazima machache uyajue. Kufika kuku 5k ndan ya mwana mmoja sio shiida ila ni kipato chako tuu japo hao kuku n wengi sana sana hivo waza gharama za chakula, wafanyakaz na materials mengine kwaajili ya hilo shamba lako.
 
Umeniita, nami nipo hapa.

Kwanza nitoe dukuduku. Huwa sipendi ubabaishaji katika mambo muhimu kama hili unalozungumzia hapa.

Stori yako haikunyooka sana, pamoja na kuwepo kwa mambo yanayoonekana kuwa ya maana.

Nitoe mfano: Umesema umri wako ni miaka mingapi?

Umesema unazo biashara nyingine zinazokuingizia pato la kukulipa mshahara wa Tsh. ngapi? Hizi biashara zinaendeleaje, na itakuwa vipi utakapojitumbukiza kwenye ufugaji wa holela usiokuwa na mpangilio kama huu ulioeleza hapa!

Sasa ukitaka nishiriki kwenye kutoa ushauri katika ufugaji, nyoosha stori yako ieleweke vizuri. Habari yako ina michongo mingi isiyo eleweka.
Ukilazimisha kufuga kwa kutegemea mpangilio huu ulioweka hapa nikwambie bila kusita, kwamba hufiki popote.

Kwa sasa nitakuacha na hayo machache.

N.B. Naona hapo mkuu 'Fursa Kibao' kakutia mori!
Kama unategemea kufuga kwa namna hiyo aliyoeleza hapo, utafuga kwa kusadikika tu!

Kumbuka, usinilaumu. Si nia yangu kukukatisha tamaa, lakini andiko lako kama ulivyoliwasilisha, lina maswali mengi yasiyoeleweka. Kwa kifupi ni kwamba siamini kuwa wewe uko tayari kufuga kuku.
Wew unataka ujue Ela aliyonayo bank ili iweje kama sio Uchawi na chuki
Personal details za biashara zake zingine zinakuhusu Nini !?
Wabongo kama ninyi wajinga sana
 
Kuku 100 watakuchelewesha;Anza na mia 300 angalau. Bajeti ulioitaja hapo inatosha Hadi kuku 500 Kwa mwezi.

Usitake kujifunza utaumia. Tumia wataalamu hakikisha vifaranga vinapata chanjo zote nitakuwekua list hapa ya chanjo na mda wa kuchanja
Mwaga nondo hapa
 
Heshima yenu wakuu
Umri wangu ni miaka 28/32, Sina mtoto wala mke na biashara kadhaa kama 3 tofauti na pia najilipa mshahara wa Mil 1.8 per month kama Gross huu nikwaajili ya matumizi yangu binafsi nakufanya saving Kwa ajili ya kuanzishia biashara mpya Sasa nimeamua niingie katika ufugaji wa kuku.

Mimi binafsi nahitaji nianze ufugaji wa kuku chotara, ambao wanataga na kuatamia, pamoja na kuku wakienyeji. Ingawa Kuna Comment ya mkuu Kalamu niliwahi isoma hapa jukwaani akiisema kuku wakienyeji hawalipi na wafugaji wengi wanafuga ufugaji wa bila faida hasa wa mazoea.

Sasa siku za hivi karibuni naona wafugaji wengine wanafakiwa kuuza kuku mmoja bei ya elfu 30 Jogoo, na jike wanauza elfu 25. Baada yakufanya utafiti kidogo nimeamua ni fanye ufugaji na target yangu ni kuku 5000, kufikia December 2025. Mpaka Sasa nakuku wanane tu, wawili wa kienyeji, sasso 5 na kroila 1. Nimeanza kuku wachache Hawa nikiwa nikiwa naandaa mabanda yakamilike ndio niongenze kuku wengine.

Je Kwa maono yenu wazoefu wa ufugaji kuku, kufuga kuku mchanganyiko wa kienyeji pure, sasso, kuchi, kroila pamoja na Mbegu nyinginezo inaleta tija?.

Je ushauri wenu ni nini juu ya Mimi kufikia target ya kuku elfu 5 ndani ya mwaka 1 na miez 6?.

Sina uzoefu wowote katika ufugaji, lakini nategemea kuwaweka vijana wakike wawili ambao wao niwazoefu katika uangalizi wakuku na ntakua nawalipa kiasi Cha pesa kulingana na makubaliano yangu na wao.

Mabanda yapo mawili Kila Moja nalijenga sehemu tofautina yako mwishoni ili niweze kujua yupi anafanya kazi nzuri ili niongenze nguvu Kwa muangalizi mzuri zaidi.

Budget yangu ni 462,000/= Tzsh. Kwa Kila mwezi ndani ya miezi sita yakwanza, hii nipamoja nakunnua chakula pamoja na kuku wakubwa, vifaranga na chakula bila kusahu dawa na chanjo zake.

Hii 462,000 Tzsh, ninje na makubaliano ya mishahara yao.

Mpango wangu nikuku watakatakapofika 1500/2000 nisinunue kuku yeyote bali wazaliane wao Kwa wao tu.

Nimepanga kuwalipa Kila muangalizi shilling elfu 70 Kila baada ya week 2, nikiwa namaana tare 16 ntawalipa elfu 70 Kila mmoja na tare 2 ntawalipa elfu 70 Kila mmoja, hii iweze kuwasaidia wao katika suala la matumizi binafsi madogo madogo. Pia Kila mtu atakua anakaa mahala hapo kwenye Banda husika, ingawa Mimi Niko mbali kidogo na Banda husika lakini nikihitaji kufika naweza kufika ndani muda mchache usiozidi nusu saa.

Nilikua naomba ushauri wenu juu ya mradi wangu huu, kuhusu masoko ya kuwauza nimepanga hapo baadae kufungua butcha za kuuza nyama za kuku , hizi butcha nimepanga kuzifungulia Dar es Salaam Kwa hapo baadae hasa 2026 kwahio ntaweza kuuza jumla na reja reja, pia ntahitaji kununua kuku wengine kutoka Kwa wafugaji wenzangu kadri soko la wanunuzi wa jumla wakuku litakavyoongezeka.

Mradi wangu naufanyia Tanga mjini wa ufugaji, maana ndipo nimeona aridhi inanunulika Kwa bei rahisi kidogo kulinganisha na Dar es Salaam.

Nimeambatanisha Banda langu mojawapo nalolimalizia pamoja na picha kuku za kuku wangu 3.

Naamini haitokua rahisi kufikia kuku elfu 5, lakini naamini pia haishindikani kufikia malengo.

Asante wakuuu wangu na karibu niweze pata mchango na mawazo yenu kama hamtojali.
Hio bei ya kuku ni ya wapi hio? Fanya utafiti ili usije lia baadae.

Sikiliza Soko zuri la kuku chotara na hao wa Kienyeji ni kuwauzia watu individual hawa wanunua kwa sh 20, 000/ wala sio hio 35, 000/ na pia hawa ni mmoja mmoja mmoja yaani ni mtu mmoja mmoja.

Soko kubwa ni la kuuza kwa mkupuoa sasa bei ya mkupuoa ni sh 10, 000/ hata chini ya hapo, hao ndio wanaweza chukua kuku hata 50 au 100.

Hakuna mtu wa mkupuo atanunua kuku kwa sh 20, 000/ au 35, 000/

Mayai yenye soko ni mahai ya kuku wa kisasa, fanya utafiti Dar hapo, mayai ya kienyeji ni ya familt level napo ni mmoja mmoja mteja.

Kuku wa Kienyeji ili uwafuge unapaswa kuwa na shamba kubwa na uwaachie humu na usiwe unawawazia yaani kwamba ndio unawategemea watoto wale hapo itakula kwako.

Kuku wa Biashara ni Layers na Broilers basi
 
Wew unataka ujue Ela aliyonayo bank ili iweje kama sio Uchawi na chuki
Personal details za biashara zake zingine zinakuhusu Nini !?
Wabongo kama ninyi wajinga sana
EEEeeenHeeeee!
Ona huyu mlevi, sijui anatafuta kitu gani huku JF. Umeona wapi nikiuliza 'details' hizo unazodai wewe?

Sasa ushauri wako kwake ni nini, akalewe kama ulivyolewa wewe?

In fact, wewe siyo mlevi, wewe ni chizi.
 
Ninajua unapolenga, lakini kama nilivyosema, wengine tupo hivyo. Nikiona umekengeuka nitakwambia waziwazi umekengeuka; na hasa ninapoona kukengeuka kwako ni kwa maksudi au kwa kutaka kupotezea watu muda wao.

"Chukia" upendavyo, lakini kama huna nia ya kujifunza haitakusaidia chochote.

Haya, lete unachojua wewe.
Wewe ni mzungu wa roho , haki na ibaki kwako daima
Pole kwakuwa hii ni Africa watu kaliba yako wanaitwa wenye roho mbaya na chuki binafsi ila hongera sana .NIMEPENDA
 
EEEeeenHeeeee!
Ona huyu mlevi, sijui anatafuta kitu gani huku JF. Umeona wapi nikiuliza 'details' hizo unazodai wewe?

Sasa ushauri wako kwake ni nini, akalewe kama ulivyolewa wewe?

In fact, wewe siyo mlevi, wewe ni chizi.
Huna mchango kwa Taifa kaa pembeni
 
Heshima yenu wakuu
Umri wangu ni miaka 28/32, Sina mtoto wala mke na biashara kadhaa kama 3 tofauti na pia najilipa mshahara wa Mil 1.8 per month kama Gross huu nikwaajili ya matumizi yangu binafsi nakufanya saving Kwa ajili ya kuanzishia biashara mpya Sasa nimeamua niingie katika ufugaji wa kuku.

Mimi binafsi nahitaji nianze ufugaji wa kuku chotara, ambao wanataga na kuatamia, pamoja na kuku wakienyeji. Ingawa Kuna Comment ya mkuu Kalamu niliwahi isoma hapa jukwaani akiisema kuku wakienyeji hawalipi na wafugaji wengi wanafuga ufugaji wa bila faida hasa wa mazoea.

Sasa siku za hivi karibuni naona wafugaji wengine wanafakiwa kuuza kuku mmoja bei ya elfu 30 Jogoo, na jike wanauza elfu 25. Baada yakufanya utafiti kidogo nimeamua ni fanye ufugaji na target yangu ni kuku 5000, kufikia December 2025. Mpaka Sasa nakuku wanane tu, wawili wa kienyeji, sasso 5 na kroila 1. Nimeanza kuku wachache Hawa nikiwa nikiwa naandaa mabanda yakamilike ndio niongenze kuku wengine.

Je Kwa maono yenu wazoefu wa ufugaji kuku, kufuga kuku mchanganyiko wa kienyeji pure, sasso, kuchi, kroila pamoja na Mbegu nyinginezo inaleta tija?.

Je ushauri wenu ni nini juu ya Mimi kufikia target ya kuku elfu 5 ndani ya mwaka 1 na miez 6?.

Sina uzoefu wowote katika ufugaji, lakini nategemea kuwaweka vijana wakike wawili ambao wao niwazoefu katika uangalizi wakuku na ntakua nawalipa kiasi Cha pesa kulingana na makubaliano yangu na wao.

Mabanda yapo mawili Kila Moja nalijenga sehemu tofautina yako mwishoni ili niweze kujua yupi anafanya kazi nzuri ili niongenze nguvu Kwa muangalizi mzuri zaidi.

Budget yangu ni 462,000/= Tzsh. Kwa Kila mwezi ndani ya miezi sita yakwanza, hii nipamoja nakunnua chakula pamoja na kuku wakubwa, vifaranga na chakula bila kusahu dawa na chanjo zake.

Hii 462,000 Tzsh, ninje na makubaliano ya mishahara yao.

Mpango wangu nikuku watakatakapofika 1500/2000 nisinunue kuku yeyote bali wazaliane wao Kwa wao tu.

Nimepanga kuwalipa Kila muangalizi shilling elfu 70 Kila baada ya week 2, nikiwa namaana tare 16 ntawalipa elfu 70 Kila mmoja na tare 2 ntawalipa elfu 70 Kila mmoja, hii iweze kuwasaidia wao katika suala la matumizi binafsi madogo madogo. Pia Kila mtu atakua anakaa mahala hapo kwenye Banda husika, ingawa Mimi Niko mbali kidogo na Banda husika lakini nikihitaji kufika naweza kufika ndani muda mchache usiozidi nusu saa.

Nilikua naomba ushauri wenu juu ya mradi wangu huu, kuhusu masoko ya kuwauza nimepanga hapo baadae kufungua butcha za kuuza nyama za kuku , hizi butcha nimepanga kuzifungulia Dar es Salaam Kwa hapo baadae hasa 2026 kwahio ntaweza kuuza jumla na reja reja, pia ntahitaji kununua kuku wengine kutoka Kwa wafugaji wenzangu kadri soko la wanunuzi wa jumla wakuku litakavyoongezeka.

Mradi wangu naufanyia Tanga mjini wa ufugaji, maana ndipo nimeona aridhi inanunulika Kwa bei rahisi kidogo kulinganisha na Dar es Salaam.

Nimeambatanisha Banda langu mojawapo nalolimalizia pamoja na picha kuku za kuku wangu 3.

Naamini haitokua rahisi kufikia kuku elfu 5, lakini naamini pia haishindikani kufikia malengo.

Asante wakuuu wangu na karibu niweze pata mchango na mawazo yenu kama hamtojali.
Kwa hali ya hewa ya Tanga ni joto na hayo mabanda yako umeyajenga mafupi mno hili litapelekea kuku kutopata hewa nzuri na hupelekea vifo kwa kuku

Kwaio mm ushauri wangu ni bora ungeyarefusha mabanda hyo na uweke madirisha makubwa ili hewa iingie vizuri

Nakushauri hivi bcz yashanikuta
 
Heshima yenu wakuu
Umri wangu ni miaka 28/32, Sina mtoto wala mke na biashara kadhaa kama 3 tofauti na pia najilipa mshahara wa Mil 1.8 per month kama Gross huu nikwaajili ya matumizi yangu binafsi nakufanya saving Kwa ajili ya kuanzishia biashara mpya Sasa nimeamua niingie katika ufugaji wa kuku.

Mimi binafsi nahitaji nianze ufugaji wa kuku chotara, ambao wanataga na kuatamia, pamoja na kuku wakienyeji. Ingawa Kuna Comment ya mkuu Kalamu niliwahi isoma hapa jukwaani akiisema kuku wakienyeji hawalipi na wafugaji wengi wanafuga ufugaji wa bila faida hasa wa mazoea.

Sasa siku za hivi karibuni naona wafugaji wengine wanafakiwa kuuza kuku mmoja bei ya elfu 30 Jogoo, na jike wanauza elfu 25. Baada yakufanya utafiti kidogo nimeamua ni fanye ufugaji na target yangu ni kuku 5000, kufikia December 2025. Mpaka Sasa nakuku wanane tu, wawili wa kienyeji, sasso 5 na kroila 1. Nimeanza kuku wachache Hawa nikiwa nikiwa naandaa mabanda yakamilike ndio niongenze kuku wengine.

Je Kwa maono yenu wazoefu wa ufugaji kuku, kufuga kuku mchanganyiko wa kienyeji pure, sasso, kuchi, kroila pamoja na Mbegu nyinginezo inaleta tija?.

Je ushauri wenu ni nini juu ya Mimi kufikia target ya kuku elfu 5 ndani ya mwaka 1 na miez 6?.

Sina uzoefu wowote katika ufugaji, lakini nategemea kuwaweka vijana wakike wawili ambao wao niwazoefu katika uangalizi wakuku na ntakua nawalipa kiasi Cha pesa kulingana na makubaliano yangu na wao.

Mabanda yapo mawili Kila Moja nalijenga sehemu tofautina yako mwishoni ili niweze kujua yupi anafanya kazi nzuri ili niongenze nguvu Kwa muangalizi mzuri zaidi.

Budget yangu ni 462,000/= Tzsh. Kwa Kila mwezi ndani ya miezi sita yakwanza, hii nipamoja nakunnua chakula pamoja na kuku wakubwa, vifaranga na chakula bila kusahu dawa na chanjo zake.

Hii 462,000 Tzsh, ninje na makubaliano ya mishahara yao.

Mpango wangu nikuku watakatakapofika 1500/2000 nisinunue kuku yeyote bali wazaliane wao Kwa wao tu.

Nimepanga kuwalipa Kila muangalizi shilling elfu 70 Kila baada ya week 2, nikiwa namaana tare 16 ntawalipa elfu 70 Kila mmoja na tare 2 ntawalipa elfu 70 Kila mmoja, hii iweze kuwasaidia wao katika suala la matumizi binafsi madogo madogo. Pia Kila mtu atakua anakaa mahala hapo kwenye Banda husika, ingawa Mimi Niko mbali kidogo na Banda husika lakini nikihitaji kufika naweza kufika ndani muda mchache usiozidi nusu saa.

Nilikua naomba ushauri wenu juu ya mradi wangu huu, kuhusu masoko ya kuwauza nimepanga hapo baadae kufungua butcha za kuuza nyama za kuku , hizi butcha nimepanga kuzifungulia Dar es Salaam Kwa hapo baadae hasa 2026 kwahio ntaweza kuuza jumla na reja reja, pia ntahitaji kununua kuku wengine kutoka Kwa wafugaji wenzangu kadri soko la wanunuzi wa jumla wakuku litakavyoongezeka.

Mradi wangu naufanyia Tanga mjini wa ufugaji, maana ndipo nimeona aridhi inanunulika Kwa bei rahisi kidogo kulinganisha na Dar es Salaam.

Nimeambatanisha Banda langu mojawapo nalolimalizia pamoja na picha kuku za kuku wangu 3.

Naamini haitokua rahisi kufikia kuku elfu 5, lakini naamini pia haishindikani kufikia malengo.

Asante wakuuu wangu na karibu niweze pata mchango na mawazo yenu kama hamtojali.
Halafu kitu kingine kuhusu soko

Kuku chotara akishafika mkubwa hna soko sana kma broilers hawa kuku lbda utegee msimu wa skukuu ndo uuze iyo bei ya 30000 na kweli utpta pesa ila kma untka kuku wa biashara fuga broilers tu ambao ndani ya mwezi unauza

Kma utategea kipindi cha skukuu tu hao kuku utauza kweli kweli ila kma unavofikiria ww hawatokulipa niamini nakwambia haya sitaki uje kuuchukia ufugaji wa kuku mna umesema huna uzoefu nao
 
Back
Top Bottom