Naomba ushauri wenu kuhusu biashara ya ufugaji wa kuku wa mayai

Naomba ushauri wenu kuhusu biashara ya ufugaji wa kuku wa mayai

vyakula vinaendana na umri wa kuku cha kufanya nitakutimia pdf tu . vingine ni kuijiongeza kutokana na maeneo ulipo wewe mfanomimi kuna majani flani kuku wangu wanayapenda sana kulikomchina wala kabeji na hayapandwi ni kipindi cha mvua tu au sehemu zenye maji maji huwa nawapa hayo
Naiomba hiyo pdf kwenye inbox yangu mkuu
 
Natamani sana nifanye ufugaji wa kuku wa mayai. Nimefanya tafiti lakini kulingana na na eneo nilipo baadhi taarifa kama bei za chanjo nimekosa. Msaada mwenye kujua bei ya chanjo zake, kama ana file la bei anaweza kushare hapa please.
 
Biashara ya kuku wa mayai sio mbaya katika uwekezaji, ila ushauri wangu Anza na kuku wachache kwanza hata kama una mtaji mkubwa, Hawa sio kuku wa nyama kuwalisha Hawa viumbe mpaka waanze kutaga inachukua miezi mpaka 6, Hawa wajomba hawalali kazi Yao kubwa iliyowaleta hapa duniani ni kupiga msosi, na gharama za vyakula vyao na vitamin na dawa za kuwachanganyia kwenye maji zimepanda pia.... Kwa hiyo unaweza kukimbilia kuwafuga wengi badae ikawa mtihani katika kuwafuga.

Nimeona watu wengi wakiwauza kabla hawajataga baada ya kushindwa kuwahudumia mpaka mwisho.

Tahadhari nyingine tafuta sehem au namna umeme uwe wa uhakika Hawa kuku umeme ukikatika ni wajinga sana watatafuta Kona Moja watarundikana na kulaliana kesho unaweza Kuta hata 50 wamekufa kwa kulaliwa na wenzao, sehemu iwe tulivu, kwenye paa lao akitokea hata mtoto mtundu akarusha jiwe watalaliana sehemu Moja kwa hofu na watakufa wengine.

Uwe na roho ngumu kidogo, kuna kaupepo ka ugonjwa kakipita wao kufa hata 30 Kila siku sio jambo la ajabu sana, lakini Mungu akisaidia inalipa maana wakianza kutaga unaongeza na mke wa pili kabisa😃😃

Nimeona nikupe baadhi ya changamoto chache wengine wataleta mengine
✌️✌️Bingo mkuu
 
Back
Top Bottom