Naomba ushauri wenu, nataka kwenda kwa mganga

Impossible is possible... Ndivyo yalivyo maisha, si kwako tu... Akili yako ni kubwa sana kuliko changamoto zako, endelea kufikiri na kupambana
 
Ukiwa na ujasiri,hakuna kinachoshindikana mkuu!!kilala kheri !
 
HONGERA kwa kuweka kisa chako hapa! Naamini kabisa kwa kufanya hivyo utapata msaada utakaokufungua toka katika masahibu yako!

Lakini pia Pole sana kwa unayopitia!

Inawezekana kabisa kujitoa kwako kwa wengine ndiyo kumekufikisha hapo! Unajua si kila unayempa utabarikiwa! Kuna mikono mingine ina roho ya kuua! Unampa mtu pesa inakurudishia majibu tofauti! Anaitumia pesa hiyo uliyompa kuvuta baraka zako kwake! Anatumia pesa hiyo kuiba nyota yako ya kifedha! Anaitumia pesa hiyo kuua kinachokuingizia kipato nk.

Cha kufanya ni kuzidisha maombi! Naona umekaribia kutoka kwenye huo mkwamo wa kiuchumi! Unachopaswa kufanya ni kutoa sadaka na kumuomba Mungu kupitia sadaka hiyo akakufanikishe katika mambo yako yote! Omba kwa nguvu, ikibidi funga na kemea kila roho ya mauti iliyoua kazi yako na uchumi wako ikuachie! Kata kamba za mauti zilizokufunga mikono, miguu na uchumi wako! Safisha mikono, miguu yako nk kwa damu ya Yesu naamini utarudi kwenye hali nzuri! Usikate tamaa wala USIJARIBU KWENDA KWA MGANGA! NARUDIA, USIENDE KWA MGANGA!

POLE SANA!
 
Asante sana kwa ujumbe wako
 
Usiende kwa Mganga wa Connections za kutoka Jf, utakuja kunishukuru....!

Uliza tu Mtaani kwako.
 
Uzuri kwenye hatua za utafutaji maisha, unaruhusiwa kufanya lolote lile ili mradi usivunje sheria za nchi. Kwahyo, kama unahisi hiyo pia ni njia sahihi kwako ya utafutaji, bhas sisi ni nani tukupinge?
 
kwenye hali ngumu hauko peke yako mkuu ,,endelea kupambana tu
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…