Naombeni mawazo yenu kuhusu hii ramani ya nyumba yangu

Naombeni mawazo yenu kuhusu hii ramani ya nyumba yangu

Wakuu mambo vipi.
Nina ramani ambayo nimeandaa kwa ajili ya kujenga nyumba ya vyumba vitatu.(1 master bedroom + 2 normal rooms).
Nyumba itapauliwa kwa mtindo wa Hidden Roof a.k.a contemporary

Naombeni mawazo yenu juu ya hii ramani.

  • Nini cha kuboresha?
  • Nini kimekosewa/hakijakaa sawa?
  • Nini cha kurekebisha?
  • Nini niondoe/nipunguze?

Nimeambatanisha hapa chini ramani yenyewe.

View attachment 2521843
Wsitting room mbona dirisha upande mmoja tuu?
Masterbedroom ukiwa unaendelea na mizagamuano upande wa pili wanakusikia. Choo cha master ndio ungekipachika katikati ya hivyo vyumba viwili.
Masterbedroom inapaswa kuwa na madirisha pande mbili
 
Hongera sana mkuu. Mimi naweza kusema haya kwanza:
1. Storage. Vyumbani weka au onyesha makabati ya nguo yatakuwa wapi. Kama watoto wakiwa wakubwa wataweza kusoma chumbani? Je wataweza kuwa na meza za kusomea na kufanyia hobbies zao kama coding na nyinginezo?

2. Sink za kuosha mikono. Sidhani kama unahitaji sink nje ya public bathroom kama ndani ipo pia.

3. Public bathroom ni nyembamba sana na siyo sawa sana kuwa na shower katikati ya sink na choo, yaani mtu anavuka maji kufika chooni. Ukienda haja baada ya mtu aliyetoka kuoga na umevaa soksi....

4. Kama utaratibu uko vizuri, laundry na store vichanganye viwe chumba kimoja kiwe scullery ama Butler's pantry with laundry.

5. Nadhani ulitaka mlango wa chumbani usionekane kutoka sebuleni, ila mtu kuingia office anapitia dining... Nadhani mtu aingie ofisini kupitia foyer maana unaweza pata mgeni wa kikazi ambaye unaweza kumalizana naye ofisini kabla hajafika maeneo mengine ya nyumba.

Hivyo mimi ningeua ukuta wa dining wa corridor ili dining iongezeke na kuhamisha mlango office uwe upande wa foyer. Ulitaka unaweza kuweka mlango wenye frosted glass kati ya bedroom/office/ washroom kutenga maeneo ya vyumbani na maeneo ya sebuleni
Point zako 6 za nguvu nimezichukua mkuu, nazifanyia kazi
 
Tafuta ramani nyingine ambayo chumba chako kitakuwa mashariki, chumba cha watoto wa kiume mashariki, halafu cha watoto wa kike kusini.

Haiwezekani ujenge nyumba halafu vyumba vyote viko upande mmoja. Mtajikuta muda wote mnaongea na kufanya mambo yenu bila ya uhuru.
Sawa mkuu, Acha niliangalie hilo
 
Nahitaji pia maoni wakuu, kwa ramani hii
 

Attachments

  • IMG_20221117_110941.jpg
    IMG_20221117_110941.jpg
    509.7 KB · Views: 51
Hiyo raman haijazingatia faragha za master bedroom, haijazingatia matumiz sahihi ya ardhi hata kama una eneo kubwa ramani upana tu sio chini ya mita 14 urefu mita 12, ramani itaku cost si chini ya matofali 4,000 wakat hayo matofali ungepata raman nzuri yenye hivyo vitu na ungeongeza chumba cha 4. Inshort raman itakugharimu pesa nyingi kama unajenga kwa pesa za vikoba
Mkuu, hebu fafanua ili kunipa mwangaza...

Unasema ramani haijazingatia matumizi makubwa ya ardhi...kivipi?
 
Point zako 6 za nguvu nimezichukua mkuu, nazifanyia kazi
Karibu sana.

Kama ungependa, acha pia nikuonyeshe post niliyoanzisha hivi karibuni ya jinsi ninavyodesign . Kuna vitu utaweza kupata hapa pia.

 
Mkuu, hebu fafanua ili kunipa mwangaza...

Unasema ramani haijazingatia matumizi makubwa ya ardhi...kivipi?
Kiwanja chako ni SqM ngapi..? (Upana mita ngapi na urefu mita ngapi..?)
Raman yako upana ni mkubwa itabana nafasi kama kiwanja chako chini ya sqm 600. Jitahidi nyumba iache mita 3.5 au 4 kulia na kushoto.
 
1. Hii kitu inaitwa "foyer" imenikera!! sijui ni ushamba?. Ondoa huo ukuta kati ya sebule na hiyo foyer sebule iwe kubwa na iwe wazi (utakuja kunishukuru). Sebule ndio maana inaitwa "living room" inatakiwa iwe kubwa isibanwe banwe, pia kuta zinaleta giza tu ndani unakuta nyumba saa nane mchana mmewasha taa!!. Hata hiyo foyer itakuwa na giza ni busara kuondoa huo ukuta.
2. Hivi vitu vinaitwa "office" au "study room" pale kwangu zimeishia kuwa store[emoji23][emoji23] Tumeweka makorokoro kibao hata hakuingiliki. Wageni wakija tunaongelea sebuleni kama kuna issue itahitaji documentation au kufanya kazi kwenye laptop kuna meza simple ya juu iko hapo pembeni sebuleni tunahamia hapo tunamalizana (otherwise sijui nature ya shughuli zako kama ni 24/7 unafanyia home).
Watoto wanasomea kule chumbani kwao kuna vimeza vidogo vya kusomea. Ni ngumu kumuhamisha mtoto akasomee "study room" kwanza wanaogopa kukaa huko peke yao hawajapazoea.
Mkuu asante kwa inputs:

1. Foyer/entryway ni vitu ambavyo wabongo hatuwekagi/hatuvijuagi... ila huko mambele more than 90% ya nyumba zao huwa na entryway.(nimekuwa inspired kutoka kwao). Entryway ina functionality zake, ambazo naona kwangu ni muhimu.

Ili kuongeza mwanga, nafikiria kuondoa huo ukuta unaoelekea dining ili kuwe na space na mwanga.

2. Kuhusu kuweka meza ya ofisi sebuleni, kwa mimi it's a turn-off. Kuchanganya makochi na meza ya ofisi naona haijanikalia vizuri kwa usmart ninaotaka kuuweka kwenye hiyo nyumba.
Mimi napenda vitu viwe EXTRA smart. Napenda sebule iwe sebule, minimal and carefully designed.

Ushauri wako wa kule juu wa kuweka master mbele ya nyumba nimeuchukua kwa 100% na nitaufanyia kazi.

Nashukuru sana mkuu
 
Nahitaji pia maoni wakuu, kwa ramani hii
Brother hii raman yako utaichukia nyumba ukiimaliza, wageni ili waingie ndani Veranda/Kibalaza kipo Master Bedroom sio vzuri haipendez... Ihamishe ikae upande wa dining...
Mwisho wa siku uzuri au ubaya wa kitu upo machoni pa mtu, kwa maana kilamtu ana namn yake ya kupenda au kuchukia kitu... All in all raman ya nyumba unapaswa kuzingatia vitu vitatu 1. Privacy ya M/bedroom 2. Ukubwa wa raman una determine gharama za ujenzi 3. Ukubwa wa eneo lako
 
Nahitaji pia maoni wakuu, kwa ramani hii
Kuna mjumbe kashasema Baraza mbele ya master bedroom siyo poa. Bora hata iwe upande wa dining.
Toilets za 1.5*1.6 siyo mbaya, ila zipangiliwe vizuri. Mwambie mchoraji akuwekee wc, shower tray na basin na ikibidi akupe na vipimo vyake.
Jiko dogo ila kuna milango/njia tatu. Sioni likiwa practical. Mchoraji akuwekee design ya jiko- sink litakaa wapi, fridge, cooker nk. Kumbuka unahitaji prep area pia Kwa kuandaa vya kupika na pakuepulia vilivyoiva.

Vyoo na jiko huwa vinasahaulika kupangwa na wachoraji wengi. Usipokee plan isiyoonyesha mpangilio wa ndani wa vitu hivi. Bedrooms pia ni muhimu ujue kitanda na kabati au meza vitakaaje.

Mlango wa master bedroom unaweza kurudishwa nyuma kwenye hicho kicorridor chake.
 
Kuna mjumbe kashasema Baraza mbele ya master bedroom siyo poa. Bora hata iwe upande wa dining.
Toilets za 1.5*1.6 siyo mbaya, ila zipangiliwe vizuri. Mwambie mchoraji akuwekee wc, shower tray na basin na ikibidi akupe na vipimo vyake.
Jiko dogo ila kuna milango/njia tatu. Sioni likiwa practical. Mchoraji akuwekee design ya jiko- sink litakaa wapi, fridge, cooker nk. Kumbuka unahitaji prep area pia Kwa kuandaa vya kupika na pakuepilia vilivyoiva.

Vyoo na jiko huwa vinasahaulika kupangwa na wachoraji wengi. Usipokee plan isiyoonyesha mpangilio wa ndani wa vitu hivi. Bedrooms pia ni muhimu ujue kitanda na kabati au meza vitakaaje.

Mlango wa master bedroom unaweza kurudishwa nyuma kwenye hicho kicorridor chake.
Sawa Engineer
 
Brother hii raman yako utaichukia nyumba ukiimaliza, wageni ili waingie ndani Veranda/Kibalaza kipo Master Bedroom sio vzuri haipendez... Ihamishe ikae upande wa dining...
Mwisho wa siku uzuri au ubaya wa kitu upo machoni pa mtu, kwa maana kilamtu ana namn yake ya kupenda au kuchukia kitu... All in all raman ya nyumba unapaswa kuzingatia vitu vitatu 1. Privacy ya M/bedroom 2. Ukubwa wa raman una determine gharama za ujenzi 3. Ukubwa wa eneo lako
Sawa Mkuu
 
Ongeza room moja ua hyo ofisi isiyo na dirisha
Nashukuru mkuu kwa wazo.
Room 4 itakuwa too much kwa familia yangu ndogo ya watoto wadogo...
Ofisi ndogo ya nyumbani ni muhimu kwangu(ina dirisha ila kwenye ramani amesahau kuliweka)
 
Nahitaji pia maoni wakuu, kwa ramani hii

Kuna vitu viwili havijakaa sawa...

1. Kutoka jikoni kwenda vyumbani inalazimu mtu apite kwanza dinning room, then sitting room kisha aende vyumbani...

2. Kingine, position ya master naona kama ajabu kukaa mbele kiasi cha kupakana na front porch/front verandah. Mfano ikitokea unafanya mambo yetu yale nyakati za mchana hautakuwa huru sana...
 
Mkuu hao watoto SI wanakua, kinatosha kama utaweka kitandaa pekee bila kabati
Sawa mkuu... Nitaongeza ukubwa wa vyumba. Kiwanja sio kikubwa sana, ni 473 sqm... so nafikiri maybe nitaongeza iwe 3.2 * 3.5 ( kutoka hiyo 3*3). Nini maoni yako juu ya hii size mpya?
 
Wsitting room mbona dirisha upande mmoja tuu?
Masterbedroom ukiwa unaendelea na mizagamuano upande wa pili wanakusikia. Choo cha master ndio ungekipachika katikati ya hivyo vyumba viwili.
Masterbedroom inapaswa kuwa na madirisha pande mbili
Mzee wa mizagamuo mzabzab ... Asante kwa mawazo mazuri.

Nimeweka dirisha moja Sebuleni kwa sababu huwa napenda kwenye sitting room sehemu ya "Entertainment area" (ie upande wa Tv) usiwe na dirisha wala mlango, uwe plain na itawaliwe na TV, sound system, game etc peke yake. Unaonaje wazo hili kwa hii ramani?

Wazo la dirisha mbili Master bedroom nimelichukua, na nitarekebisha hapo.
 
Karibu sana.

Kama ungependa, acha pia nikuonyeshe post niliyoanzisha hivi karibuni ya jinsi ninavyodesign . Kuna vitu utaweza kupata hapa pia.

Asante mkuu, naipitia hiyo post yako... naona iko njema sana
 
Back
Top Bottom