Naombeni mawazo yenu kuhusu hii ramani ya nyumba yangu

Naombeni mawazo yenu kuhusu hii ramani ya nyumba yangu

Mzee wa mizagamuo mzabzab ... Asante kwa mawazo mazuri.

Nimeweka dirisha moja Sebuleni kwa sababu huwa napenda kwenye sitting room sehemu ya "Entertainment area" (ie upande wa Tv) usiwe na dirisha wala mlango, uwe plain na itawaliwe na TV, sound system, game etc peke yake. Unaonaje wazo hili kwa hii ramani?

Wazo la dirisha mbili Master bedroom nimelichukua, na nitarekebisha hapo.
Sawa nimekupata basi kwenye huo huo ukuta mwishoni karibu na upande wa kuta ya store weka dirisha mkuu kusaidia ventilation.
Alafu pia hapo kwenye entrance kati ya foyer na sitting room weka french doors. Hii ni kwa sababu ya ufaniai wa ac kama utaweka kwenye siting room.
 
Kwanza sijajua ukubwa wa kiwanja chako ili kushauri dimension za vyumba.
3x3 ni tu vyumba tudogo sana atlist 4x4 na master walau 5x6 pia umeweka kuta nyingi ambazo zinakaba space mfano kweny entrace kushoto huo ukuta unakaba space ya sebule... hata hiyo uliyoita ofisi ni kadogo mno 2x2.8m ni kama choo? Iliyochangamka. Kingine vyumba vinavyo share public toilet vinakuwa mbali na toilet yenyewe, pia master iwe mbali kidogo na vyumba vya watoto.

Then angalia pia budget na uharaka wako wa kuwa na nyumba uamue kwa usahihi.
Chumba cha metre 3×3 ni standard mkuu
 
Hongera sana mkuu. Mimi naweza kusema haya kwanza:
1. Storage. Vyumbani weka au onyesha makabati ya nguo yatakuwa wapi. Kama watoto wakiwa wakubwa wataweza kusoma chumbani? Je wataweza kuwa na meza za kusomea na kufanyia hobbies zao kama coding na nyinginezo?
Kuna hii kanuni ya kujifunza lay out ya kabati la nguo na kitanda vinapaswa kupangiliwaje ndani ya chumba ukizingatia dirisha/madirisha ya chumba. Hapo utaweza kujua ni wapi pa kuweka kiti na meza ya kusomea
Screenshot_20230215-160736_Instagram.jpg
 
1. hiyo laundry kuwa ndani ya jiko haijakaa vizuri
2. corridor ilivyokaa lazima itakuwa na giza itakulazim kuwasha taa hata mchana.
3. master bedroom umeificha nyuma mno ni vyema ukaona wanaoingia na kutoka ndani kwako
 
Sawa mkuu... Nitaongeza ukubwa wa vyumba. Kiwanja sio kikubwa sana, ni 473 sqm... so nafikiri maybe nitaongeza iwe 3.2 * 3.5 ( kutoka hiyo 3*3). Nini maoni yako juu ya hii size mpy

Sawa mkuu... Nitaongeza ukubwa wa vyumba. Kiwanja sio kikubwa sana, ni 473 sqm... so nafikiri maybe nitaongeza iwe 3.2 * 3.5 ( kutoka hiyo 3*3). Nini maoni yako juu ya hii size mpya?
Hiyo based on size ya kiwanja inatosha.
 
3. Public bathroom ni nyembamba sana na siyo sawa sana kuwa na shower katikati ya sink na choo, yaani mtu anavuka maji kufika chooni. Ukienda haja baada ya mtu aliyetoka kuoga na umevaa soksi....
💯🤝 nakuunga mkono hapo kwenye arragement ya shower na toilet kwenye choo cha public sio sahihi

Kikawaida ilitakiwa iwe kama alivyofanya kwenye master.

Plumbers (mafundi bomba) wengi bongo huwa wanafail hapa utakuta ukiingia kwenye choo ukifungua mlango unaanza na sink, shower halafu choo

Lakini layout inayotakiwa ni sink, choo then shower
Screenshot_20221225-065133_Pinterest.jpg
 
Standard kwenye ordinary sio moden. Vinyumba vya nation housing enzi hizo. Huwezi hata kuweka kabati, kitanda, meza na kiti chumba kimejaa. Nyumba za kishamba kabisa. We ukiwa na eneo la kutosha kwanini ung'ang'ane na tuchumba tudogo.
Au kiwanja cha 20x20 400sqm cha kazi gani? Ndio maana nilikubaliana na Mabula kwenye kupiga marufuku huto tu viwanja... anyway kila mtu na standard zake pambana mwanaume. Ila binafsi out of 1200sqm and above sihangaiki napo.
Chumba cha metre 3×3 ni standard mkuu
 
4. Kama utaratibu uko vizuri, laundry na store vichanganye viwe chumba kimoja kiwe scullery ama Butler's pantry with laundry.
Modern laundry room inahitaji kuwa na iron board/table, sink, kabati la kuwekea nguo zilizonyooshwa temporarily na vifaa vingine na hangers za kutundikia nguo. Ili kuzuia purukushani za store zetu za kibongo ni bora kutenganisha
Screenshot_20220428-145655_Pinterest.jpg


Screenshot_20220428-144927_Pinterest.jpg


Screenshot_20220428-150623_Pinterest.jpg


Screenshot_20220428-145712_Pinterest.jpg
 
Wakuu mambo vipi.
Nina ramani ambayo nimeandaa kwa ajili ya kujenga nyumba ya vyumba vitatu.(1 master bedroom + 2 normal rooms).
Nyumba itapauliwa kwa mtindo wa Hidden Roof a.k.a contemporary

Naombeni mawazo yenu juu ya hii ramani.

  • Nini cha kuboresha?
  • Nini kimekosewa/hakijakaa sawa?
  • Nini cha kurekebisha?
  • Nini niondoe/nipunguze?

Nimeambatanisha hapa chini ramani yenyewe.

View attachment 2521843
Hiyo corridor maeneo ya vyumbani itakuwa na giza sana...
 
Kweli kabisa mkuu. Ndiyo maana nikasema kama utaratibu uko vizuri aunganishe. Wazo langu lilikuwa Kwa combo ya namna hii zaidi...

Laundry and Pantry Room - Country - Utility Room - (1).png

Ila kama ni ngumu kumaintain ni Bora kutenganisha kama ulivyoshauri.

Modern laundry room inahitaji kuwa na iron board/table, sink, kabati la kuwekea nguo zilizonyooshwa temporarily na vifaa vingine na hangers za kutundikia nguo. Ili kuzuia purukushani za store zetu za kibongo ni bora kutenganisha
View attachment 2523974

View attachment 2523962

View attachment 2523963

View attachment 2523965
 
Mzee wa mizagamuo mzabzab ... Asante kwa mawazo mazuri.

Nimeweka dirisha moja Sebuleni kwa sababu huwa napenda kwenye sitting room sehemu ya "Entertainment area" (ie upande wa Tv) usiwe na dirisha wala mlango, uwe plain na itawaliwe na TV, sound system, game etc peke yake. Unaonaje wazo hili kwa hii ramani?

Wazo la dirisha mbili Master bedroom nimelichukua, na nitarekebisha hapo.
Hakikisha sebule ina madirisha si chini ya mawili lli kuweza kutembeza natural air and light kwa uhakika. Ogopa nyumba sebuleni inawashwa taa saa 7 mchana.
 
..Kwa nini master bedroom inakaa uwani? Yaani watoto wakae mbele wewe mwenye nyumba ujifiche uwani! Fanya uwezavyo chumba chako kikae mbele uwe na uwezo wa kuona chochote kinachotokea eneo la mbele la nyumba ikiwezekana uone na gate kubwa la mbele.
Wapita njia watakuwa wanasikia akiwa anapiga miti
 
Standard kwenye ordinary sio moden. Vinyumba vya nation housing enzi hizo. Huwezi hata kuweka kabati, kitanda, meza na kiti chumba kimejaa. Nyumba za kishamba kabisa. We ukiwa na eneo la kutosha kwanini ung'ang'ane na tuchumba tudogo.
Au kiwanja cha 20x20 400sqm cha kazi gani? Ndio maana nilikubaliana na Mabula kwenye kupiga marufuku huto tu viwanja... anyway kila mtu na standard zake pambana mwanaume. Ila binafsi out of 1200sqm and above sihangaiki napo.
Kuongeza ukubwa wa chochote ni kuongeza maradufu gharama ya ujenzi. Hata kama ungekuwa na kiwanja cha 400sqm kama budget yako haitoshi huwezi kufanya kitu. Ungeuliza kwanza kama mhusika ana "unlimites budget" ndio utoe ushauri wako huo.

Jamaa yangu tulianza nae ujenzi mwaka 2016 yeye akajenga mjengo mkubwa balaa (hiyo veranda mzunguko wake pekee ni hatari na inatakiwa kumiminwa) mimi nikajenga simple/standard family house, mwaka 2017 nikahamia kwangu. Yeye mpaka leo lile jumba lake halijaisha (tunakaribia kuliita gofu/pagale) na bado amepanga mpaka leo.
 
Back
Top Bottom