Naombeni mwongozo wa kupata simu kali iliyotengenezwa kati ya 2023/24

Naombeni mwongozo wa kupata simu kali iliyotengenezwa kati ya 2023/24

Reuben Challe embu toa maelezo ya kiteknolojia kuhusu samsung note 10+ kama ni nzuri kutumia
Samsung Galaxy Note 10+ ni simu nzuri kutumia ila ni flagship ya 2019 kwa hiyo nyingi zitakuwa ni used au refurbished. Utakapoenda kununua kama ni used hakikisha ina condition nzuri. Test kila kitu dukani hapohapo
Samsung Galaxy Note 10+ ukiipata kwenye condition nzuri ina advantage nyingi kama kioo kizuri cha AMOLED, ukaaji wa chaji ni mzuri, speaker kali, fast charging, kamera nzuri mbele na nyuma,
storage kubwa 256GB/512GB, sehemu ya kuwekea memory card, design nzuri. Inakuja na Android 9 na uki update inaenda hadi Android 12 mwisho, na kumbuka Android 15 Beta imeshatoka, kama haujali kuhusu matoleo mapya ya Android basi itakufaa.
Pia inakuja na USB Type C 3.1 kwa hiyo ina support Video Out na Samsung DeX
 
Mkuu naomba uzungumzie hii redimi 13c
Redmi 13C ni simu nzuri tu, ila nunua kwa bei ya around 270K. Ina design nzuri, kioo kizuri chenye 90Hz refresh rate, kamera nzuri wakati wa mchana (kwa bei hii), unaweza kuweka memory card na charger unakuta kwenye box.
Kuna vitu vya kuzingatia lakini, kama wewe ni gamer, hii simu haitafaa. MediaTek Helio G85 ni low end chipset kwa hiyo hata GPU ni low end, so consider kuongeza hela kidogo upate simu yenye advantage kadhaa kama Samsung Galaxy A24 au Galaxy A15 hivi kwa 350K, sio kwamba ziko vizuri sana kwenye gaming ila kwa bei hii zina angalau kuliko hii Redmi 13C.

Kama wewe unataka kuitumia kuangalia movie keep in mind, ina speaker moja tu, sio stereo na hata sauti yake pia sio kubwa ipasavyo ni ya kawaida tu.

Kama hujali hizo weakness ni simu nzuri kwa 260K-280K
 
Wakuu kama kichwa kinavyojieleza hapo juu, nahitaji kujua Smartphone iliyotengenezwa hivi karibuni, isipokuwa TECNO, INFINIX NA ITEL..

Ninahitaji kununua Smartphone mpya, Budget yangu 450k hadi 500k pia processor isiwe ya SPD au MTK, hii sizihitaji katika list yangu.
Tecno pop 7 pro ya mwaka 2023 hahahahaha
 
Redmi 13C ni simu nzuri tu, ila nunua kwa bei ya around 270K. Ina design nzuri, kioo kizuri chenye 90Hz refresh rate, kamera nzuri wakati wa mchana (kwa bei hii), unaweza kuweka memory cardna charger unakuta kwenye box.
Kuna vitu vya kuzingatia lakini, kama wewe ni gamer, hii simu haitafaa. MediaTek Helio G85 ni low end chipset kwa hiyo hata GPU ni low end, so consider kuongeza hela kidogo upate simu yenye advantage kadhaa kama Samsung Galaxy A24 au Galaxy A15 hivi kwa 350K, sio kwamba ziko vizuri sana kwenye gaming ila kwa bei hii zina angalau kuliko hii Redmi 13C.

Kama wewe unataka kuitumia kuangalia movie keep in mind, ina speaker moja tu, sio stereo na hata sauti yake pia sio kubwa ipasavyo ni ya kawaida tu.

Kama hujali hizo weakness ni simu nzuri kwa 260K-280K
Kwa ajili ya kuperuzi tu nimependa screen size. Naomba pia ugusie ukaaji wake wa chaji nitashukuru
 
Kwa ajili ya kuperuzi tu nimependa screen size. Naomba pia ugusie ukaaji wake wa chaji nitashukuru
Hiyo simu inatunza chaji vizuri tu. Kama unaitumia kwa kuperuzi mitandaoni, kuangalia video, kusikiliza mziki nk inafaa sana, utakuwa unaichaji mara moja kwa siku.
Utunzaji wake wa chaji ni mbovu kwenye gaming tu. Haikufikishi hata masaa 6 ukiwa unacheza games. Ila tasks nyingine tofauti na gaming inatunza chaji vizuri sana.
Mwisho kuchaji kutoka 0 hadi ijae 100 ni masaa 2 na dakika kama 10 hivi kwa test za gsmarena
 
Aiseee this time nahitaji simu ambayo haina ishu za overheating, huwa nacreate content kwa simu sasa niliikimbia sd888 maana nilitaka kuchukua note 20 ultra ila nikakimbia ishu za overheating. 8 gen 1 sikujua pia kama ina hizo ishu,

Nikataka kuhamia kwenye Google pixel 6 pro na yenyewe nikasikia ina ishu za overheating, hapa sijui kama nilifanganywa au lah, mwisho nikadondokea Bionic A14 ila Nimeanza kuregret maana simu inaoverheat na hili ndio nilikuwa nalikimbia.

Nishauri kama kuna soc yenye thermal efficiency nzuri.
Mkuu inategemea bei yako ni ipi ila chipset zenye thermal management nzuri zipo nyingi sana
*Kuna Qualcomm Snapdragon 7+ Gen 2 kwenye Redmi Note 12 Turbo/ Poco F5 (laki 6 bei AliExpress)
*Kuna MediaTek Dimensity 9200 kwenye Xiaomi 13T Pro (milioni 1 na laki 2 AliExpress)
*Kuna MediaTek Dimensity 8200 kwenye Xiaomi 13T (Laki 8 na nusu AliExpress)
*Kuna Samsung Exynos 1480 kwenye Samsung Galaxy A55 (Milioni 1 kwa hapa Tanzania)
*Kuna Qualcomm Snapdragon 7s Gen 2 ya kwenye Redmi Note 13 Pro 5G na Xiaomi Poco X6 (laki 5 na nusu AliExpress)
*Kuna Qualcomm Snapdragon 8+ Gen 1 kwenye Nothing Phone 1, Xiaomi 12S Ultra, Motorola Edge S30 Ultra, Poco F5 Pro, etc.
*Qualcomm Snapdragon 8 Gen 3 kwenye vivo X100 Ultra na Samsung Galaxy S24 Ultra (Ila Snapdragon 8 Gen 3 ina overheat kwenye baadhi ya simu mfano Xiaomi 14 Ultra na Oppo Find X7 Ultra)
*Kuna Apple A16 Bionic ya kwenye iPhone 15

Zipo nyingi kwa bei tofauti tofauti kwa hiyo unapochagua chipset angalia bei uliyo nayo na simu zinazotumia hizo SoC zina manage vipi heat.
Huku kwenye flagship hakueleweki, unaweza kuta simu mbili zinatumia chipset moja ila hii ina overheat nyingine hai overheat. Mfano Google Tensor G3 hai overheat kwenye Google Pixel 8 na 8Pro ila ina overheat kwenye Google Pixel 8A na ni chipset moja ileile. Cha msingi kuwa makini wakati wa kuchagua, simu ipi ina oveheat ipi hai overheat.
Soma na reviews za gsmarena kwenye Performance section zitakusaidia kukupa vitu vingi unavyotaka kujua
 
Redmi Note 13 Pro 5G ni simu nzuri, hiyo Note 13 Pro Plus ni nzuri zaidi ya Note 13 pro 5G. Ingawa niliyokuwa naongelea hapo juu ni Redmi Note 13 Pro 5G ya kawaida.
Simu ambayo sio ya kununua kwa bei hiyo ni Redmi Note 13 Pro 4G, hii simu haifai kuuzwa hata kwa laki 6 ila hizo za 5G ndio ziko vizuri

Kuhusu battery test zote mbili utunzaji wake wa chaji ni average. Advantage yake ni kwamba hazichukui muda kujaa chaji. Hiyo Note 13 Pro 5G inatumia around dakika 45 kujaa chaji kutoka asilimia 0 hadi 100 na hiyo Note 13 Pro Plus 5G ni around dakika 20. Charger unazikuta kwenye boxView attachment 3027793View attachment 3027794
Ahsante sana mkuu kwa ufafanuzi ulionipa. Ninatumia Redmi 9C sasa nataka ku-upgrade maana hii imeanza majolijoli, japo imenifaa sana kwa muda wote nilioitumia. Nimeona nijichape hii, Redmi Note 13 pro 5G, kuna ile nimeona ina Ram 16GB na Storage 512GB, nafikiri itakua poa sana. Ingawa kwa aliexpress bei yake ni 850,000/=, kwa Bongo nimeona bei hiyo inauzwa kwa Redmi Note 12 pro 5g ya 8/256gb
 
Hakuna flagshiphata moja kati ya simu ulizotaja hapa mkuu
Flag ship ni topline or top tier na hii ninkwasababu ya features flani, A52 samsung sio actually flagship au fan edition lakin features ilizo nazo baadhi ni kama flag tu mfano resolution, processor ns camera, imekosa premium design tu labda glass au metal.
S9 still mpaka leo ipi kwenye kundi la flagship phone lakin ww api ukiwekewa s9 na a52 utachagua ipi?
 
Flag ship ni topline or top tier na hii ninkwasababu ya features flani, A52 samsung sio actually flagship au fan edition lakin features ilizo nazo baadhi ni kama flag tu mfano resolution, processor ns camera, imekosa premium design tu labda glass au metal.
S9 still mpaka leo ipi kwenye kundi la flagship phone lakin ww api ukiwekewa s9 na a52 utachagua ipi?
Nakazia hakuna A series ya samsung ilio flagship Au fan edition yeyote ikawa flagship hilo liweke kichwani ,kwa sasa Flagship ni S series tu na wayback walikua Note na S . Jikumbushe kidogo maboksi yaA series hua yameandikwa kaneno kapi vile (Samsung for Africa)
 
Nakazia hakuna A series ya samsung ilio flagship Au fan edition yeyote ikawa flagship hilo liweke kichwani ,kwa sasa Flagship ni S series tu na wayback walikua Note na S . Jikumbushe kidogo maboksi yaA series hua yameandikwa kaneno kapi vile (Samsung for Africa)
😂😂😂😂 Hapa sasa simo, samsungi for afrika,
Nacho sema baadhi ya feature zinazo
 
Back
Top Bottom