Follow along with the video below to see how to install our site as a web app on your home screen.
Note: This feature may not be available in some browsers.
Maza alikuwa anachepuka huyoMiezi 8 mother anavuta jiko duuh
Nalo neno[emoji16]...yani mzee baba atabaki humo anajitutumua si kwake bana.....Kuuliza si ujinga ndugu zangu. Endapo wakakubaliana Mama mtu aishi na huyo marioo wake wa uzeeni hapo kwake kwa bahati mbaya huyo Mama akafariki! Huyo Baba wa Kambo ndo atashikilia madaraka Kama Baba wa nyumba au?
Ni kwake alikokua anakaa na mume wake wa zamani...aliyemuoa...Umeongea mengi lakini hapo nilipobold pazingatie sana, kwani huna nafasi ya kumpangia mzee wako vipi Aishi. Vile vile kama mzee (baba) alifariki basi mama yako anao uwezo wa kuja kuishi na huyo mwanaume atakaemuoa kwenye boma lenu kwani hapo mama yako pia ni kwake labda kama apende kuondoka kwake.
Habari ndugu zangu. Naombeni ushauri wenu juu ya mada tajwa.
Mzee wetu amefariki miezi 8 iliyopita baada ya maisha yake yote kuwa katika ndoa na mama yetu. Mama Sasa ana umri wa miaka 68. Kwa kipindi chote tangu sisi watoto wake tuanze kujitegemea tumekuwa tukijitahidi kuwawekea mazingira mazuri ya wazee wetu.
Pamoja na kuwajengea nyumba yenye hadhi na ya kisasa lakini tumehakikisha wazee wetu wanaishi maisha standard kuanzia chakula na mahitaji yote kiasi kwamba familia ya mzee wetu imetazamwa kama familia yenye nafuu pale kijijini.
Juzi ndugu zangu waliopo kijijni wamenitaarifu kwamba kajitokeza mzee anasema anataka kumuoa bi mkubwa. Nikauliza akishamuoa ataondokanae kwa maana bi mkubwa atahama mji tuliomjengea na mzee? Wakaniambia hapana inavyoonyesha huyu mzee kafuata maisha mseleleko.
Binafsi nimejiuliza je ni sahihi mama alete mwanaume kwenye kitanda alicholala na mzee wetu? Je ni kweli nyumba tuliowajengea wazee wetu mama atumie kuishi na mzee mwingine? Alifanyalo mama sio kutufedhehesha sisi watoto tunaohakikisha anapatiwa chochote akitakacho?
Uamuzi wangu nimepanga kuvuruga mpango wa bi mkubwa. Nataka nimwite nimuombe nije niishi nae mjini kwa maisha yake yote ili nizuie mipango yake na akikataa nimepanga sitomuhudumia chochote maana Mimi ndie mwanawe mpendwa.
Je, ndugu uamuzi wangu huu nitakuwa namkosea mama yangu? Au nimwachie tu ahangaike na maisha yake? Kinachoumiza mzee muoaji mwenyewe kachoka mno hata ndala anazovaa ukute zina matundu nusu anagusa ardhi nusu malapa.
Naona kama bi mkubwa atatuongezea mzigo wa kuangalia watu wawili kwa maana akibaki mwenyewe inakuwa rahisi hata kumchukua wakati wowote. Ushauri wenu
Hapana uchumi si shida kama wataamua kuishi kwa muoaji. Tatizo naona kama fedheha kwa marehemu baba kama yule mwanaume atahamia pale. Nikiri kwamba kama wataondoka basi nitamuhudumia bila kinyongo. Hata baba zetu wadogo wanapinga boma la kaka yao kutwaliwa na huyo mtu.Kinachomzuia mwanadamu sio umri kwani matamanio hayaishi isipokuwa isipokuwa busara na hekima.......
Moja ya sehemu ya kujitambua mwanadamu ni kuishi kwa kulingana na nyakati na kujitahidi kuyadhibiti matamanio yake...........
Kuna muda kimaumbile unawatamani mabinti lakini ukitazama nyakati na umri unapuuzia na kuhamisha fikra kwenye mambo mengine......
Wale wazee wasiojitambua na kushindwa kuyadhibiti matamanio yao ndio wanakuwa vituko na kichekesho kwenye jamii..........
NB;
Unaochokipigania ni sahihi lakini umekosa hoja ya msingi na yenye nguvu kusimamia maamuzi yako.........
Unaonekana unapingana na uchumi wa huyo muoaji na sio uamuzi wa mama kuolewa.....
Haya yapo inategemea na ustaarabu wa familia. Binafsi mzee katulea ktk maadili na hatukutegemea mazingira ya namna hii. Sijajua huyo Shamte ambae kwako ww ni kioo chako.Kwahiyo shamte wa mama diamond kamchukua mama diamond kwenye nyumba yake?
Au anaishi kwa mama diamond??
Mtoa maada akijibu hapa basi atapata majibu