Naombeni ushauri ndugu zangu, seriously kabisa. Kuna sauti kila siku haiishi kuniambia kuwa mke niliye nae sio!

Ahsante sana! Sio mahiri wa hii lugha lakini kipo nilichokielewa.
 
Me navyoona huyo ulonae unampotezea muda na utapata mwingine itakua vivohivyo, yani kama uwez kutunza mapungufu ya mwenzio na kuyafurahia mazuri yake ww shimo lako ni wale wadada wa buku buku basi.
🙏🙏
 
Ukweli najivuta sana, huo ndo ukweli
Sawa mkuu nimekuelewa

Ni hivi hujampenda huyo mdada na ndio nilichoona katika maelezo yako,ingawa watu hawakuelewi,na kibaya Zaidi huenda hata wewe umeshindwa kujieleza vizuri

Nilipitia hiyo Hali ndio maana imekuwa rahisi Mimi kukuelewa.

Pole Sana Kwa changamoto
 
Ahsante, pamoja.
 
Mume ndo kiongozi mkuu, yaani aishi vyovyote anavyotaka?
 
Shukrani
 
Kosea vitu vyote, lakini, usikosee kuoa.

Ushauri wangu kwako :
Kwakuwa tayari umeshamuoa na nafsi yako inakwambia umeingia chaka, kilichobakia huwezi kumwacha, maana ukimwacha utakuwa unatenda dhambi.

Cha kufanya, jifunze na jizoeze "kukubaliana kutokubaliana".
 
Kusema za kweli haki we unamtafutia sababu tu huyu Dada umuache. Na hapa Kuna mawili, eiza una limchepuko linakuharibu akili au umerogwa. Au vyote fullstop
Hata hakuna uchepukaji wa kuharibu ndoa, basi tu
 
Kabla hamjaoana mlikuwa wachumba kwa muda gani? Kabla hujamuoa alikuwa anavaa mavazi gani? kama ni dera imemkuta nalo hivyo huna budi kukubali hali.

Umeongelea kulima je ulimuoa awe jembe au ulimuoa awe msaidizi wako.
Sitachangia sababu unayemhofia kuwa yeye, ndiye huyo anayelala mapema sababu za uchovu.
Je, chakula anachopika kianatoka wapi?
 
Mama yake ndio binadamu wa kwanza kumuona alipoanza kupata ufahamu,huwezi kuzuia hilo.....sema tu humtaki
Uonwaji wa mama uwe wa kiasi.....mtoto ameshakuwa sio mtoto tena
 
Ahsante sana dada, nitazingatia.
 
Hapa kwenye [emoji116]

5. Uchapakazi hafifu (si mwenye kuweza kulima ipasavyo),

Nakushauri:
Nunua powertiller, inalima speed mno.
Ni million 10 TU unaepuka hii kero mkuu[emoji41]
Dah!
 
On serious note,
Yote uliyoelezea nmegundua
Mkeo ana tatizo la ujuaji mwingi.

Yaan she's is too much know,

Na hili Ni janga sana pale baba unapotaka kusimama fully Kama Kichwa Cha familia.

Cha kufanya,
Tumia "martial law" atarudi mstarini[emoji41]
Safi, ahsante
 
Daah basi ningekupa huyu nilienae basi ungekufa mapema,..vumilia ndugu kunamahali unaweza ukamuacha huyo ukapata kituko ambacho utajuta zaidi.hayo mapungufu yakawaida kabisa
Ahsante
 
Usijekuwa unanyemelewa na Schizophrenia mkuu, hilo lisauti linalopaza ndani yako kiasi cha kukuvuruga hivyo si hali ya kawaida! Kuna watu wamefanya maamuzi ya ajabu kwa sababu ya sauti kama hizo!
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…