Naona Maulid Kitenge na Wasafi FM ulikohamia rasmi mmeshaanza ‘ kuchemsha ‘ mapema tu

Naona Maulid Kitenge na Wasafi FM ulikohamia rasmi mmeshaanza ‘ kuchemsha ‘ mapema tu

Hiki ninachosikia hapa kama ni kweli, basi watangazaji wa Tanzania wanapanda bei kama wacheza mpira wa ulaya.
Yaani unaambiwa watangazaji wanaletwa kwa helicopter, hizi mbwembe sidhani hata BBC wamewahi kufanya.
 
Nimeshangaa tu Makonda hajaalikwa

Amesajiliwa rasmi na Majizo kuwa Msoma Vichwa vya Habari vya Magazeti katika Kipindi cha Joto la Asubuhi huku Uongozi wa Mkoa wa Dar es Salaam akituachia Sisi wana Dar es Salaam wenyewe.
 
saa mbili asubuhi unapata muda wa kusikiliza radio..shughuli zako za kukuingizia kipato unazifanya saa ngapi au huna kazi za kufanya?
Shughul zinatofautiana mzeee. Kuna mwingine ni dalali, mwingine ni mjasiliamal mambo yake anayaamua mwenyewe na kutoa malekezo kwa watu wake.

Mwingine yupo likizo. Kuna sababu nyingin hapa mzee
 
Maelezo meeeengi
Tokea nizaliwe hadi leo hii nipo Mkubwa hivi Kula yangu au Ustawi wangu mzima wa Kimaisha ulikuwa unakutegemea ' Mpumbavu ' Wewe? Nimeshawahi hata Siku moja kuja Kukugongea Kwako kuwa nataka Unipe Ugali wako na Matembele unayoshindia 24/7? Nilikuwa sijui kumbe kwa Tanzania hii ili Mtu aonekane umeenda Kazini ni mpaka uamke Alfajiri upambane na Madalala na urejee Jioni ndiyo unajulikana umeenda Kazini? Sasa nakubaliana tena kwa 100% yale ' Matusi ' ambayo Waafrika wengi tumekuwa tukipewa na Rais Trump wa Marekani. Tuna matatizo makubwa ' Ubongoni ' mwetu. Na ulivyo ' Mpumbavu ' wa ' Kutukuka ' hujui kuwa wengine ' Fani ' zao ni za Kutegemeana ambapo wakisikiliza Kipindi husika basi na Wao hapo hapo wanapata ' Tips ' za Kihabari / Kitaarifa na pia wanatengeneza vyema ' News Angles ' zao kisha wanazitumia kwa Matumizi yao mengine ambayo baadae pia yanawaongezea Vipato vyao na Maisha yao yanaenda. Nimefurahi Kukutana na ' Mpumbavu ' Mmoja Wewe mapema Asubuhi hii.
 
Hiki ninachosikia hapa kama ni kweli, basi watangazaji wa Tanzania wanapanda bei kama wacheza mpira wa ulaya.
Yaani unaambiwa watangazaji wanaletwa kwa helicopter, hizi mbwembe sidhani hata BBC wamewahi kufanya.

Hiyo ni mbinu nzuri tu ya Kujitambulisha na Kujitangaza zaidi hivyo wala sioni tatizo juu ya hilo. Lakini pia mambo kama haya pia yanaibua mwamko, kuongeza chachu na kuibua Ubunifu zaidi hasa kwa Wanafunzi wa Fani husika ya Habari na Utangazaji na hata kwa Watangazaji wa Vipindi vingine katika Redio zingine.
 
Tokea Siku ya Alhamisi iliyopita tena katika Kurasa zako mbalimbali za Mitandao Wewe Maulid Kitenge na mpaka Jana Usiku ulikuwa ‘ ukituhimiza ‘ kuwa Sisi Wapenzi wa Michezo vya Redio hasa vile ambavyo huwa unaviendesha Wewe tusikose na wala tusithubutu ‘ Kubanduka ‘ katika 88.9 Wasafi fm kwani Kuanzia Saa 2 Kamili asubuhi hadi Saa 5 Kamili asubuhi utakuwa ‘ unazindua ‘ hicho Kipindi chako Kipya cha ‘ Sports Arena ‘ lakini cha Kusikitisha hadi hivi sasa Saa 2 hii na Robo Kipindi hakijaanza na nasikia tu Kipindi sijui cha Jogoo na ‘ Upuuzi ‘ mwingine.

Sasa nimeamini rasmi kuwa duniani kote anayejua kwenda na muda, ahadi na kuheshimu Ratiba zake na huwa hakosei ni Mzungu tu peke yake. Kama Siku zingine mkiwa mnajua kabisa kuwa hamna huo ‘ Ustaarabu ‘ walionao Wazungu basi msiwe ‘ mnajitutumua ‘ kujifanya nanyi mnauweza ‘ Ustaarabu ‘ Wao.

Hakuna Kitu ambacho nakichukia kama ‘ Uswahili Uswahili ‘ na ‘ Uwongo ‘ au Mtu kutotimiza ‘ Ahadi ‘ yake. Hata kabla ya Kipindi chako tu Kuanza tayari ‘ umeshanikwaza ‘ na sasa nadhani nitaendelea tu Kusikiliza Kipindi cha ‘ Sports Headquarters ‘ ambacho naona kina ‘ Ustaarabu ‘ na Watu makini na siyo huu ‘ Upuuzi ‘ wako wa Kutuambia tukutegee Masikio Saa 2 hii halafu mnatupigia tu miziki yenu. Hovyo kabisa!

Kwanza hata Li ' Redio ' lenyewe halisikiki vizuri kwani ' Frequency ' yake nayo ni mpaka ukae sehemu nzuri au uipindue pindue Redio au uiweke chini ya Uvungu kama si Dirishani ndipo unaishika vizuri vinginevyo utabaki kusikia Makelele tu. Efm au Clouds fm au Magic fm ambazo zote zina Vipindi vizuri kabisa vya Michezo havina hili tatizo na huu ' Upuuzi ' hivyo kwa dalili hii mpaka unaona GENTAMYCINE ' nimekwazika ' hivi tayari ' Nuksi ' imeshaanza na sijui kama hata Wasikilizaji nao mtawapata wengi. Yaani naamka mapema Kujiandaa Kusikiliza Kipindi cha Michezo nakutana na Kipindi kinaongelea Kuku kwahiyo umeambiwa / mmeambiwa Sisi Wasikilizaji wenu / wako mliotuambia tusikose Kusikiliza Kipindi leo ni Kuku?
kuna clip moja hivi Kitenge alinifurahisha sana.... alikuwa EFM studio akisoma magazeti mara paap kanyanyua kiti anataka kumtwanga nacho Musiba mtandaoni.
sijui kiti angekiingizaje mtandaoni!!
 
HIVI WACHANGIAJI WA UZI HUU KWELI WANASIKILIZA WASAFI FM??!! LEO SIO SIKU YA KUANZA KIPINDI BALI NI UZINDUZI WA KIPINDI NA WAGENI WAMEANZA KUWASILI PALE MIDA YA SAA MBILI NA KUMEKUWA NA MAHOJIANO YANAYOENDELEA KATI YA WAGENI WANAOWASILI NA WATANGAZAJI WA WASAFI
NI SHEREHE ZA UZINDUZI WA KIPINDI NA SIO KIPINDI KAMILI
 
Mod mpigeni ban huyu .kwani yeye nani anatulisha maneno
 
Nimepoteza Marafiki wengi na hata Kushindwana na Mademu wengi kutokana tu na Suala zima la Muda ( Ahadi ) na Kujali Ratiba. Hakuna Kitu ambacho GENTAMYCINE nakipenda na nakiheshimu kama kwenda na muda, kuwa Mtu wa Ahadi na Kujali / Kuheshimu Ratiba. Ukitaka ' nikuchukie ' na ' tugombane ' Wewe niambie Uwongo au nipoteze muda na hapo ndiyo utanijua vizuri na huenda hata ' ukanichukia ' Maisha yako yote.

Kuna Demu Mmoja nakumbuka niliwahi Kupendana nae mno tu na alijua kuwa Mimi ndiyo nitakuja kuwa Mumewe lakini kuna Siku tulikubaliana kukutana muda fulani ( siyo kwenda Kufanya Mapenzi ) na nilifika eneo husika dakika 15 kabla ya muda wetu na Yeye alifika dakika 45 baadae tofauti na muda tuliokubaliana na kilichofuatia pale pale nilimpa ' Makavu ' yangu na kuwambia Mimi na Yeye Safari yetu ndiyo imeishia pale rasmi. Hadi hivi leo haamini Mkuu japo nakiri kuwa alikuwa ni Mwanadada Mmoja Mrembo sana lakini sikuliangalia hilo kwani GENTAMYCINE Kiasili ni Mtu wa ' PRINCIPLES ' na nitakuwa hivyo hadi nazama zangu Shimoni Kaburini pale Mwenyezi Mungu akiniita Siku aliyonipangia.

Na kilichonikasirisha zaidi kwa huyo Demu ni kwamba nakumbuka kabla kabisa ya Kukubaliana nae kuhusu muda wetu wa Kukutana nilimuuliza zaidi ya mara tano kuwa je, ana uhakika huo muda atauweza na atawahi nae kwa Kujiamini kabisa na ' Mikogo ' kibao ( kama mnavyowajua Wanawake wetu / Dada zetu ) akanihakikishia kuwa atawahi lakini hatimaye hakutimiza Ahadi yake na Urafiki wetu ukafiki Kikomo hapo hapo.

Desturi yangu mara zote nikiwa napanga ' appointment ' na Mtu yoyote yule huwa napenda kumpa Yeye nafasi ya Kupanga au Kuchagua muda husika ili ' ajinyonge ' mwenyewe na kama asipoenda na huo muda basi Kazi yangu ya Kumpa ' Makavu 'iwe rahisi na Kumalizana hapo hapo. Kama unajua huna uhakika basi usiniahidi muda wa Kukutana / Kuonana na huwa napenda mno wale Watu ambao hufika mahala dakika 15 au hata 30 kabla ya ule muda wetu tuliokubaliana. au hata kama unaona utachelewa basi nijulishe mapema hapo nitakuheshimu kuliko unanichelewesha halafu hunipi taarifa zozote za sababu ya Kuchelewa Kwako.

Sasa kwa mfano kama Maulid Kitenge na Kituo chake cha Wasafi fm kumbe walijua kuwa kwa leo Jumatatu hii hawatakuwa na Kipindi muda ule aliotuambia tokea Siku ya Alhamisi katika Kurasa zake mbalimbali za Mitandao kwakuwa watakuwa katika Sherehe za Uzinduzi kama ambazo zinaendelea sasa basi hata Jana tu kupitia Kurasa zake zile zile angetuambia au hata Kutuomba Radhi Wasikilizaji wake tofauti na ambavyo amefanya na ndiyo maana hata Mimi nimekuwa ' Mkali ' hivi Kwake / Kwao. Mawasiliano ni jambo zuri na jema sana na kwa hili kidogo ' PR ' ya Wasafi fm ' imenajisiwa ' hasa kama Wewe ukiwa ni Mwana Taaluma ' tukuka ' wa Mawasiliano ya Umma na Uhusiano. Hili Kosa lisijirudie tena tafadhali.
notisi zote hizi mwamba!!!..jua kufanya muhtasari
 
saa mbili asubuhi unapata muda wa kusikiliza radio..shughuli zako za kukuingizia kipato unazifanya saa ngapi au huna kazi za kufanya?
Mkuu ratiba za watu tofauti what if kama yuko likizo au anaingia shift ya mchana au yuko kwenye gari akisikiliza au anauza duka lake huku akisikiliza.....
 
HIVI WACHANGIAJI WA UZI HUU KWELI WANASIKILIZA WASAFI FM??!! LEO SIO SIKU YA KUANZA KIPINDI BALI NI UZINDUZI WA KIPINDI NA WAGENI WAMEANZA KUWASILI PALE MIDA YA SAA MBILI NA KUMEKUWA NA MAHOJIANO YANAYOENDELEA KATI YA WAGENI WANAOWASILI NA WATANGAZAJI WA WASAFI
NI SHEREHE ZA UZINDUZI WA KIPINDI NA SIO KIPINDI KAMILI

Kwahiyo Kosa ni letu tulioaminishwa tena hadi Kuhakikishiwa kuwa leo Saa 2 asubuhi hadi Saa 5 asubuhi Kipindi kitakuwa hewani na Maulid Kitenge au ni Wahusika wao wenyewe? Na kama walijua kuwa leo hawatakuwa na Kipindi na badala yake watakuwa na ' Uzinduzi ' kwanini pia hawakutuambia mapema kupitia ' njia ' zao zile zile kama walivyokuwa wakituambiwa hapo awali? Hata muwatetee vipi ila kwa hili la leo wametukosea mno Sisi Watu makini wakiongozwa na Mimi GENTAMYCINE.
 
Mod mpigeni ban huyu .kwani yeye nani anatulisha maneno

Bahati nzuri Moderators wa JamiiForums hawana ' Upumbavu ' ulionao na wanajitambua vile vile na huenda ' wamekudharau ' kuliko unavyodhani.

This is GENTAMYCINE ANTIBIOUTIQUE a.k.a Purely Talented, Charismatic Fella, Game Changer and Entertainer.
 
Back
Top Bottom