Napata shaka, kuna kikundi ndani ya CCM kinaratibu kumkwamisha Rais Samia 2025

Napata shaka, kuna kikundi ndani ya CCM kinaratibu kumkwamisha Rais Samia 2025

Prof Koboko

JF-Expert Member
Joined
Aug 15, 2020
Posts
350
Reaction score
2,550
Napata shaka ndani ya CCM kinaratibu mipango kiufundi sana kumkwamisha Mama 2025 ikiwa anatahitaji tena kugombea. Hili jambo tunaweza kuona kama masihara lakini tutaelewana tu mbele ya safari. Wanataka kumchonganisha Mama na wananchi na jumuiya za kimataifa ili kufikia 2025 waseme ameshindwa kutuvusha, ili waseme tunahitaji mwanaume asimame.

Haiwezekani unatuma vyombo vya usalama wanaenda usiku kukamata kiongozi wa chama kikubwa cha upinzani, chama ambacho ndio mbadala wa chama tawala kwa sababu tu anataka kufanya kongamano la kujadili katiba mpya kitu ambacho hakuna kosa lolote kisheria alilofanya. Kitu hiki kimeripotiwa media zote za kimataifa na sasa inafahamika kua Tanzania hakuna utulivu wa kisiasa (Political instability). Mwekezaji gani ataamini kua Tanzania mazingira yamebadilika kama vyombo vya usalama vinakamata mtu bila kosa lolote? Mambo ya kubambikiziana kesi kweli yamekwisha? Ni mfadhili gani alete misaada yake eneo ambalo sasa litssomeka kuna migogoro ya kikatiba?

Hili kundi linaelewa madhara makubwa ya kumkamata Mwenyekiti wa chama kikuu cha upinzani, hiki chama kina mahusiano na Democratic parties mbali mbali duniani tena vyenye dola katika mataifa makubwa makubwa. Kufanya hivi kumeichafua sana taswira ya nchi na ndio hapa Mama atakwamishwa makusudi.

Bado kuna suala la tozo za miamala, ukiliangalia kwa makini utaona ni kama lineratibiwa kiufundi sana kumchonganisha Mama na wananchi ingawa ameshtuka mapema. Hii haijawahi kutokea wananchi wanapandishiwa Tozo maradufu zaidi kwenye huduma wanayotegemea kwa kiasi kikubwa, halafu bado waziri anatoka hadharani na kuwatukana wananchi wanaolalamika tena anaongea kwa kibri bila kupima madhara yake. Huyu kiongozi unaweza kuhisi ni kama alitumwa kumharibia Mama makusudi.

Naweza kuandika haya na yakachukuliwa poa lakini tutajuana mbele ya safari. Kinachofuata ni kuibuka kwa migogoro ndani ya CCM yenyewe muda si mrefu. Hali hii itamkatisha tamaa sana Mama.
 
Napata shaka ndani ya CCM kinaratibu mipango kiufundi sana kumkwamisha Mama 2025 ikiwa anatahitaji tena kugombea. Hili jambo tunaweza kuona kama masihara lakini tutaelewana tu mbele ya safari...
Sasa kitakachofuata ni CCM hawa hawa wanaojifanya kumsifu kinafki hasa team mwendazake watamgeuka kua hafai anakidhoofisha chama kisha wataweka mtu wao.

Wanajua kabisa Mama hawezi kuja kusimama na Tundu Lissu 2025 ikiwa atasimamishwa tena. Wanachofanya nilimtoa kwenye reli mapema kwa kumchonganisha na wapinzani
 
Hivi viongozi wa Tanzania wanaisoma Katiba iliyopo ambayo wametumia kuapa? Wanajua maana ya utawala wa sheria? Wanajua kuwa CCM ndiyo ilipitisha uamuzi wa mfumo wa vyama vingi vya siasa. Hivi viongozi wanadhani wote wanaotaka Katiba na Sheria zifuatwe ni WAPINZANI?
 
CCM ni chama cha Mapaka
AABSll.jpg
 
Prof Kaboko,

Naona kitu ambacho ama hukioni au unajifanya hukioni.

Freeman Mbowe alimsonya Rais Samia hadharani na kuazimia kuangusha serikali kwa njia ya makongamano, mikutano ya hadhara na maandamano.

Kwa ufupi, Mbowe alitangaza nia ya kufanya uhaini, pure and simple.

Hauzifahamu kanuni za kuwashughulikia watu wenye dhamira ya kufanya uhaini?

Wewe ungekuwa mkuu wa serikali usingezitumia?

We have to call a spade not a spoon.
 
Prof Kaboko,
Naona kitu ambacho ama hukioni au unajifanya hukioni.
Mbowe alimsonya Rais Samia hadharani na kuazimia kuangusha serikali kwa njia ya makongamano, mikutano ya hadhara na maandamano.
Kwa ufupi, Mbowe alitangaza nia ya kifanya uhaini, pure and simple.
A spade is not a spoon.
Yaani unaleta habari za "kusonyana", hayo mambo ya kikekike peleka Saluni.
Asonywe asisonywe inabidi atii katiba na kiapo cha urais alichoapa yaani kutawala kwa mujibu wa sheria!
 
Yaani unaleta habari za "kusonyana", hayo mambo ya kikekike peleka Saluni.
Asonywe asisonywe inabidi atii katiba na kiapo cha urais alichoapa yaani kutawala kwa mujibu wa sheria!
Haya ni maoni yangu.

Nawe una yako.

Uhuru wa kusema ni pamoja na kuchagua cha kusema, lini na mahali gani kisemwe.

Kama unaona saluni kunakufaa wewe peleka disinformation yako huko.

Nukta.
 
Back
Top Bottom