Nape ataka Akaunti ya Deni la Taifa ichunguzwe na iwekwe bayana Fedha hizo zilikopwa na kupelekwa wapi?

Nape ataka Akaunti ya Deni la Taifa ichunguzwe na iwekwe bayana Fedha hizo zilikopwa na kupelekwa wapi?

Siyo uchonganishi ,ukichunguza madeni ya nyuma lazima umuhoji Dr Mpango

Sawa sio Mpango tu ndiye atakayetakiwa kutoa maelezo bali wako wakina Mustapha Mkullo aliyekuwa waziri wa fedha wa Kikwete . Bahati mbaya Basi Mramba katutoka hivi karibuni lakini aliyekuwa katibu wake Mkuu Grey Mgonja anaweza kutoa maelezo akitakiwa kufanya hivyo kwani nyaraka pia zipo!!
 
Nape asisahau waliokuwa viongozi waandamizi wa hiyo serikali anayoilaumu ndio hawa waliopo kwenye serikali mpya anayojipendekeza kwao ili apate teuzi.

Na msilete zile sababu za kukariri kwamba wasingeweza kumzuia Magufuli kwasababu alikuwa katili, kama waliona tatizo lipo na halifanyiwi kazi wote wangetakiwa kujiuzulu ili kuonesha kutokubaliana nae, lakini kukaa kwao kimya maana yake walimuunga mkono.

Anyway, nimemkumbuka Nape siku ile aliyoenda pale ikulu baada ya kuomba msamaha, alipopiga picha na Magufuli akiwa ameweka mikono yake karibu na paji la uso kama vile anamsujudia mwanadamu yule anayemuita leo mwizi.
Katika watu nawakubali hapa jf ni wewe mkuu!

Huna unafiki kabisa.
 
Viongozi wakuu wote wa sasa walikuwa viongozi wakuu wa awamu ya 5. Aliyekuwa makamu ndio Rais wa sasa, Aliyekuwa mkopaji(Waziri wa Fedha) ndio makamu wa sasa, aliyekuwa Waziri Mkuu ndio Waziri Mkuu.

Kama hajatumwa, basi anawatukana viongozi wake wakuu.

Nape acha matusi kwa viongozi wakuu wa nchi. Utapotea bila kujua. Acha kujadili na kushauri mambo mazito ukiwa na furaha sana.
 
Nape asisahau waliokuwa viongozi waandamizi wa hiyo serikali anayoilaumu ndio hawa waliopo kwenye serikali mpya anayojipendekeza kwao ili apate teuzi...
Too theoretical kuliko mazingira halisi. Nani alikuwa na ubavu wa kufanya unayoyasema!
 
Pamoja na kwamba Nape ni mnafiki, lakini kasema ukweli kuwa dhalimu alikuwa anakopa kiboya ili kusaka sifa za kijinga. Uchunguzi ufanyike ili ifahamike dhalimu alipeleka wapi hela na genge lake la sukuma gang.
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Dhalimu wako bado anakuchapa hata baada ya kufa!

Vipi nasikia mmesusia uchaguzi mdogo,, mmesusia kwani dhalimu wemu bado yupo?
 
Masikini Bashiru reeooo yupo hoiiiiii
[emoji23][emoji23][emoji23][emoji23]Mtu uko unakula vumbi na ukoo wako hakuna wa kumfikia bashiru pale alipo ila chaa jabu eti unamhurumia
 
Watamuua ingekua kipindi cha jiwe angeshatekwa , nakumbuka huyu jamaa alipotolewa bastola , nchi imepitia wakati mgumu sana hii, naona sasa wabunge wanaanza kufunguka, nimemsikia shabiby anahangaikia watumishi wa umma kwamba miaka 7 sasa hakuna nyongeza ya mishahara nikakumbuka enzi za jiwe jinsi walivyokua wameufyata mkia pamoja na kusifia sifia tu bila sababu.
 
Nape naye kenge tu. Lilipokuwa liwaziri nalo lilikua jizi, nafiki na punguani. Eti Leo linahoji kwa nini lilikunya kwenye uji. Leo eti kasahau kama alizima Bunge live na kujiona msafiiii....

CCM yote wezi tu, Sema wanatofautiana style.

Siasa ni upuuzi upuuzi tu.
 
Mbunge wa MTAMA Nape Nnauye amesema deni la Taifa limekuwa kwa kasi sana ndani ya miaka 5 iliyopita na kusema japo Serikali inadai ni himilivu hali sio nzuri...
CCM kuchunguza CCM. Waziri wa Fedha aliyekopa ndio Makamu wa Rais. Muendelezo wa Zee Commedy za CCM
 
Nape si ulionywa wewe usiwe kimbelembele bungeni au umesahau?
 
Nape naye kenge tu. Lilipokuwa liwaziri nalo lilikua jizi, nafiki na punguani. Eti Leo linahoji kwa nini lilikunya kwenye uji. Leo eti kasahau kama alizima Bunge live na kujiona msafiiii....

CCM yote wezi tu, Sema wanatofautiana style.

Siasa ni upuuzi upuuzi tu.
Turudi kwenye hoja
Matumizi ya mkopo trillion 20 yako wapi
 
Mbunge wa MTAMA Nape Nnauye amesema deni la Taifa limekuwa kwa kasi sana ndani ya miaka 5 iliyopita na kusema japo Serikali inadai ni himilivu hali sio nzuri
nape muongo, mbona tuliambiwa ndege zinanunuliwa kwa cash na ni kweli, pia akiba ya taifa benki kuu inaweza kulilisha taifa kwa miezi 6 bila kuyumba, na tuliambiwa sisi ni matajiri tutembee kifua mbele, sasa tena ?
 
Mbunge wa Jimbo la Mtama, Nape Nnauye amesema Deni la Taifa limefikia Tsh. Trilioni 64, ambapo awamu ya tano ilikopa Dola Bilioni 9 (takribani Tsh. Trilioni 20) bila kuwa na uwazi
-
Ametaka Deni la Taifa kuchunguzwa na miradi iliyofanywa kwa mikopo katika Serikali ya Awamu ya Tano iangaliwe kama inaendana
-
Aidha, Nape ameshauri uwazi uliopo kwenye Tsh. Trilioni 1.3 za IMF alizokopa Rais Samia uendelee kwa fedha nyingine
-
 
Back
Top Bottom