Nape ataka Akaunti ya Deni la Taifa ichunguzwe na iwekwe bayana Fedha hizo zilikopwa na kupelekwa wapi?

Nape ataka Akaunti ya Deni la Taifa ichunguzwe na iwekwe bayana Fedha hizo zilikopwa na kupelekwa wapi?

Nape asisahau waliokuwa viongozi waandamizi wa hiyo serikali anayoilaumu ndio hawa waliopo kwenye serikali mpya anayojipendekeza kwao ili apate teuzi.

Na msilete zile sababu za kukariri kwamba wasingeweza kumzuia Magufuli kwasababu alikuwa katili, kama waliona tatizo lipo na halifanyiwi kazi wote wangetakiwa kujiuzulu ili kuonesha kutokubaliana nae, lakini kukaa kwao kimya maana yake walimuunga mkono.

Anyway, nimemkumbuka Nape siku ile aliyoenda pale ikulu baada ya kuomba msamaha, alipopiga picha na Magufuli akiwa ameweka mikono yake karibu na paji la uso kama vile anamsujudia mwanadamu yule anayemuita leo mwizi.
Uchunguzi ufanyike TU tuliaminishwa Kila kitu kufanywa Kwa fedha za ndani
 
Zilikopwa likajengwa Listiggler pale watu wapate umeme nafuu.... zilikopwa ijengwe SGR chap...Zilikopwa Bandari ya Dar iongezewe uwezo kwa maana ya no of berth, zilikopwa daraja la busisi lijengwe, zilikopwa meli ziwa victoria na vivuko nchi nzima viwe kazini..
Zilikopwa kujenga stand za kisasa nchi nzima, zilikopwa kujenga masoko ya kisasa nchi nzima.
Mkopaji alikopa ili miundombinu ya umeme iwe madhubuti...Mkopaji alikopa kufufua shirika la ndege na usafiri wa reli nchi nzima..

Mkopaji akasimamia mwenyewe alichokopa ili kinachokusudiwa kipatikane... Uzuri zaidi mkopaji alifocus kuspeed up uzarishaji..Uzuri wake hata mtoto mdogo anaona tafsiri sahihi ya mkopaji ni nini alichokusudia kwa Tanzania..

Mkopaji alidhamiria kuondoa kelele za umeme wa dharula kila siku na makesi yanayonufaisha Pumbavu kila kukicha, mkopaji alidhamiria tupate umeme nafuu na uwe mwingi kiasi cha kuuza nje...mkopaji alikuwa na dhamira ya kukopa leo lakini tusikope tena kesho kwa kuwekeza kwenye maeneo ambayo yatatufanya tuwe strong na strong huko mbeleni...

Bila ushabiki, mkopaji wa awamu ya tano alikuwa anajua nini anafanya inawezekana kuliko wakopaji woote huko nyuma...Pumbavu hazitaki nchi ijitegemee na tuache kuwa ombaomba ili Pumbavu na waume zao waendelee kutunyonya leo kesho, vizazi na vizazi... vibaraka na wengine wafuata upepo hawajui wanashabikia Cartel za wahuni ambazo dhumuni kuu ni kuwanyonya ndugu zao na nchi..
Kwani wewe ndiye uliyekopa.
Wacha CAG akafanye kazi yake.
 
Mbunge wa MTAMA Nape Nnauye amesema deni la Taifa limekuwa kwa kasi sana ndani ya miaka 5 iliyopita na kusema japo Serikali inadai ni himilivu hali sio nzuri

Nape ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya 5 ilikopa mikopo mingi huku asilimia 40 ya mikopo hiyo ikiwa ni ya kibiashara hivyo kuwa na riba kubwa

Ameongeza kwa kutaka uchunguzi ufanyike juu ya mikopo hiyo na ilinganishwe na thamani ya miradi ambayo mikopo hiyo ilifanya

Ameipongeza Serikali ya awamu ya 5 kwa kuweka wazi mkopo wa 1.3 trilioni iliyokopa kitu ambacho hakikuwepo kipindi kilichopita na kutaka uwazi huu uigwe

Nape Aache chuki na unafki
 
Ukweli wakati mwingine wabunge wetu siwaelewi.

Mfano wakati wa awamu ya 4 ule Mradi wa bandari ya Bagamoyo ulikuwa sawa.

Wakati wa awamu ya 5 Mradi ukawa haramu.

Wakati wa awamu ya 6 Mradi unaelekea kuwa.......

Na hizo awamu zote wabunge ni ndiyooooo!

Leo hii tena wabunge wengi wanatoa kauli kama siyo wao waliokuwepo, wengine awamu zote 3.

Na sisi raia kimyaaaa!

Nahisi tuna matatizo makubwa ya msingi.
 
Mbunge wa MTAMA Nape Nnauye amesema deni la Taifa limekuwa kwa kasi sana ndani ya miaka 5 iliyopita na kusema japo Serikali inadai ni himilivu hali sio nzuri

Nape ameongeza kuwa Serikali ya awamu ya 5 ilikopa mikopo mingi huku asilimia 40 ya mikopo hiyo ikiwa ni ya kibiashara hivyo kuwa na riba kubwa

Ameongeza kwa kutaka uchunguzi ufanyike juu ya mikopo hiyo na ilinganishwe na thamani ya miradi ambayo mikopo hiyo ilifanya

Ameipongeza Serikali ya awamu ya 5 kwa kuweka wazi mkopo wa 1.3 trilioni iliyokopa kitu ambacho hakikuwepo kipindi kilichopita na kutaka uwazi huu uigwe

Kwa kuwa AMEKUFA
 
Polepole ajibu hizi tuhuma akaguliwe na yeye
 
Kwa vyovyote vile Nape alivyo haiondoi uzito wa hoja yake kwa sababu,

1 Tuliaminishwa kuwa fedha zote za miradi zilikuwa za kwetu, na hapa ndipo tatizo linapoanzia. Watetezi mtueleweshe nini hasa maana ya fedha zetu za ndani na si kutudanganya kuwa eti "ukikopa ukija kulipa ndo zako" huu ni utoto. Na nini lilikuwa lengo la udanganyifu huu?

2 Fedha zilizokopwa ni nyingi Sana tena
kinyume na matakwa ya sheria za bunge na katiba ya nchi. Lengo la kutofuata sheria lilikuwa ni lipo?

3. Miradi mingi mikubwa inayotekelezwa hadi sasa bado haijakamilika ukilinganisha na wingi wa fedha zilizokopwa mbali na yale makusanyo ya 1.4 tr kila mwezi tuliyokuwa tunatangaziwa. Je ni kweli fedha zote hizi ndo ziliishia hapo?

4.Mikopo zaidi ya 40% ni yakibiashara inayohitaji kuzaa riba ndani ya muda mfupi ambapo hadi sasa tumeshaanza kuumia kwa kuzalisha riba ya 5tr hata kabla ya kupata faida ya miradi yenyewe. Je hapa napo utadai eti uzalendo upo? Kumbuka kila alipopanda jukwaa aliponda Sana mikopo ya mabeberu, je ni Jpm kweli aliyekopa au ni mwingine? Hili linahitaji uchunguzi kama Nape alivyo toa maoni.

Wanaopinga hoja ya Nape wajikite hapo waaache kumshambulia kwa hoja nyepesi za kuorodhesha vitu bila kuzingatia thamani ya fedha maana bila hili nao ni ufisadi mkubwa katika ofisi ya Rais na si Magufuli kama wanavyodhani.
 
Nape asisahau waliokuwa viongozi waandamizi wa hiyo serikali anayoilaumu ndio hawa waliopo kwenye serikali mpya anayojipendekeza kwao ili apate teuzi.

Na msilete zile sababu za kukariri kwamba wasingeweza kumzuia Magufuli kwasababu alikuwa katili, kama waliona tatizo lipo na halifanyiwi kazi wote wangetakiwa kujiuzulu ili kuonesha kutokubaliana nae, lakini kukaa kwao kimya maana yake walimuunga mkono.

Anyway, nimemkumbuka Nape siku ile aliyoenda pale ikulu baada ya kuomba msamaha, alipopiga picha na Magufuli akiwa ameweka mikono yake karibu na paji la uso kama vile anamsujudia mwanadamu yule anayemuita leo mwizi.
Nape alichoka sana kutoka geti la ikulu mpaka kumfuata alipo JPM

atakuwa alijambajamba na hivi GYM haijui...
 
Hii ndio CCM Ina democrasia ndani yake sio Ile saccos ya chadema mwenyekiti alikuwa anawakata mishahara na posho wabunge wa wake na ni marufuku kuhoji na mpaka sasa hazijulikani zilienda wapi hizo pesa
Huyo kasemea Bungeni kwa sababu ana Kinga. Hoja hiyo hawezi kuiongelea nje ya Bunge. Angeitisha Press Conference halafu akaongea hiyo hoja hapo ningemuona wa maana. Kinachoendelea Bungeni ni Maigizo tu ili kuwahadaa Watz kwamba Wapinzani sio muhimu hata Wabunge wa CCM wanaweza kuikosoa Serikali.
 
Dola mil 30 iko njiani kupigwa huko sijui ni tilioni au bilioni ngapi
 
Zilikopwa likajengwa Listiggler pale watu wapate umeme nafuu.... zilikopwa ijengwe SGR chap...Zilikopwa Bandari ya Dar iongezewe uwezo kwa maana ya no of berth, zilikopwa daraja la busisi lijengwe, zilikopwa meli ziwa victoria na vivuko nchi nzima viwe kazini..
Zilikopwa kujenga stand za kisasa nchi nzima, zilikopwa kujenga masoko ya kisasa nchi nzima.
Mkopaji alikopa ili miundombinu ya umeme iwe madhubuti...Mkopaji alikopa kufufua shirika la ndege na usafiri wa reli nchi nzima..

Mkopaji akasimamia mwenyewe alichokopa ili kinachokusudiwa kipatikane... Uzuri zaidi mkopaji alifocus kuspeed up uzarishaji..Uzuri wake hata mtoto mdogo anaona tafsiri sahihi ya mkopaji ni nini alichokusudia kwa Tanzania..

Mkopaji alidhamiria kuondoa kelele za umeme wa dharula kila siku na makesi yanayonufaisha Pumbavu kila kukicha, mkopaji alidhamiria tupate umeme nafuu na uwe mwingi kiasi cha kuuza nje...mkopaji alikuwa na dhamira ya kukopa leo lakini tusikope tena kesho kwa kuwekeza kwenye maeneo ambayo yatatufanya tuwe strong na strong huko mbeleni...

Bila ushabiki, mkopaji wa awamu ya tano alikuwa anajua nini anafanya inawezekana kuliko wakopaji woote huko nyuma...Pumbavu hazitaki nchi ijitegemee na tuache kuwa ombaomba ili Pumbavu na waume zao waendelee kutunyonya leo kesho, vizazi na vizazi... vibaraka na wengine wafuata upepo hawajui wanashabikia Cartel za wahuni ambazo dhumuni kuu ni kuwanyonya ndugu zao na nchi..

Kama alikopa ili ajenge umeme wetu ili tupate umeme wa bei rahisi, mbona ndege alisema ni zetu na alinunua kwa cash, kwanini nauli sio nafuu kama ilivyokuwa fastjet? Kipi kinakuaminisha umeme ungekuwa nafuu, iwapo ndege ni zetu na bado sio nafuu?
 
Ya Kikwete ilikopa ngapi ?Sasa mnamuonea Magufuli kwa vile hawezi kusema tena.Wewe Nape unajiona msafi wakati ni fisadi tu.Hivi Magufuli angekuwa ni Rais mstaafu na yupo hai ungetoa hayo maoni ?.Akiwa hai nyote mlimuogopa kama Ukoma. Akiwa kafa muogopeni hivyo hivyo.Idiots.
Kipindi cha yule kiongozi muovu aliongea ukweli akatolewa bastola hadharani. Sasa acha aseme ukweli akiwa yuko kuzimu maana hakutaka ukweli usemwe akiwa hai.
 
NAPE;JPM KALA MKOPO.

Jpm kala mkopo kwa kujenga mradi wa umeme mkubwa,Bwawa la Rufiji (Bwawa la Mwalimu Nyerere) unaozidi uwezo wa umeme wote unaozalishwa tangu mkoloni,Nyerere,Mwinyi,Mkapa na Kikwete na Sasa hakuna tena mgao wa Umeme,tutapata Umeme na kusaza,tutasahau habari ya iptl,dowans,Richmond na Escrow!.

Jpm kala mkopo kwa kujenga Reli ya Umeme,Reli ya kisasa yenye uwezo mkubwa wa kwenda kwa haraka na kubeba mzigo mkubwa kuliko Reli zote nchini,Treni ambayo itatumia saa moja na nusu toka Dar hadi Morogoro,na Masaa matano tu toka Dar hadi Mwanza,hii imefanya kuharakisha Maendeleo,badala ya kusafiri Masaa 17 toka Dar hadi Mwanza,sasa hivi ni masaa 5 tu kwa treni ya Umeme ya SGR.

Jpm kala mkopo kwa kujenga maghala ya kutunzia vyakula kwa mikoa yote inayozalisha vyakula kwa hifadhi za taifa letu,Sasa Taifa limekuwa na hifadhi ya kutosha ya Mazao ya Chakula.!.

Jpm kala mkopo kwa kufufua shirika la ndege la atcl na ununuzi wa ndege zake kumi na moja kwa ajili ya kukuza na kuboresha sekta ya Utalii,hivi sasa tunashuhudia Watalii zaidi ya 1,000 wakitua nchini.

Jpm kala mkopo kwa kutoa ruzuku ya kielimu ( elimu bure) kwa shule za misingi na sekondari,hivi sasa hakuna mtoto asiyejua kusoma wala kuandika.!.

Jpm kala mkopo kwa kujenga hospitali kwa wilaya zote ambazo hazikuwa na hospitali za wilaya na vituo vya Afya zaidi ya 300 nchini baada ya kuvikuta vituo 67 tu!

Jpm kala mkopo kwa kumalizia miradi iliyoanzishwa na watangulizi wake ambayo ilikwama kuendelea baada ya pesa kupigwa ama ujenzi usioridhisha kama barabara,Madaraja,Viwanja vya ndege vya zamani na Vipya,Kujenga barabara za juu na zile za kukatisha bahari ya hindi na kule ziwa Victoria na vivuko mbalimbali.

Jpm kala mkopo kwa kuendelea kujenga miundombinu ya bandari na ujenzi wa meli mpya kwa maziwa ya Nyasa,Victoria na Tanganyika!.

-Kwa nini Jpm alikula mkopo,

JPM alikula mkopo kwa sababu ni Mzalendo na aliyoyafanya kila Mtanzania ameyaona hata watoto wadogo wanajua,Jpm aliyoyafanya yalikuwa damuni mwakw,ukimchana hivi damu yake inasema Mimi ni Mtanzania,nitapenda kuiona Tanzania ikiwa Taifa kubwa kama China.

-Jpm alikula mkopo mara tu baada ya kuapishwa kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuanza miradi mingi nchi nzima,miradi inayoonekana kwa macho na sio miradi hewa ama ya kitapeli kama miradi tuliyowahi kuisikia siku za nyuma,Miradi aliyofanya Jpm inaonekana wazi na Wananchi wanapata faraja,ni miradi ya barabara nchi nzima,meli,vivuko,umeme,maji,afya,utalii,bandari,na viwanja vya ndege,Siku za nyuma tulikuwa tunaambiwa maneno tu ama kuishia kuona ujenzi usioridhisha.

-Mwaka 2016 Jpm alikula mkopo pale alipoanza kwa vitendo kupiga kazi,Wazanzibari walimuita "Bosi kazi" Wazee wa Awamu ya nne waliita nguvu ya soda,lakini siku zilivyozidi kwenda wazee wa kitonga waligundua si povu wala nguvu ya soda bali mtendakazi yupo kazini.Ujenzi ulioanza na kumalizika ulitoa picha ya utendaji wa kutukuka katika awamu ya tano,Mwaka 2016 tulianza kuona matunda halisi ya maneno,ahadi na utendaji kazi wa Awamu ya tano na ukamilishwaji wa ilani ya CCM kwa asilimia 120.

-Jpm kala mkopo katenda haya yafuatayo,wenzangu na Mimi wale walikula mkopo sijui walifanya nini? Nothing to write home about!

1.Hostel za Chuo cha UDSM.

2.Hostel za Askari Magereza.

3.Ununuzi wa Ndege 11 (Nyingine 3 zinakuja mwakani).

4.Ujenzi wa Flyover Tazara na Ubungo.

5.Upanuzi wa Airport Mwanza
Upanuzi barabara ya Moroco Dar es Salaam.

6.Ujenzi wa Meli kubwa 6 katika Ziwa Victoria,Ziwa Tanganyika na Ziwa Nyasa.

7.Kukomesha Rushwa
Kurejesha nidhamu Makazini.

-Mwaka 2017 Jpm alikula mkopo pale tulipoona ujenzi mkubwa miradi mbalimbali ukianza.

-Uzinduzi ujenzi wa reli kwa ajili ya treni ya Umeme.

Ujenzi wa barabara ya Mtwara-Tandahimba

-Jpm alikula mkopo kwa kukomesha Watumishi Wenye Feki hivyo kuokoa Mabilioni ya Fedha.

Barabara ya kuunganisha Wilaya za Kibondo kigoma Kaliua huko Tabora.

Miradi Mikubwa ya Maji,Dar,Morogoro,Dodoma,Kigoma,Tabota,na Shinyanga.

Uwezeshaji Ujenzi Bomba la Mafuta kutoka Hoima mpaka Tanga.

-Jpm alikula mkopo kwa kuwa katika miaka yake mitano kila upitapo ujenzi ulikuwa unaendelea.

Dar es Salaam kila kona Barabara ya Tandale-Sinza- Mawasiliano barabara imejengwa,Mitaa ya Kinondoni hivi ina lami,Ubungo Interchange inajengwa
Madaraja yanajengwa

Upanuzi wa barabara kuu ya Ubungo hadi chalinze unafanywa kwa kiwango cha barabara nane.

-Jpm alikula mkopo kwa ujenzi wa Flyovers zinajengwa pamoja na barabara za ziwani na baharini.

-Jpm alikula mkopo kwa kuisimama vyema miradi ya umeme inajengwa na miradi mingi ni kwa hela za watanzania wenyewe,Miradi wa Umeme wa Gas wa Kinyerezi,na mradi wa Bwawa la Umeme la Rufiji (Bwawa la Umeme la Mwalimu Nyerere)

Miaka yote maeneo ya Mbezi na kimara walikuwa hawapati maji japo yanapita njia hiyo hiyo lakini sasa maji yamefika mbezi, na bado wanaendelea kutandaza mabomba ili kupeleka maji.

Awali waliokuwa wanakula hela za wananchi ni wenye miradi ya kuuza maji kwa magari. Ila sasa wananchi wamekombolewa.

-Jpm kala mkopo kwa kusimamia utendaji kazi na kufanya performance appraisals, Utendaji kazi umeimarika, sasa hivi kila mmoja anaona cheo akipewa ni kama kakalia kaa la moto.Yale mambo ya kupiga hela na kukaa ofisini kupiga usingizi yameisha watu ni kazi la sivyo unawajibishwa.

Madawa sasa yanapatikana hospitali, ile hali ya madawa ya hospitali yanapelekwa katika Pharmas binafsi imeisha.

Hospitali sasa za serikali ukienda mgonjwa anajaliwa sio kama ilivyokuwa awali.

-Jpm kala mkopo kwa kuleta Uwajibikaji,Taasisi za serikali wafanyakazi wamekuwa wanawajibika,hakika nidhamu imeimarika.

-Jpm kala mkopo kwa usimamizi madhubuti wa mapato ya Serikali, sasa taasisi za serikali zinajiendesha kibiashara na si kihasara kama ilivyokuwa awali, ilikuwa ni ulaji tuu wa hela, upigaji dili, taasisi zinakufa, hakuna gawio kwa serikali, ila sasa zinatoa gawio.

Hakika kila kitu ni usimamizi imara, ukicheka na kima utavuna mabua.

-Jpm kala mkopo kwa kusimamia nidhamu kazini,Awali watu walikuwa wanaulilia uongozi, hata wasio kuwa na elimu walikuwa wanagombea kupata uongozi, katika miaka yake mitano uongozi ulikuwa mgumu sababu kama wewe si muwajibikaji una ndoto za kupiga tuu, hupati nafasi, Uongozi umekuwa una hadhi kwa sasa.

@Nape pokea Salaam za mkopo aliokula JPM,hii ni robo tu ya mkopo aliokula JPM.
 
Mafumbo ya nini si aongee tyu ya moyoni Kala mkopo Kala mkopo
JamiiForums2022177639.jpg
 
Back
Top Bottom