Nape: Kampuni za simu acheni kutuma ujumbe ambao mteja hajaomba, hii tabia ikome

Nape: Kampuni za simu acheni kutuma ujumbe ambao mteja hajaomba, hii tabia ikome

"Kumekuwa na kelele nyingi kutoka kwa wananchi ambao wanalalamikia suala la kuendelea kupokea jumbe mbalimbali ambazo hawakuziomba katika huduma na hivyo kugeuka kuwa ni kero badala ya huduma,naomba tuliangalie hili," alisema.

Kutokana na hali hiyo, Waziri huyo wa Mawasiliano aliyataka makampuni yote yakae na watoa huduma kujadiliana kuhusu jambo hilo na kuona namna ya kuondoa tabia hiyo (ujumbe) kwa mtu ambaye hakuomba.
Malalamiko kwake ni kelele!!!

Hivi ule uzinduzi wa line moja mitandao yote uliishia wapi au walitupiga changa la macho wachote pesa
 
Pia Waache kutuunganisha huduma ambazo hatujaomba
Aisee mimi kuna siku nimewapigia voda nikawatolea uvivu. Nilikua nashangaa unakuta nna bando la data, nna bando la dakika na nna bando la sms. Cha ajabu kila nikiweka muda wa maongezi ili nifanye miamala ya simbanking nakuta hela yote imeliwa! Saa nyingine unakuta nimeweka hela dakika hiyo hiyo nikicheki balance nakuta 0.

Kuwapigia wananiambia eti nimejiunga sijui huduma ya miito, sijui whatsap status, sijui huduma gani kanitajia huduma zaidi ya 5! Wakati mimi huduma hizo kwanza sijawahi kujiunga wala siihitaji! Nikamuambia acheni ujinga wa kuunganisha watu maujinga yenu automaticaly halafu mnakata hela. Tangu siku hiyo nikiweka hela naikuta kama ilivyo.
 
Back
Top Bottom