Nape: Kampuni za simu haziibi vifurushi vya intaneti vya wateja

Nape: Kampuni za simu haziibi vifurushi vya intaneti vya wateja

beth

JF-Expert Member
Joined
Aug 19, 2012
Posts
3,880
Reaction score
6,368

Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Bungeni kuwa Serikali inaendelea kuchambua malalamiko ya matumizi ya Bundle kwenye simu.

Amefafanua, "Malalamiko kwamba kuna Bundle zinawekwa kwenye Simu, zinatumika bila Mtumiaji kuzitumia yamekuwepo, yamefikishwa Mamlaka husika na Uchambuzi umefanyika. Matokeo yanaonesha hakuna wizi uliotokea, isipokuwa kuna tatizo la matumizi ya simu za kisasa".

Ameongeza, "Matatizo hayo yamejikita kwenye maeneo mawili; 1) Hizi simu za kisasa wakati mwingine hata ukiwa hutumii kuna baadhi ya Applications zinaendelea kufanya kazi nyuma ya simu. 2) Simu hizi unaweza kuweka Bundle lako ukawasha 'Hotspot' kinachoruhusu mtu mwingine kutumia Data uliyonayo".

Kupitia Twitter Waziri Nape ameandika.

"YEYOTE ANAYEAMINI KAIBIWA KIFURUSHI KABLA HAJATUMIA AKAKUTA KIMEISHA, ALETE USHAHIDI TUTAFANYA UCHAMBUZI KWA KUTUMIA VIFAA VYA KISASA NATUTAWEKA HADHARANI KUONYESHA TATIZO LILIPO. Lakini mpaka leo malalamiko yote yaliyopokelewa tatizo limekutwa ni uelewa wa matumizi ya simu JANJA"
 
Waziri wa Habari, Mawasiliano na Teknolojia ya Habari, Nape Nnauye amesema Serikali inaendelea kuchambua malalamiko ya matumizi ya Bundle kwenye simu...

Hahahahahah[emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji1787][emoji23][emoji23][emoji23][emoji23] Nape Nnauye kashiba sasa hivi ana jiandaaa kutoa wimbo akiwa anapiga geeter hahahahaba
 
Back
Top Bottom