Nape: Mradi wa umeme wa Stiegler's Gorge haupo kwenye ilani, sie tulinadi mradi wa gesi. Huu tumedandia tu

Nape: Mradi wa umeme wa Stiegler's Gorge haupo kwenye ilani, sie tulinadi mradi wa gesi. Huu tumedandia tu

[HASHTAG]#KutokaBungeni[/HASHTAG]: Waziri wa zamani na Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye (CCM) ameishangaa Serikali kuweka nguvu nyingi kwenye mradi wa umeme wa Stigler’s George ambao haupo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2015 na kuachana na umeme wa gesi ambao waliunadi wakati wa kampeni.
Ni aibu na fedheha kwake Nape, aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM na pia Rais kusahau Mipango ya Maendeleo kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Chama chake na Mikakati mbalimbali ya Kitaifa.

Kuhusu nishati, si kweli uzalishaji wa nishati ya gesi haujapewa kipaumbele, wakati mradi wa Kinyerezi ni kielelezo tosha.

Pia siyo kweli 'Stiglers Hydropower Project', ni nje ya Ilani ya CCM kuhusu nishati. Asome Kifungu cha 43(a) cha Ilani ya Uchaguzi kwa pamoja na Mkakati wa Nishati wa Wizara ya Nishati (Power System Master Plan (PSMP 2016–2040)).
 
Tunachotaka ni Umeme ili Mgao Upungue,Viwanda Vijengwe,Bei ya Umeme Ishuke,
Umeme wa Gas ni Ghali kuliko Umeme wa Maji na huo ndo Ukweli Mchungu....sasa MTU anasema Sijui LNG, sijui Magu mi naona Anachelewa tuu Kuanzisha Stiegliers gorge tuu Mapema...wanaopinga wana Interest Zao...
 
Nape kweli amechanganyikiwa kabisa hivi ni lini na ni wapi serikali imetelekeza miradi ya gas? Si ni juzi tuu Mh Rais kazindua mradi wa kuongeza megawati kupitia nishati ya gas?
Hivi kweli Nape yuko timamu? Hivi kweli hajui mipango na hatua za utekelezaji wa miradi ya gas? Hii ni aibu kubwa sana tena sana......
Hivi kweli amesema akimaanisha au ametania? Hahahaha Hivi anavyo sikia tanzania ya viwanda anafikiri nini? Hahaha aisee Nape ana shida ya kisaikolojia...
 
kama vyote vitasaidia kupunguza tatizo la umeme sioni tatizo.
Issue ni kupaendeleza kusini ambapo Nnape anatokea.Nafikiri ndio msingi wa hoja yake.Anawawakilisha watu wake.
 
Nnape anapewa kichwa na Membe kuongea umbea hadharani bila kufikiria. Hii serikali inaona mbali sana isipokuwa watanzania hawapendi kasi ya maendeleo kwani hawataki kuendelea, wanataka wabaki vile vile huku wakiaminishwa hii nchi ni masikini. Weka miundombinu ya uhakika, then uone maendeleo yatakavyokuja. Naomba Nnape akamatwe na kuhojiwa uraia wake.
 
Basi ata stiegler gorge ilikuwepo tokea enzi za Nyerere pia mkuu.

Nape kaonesha dhahiri ana chuki dhidi ya Mheshimiwa tokea afutwe Uwaziri.
Kwakweli Nape kwenye hili ameonesha anayo chuki kubwa maana ni juzi tuu Mh kazindua mradi wa kuongeza megawati kwenye grid ya taifa kupitia nishati ya gas sasa sijui Nape hakuwepo nchini au asikilizi habari? Sijui anafikiri Tanzania ya viwanda maana yake nini?
 
Nape kweli amechanganyikiwa kabisa hivi ni lini na ni wapi serikali imetelekeza miradi ya gas? Si ni juzi tuu Mh Rais kazindua mradi wa kuongeza megawati kupitia nishati ya gas?
Hivi kweli Nape yuko timamu? Hivi kweli hajui mipango na hatua za utekelezaji wa miradi ya gas? Hii ni aibu kubwa sana tena sana......
Hivi kweli amesema akimaanisha au ametania? Hahahaha Hivi anavyo sikia tanzania ya viwanda anafikiri nini? Hahaha aisee Nape ana shida ya kisaikolojia...


Huyu bado ana hasira na serikali kushushwa cheo, pia Membe na Kikwete wanamtumia vibaya bila yeye mwenyewe kujigundua. Akamatwe tu kwa upotoshaji.
 
Kwakweli Nape kwenye hili ameonesha anayo chuki kubwa maana ni juzi tuu Mh kazindua mradi wa kuongeza megawati kwenye grid ya taifa kupitia nishati ya gas sasa sijui Nape hakuwepo nchini au asikilizi habari? Sijui anafikiri Tanzania ya viwanda maana yake nini?
Kabisa mkuu.

Jamaa ana chuki sana.
 
Dikteta ni yule ambae amebadili katiba ya Chadema na kufanya nafasi ya mwenyekiti wa chama haina ukomo wa uongozi. Dikteta niyule ambae pesa za ruzuku za chadema anajilipa madeni ambayo hayaeleweki na hayana mwisho.Dikteta ni yule nafasi za Viti maalumu anazigawa kwa rushwa ya ngono.
Chadema sio serikali wala hakikuhusu ila serikali inatuhusu wote hata mrema na cheyo ni wenyeviti wakudumu hatuwasemi maana vyama ni vyao walianzisha wenyewe hapa tunaongelea serikali yetu wote
 
Kwa hiyo Nape anamaanisha 100Mil za Mzee Ngoma, Hela ya kununulia Bombadier, Hostel za UD, na mengineyo yalikuwepo kwenye ilani ya CCM??
Alichohoji ni miongoni mwa hayo mengine kama 10bn za kujengea polisi, ukuta nk..
 
[HASHTAG]#KutokaBungeni[/HASHTAG]: Waziri wa zamani na Mbunge wa Mtama, Nape Nnauye (CCM) ameishangaa Serikali kuweka nguvu nyingi kwenye mradi wa umeme wa Stigler’s George ambao haupo kwenye Ilani ya Uchaguzi ya CCM ya Mwaka 2015 na kuachana na umeme wa gesi ambao waliunadi wakati wa kampeni.
Ikulu ni ya wapiga deal nowadays
 
Chadema inapokea Fedha za watanzania kama ruzuku,Ndio maana sija mzungumzia Cheyo wala Mrema. Kama mkitaka msikosolewe kama chama, msipokee Fedha za walipakodi kupitia Ruzuku.
 
Kama anakereka atupishe kwanza..atarudi tukiwa tumekamilisha miradi yetu..ye amesahau jk ndio aliingia mikataba ya hovyo kwenye gas hadi watu kuuawa mtwara
 
Huyu jamaa mkuu anamuangaliaaaaaa anamchekiiiiiii halafu anasema hiiiiiiiiiiiiìiiiiiiiiii.
 
Point ya Nape inavitu viwili ambavyo ameongea kwa wakati mmoja ,nafikiri nape ameongea uchumi wa wanamtwara kwa kutegemea gas, sasa hapo either anaongelea shughuli za uzalishaji akiwa maana ya kuchakata na kuanza kuuza zifanyike, pili suala la gas asilia kutumika katika kama nishati ya umeme, kuhusu suala la gasi kutumika katika nishati ya umeme hili linafanyika maana kuna ujenzi kinyerezi I umeshakamilika na uliingiza kiasi cha umemem katika grid ya taifa, pia upanuzi wake wa kinyerezi I unaendelea na utakamilika mwakani, kinyerezi II pia juzi magufuli kazindua, zifuatazo kinyerezi III, na kuendelea zitaendelea kulingana na ratiba na upatikanaji wa pesa, haya ni kwa mujibu wa taariza zao serikali.

Nahisi kikubwa ambacho nape anashangaa ni kwamba mradi wa gas mbona serikali hawaufatilii, au kwa nini hauko kwenye hotuba ya waziri mkuu kama shughuli za uzalishaji kuanza na kupatikana kwa gasi ,uuzaji ndani na nje ili kuwakomboa watu wa mtwara ,lindi na watanzania kwa ujumla, hapa ndipo nape nafikiri kichwa kinamuuma, kwa kweli sio yeye tu, ni watanzania wengi, ila tuliuza kwa wawekezaji, kipindi kile kile cha awamu ya nne, pengine serikali ya awamu ya tano ifuatilie na itueleze kuna nini? mbona mradi kwa ujumla umekuwa kimya? awamu ya tano wao wamekuta mambo yalishakwisha, mikataba ilishafungwa,kinachofuata ni wawekezaji watekeleze,kwa hiyo serikali watueleze ni lini shughuli rasmi za uzalishaji zitaanza,maana wana mtwara wengi wanasubiri ili waweze kujikwamua, kwa kweli ni swali zuri na jambo jema kuuliza, hapa nakubaliana na nape.

Umeme wa gasi kuanzia phase I, II, III ...., kwa ujumla yake tutapata 2400MW+lakini hazizidi 3000MW, je kama taifa umeme wa kwa ujumla wa 3000MW unatutosha? unatufanya tulizike au tuendelee kuongeza ili tuwe na options mbalimbali na tuweze kupata umeme mwingi na kwa bei ndogo? jibu ni ndio, hivyo magufuli kwenda na Stiegler's bado ni option nzuri ukizingatia nia yake ya uchumi wa viwanda.
 
Back
Top Bottom