Ni aibu na fedheha kwake Nape, aliyekuwa Katibu Mwenezi wa CCM na pia Rais kusahau Mipango ya Maendeleo kama ilivyoainishwa kwenye Ilani ya Chama chake na Mikakati mbalimbali ya Kitaifa.
Kuhusu nishati, si kweli uzalishaji wa nishati ya gesi haujapewa kipaumbele, wakati mradi wa Kinyerezi ni kielelezo tosha.
Pia siyo kweli 'Stiglers Hydropower Project', ni nje ya Ilani ya CCM kuhusu nishati. Asome Kifungu cha 43(a) cha Ilani ya Uchaguzi kwa pamoja na Mkakati wa Nishati wa Wizara ya Nishati (Power System Master Plan (PSMP 2016–2040)).