Nape Nnauye amjibu Mangula, ni Ujenzi wa Bandari ya Bagamoyo

Uwanja wa ndege wa Chato atuambie upo kwenye ilani ipi?
ule mbona umekuwa sawasawa na ulivyo uwanja wa ndege wa mobutu. watu walisema sana hili wakati wa ujenzi. sasahivi ni ndege gani itaacha kutua au kupeleka wasafiri Mwanza ambao ni jiji la biashara, ikaenda kupeleka abiria chato? tuwe wakweli.

nashauri kwasababu pale ni karibu na majirani, tuweke tu uwe uwanja wa Jeshi, tuwakabidhi jeshi kabla haujaota majani. jeshi watautumia vizuri na itakuwa strategic sana pale kwao kutumia kuruka kwenda kokote iwe uganda, rwanda, burundi au dr congo. kwani tangu iwe vile, ni ndege gani nyingine imendoka pale? zaidi ya hizi chache za Mr. Rais anapotembelea kule? za abiria hakuna na hazitakuja ziende. na burugi national park ndio inaenda kufa hivyo. huwezi kulazimisha nature.
 
Nadhan utoto tu,vp kuhusu vyombo vya dola???
Mangula ndiye ameshikilia CCM,
JK yalimshinda,mzee alifuatwa shambani kwenye viazi.Safu zote za juu Hangaya kawang'oa.Jiulize kwanini mzee yupo na kwanini alisimama na member kutofukuzwa chamani.Mzee wa utaratibu na haki.
 
Ndiyo umjibu Mangula na upuuzi wake
 
Nape should learn to keep quiet

Apunguze u-much know

He is not special in any way
 
Nape naye bwana...ameshakomaa mishipa ya shingo siku anaropoka tu 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂 😂
 
CCM huwa mfumo wake wa kujiimarisha ni kuparurana baada yapo huwa imara mpaka upite uchaguzi wala usishangae utaachwa wewe kama alivyowachwa Lissu!
Mbona kipindi cha mwenda kuzimu haikuwepo hiyo?sasa kuwa imala vipi , unawezaje kujiona kuwa upo imala wakati huyo mpinzani wako kila akijitutumua rungu!!!
 
Kwani bandari ya "Bwagamoyo" ni kipaumbele cha wananch?
 
Umefanya total personal attack badala ya kujikita kwa hoja yake. Amehoji vizuri sana, tena kwa mifano..
 
Ni hatari sana eti kuzunguka nchi nzima kuitangaza Ilani yako ili uchaguliwe kumbe ni danganya toto. Hii ni hatari sana! Kama Ilani inashindwa kudumu kwa miaka 5, hii ni zaidi ya hatari. Inamaanisha .P W Boatha ni ukweli maneno ya aliyekuwa Rais wa Afrika kusini aliyesema- Mtu mweusi plan yake ni ya siku moja tu, na ya keshokutwa yatajulikana kesho kutwa. Du, hapa ndipo Nape anapotueleza kuwa CCM fikra zake haziwezi kuplan kwa miaka 5.

Kwa kawaida vitu vya dharura ndio hubadilika, kwa Nape ni amka na uje na wazo jipya kila kukicha - Populist! Makosa ni makosa hata kama yalifanyika toka kwa baba wa Taifa aka Mazoea...Tusihalalishe. Inawezekana hii ndio sababu ya kuwa hapa tulipo baada ya miaka 60 toka mkoloni atuachie nchi yetu aka tupate uhuru.

Jamani, kama hiki chama hakiwezi kuplan kwa miaka 5, kitaweza kweli kuwa na plan ya miaka 10, 15, 20........... Kama hivyo ndivyo, samahani nitakopa neno la Mh Rais "Nonsens" kuwa kuisoma Ilani ya uchaguzi ya CCM ni NONSENS.

M/ mwenye kiti Mangula yupo sahihi 100%, kama tunahitaji kutekeleza vipaumbele vya miaka 5 (2020-2025)wananchi walivyoiingiza CCM madarakani kwa bajeti yetu Finyu ya max 1.9 trilion kwa mwezi. Vipaumbele ndio kila kitu, leo yaliyoelezwa kwenye kilimo yamesahaulika kabisa na yalisahaulika vile vile (2015-2020). Hii inamaanisha miaka 10 bila kilimo, sigusii sakata la kilimo cha miwa/sukari.... Ah acha tu Pole waziri wa kilimo Profesa Mkenda - Pesa yako inakwenda Bagamoyo/Bandari....
 
Hawa vijana wasioweza kulitumikia taifa mpaka wawe mawaziri hawafai, wanajiona bora zaidi ya wengine, uongozi wa serikalini usitafutwe kwa kelele nyingi za mitandaoni, uadilifu wa mtu na uchapakazi wake ndio uwe vigezo.
Bado niko na Nape, hoja yake ndiyo ijadiliwe, je kuhamia Dodoma, bwawa la Nyerere etc vilikuwa kwenye ilani?? Jamani tujikite hapaaa!!
 
Kaka toa maoni kutokana na hoja ya nappe mbona tunapenda majungu sio poa. Nape katoa mawazo yake toa na wewe yakwako. Tabia ya usaka fursa ipo miaka mingi hata ingekuwa wewe
[emoji1666][emoji1666] Hili ndilo tatizo kubwa la vijana wa kizazi hiki, hawana uwezo wa kujadili na kusimamia hoja iliyoko mezani badala yake wao hukimbilia kumrarua rarua mleta hoja.
 
ATCL ina trip mbili kwa wiki kama hujui nakupa taarifa! Vipi unaikubali taarifa au hapana mkuu??
 
Namheshimu sana mzee Mangula lakini kwa hili la bandari ya Bagamoyo amenifanya nijiulize maswali mengi sana.1) Wakati JPM anatekeleza miradi mingi tu ambayo haikuwa kwenye ilani mzee alikuwa wapi? Mifano michache sana ni mradi wa uwanja wa ndege Chato, kununua ndege za ATC kabla ya budget, mradi wa bwawa la Nyerere, daraja la busisi na mingine mingi iliyochangia kuwepo na tofauti ya zaidi ya tril. 1.5 kati ya matumizi yaliyopitishwa na bunge na matumizi halisi.
2) kwa nini JPM alipokataa kutekeleza miradi iliyopitishwa kwenye ilani kama wa kumalizia mchakato wa katiba mpya mbona hakujitokeza kuuliza?
3) Mambo aliyofanya JPM kwa kukiuka katiba na sheria za nchi ni mengi mbona hakukemea au hata kujitokeza na kusema hayaendani na matarajio ya chama. Nachelea kusema kuwa labda mzee ana "personal issues na mradi huu wa Bagamoyo!
 
Shida iko kwa ambayo hayakuwahi kuahidiwa lakini yakatekelezwa kwa matakwa ya mtu.
 
Cookies are required to use this site. You must accept them to continue using the site. Learn more…