Nape Nnauye: Hatukuwakatalia Starlink kufanya kazi Nchini, walikwama wenyewe

Nape Nnauye: Hatukuwakatalia Starlink kufanya kazi Nchini, walikwama wenyewe

Ndugu zangu Watanzania,

Mheshimiwa Nape Nnauye waziri wa Habari ,Mawasiliano na teknolojia ya habari amesema ya kuwa serikali haikuwakatalia Starlink kufanya kazi Nchini bali walikwama wenyewe kutimiza mashariti yaliyohitajika kukamilishwanl ili kupewa lesseni.

Kauli hii imekuja kutokana na manung'uniko na kelele nyingi sana za watanzania mbalimbali mitandaoni kuilaumu serikali hususani waziri mwenye dhamana wakati huu ambao mtandao wa internet umesumbua sana na kukwamisha shughuli nyingi sana katika maofisi mbalimbali ya watu binafsi pamoja na serikali yenyewe.

Ambapo watu mbalimbali na wadau mbalimbali wa habari na mawasiliano wameonekana kutoa maoni yao mitaani na mitandaoni kuwa pengine kama Starlink angekuwepo hapa nchini ,suala lililokuwa limejitokeza hapa nchini la kukatika kabisa kwa huduma ya internet pengine lisingeathiri shughuli za watu binafsi pamoja na serikali yenyewe kama ilivyotokea.

Naweka kalamu chini na kuishia hapa. Chanzo cha taarifa yangu Ni clouds. Ukitaka kwa undani sana ingia clouds ujionee video yake kama una Mb au bando la kutosha kiasi.kama huna mb za kutosha basi wewe chukua hii taarifa kuwa serikali haikuwakatalia Starlink kufanya kazi Nchini bali wao ndio walikwama wenyewe kutimiza mashariti ya kupatiwa lesseni.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
HAya mabumunda ya ccm ni shida sana

sasa kama waliwama si awakwamue walete huduma kusaidia wananchi
 
HIZI SIASA ZA UONGO UONGO NI ZA MUDA MFUPI TU Lucas,utakumbuka Haya menono.
Ulipaswa kuwa mtu wa kohoji vitu kama kijana badala ya kusifia sifia hovyo,

Kwa faida ya Nani?Nikuambie kwa hizi ngonjera hawatawajibika hawa watawala.Bibi zetu akiwemo wa kwako na ndugu zetu wataendelea kulala chini wakiwa hospitalini,Bima ya Afya ya kilaghai, Dhuruma zaidi ya wananchi kwenye matumizi mabaya ya serikali.

Sijawahi sikia hata siku moja ukihoji kuhusu kupuuziwa riport ya CAG iliyojaa wizi ufisadi,wewe kazi yako ni kusifia tu vitu visivyo na kichwa wala miguuu.

Mashart gani?kwanini asiyaweke wazi,Je walikataa kulipa kodi?

Je walitaka makampuni mengine Ya simu/Mtandao yafutwe au?

Kwakuwa ni swala la uma basi iwekwe wazi walipewa masharti gani.

Mbona Magufuli alikataa mradi wa bandari ya Bagamoyo na kusema wazi sababu,iwaje kuwe na usiri kwenye mawasiliano.

Mama alienda kuzindua Kiwanda cha Howo Juzi kati Hapo alisema jamaa wanataka Hili na lile,sisi tumewapa Hili na lile,shida iko wapi.

Nape aache,Acheni ujanja ujanja sisi sio wajinga.

Alienda media tour kufanya nini si angeeleza sababu moja kwa moja?

Hilo Taifa ifike mahali mnaposema maslahi ya nchi mbele muwe mba maanisha sio porojo tuu.
Lucas hizi siasa za uongo uongo ni za muda tuu narudia ni za muda tuuu.
Any way nalala maana naijepandisha sukari buree bila sababu.
Hawa mabumunda walitaka share za kifisadi tu. .. link wakagoma kwa kuwa siyo policy yao na hawana njaa wakasepa

Ndo mode ya biashara kubwa nchini

Lazime utoe share kwa maccm kwanza,
Wawekezaji serious hawawezi kuja hapa labda wale wahuni tu
 
Ndugu zangu Watanzania,

Mheshimiwa Nape Nnauye waziri wa Habari ,Mawasiliano na teknolojia ya habari amesema ya kuwa serikali haikuwakatalia Starlink kufanya kazi Nchini bali walikwama wenyewe kutimiza mashariti yaliyohitajika kukamilishwanl ili kupewa lesseni.

Kauli hii imekuja kutokana na manung'uniko na kelele nyingi sana za watanzania mbalimbali mitandaoni kuilaumu serikali hususani waziri mwenye dhamana wakati huu ambao mtandao wa internet umesumbua sana na kukwamisha shughuli nyingi sana katika maofisi mbalimbali ya watu binafsi pamoja na serikali yenyewe.

Ambapo watu mbalimbali na wadau mbalimbali wa habari na mawasiliano wameonekana kutoa maoni yao mitaani na mitandaoni kuwa pengine kama Starlink angekuwepo hapa nchini ,suala lililokuwa limejitokeza hapa nchini la kukatika kabisa kwa huduma ya internet pengine lisingeathiri shughuli za watu binafsi pamoja na serikali yenyewe kama ilivyotokea.

Naweka kalamu chini na kuishia hapa. Chanzo cha taarifa yangu Ni clouds. Ukitaka kwa undani sana ingia clouds ujionee video yake kama una Mb au bando la kutosha kiasi.kama huna mb za kutosha basi wewe chukua hii taarifa kuwa serikali haikuwakatalia Starlink kufanya kazi Nchini bali wao ndio walikwama wenyewe kutimiza mashariti ya kupatiwa lesseni.

Kazi iendelee, mama Ametufikia na kuwafikia watanzania kwa utumishi wake uliotukuka wa kugusa maisha ya watanzania wanyonge wasio na Sauti.

Lucas Hebel Mwashambwa.Mama ANATOSHA kuendelea kuliongoza Taifa letu kwa muhula wa pili.
Mumeo Nape amefurushwa
 
Taarifa ya Starlink ilisema wameamua kutoendrlea na mipango ya kuwekeza Tanzania kutokana na kuwekewa mazingira magumu. Hawakufafanua. Nape ndiye anatakiwa kutoa maelezo ni masharti gani hayo waliyowekewa Starlink. Dunia nzima, wawekezaji wanatafutwa. Sisi tunashindwa kumpata hata mwekezaji aliyekuja mwenyewe nchini. Halafu tunajificha kwenye hadithi kuwa alishi dwa masharti; ni masharti gani hayo, si aseme.

Ifahamike kuwa nchi inawahitaji zaidi wawekezaji kuliko wawekezaji wanavyoihitaji Tanzania.

Fikiria nchi kama China, inatoa vivutio vingi kwa wawekezaji wa nje kuliko hata wawekezaji wa ndani. Na hiyo ndiyo imeisaidia China kuwa mahali hapo ilipo leo. FDI ya China kwa kila mwaka ni kati ya dola bilioni 80 mpaka 100. Sisi haifiki hata bilioni 2 kwa mwaka. China ina makampuni ya kigeni zaidi ya milioni 1, sisi nchi kapuku tunawawekea vikwazo wawekezaji, na tukiwapokea wawekezaji, tunaingia mikataba ya hovyo inayolenga kuwanufaisha watu wachache badala ya Taifa zima.

"China's FDI Policies

China's laws and regulations on FDI also include related preferential policies and stipulations for special economic zones in the country. In a nutshell, China encourages favorable FDI policies. Therefore, FIEs enjoy preferential treatment when compared to domestic enterprises."
KATIBA mpya ndio itakuwa mwokozi wetu na si vinginevyo
 
Back
Top Bottom