Pre GE2025 Nape Nnauye: Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza, ili mradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe!

Pre GE2025 Nape Nnauye: Matokeo ya kura inategemea nani anahesabu na nani anatangaza, ili mradi ukimaliza unasema Mungu nisamehe!

Mijadala ya Uchaguzi Mkuu wa Tanzania 2025 (Kabla, wakati na baada)
Hata, hivyo, kuna kosa gani alilofanya katika serikali hii!? 🤔...

Mimi binafsi, kutoka katika sakafu ya moyo wangu, sioni ajabu, sishangai na wala sikasirishwi na alichokisema Mh. Nape (tena natumia neno Mh. nikimaanisha anastahili kuitwa Mh.)...

Jamani, si tunataka kiongozi mkweli, ambaye si mnafiki?

Sasa Mh. Nape amekosea kitu gani kuweka wazi kile ambacho wasimamizi wa uchaguzi (inayoitwa tume huru ya uchaguzi) wamekuwa wakikifanya kwa miaka yote?

Kosa lake ni lipi jamani? Kusema ukweli? Mnataka kusema kwamba mlikuwa hamjui kwamba anachokisema Nape ndo huwa kinafanyika siku zote? Uchaguzi wa 2019 (serikali za mitaa) na 2020 (madiwani, wabunge na Rais) anachosema Nape si ndo kilifanyika?

Wote mnajua na mmeshuhudia kile alicho kisema Nape!

Kwa maoni yangu, tunawahitaji viongozi wengi aina ya Nape Mnauye. Pengine umma utawaelewa...na hatimaye labda ufanye uamzi stahiki wa kuchukua hatua.

Nionavyo mimi,Nape ni kama Yuda Iskariotu, mpango wa Mungu usingekamilika bila Yuda Iskarioti kufanya alicho fanya!

Wenye kunielewa wameelewa, ambao hamjanielewa, KAZI IENDELEE
 
Back
Top Bottom